< Ufunuo 2 >
1 “Kwa malaika wa kanisa la Efeso andika hivi: “Huu ndio ujumbe kutoka kwake yeye ashikaye nyota saba katika mkono wake wa kulia, na ambaye hutembea katikati ya vinara saba vya taa vya dhahabu.
»Angelu cerkve v Efezu piši: ›Te stvari govori on, ki v svoji desnici drži sedem zvezd, ki hodi v sredi sedmih zlatih svečnikov;
2 Najua mambo yako yote; najua bidii yako na uvumilivu wako. Najua kwamba huwezi kuwavumilia watu waovu, na kwamba umewapima wale wanaojisemea kuwa mitume na kumbe sio, ukagundua kwamba ni waongo.
poznam tvoja dela in tvoj trud in tvojo potrpežljivost in kako ne moreš prenašati teh, ki so hudobni in preizkusil si tiste, ki pravijo, da so apostoli, pa to niso in si jih našel lažnivce.
3 Wewe unayo saburi, umestahimili taabu nyingi kwa ajili ya jina langu, wala hukuvunjika moyo.
In prenašal si in imaš potrpežljivost in si se trudil zaradi mojega imena in nisi izgubil poguma.
4 Lakini ninayo hoja moja juu yako: wewe hunipendi tena sasa kama pale awali.
Vendar imam nekaj proti tebi, kajti zapustil si svojo prvo ljubezen.
5 Basi, pakumbuke pale ulipokuwa kabla ya kuanguka, ukayaache madhambi yako, na kufanya kama ulivyofanya pale awali. La sivyo, naja kwako na kukiondoa kinara chako mahali pake.
Spomni se torej, od kod si padel in se pokesaj in opravljaj prva dela, sicer bom hitro prišel k tebi in bom odstranil tvoj svečnik z njegovega mesta, razen če se ne pokesaš.
6 Lakini nakusifu juu ya kitu kimoja: wewe unayachukia wanayoyatenda Wanikolai kama ninavyoyachukia mimi.
Toda to imaš, da sovražiš dejanja nikolajevcev, ki jih tudi sam sovražim.‹
7 “Aliye na masikio, basi, na asikie yale Roho anayoyaambia makanisa! “Wale wanaoshinda nitawapa haki ya kula matunda ya mti wa uzima ulioko ndani ya bustani ya Mungu.
Kdor ima uho, naj sliši, kaj Duh govori cerkvam: ›Tistemu, ki premaga, bom dal jesti od drevesa življenja, ki je na sredini Božjega raja.‹«
8 “Kwa malaika wa kanisa la Smurna andika hivi: “Huu ndio ujumbe kutoka kwake yeye wa kwanza na wa mwisho, ambaye alikufa na akaishi tena.
»In angelu cerkve v Smirni piši: ›Te stvari govori prvi in zadnji, ki je bil mrtev in je živ;
9 Najua taabu zako; najua pia umaskini wako, ingawaje kwa kweli wewe ni tajiri; najua kashfa walizokufanyia wale wanaojiita Wayahudi lakini si Wayahudi wa kweli, bali ni kundi lake Shetani.
poznam tvoja dela in stisko in revščino (toda bogat si) in poznam bogokletje teh, ki pravijo, da so Judje, pa niso, temveč so Satanova sinagoga.
10 Usiogope hata kidogo yale ambayo itakulazimu kuteseka. Sikiliza! Ibilisi anataka kuwajaribu kwa kuwatia baadhi yenu gerezani; nanyi mtapata dhiki kwa muda wa siku kumi. Muwe waaminifu hata mpaka kufa, nami nitawapeni taji ya uzima.
Ne boj se nobene od teh stvari, ki jih boš pretrpel. Glej, hudič bo nekatere izmed vas vrgel v ječo, da boste lahko preizkušeni in deset dni boste imeli stisko. Bodi zvest do smrti in dal ti bom krono življenja.‹
11 “Aliye na masikio, basi, na asikie yale Roho anayoyaambia makanisa! “Wale wanaoshinda hawataumizwa na kifo cha pili.
Kdor ima uho, naj sliši, kaj Duh govori cerkvam: ›Kdor premaga, ne bo poškodovan od druge smrti.‹«
12 “Kwa malaika wa kanisa la Pergamoni andika hivi: “Huu ndio ujumbe wake yeye aliye na upanga mkali wenye kuwili.
»In angelu cerkve v Pêrgamonu piši: ›Te besede govori on, ki ima oster meč z dvema ostrinama;
13 Najua unakoishi: Wewe unaishi kwenye makao makuu ya Shetani! Lakini bado unashikilia jina langu; hukuikana imani yako kwangu hata siku zile Antipa shahidi wangu mwaminifu, alipouawa pale mahali anapoishi Shetani.
poznam tvoja dela in kje prebivaš, celó kjer je Satanov prestol. In trdno držiš moje ime in moje vere nisi zanikal celó v tistih dneh, v katerih je bil Antípa, moj zvesti mučenec, ki je bil umorjen med vami, kjer prebiva Satan.
14 Lakini ninayo machache dhidi yako: baadhi yenu ni wafuasi wa Balaamu aliyemfundisha Balaki kuwatega wana wa Israeli wale vyakula vilivyotambikiwa sanamu za kufanya uzinzi.
