< Ufunuo 5 >
1 Kisha katika mkono wa kulia wa huyo aliyeketi juu ya kiti cha enzi, nikaona kitabu; nacho kilikuwa kimeandikwa ndani na nje na kufungwa na mihuri saba.
Then I saw lying upon the right hand of Him who sat upon the throne, a book written within and on the back, close sealed with seven seals.
2 Tena nikamwona malaika mwenye nguvu akitangaza kwa sauti kubwa: “Nani anayestahili kuvunja hiyo mihuri na kukifungua kitabu hicho?”
And I saw a strong angel proclaiming with a loud voice, "Who is worthy to open the book, and to loose its seals."
3 Lakini hakupatikana mtu yeyote mbinguni, wala duniani, wala chini Kuzimu, aliyeweza kukifungua hicho kitabu au kukitazama ndani. ()
And no one in the heavens or on the earth, or under the earth, was able to open the book, or to look into it.
4 Basi, mimi nikalia sana kwa sababu hakupatikana mtu aliyestahili kukifungua, au kukitazama ndani.
so I began to weep bitterly because no one was found worthy to open the book, or to look into it.
5 Kisha mmoja wa wale wazee akaniambia, “Usilie! Tazama! Simba wa kabila la Yuda, mjukuu maarufu wa Daudi, ameshinda. Yeye anaweza kuivunja mihuri yake saba na kukifungua hicho kitabu.”
But one of the Elders said to me. "Do not weep! Behold, the Lion of the tribe of Judah, the Root of David, has conquered, and so can open the book with its seven seals."
6 Kisha nikaona pale katikati ya kiti cha enzi Mwana kondoo amesimama, akizungukwa kila upande na vile viumbe hai vinne, na wale wazee. Huyo Mwanakondoo alionekana kana kwamba amechinjwa. Alikuwa na pembe saba na macho saba ambayo ni roho saba za Mungu zilizokuwa zimepelekwa kila mahali duniani.
Then I beheld a Lamb standing as if slain in the midst of the throne and of the four Living Creatures, and in the midst of the Elders. He had seven horns and seven eyes (which are the seven Spirits of God, sent forth into all the earth).
7 Mwanakondoo akaenda, akakitwaa hicho kitabu kutoka mkono wa kulia wa yule aliyeketi juu ya kiti cha enzi.
And he went, and now he has taken the book out of the right hand of Him who was seated on the throne.
8 Mara tu alipokwisha twaa hicho kitabu, vile viumbe hai vinne pamoja na wale wazee ishirini na wanne walianguka kifudifudi mbele ya Mwanakondoo. Kila mmoja, alikuwa na kinubi na bakuli za dhahabu zilizojaa ubani, ambao ni sala za watu wa Mungu.
When he took the book, the four Living Creatures and the four and twenty Elders fell down before the Lamb. And each had a harp and a golden bowls full of incense, which are the prayers of the saints.
9 Basi, wakaimba wimbo huu mpya: “Wewe unastahili kukitwaa hicho kitabu na kuivunja mihuri yake. Kwa sababu wewe umechinjwa, na kwa damu yako umemnunulia Mungu watu kutoka katika kila kabila, lugha, jamaa na taifa.
And they sang a new song, saying, "Worthy art thou to take the book And to open its seals; For thou wast slain and didst ransom for God Men out of every tribe and tongue and people and nation;
10 Wewe umewafanya wawe ufalme wa makuhani wamtumikie Mungu wetu nao watatawala duniani.”
Thou hast made them kings and priests unto our God, And they shall reign on earth."
11 Kisha nikatazama, nikasikia sauti ya malaika wengi sana, idadi isiyohesabika, maelfu na maelfu. Walikuwa wamekaa kuzunguka kiti cha enzi, vile viumbe hai vinne na wale wazee;
Then I looked and heard a voice of many angels encircling the throne and a voice of the Living Creatures and of the Elders; and the number of them was ten thousand times ten thousand, and thousands of thousands,
12 wakasema kwa sauti kuu: “Mwanakondoo aliyechinjwa anastahili kupokea uwezo, utajiri, hekima, nguvu, utukufu na sifa.”
singing aloud, "Worthy is the Lamb who has been slain, To receive power and riches and wisdom And might and honor and glory and blessing."
13 Nikasikia viumbe vyote mbinguni, duniani, chini kuzimuni na baharini—viumbe vyote ulimwenguni—vikisema: “Kwake yeye aketiye katika kiti cha enzi, na kwa Mwanakondoo, iwe sifa na heshima na utukufu na enzi milele na milele.” (aiōn , questioned)
And I heard every created thing that is in heaven, or on earth, or beneath the earth, or on the sea, and all things that are in them, saying, "To him who sits on the throne, And to the Lamb, Be the blessing and the honor, And the glory and the power, Forever and ever!" (aiōn )
14 Na vile viumbe vinne hai vikasema, “Amina!” Na wale wazee wakaanguka kifudifudi, wakaabudu.
And the four Living Creatures kept saying, "Amen!" And the Elders fell down and worshiped.