< Ufunuo 22 +
1 Kisha malaika akanionyesha mto wa maji ya uzima maangavu kama kioo yakitoka kwenye kiti cha enzi cha Mungu na Mwanakondoo.
The angel showed me the river of water [that causes people who drink from it] to live [forever]. The water was sparkling and clear like crystal. The river was flowing out from the throne where God and the [one who is like a] lamb [were sitting].
2 Mto huo ulitiririka kupitia katikati ya barabara kuu ya mji. Kandokando ya mto huo kulikuwa na mti wa uzima unaozaa matunda mara kumi na mbili kwa mwaka, yaani kila mwezi; na majani yake ni dawa ya kuwaponya watu wa mataifa.
It flowed down through the middle of the [main] street of the city. On each side of the river were trees [bearing fruit that causes people who eat it] to live forever. [The trees] bear twelve [crops] (OR, twelve [kinds]) of fruit; [they] produce one crop each month. The [people of the] nations [MTY] [use] the leaves of these trees [as medicine] in order that they may feel stronger
3 Hapana kitu chochote kilicholaaniwa kitakachokuwa katika mji huo. Kiti cha enzi cha Mungu na cha Mwanakondoo kitakuwa katika mji huo, na watumishi wake watamwabudu.
There will never be [anyone or anything there that God] will be [under God’s] curse. The throne of God and the [one who is like a] lamb will be in the city. And God’s servants will worship him there.
4 Watauona uso wake, na jina lake litaandikwa juu ya paji za nyuso zao.
They will see him face-to-face, and his name will be [written] {[he] will [write] his name} on their foreheads.
5 Usiku hautakuwako tena, wala hawatahitaji mwanga wa taa au wa jua, maana Bwana Mungu atawaangazia, nao watatawala milele na milele. (aiōn )
There will never again be night. [God’s servants] will not need the light of a lamp or the light of the sun, because the Lord God will shine his light upon them. And they will rule forever. (aiōn )
6 Kisha malaika akaniambia, “Maneno haya ni ya kweli na ya kuaminika. Bwana Mungu ambaye huwapa manabii Roho wake, alimtuma malaika wake awaonyeshe watumishi wake mambo ambayo lazima yatukie punde.
The angel said to me: “These words that [God has revealed to you] are true, and he will certainly do what he has promised to do. The Lord God who ([inspires] the prophets/tells the prophets what to say) sent his angel to show the people who serve him the events that must happen soon.”
7 “Sikiliza! Naja upesi. Heri yake anayeyazingatia maneno ya unabii yaliyo katika kitabu hiki.”
[Jesus says to all his people], “Listen [to] this! I am coming soon; [God will abundantly] bless everyone who obeys what [has been commanded] in this book.”
8 Mimi Yohane, niliyaona na kusikia mambo haya. Nilipokwisha sikia na kuona nikajitupa chini mbele ya miguu ya huyo malaika aliyenionyesha mambo hayo, nikataka kumwabudu.
I, John, am the one who heard and saw [in a vision] these things [that I have written down]. When I had heard and seen [them], I immediately knelt down at the feet of the angel who was showing them to me, in order to worship him.
9 Lakini yeye akaniambia, “Acha! Mimi ni mtumishi tu kama wewe na ndugu zako manabii na wote wanaoyatii maagizo yaliyomo katika kitabu hiki. Mwabudu Mungu!”
But he said to me, “Do not [worship me] I am [just] your fellow servant! I am also the fellow servant of your fellow believers who are (the prophets/the ones who tell messages that come directly from God), and I am a fellow servant of those who obey what has been commanded in this book. [Instead], worship God!”
10 Tena akaniambia, “Usiyafiche kama siri maneno ya unabii yaliyomo katika kitabu hiki, maana wakati wa kutimizwa kwake umekaribia.
He also said to me, “Do not keep secret the message about what [God] has foretold in this book, because it is almost time [MTY] for him to [what he has promised to do in this message].
11 Kwa sasa anayetenda mabaya na aendelee kutenda mabaya, na aliye mchafu aendelee kuwa mchafu. Mwenye kutenda mema na azidi kutenda mema, na aliye mtakatifu na azidi kuwa mtakatifu.”
