< Ufunuo 22 +
1 Kisha malaika akanionyesha mto wa maji ya uzima maangavu kama kioo yakitoka kwenye kiti cha enzi cha Mungu na Mwanakondoo.
And he shewed me a pure river of the water of life, clear as crystal, proceeding out of the throne of God, and of the Lamb.
2 Mto huo ulitiririka kupitia katikati ya barabara kuu ya mji. Kandokando ya mto huo kulikuwa na mti wa uzima unaozaa matunda mara kumi na mbili kwa mwaka, yaani kila mwezi; na majani yake ni dawa ya kuwaponya watu wa mataifa.
And in the midst of the street, and of the river, which ran on each side, was the tree of life, producing fruits twelve times in the year, yielding its different fruit every month. And the leaves of the tree are for the healing of the nations.
3 Hapana kitu chochote kilicholaaniwa kitakachokuwa katika mji huo. Kiti cha enzi cha Mungu na cha Mwanakondoo kitakuwa katika mji huo, na watumishi wake watamwabudu.
And every curse shall cease: and the throne of God and of the Lamb shall be in it, and his servants shall serve Him.
4 Watauona uso wake, na jina lake litaandikwa juu ya paji za nyuso zao.
And they shall see his face; and his name shall be on their foreheads.
5 Usiku hautakuwako tena, wala hawatahitaji mwanga wa taa au wa jua, maana Bwana Mungu atawaangazia, nao watatawala milele na milele. (aiōn )
And there shall be no night there: and they have no need of a candle, nor of the light of the sun; for the Lord God giveth them light; and they shall reign for ever and ever. (aiōn )
6 Kisha malaika akaniambia, “Maneno haya ni ya kweli na ya kuaminika. Bwana Mungu ambaye huwapa manabii Roho wake, alimtuma malaika wake awaonyeshe watumishi wake mambo ambayo lazima yatukie punde.
And he said unto me, These words are faithful and true: and the Lord God of the holy prophets hath sent his angel to shew unto his servants what must soon be.
7 “Sikiliza! Naja upesi. Heri yake anayeyazingatia maneno ya unabii yaliyo katika kitabu hiki.”
For behold I come quickly: happy is he that keepeth the words of the prophecy of this book.
8 Mimi Yohane, niliyaona na kusikia mambo haya. Nilipokwisha sikia na kuona nikajitupa chini mbele ya miguu ya huyo malaika aliyenionyesha mambo hayo, nikataka kumwabudu.
And I John am he who saw and heard these things: and when I had heard and seen them, I fell down to worship before the feet of the angel, who shewed me these things.
9 Lakini yeye akaniambia, “Acha! Mimi ni mtumishi tu kama wewe na ndugu zako manabii na wote wanaoyatii maagizo yaliyomo katika kitabu hiki. Mwabudu Mungu!”
And he said unto me, See thou do it not: for I am a fellow-servant of thine, and of thy brethren the prophets, and of those who observe the words of this book: worship God.
10 Tena akaniambia, “Usiyafiche kama siri maneno ya unabii yaliyomo katika kitabu hiki, maana wakati wa kutimizwa kwake umekaribia.
And he said unto me, Seal not the words of the prophecy of this book; for the time is near.
11 Kwa sasa anayetenda mabaya na aendelee kutenda mabaya, na aliye mchafu aendelee kuwa mchafu. Mwenye kutenda mema na azidi kutenda mema, na aliye mtakatifu na azidi kuwa mtakatifu.”
Let him, that is unjust, be unjust still: and let him, that is filthy, be filthy still: and let him, that is righteous, be righteous still; and let him, that is holy, be holy still.
12 “Sikiliza!” Asema Yesu, “Naja upesi, pamoja na tuzo nitakalompa kila mmoja kufuatana na matendo yake.
And behold, I come quickly; and my reward is with me, to recompense every one according to his work.
13 Mimi ni Alfa na Omega, Mwanzo na Mwisho, wa kwanza na wa mwisho.”
I am the Alpha and the Omega, the beginning and the end, the first and the last.
14 Heri yao wale wanaoosha mavazi yao, kwani watakuwa na haki ya kula tunda la mti wa uzima, na haki ya kuingia mjini kwa kupitia milango yake.
Happy are they that do his commandments, so shall they have a right to the tree of life, and may enter in by the gates into the city.
15 Lakini mbwa, wachawi, wazinzi, wauaji, waabudu sanamu na wote wanaopenda kusema uongo, watakaa nje ya mji.
But without are dogs, and sorcerers, and whoremongers, and murderers, and idolaters, and every one that loveth and practiseth falshood.
16 “Mimi, Yesu, nimemtuma malaika wangu awathibitishieni mambo haya katika makanisa. Mimi ni mzawa wa ukoo wa Daudi. Mimi ni nyota angavu ya asubuhi!”
I Jesus have sent my messenger to testify unto you these things in the churches. I am both the root and the offspring of David, the bright and morning star.
17 Roho na Bibiarusi waseme, “Njoo!” Kila mtu asikiaye hili, na aseme, “Njoo!” Kisha, yeyote aliye na kiu na aje; anayetaka maji ya uzima na apokee bila malipo yoyote.
And the Spirit and the bride say, Come; and let him that heareth say, Come. And let him, that thirsteth, Come. And let him, that desireth it, take the water of life freely.
18 Mimi Yohane nawapa onyo wote wanaosikia maneno ya unabii yaliyomo katika kitabu hiki: mtu yeyote akiongeza chochote katika mambo haya, Mungu atamwongezea mabaa yaliyoandikwa katika kitabu hiki.
I testify to every one that heareth the words of the prophecy of this book, If any one add to these things, God shall add unto him the plagues that are written in this book:
19 Na mtu yeyote akipunguza chochote katika maneno ya unabii yaliyomo katika kitabu hiki, Mungu atamnyang'anya sehemu yake katika ule mti wa uzima, na sehemu yake katika mji mtakatifu, ambavyo vimeelezwa katika kitabu hiki.
and if any one take away from the words of the book of this prophecy, God will take away his part from the book of life, and out of the holy city, and from the things that are written in this book.
20 Naye anayetoa ushahidi wake juu ya mambo haya asema: “Naam! Naja upesi.” Amina. Na iwe hivyo! Njoo Bwana Yesu!
He who testifieth these things saith, I surely come quickly. Amen, even so come, Lord Jesus.
21 Nawatakieni nyote neema ya Bwana Yesu. Amen.
The grace of our Lord Jesus Christ be with you all. Amen.