< Ufunuo 3 >
1 “Kwa malaika wa kanisa la Sarde andika hivi: “Huu ndio ujumbe kutoka kwake yeye aliye na roho saba za Mungu na nyota saba. Nayajua mambo yako yote; najua unajulikana kuwa na uhai kumbe umekufa!
你給撒爾德教會的天使寫:「那持有天主的七神和七顆星的這樣說:我知道你的作為,也知道你有生活之名,其實你是死的。
2 Amka! Imarisha chochote chema kilichokubakia kabla nacho hakijatoweka kabisa. Maana, mpaka sasa, sijayaona matendo yako kuwa ni makamilifu mbele ya Mungu wangu.
你該儆醒,堅固其餘將要死的人,因為我沒有發見你的作為,在我天主面前是齊全的,
3 Kumbuka, basi, yale uliyofundishwa na jinsi ulivyoyasikia, uyatii na ubadili nia yako mbaya. Usipokesha nitakujia ghafla kama mwizi, na wala hutaijua saa nitakapokujia.
所以你應回想當初你是怎樣接受了,是怎樣聽了天主的道:你該遵守,又該悔改;假如你不儆醒,我必要像盜賊一樣來臨,你也不知道我何時臨於你。
4 Lakini wako wachache huko Sarde ambao hawakuyachafua mavazi yao. Hao wanastahili kutembea pamoja nami wakiwa wamevaa mavazi meupe.
可是,在撒爾德你還有幾個沒有玷污自己的衣服,他們必要穿上白衣,與我同行,因為他們當得起。
5 “Wale wanaoshinda, watavikwa mavazi meupe kama hao. Nami sitayafuta majina yao kutoka katika kitabu cha uzima; tena nitawakiri kwamba ni wangu mbele ya Baba yangu na mbele ya malaika wake.
勝利的必要這樣穿上白衣,我決不將他的名字從生命冊上抹去;反之,我要在我父面前,在他的天使面前,承認他的名字。
6 “Aliye na masikio, basi, na ayasikie yale Roho anayoyaambia makanisa!
有耳朵的,應聽聖神向各教會說的話。」
7 “Kwa malaika wa kanisa la Filadelfia andika hivi: “Huu ndio ujumbe kutoka kwake yeye aliye mtakatifu na wa kweli, ambaye anao ule ufunguo wa Daudi, na ambaye hufungua na hakuna mtu awezaye kufungua.
你給非拉德非雅教會的天使寫:「那聖潔而真實的,掌有達味鑰匙的,開了不無人能關,關了無人能開的這樣說:
8 Nayajua mambo yako yote! Sasa, nimefungua mbele yako mlango ambao hakuna mtu awezaye kuufunga; najua kwamba ingawa huna nguvu sana, hata hivyo, umezishika amri zangu, umelitii neno langu wala hukulikana jina langu.
我知道你的作為;看,我在你面前安置了一個敞開的門,誰也不能關閉它;我知道你能力雖小,卻遵守了我的話,沒有否認我的名字。
9 Sikiliza! Nitawapeleka kwako watu wa kundi lake Shetani, watu ambao hujisema kuwa ni Wayahudi, kumbe ni wadanganyifu. Naam, nitawapeleka kwako na kuwafanya wapige magoti mbele yako wapate kujua kwamba kweli nakupenda wewe.
看,我要從撒殫的會眾,即從那些自稱為猶太人的人中--其實不是,而只是撒謊的人--把一些人交給你;看,我要使他們前來,俯伏在你腳前,使他們承認我愛了你。
10 Kwa kuwa wewe umezingatia agizo langu la kuwa na uvumilivu, nami pia nitakutegemeza salama wakati ule wa dhiki inayoujia ulimwengu mzima kuwajaribu wote wanaoishi duniani.
