< Ufunuo 4 >

1 Baada ya hayo nilitazama nikaona mlango umefunguliwa mbinguni. Na ile sauti niliyoisikia pale awali ambayo ilikuwa kama sauti ya tarumbeta, ikasema, “Njoo hapa juu nami nitakuonyesha mambo yatakayotukia baadaye.”
After this I saw, and lo! an open door in heaven; and the former voice, which I heard as of a trumpet speaking with me, said, Come up hither, and I will show thee what things must take place after these.
2 Mara nikachukuliwa na Roho. Kumbe, huko mbinguni kuna kiti cha enzi na juu yake ameketi mmoja.
Immediately I was in the Spirit; and lo! a throne was set ha heaven, and one sat on the throne.
3 Huyo aliyeketi juu yake alikuwa kama almasi na jiwe zuri jekundu. Upinde wa mvua ulikuwa unang'aa kama zumaridi na ulikizunguka kiti cha enzi pande zote.
And he who sat was in appearance like a jasper stone and a sardius; and there was a rainbow around the throne like in appearance to an emerald.
4 Kulikuwa na duara la viti ishirini na vinne kukizunguka kiti cha enzi, na juu ya viti hivyo wazee ishirini na wanne walikuwa wameketi wamevaa mavazi meupe na taji za dhahabu vichwani.
And around the throne were twenty-four thrones; and upon the thrones I saw the twenty-four elders sitting, clothed in white garments, and on their heads crowns of gold.
5 Umeme, sauti na ngurumo, vilikuwa vinatoka kwenye hicho kiti cha enzi. Taa saba za moto zilikuwa zinawaka mbele ya hicho kiti cha enzi. Taa hizo ni roho saba za Mungu.
And out of the throne proceed lightnings, and voices and thunders; and there were seven lamps of fire burning before the throne, which are the seven spirits of God;
6 Mbele ya kiti cha enzi kulikuwa na kitu kama bahari ya kioo, angavu kama jiwe linga'aalo sana. Katika pande zote za hicho kiti cha enzi na kukizunguka, kilikuwa na viumbe hai vinne. Viumbe hivyo vilikuwa vimejaa macho mbele na nyuma.
and before the throne there was as it were a sea of glass like to crystal; and in the middle before the throne, and around the throne, were four living creatures full of eyes before and behind.
7 Kiumbe cha kwanza kulikuwa kama simba, cha pili kama ng'ombe, cha tatu kilikuwa na sura kama mtu, na cha nne kilikuwa kama tai anayeruka.
And the first living creature was like a lion, and the second living creature like a calf, and the third living creature had the face of a man, and the fourth living creature was like a flying eagle.
8 Viumbe hivyo vinne vilikuwa na mabawa sita kila kimoja, na vilikuwa vimejaa macho, ndani na nje. Usiku na mchana, bila kupumzika huimba: “Mtakatifu, mtakatifu, mtakatifu ni Bwana, Mungu Mwenye Uwezo, aliyekuwako, aliyeko na anayekuja!”
And the four living creatures, having each of them six wings, around and within are full of eyes; and they have no rest day and night, saying, Holy, holy, holy, Lord God Almighty, who was, and who is, and who is to come.
9 Kila mara viumbe vinne vilipoimba nyimbo za kumtukuza, kumheshimu na kumshukuru huyo aliyeketi juu ya kiti cha enzi, ambaye anaishi milele na milele, (aiōn g165)
And when the living creatures give glory, and honor, and thanksgiving to him that sitteth on the throne, who liveth for ever and ever, (aiōn g165)
10 wale wazee ishirini na wanne hujiangusha mbele ya huyo aliyeketi juu ya kiti cha enzi na kumwabudu huyo ambaye anaishi milele na milele; na huziweka taji zao mbele ya kiti cha enzi wakisema: (aiōn g165)
the twenty-four elders fall down before him that sitteth on the throne, and worship him that liveth for ever and ever, and cast their crowns before the throne, saying, (aiōn g165)
11 “Wewe ni Bwana na Mungu wetu, unastahili utukufu na heshima na nguvu; maana wewe uliumba vitu vyote, na kwa matakwa yako kila kitu kimepewa uhai na uzima.”
Worthy art thou, O Lord, and our God, to receive the glory, and the honor, and the power; for thou didst create all things, and on account of thy will they were, and were created.

< Ufunuo 4 >