[Since that time is near, if] those who act in an evil manner [want to] continue to act that way [IRO], [that is up to them. God will soon] ([pay them back/punish them]) [for that. If] those who are vile [want to] continue to be vile [IRO], [that is up to them. God will soon] ([pay them back/punish them]) [for that]. Those who are [acting] righteously should continue to act righteously. And those who are holy should continue to be holy.”
12 “Sikiliza!” Asema Yesu, “Naja upesi, pamoja na tuzo nitakalompa kila mmoja kufuatana na matendo yake.
[Jesus says this to everyone]: “Listen! I am coming soon! And I will pay back everyone according to what each one has done, by [punishing or] rewarding them.
13 Mimi ni Alfa na Omega, Mwanzo na Mwisho, wa kwanza na wa mwisho.”
I [am] the one who began all things [MET] and the one who will cause all things to end [MET]. I existed before [all things existed] and I will exist at the end [of all things] [DOU].
14 Heri yao wale wanaoosha mavazi yao, kwani watakuwa na haki ya kula tunda la mti wa uzima, na haki ya kuingia mjini kwa kupitia milango yake.
[God] is very pleased with the people who wash their robes, [making themselves spiritually clean] [MET], because they will be able to [eat the fruit of] [MTY] the tree [that enables people] to live [forever], and because they will [be able] to enter the gates into the [holy] city.
15 Lakini mbwa, wachawi, wazinzi, wauaji, waabudu sanamu na wote wanaopenda kusema uongo, watakaa nje ya mji.
[People who are unholy] will not be allowed to enter the city. They include people who practice sorcery, people who sin sexually, murderers, idol worshipers, and everyone who enjoys telling lies and are continual liars. [They can never enter that city].”
16 “Mimi, Yesu, nimemtuma malaika wangu awathibitishieni mambo haya katika makanisa. Mimi ni mzawa wa ukoo wa Daudi. Mimi ni nyota angavu ya asubuhi!”
“I, Jesus, sent my angel in order that he might tell you who are in the congregations [that all] these things [that have been said are true]. I am the descendant of [King] David [whom the prophets promised would come] [MET]. I am the [one who is like] the bright morning star [MET], the one [that Moses promised would come].”
17 Roho na Bibiarusi waseme, “Njoo!” Kila mtu asikiaye hili, na aseme, “Njoo!” Kisha, yeyote aliye na kiu na aje; anayetaka maji ya uzima na apokee bila malipo yoyote.
[God’s] Spirit and [his people, who are like] [MET] the bride [of Christ], say [to each one who desires to believe], “Come!” Whoever hears [this] should also say [to each one who desires to believe], “Come!” [Spiritually thirsty people should come] [MET]! Everyone who desires the water [that enables people to] live [forever] should take it as a free gift!
18 Mimi Yohane nawapa onyo wote wanaosikia maneno ya unabii yaliyomo katika kitabu hiki: mtu yeyote akiongeza chochote katika mambo haya, Mungu atamwongezea mabaa yaliyoandikwa katika kitabu hiki.
“I, [Jesus, solemnly] warn everyone who hears what [I] have foretold in this book: If anyone adds anything to this message, God will cause him to experience the plagues that are {that [I] have} described in this book.
19 Na mtu yeyote akipunguza chochote katika maneno ya unabii yaliyomo katika kitabu hiki, Mungu atamnyang'anya sehemu yake katika ule mti wa uzima, na sehemu yake katika mji mtakatifu, ambavyo vimeelezwa katika kitabu hiki.
If anyone omits any of the message about what [I] have foretold in this book, God will take away that person’s right [to eat fruit from] [MTY] the tree [that enables people] to live [forever]. He [will also take away] that person’s right [to enter] God’s city. [Both these things] are described {[I] have described [both these things]} in this book.”
20 Naye anayetoa ushahidi wake juu ya mambo haya asema: “Naam! Naja upesi.” Amina. Na iwe hivyo! Njoo Bwana Yesu!
[Jesus], who says that [all] the things written here are true, says, “Certainly I am coming soon!” [I, John, reply], “(May it be so!/Amen!) Lord Jesus, come!”
21 Nawatakieni nyote neema ya Bwana Yesu. Amen.
[I pray that our] Lord Jesus [will continue to] act kindly to all [of you who are God’s people]. (Amen!/May it be so!)