因為你遵守了我論堅忍的訓言,我也要在試探期中保存你,這時期將要臨於這世界,為試探這世界上的居民。
11 Naja kwako upesi! Linda, basi, ulicho nacho sasa, ili usije ukanyang'anywa na mtu yeyote taji yako ya ushindi.
我快要來;你應堅持你所有的,免得人拿去你的花冠。
12 “Wale wanaoshinda nitawafanya wawe minara katika Hekalu la Mungu wangu, na hawatatoka humo kamwe. Pia nitaandika juu yao jina la Mungu wangu na jina la mji wa Mungu wangu, yaani Yerusalemu mpya, mji ambao utashuka kutoka juu mbinguni kwa Mungu wangu. Tena nitaandika juu yao jina langu jipya.
勝利的,我要使他成為我天主殿宇的柱子,決不再讓他到外面去;我還要把我天主的名號,和從天上我天主那裏降下的我天主的城邑,即新耶路撒冷的名號,以及我的新名號,寫在他身上。
13 “Aliye na masikio, basi, na ayasikie yale Roho anayoyaambia makanisa!
有耳朵的,應聽聖神向各教會說的話。」
14 “Kwa malaika wa kanisa la Laodikea andika hivi: “Huu ndio ujumbe kutoka kwake yeye aitwaye Amina. Yeye ni shahidi mwaminifu na wa kweli, ambaye ni chanzo cha viumbe vyote alivyoumba Mungu.
你給勞狄刻雅教會的天使寫:「那做『阿們,』做忠信而真實見證的,做天主創造萬物根源的這樣說:
15 Nayajua mambo yako yote! Najua kwamba wewe si baridi wala si moto. Afadhali ungekuwa kimojawapo: baridi au moto.
我知道你的作為:你也不冷,也不熱;巴不得你或冷或熱!
16 Basi, kwa kuwa hali yako ni vuguvugu, si baridi wala si moto, nitakutapika!
但是,你既然是溫的,也不冷,也不熱,我必要從我口中把你吐出來。
17 Wewe unajisema, Mimi ni tajiri; ninajitosheleza, sina haja ya kitu chochote. Kumbe, hujui kwamba wewe ni mnyonge, unahitaji kuhurumiwa, maskini, kipofu tena uko uchi!
你說:我是富有的,我發了財,什麼也不缺少;殊不知你是不幸的,可憐的,貧窮的,瞎眼的,赤身裸體的。
18 Nakushauri ununue kwangu dhahabu iliyosafishwa kwa moto upate kuwa tajiri kweli. Tena afadhali ununue pia vazi jeupe, uvae na kufunika aibu ya uchi wako. Nunua pia mafuta ukapake machoni pako upate kuona.
我給你出個主意:你要向我買用火煉好的黃金,為使你富有,也買件白衣穿上,為不顯露你裸體的羞恥,又買點眼藥,抹在你的眼上,為使你能看見。
19 Mimi ndiye mwenye kumwonya na kumrudi yeyote ninayempenda. Kwa hiyo kaza moyo, achana na dhambi zako.
凡我所疼愛的人,我要譴責他,管教他;所以你應當發奮熱心,痛悔改過!
20 Sikiliza! Mimi nasimama mlangoni na kubisha hodi. Mtu akisikia sauti yangu na kufungua mlango, nitaingia nyumbani kwake na kula chakula pamoja naye, naye atakula pamoja nami.
看,我立在門口敲門,誰若聽見我的聲音而給我開門,我要進到他那裏,同他坐席,他也要同我一起坐席。
21 “Wale wanaoshinda nitawaketisha pamoja nami juu ya kiti changu cha enzi, kama vile mimi mwenyewe nilivyoshinda nikaketi pamoja na Baba yangu juu ya kiti chake cha enzi.
勝利的,我要賜他同我坐在我的寶座上,就如我得勝了,同我的父坐在他的寶座上一樣。
22 “Aliye na masikio, basi, na ayasikie yale Roho anayoyaambia makanisa!”
有耳朵的,應聽聖神向各教會說的話。」