Toda zoper tebe imam nekaj stvari, ker imaš tam tiste, ki se drže Bileámovega nauka, ki je učil Baláka metati kamen spotike pred Izraelove otroke, da jedo stvari žrtvovane malikom in da zagrešijo prešuštvo.
15 Vivyo hivyo, wako pia miongoni mwenu watu wanaofuata mafundisho ya Wanikolai.
Tako imaš tudi tiste, ki se držijo nauka nikolajevcev, katerih besedo sovražim.
16 Basi, achana na madhambi yako. La sivyo, nitakuja kwako upesi na kupigana na watu hao kwa upanga utokao kinywani mwangu.
Pokesaj se, sicer bom hitro prišel k tebi in proti njim se bom boril z mečem svojih ust.‹
17 “Aliye na masikio, basi, na asikie yale Roho anayoyaambia makanisa! “Wale wanaoshinda nitawapa ile mana iliyofichika. Nitawapa pia jiwe jeupe lililoandikwa jina jipya ambalo hakuna mtu aliyelijua isipokuwa tu wale wanaolipokea.
Kdor ima uho, naj sliši, kaj Duh govori cerkvam: ›Tistemu, ki premaga, bom dal jesti od skrite mane in dal mu bom bel kamen in na kamnu napisano novo ime, ki ga ne pozna noben človek, razen, kdor ga prejme.‹«
18 “Kwa malaika wa kanisa la Thuatira andika hivi: “Huu ndio ujumbe wa Mwana wa Mungu, ambaye macho yake yametameta kama moto, na miguu yake inang'aa kama shaba iliyosuguliwa.
»In angelu cerkve v Tiatiri piši: ›Te stvari govori Božji Sin, ki ima svoje oči podobne plamenu ognja in so njegova stopala kakor čist bron;
19 Najua mambo yako yote. Najua upendo wako, imani yako, utumishi wako na uvumilivu wako. Wewe unafanya vizuri zaidi sasa kuliko pale awali.
poznam tvoja dela in ljubezen in služenje in vero in tvojo potrpežljivost in tvoja dela; in zadnjih je več kakor prvih.
20 Lakini nina hoja moja juu yako: wewe unamvumilia yule mwanamke Yezabeli anayejiita nabii wa Mungu. Yeye huwafundisha na kuwapotosha watumishi wangu wafanye uzinzi na kula vyakula vilivyotambikiwa sanamu.
Vendar imam zoper tebe nekaj stvari, ker trpiš to žensko Jezabelo, ki sebe imenuje prerokinjo, da uči in da zapeljuje moje služabnike, da zagrešijo prešuštvo in da jedo stvari, žrtvovane malikom.
21 Nimempa muda wa kutubu dhambi zake, lakini hataki kuachana na uzinzi wake.
In dal sem ji čas, da se pokesa od svojega prešuštvovanja, pa se ni pokesala.
22 Sikiliza! Sasa namtupa kitandani ambapo yeye pamoja na wote waliofanya uzinzi naye watapatwa na mateso makali. Naam, nitafanya hivyo, kama wasipotubu matendo yao mabaya waliyotenda naye.
Glej, vrgel jo bom na posteljo in te, ki z njo grešijo zakonolomstvo, v veliko stisko, razen če se ne pokesajo od svojih dejanj.
23 Tena nitawaua wafuasi wake, ili makanisa yote yatambue kwamba mimi ndiye ninayechunguza mioyo na fikira za watu.
In njene otroke bom pobil s smrtjo in vse cerkve bodo vedele, da sem jaz tisti, ki preiskujem notranjosti in srca; in vsakemu od vas bom dal glede na vaša dejanja.
24 “Lakini ninyi wengine mlioko huko Thuatira ambao hamfuati mafundisho yake Yezabeli, na ambao hamkujifunza kile wanachokiita Siri ya Shetani, nawaambieni kwamba sitawapeni mzigo mwingine.
Toda tebi in ostalim iz Tiatire pravim, kdor nima tega nauka in tem, ki niso spoznali Satanovih globin, kakor govorijo; na vas ne bom nadel nobenega drugega bremena.
25 Lazima mzingatie yale mliyo nayo sasa mpaka nitakapokuja.
Temveč da trdno držite to, kar že imate, dokler ne pridem.
26 “Wanaoshinda, na wale watakaozingatia mpaka mwisho kutenda ninayotaka, nitawapa mamlaka juu ya mataifa.
In kdor zmaga in moja dela ohrani do konca, njemu bom dal oblast nad narodi.
27 Naam, nitawapa uwezo uleule nilioupokea kwa Baba: yaani, watayatawala mataifa kwa fimbo ya chuma na kuyavunjavunja kama chombo cha udongo.
In vladal jim bo z železno palico; kakor lončena posoda bodo razbiti do črepinj; celo kot sem jaz prejel od svojega Očeta.
28 Tena nitawapa nyota ya asubuhi.
In dal mu bom jutranjo zvezdo.
29 “Aliye na masikio, basi, na ayasikie yale Roho anayoyaambia makanisa!
Kdor ima uho, naj sliši, kaj Duh govori cerkvam.‹«