< Ufunuo 21 >

1 Kisha nikaona mbingu mpya na dunia mpya. Mbingu ile ya kwanza na dunia ile ya kwanza vilikuwa vimetoweka, nayo bahari pia haikuweko tena.
And I sawe a newe heven and a newe erth For the fyrst heven and the fyrst erth were vanysshed awaye and there was no more see.
2 Nikaona mji mtakatifu, Yerusalemu mpya, ukishuka kutoka kwa Mungu mbinguni. Ulikuwa umetayarishwa vizuri kama bibi arusi aliyepambwa tayari kukutana na mumewe.
And I Iho sawe that holy cite newe Ierusalem come doune from God oute of heven prepared as a bryde garnysshed for hyr husband.
3 Kisha nikasikia sauti kubwa kutoka katika kiti cha enzi ikisema, “Tazama! Mungu amefanya makao yake kati ya watu. Atakaa kati yao, nao watakuwa watu wake, naye atakuwa Mungu wao.
And I herde a grett voyce out of heaven sayinge: beholde the tabernacle of God is with men and he will dwell with the And they shalbe his people and God him sylffe shalbe with the and be their god.
4 Yeye atayafuta machozi yao yote; maana hakutakuwako tena na kifo, wala uchungu, wala kilio, wala maumivu; maana ile hali ya kale imepita!”
And God shall wype awaye all teares fro their eyes. And there shalbe nomore deeth nether sorowe nether cryinge nether shall there be eny more payne for the olde thynges are gone.
5 Kisha yule aliyeketi juu ya kiti cha enzi akasema, “Tazama, nafanya yote mapya.” Tena akaniambia, “Andika hili, maana maneno haya ni ya kuaminika na ya kweli!”
And he that sate apon the seate sayde: Behold I make all thynges newe. And he sayde vnto me: wryte for these wordes are faythfull and true.
6 Kisha akaniambia, “Yametimia! Mimi ni Alfa na Omega, Mwanzo na Mwisho. Aliye na kiu nitampa kinywaji cha bure kutoka katika chemchemi ya maji ya uzima.
And he sayde vnto me: it is done I am Alpha and Omega the begynnynge and the ende. I will geve to him yt is a thyrst of the well of the water of lyfe fre.
7 Yeyote atakayeshinda atapokea hiki, nami nitakuwa Mungu wake, naye atakuwa mwanangu.
He that overcometh shall inheret all thynges and I will be his God and he shalbe my sonne.
8 Lakini watu waoga, wasioamini, wapotovu, wauaji, wazinzi, wachawi, waabudu sanamu, na waongo wote, mahali pao patakuwa ndani ya lile ziwa linalowaka moto na kiberiti; hicho ndicho kifo cha pili.” (Limnē Pyr g3041 g4442)
But the fearefull and vnbelevynge and the abhominable and murdrers and whormongers and sorcerers and ydolaters and all lyars shall have their parte in the lake which burnyth with fyre and brymstone which is the seconde deth. (Limnē Pyr g3041 g4442)
9 Kisha mmoja wa wale malaika saba waliokuwa na yale mabakuli saba yaliyokuwa yamejaa mabaa saba ya mwisho, akaja na kuniambia, “Njoo! Mimi nitakuonyesha bibi arusi, mkewe Mwanakondoo!”
And there cam vnto me one of the vii. angels which had the vii. vyals full of the vii. laste plages: and talked with me sayinge: come hydder I will shewe the the bryde the lambes wyfe.
10 Basi, Roho akanikumba, naye malaika akanipeleka juu ya mlima mrefu sana. Akanionyesha mji mtakatifu, ukishuka kutoka kwa Mungu mbinguni,
And he caryed me awaye in the sprete to a grett and an hye mountayne and he shewed me the grett cite holy Ierusalem descendinge out of heven fro God
11 uking'aa kwa utukufu wa Mungu. Mwangaza wake ulikuwa kama wa jiwe la thamani kubwa kama yaspi, angavu kama kioo.
havynge the brightnes of God. And her shynynge was lyke vnto a stone moste precious even a Iaspar cleare as cristall:
12 Ulikuwa na ukuta mrefu na mkubwa, wenye milango kumi na miwili, na malaika wanangojea kumi na wawili. Majina ya wangoja milango kumi na mawili ya Israeli yalikuwa yameandikwa juu ya milango hiyo.
and had walles grett and hye and had xii gates and at the gates xii. angels: and names written which are the xii. trybes of Israell:
13 Kila upande ulikuwa na milango mitatu: upande wa mashariki, milango mitatu, kaskazini milango mitatu, kusini milango mitatu na magharibi milango mitatu.
on the est parte iii gatis and on the north syde iii gates and to wardes the south iii gates and from the west iii gates:
14 Kuta za mji huo zilikuwa zimejengwa juu ya mawe ya msingi kumi na mawili, na juu ya mawe hayo yalikuwa yameandikwa majina na mitume kumi na wawili wa Mwanakondoo.
and the wall of the cite had xii foundacions and in them the names of the lambes. xii. Apostles.
15 Basi, yule malaika aliyekuwa anasema nami alikuwa na kijiti cha dhahabu cha kupimia, kwa ajili ya kuupima huo mji, milango yake na kuta zake.
And he that talked with me had a golden read to measure the cite with all and the gates therof and the wall therof.
16 Mji wenyewe ulikuwa wa mraba, upana na urefu wake sawa. Basi, malaika akaupima mji huo kwa kijiti chake: ulikuwa na urefu, upana na urefu wa kwenda juu, kama kilomita elfu mbili na mia nne.
And the cite was bylt iiii. square and the length was as large as the bredth of it and he measured the cite with the rede. xii M. fur longes: and the lenght and the bredth and ye heyth of it were equall.
17 Kisha akaupima ukuta wake pia; nao ulikuwa mita sitini kwa kipimo cha macho cha kibinadamu ambacho malaika alitumia.
And he measured the wall therof. an cxliiii. cubittes: the measure that ye angell had was after the measure that man vseth.
18 Ukuta huo ulikuwa umejengwa kwa mawe mekundu ya thamani, na mji wenyewe ulikuwa umejengwa kwa dhahabu safi, angavu kama kioo.
And the byldinge of the wall of it was of iaspar. And the cite was pure gold lyke vnto cleare glasse
19 Mawe ya msingi wa ukuta huo yalikuwa yamepambwa kwa kila aina ya mawe ya thamani. Jiwe la kwanza la msingi lilikuwa jiwe la thamani jekundu, la pili yakuti samawati, la tatu kalkedoni, la nne zamaradi,
and the foundacions of the wall of ye cite was garnisshed with all maner of precious stones The fyrste foundacion was iaspar the seconde saphyre the thyrde a calcedony the fourth an emeralde:
20 la tano sardoniki, la sita akiki, la saba krisolito, la nane zabarijadi, la tisa topazi, la kumi krisopraso, la kumi na moja yasinto, na la kumi na mbili amethisto.
the fyft sardonix: the sixt sardeos: the seventh crysolite the ayght berall: the nynth a topas: the tenth a crysoprasos: the eleventh a iacyncte: the twelfe an amatist.
21 Na ile milango kumi na miwili ilikuwa lulu kumi na mbili; kila mlango ulikuwa umetengenezwa kwa lulu moja. Barabara kuu ya mji ilikuwa imetengenezwa kwa dhahabu safi, angavu kama kioo.
The xii. gates were xii pearles every gate was of one pearle and the strete of the cite was pure golde as thorowe shynynge glasse.
22 Sikuona hekalu katika mji huo, maana Bwana Mungu Mwenye Uwezo na yule Mwanakondoo ndio Hekalu lake.
And there was no temple therin. For the lord god allmyghty and the lambe are the temple of it
23 Mji huo hauhitaji jua wala mwezi kuangazia, maana utukufu wa Mungu huuangazia, na taa yake ni yule Mwanakondoo.
and the cite hath no nede of the sonne nether of the mone to lyghten it. For the bryghtnes of God dyd light it: and the lambe was the light of it.
24 Watu wa mataifa watatembea katika mwanga wake, na wafalme wa dunia watauletea utajiri wao.
And the people which are saved shall walke in the light of it: and the kynges of the erth shall brynge their glory vnto it.
25 Milango ya mji huo itakuwa wazi mchana wote; maana hakutakuwa na usiku humo.
And ye gates of it are not shut by daye. For there shalbe no nyght there.
26 Fahari na utajiri wa watu wa mataifa utaletwa humo ndani.
27 Lakini hakuna chochote kilicho najisi kitakachoingia humo; wala mtu yeyote atendaye mambo ya kuchukiza au ya uongo hataingia humo. Ni wale tu walioandikwa katika kitabu cha uzima cha Mwanakondoo ndio watakaoingia ndani.
And there shall entre into it none vnclene thynge: nether what soever worketh abhominacion: or maketh lyes: but they only which are wrytten in the lambes boke of lyfe.

< Ufunuo 21 >