< Ufunuo 2 >
1 “Kwa malaika wa kanisa la Efeso andika hivi: “Huu ndio ujumbe kutoka kwake yeye ashikaye nyota saba katika mkono wake wa kulia, na ambaye hutembea katikati ya vinara saba vya taa vya dhahabu.
« Écris à l'ange de l'Église qui est dans Éphèse: Voici ce que dit celui qui tient les sept étoiles dans sa main droite, celui qui marche au milieu des sept candélabres d'or:
2 Najua mambo yako yote; najua bidii yako na uvumilivu wako. Najua kwamba huwezi kuwavumilia watu waovu, na kwamba umewapima wale wanaojisemea kuwa mitume na kumbe sio, ukagundua kwamba ni waongo.
Je connais tes œuvres et ta peine et ta constance, car tu ne peux supporter les méchants; et tu as mis à l'épreuve ceux qui se disent apôtres et qui ne le sont point, et tu les as trouvés menteurs.
3 Wewe unayo saburi, umestahimili taabu nyingi kwa ajili ya jina langu, wala hukuvunjika moyo.
Et tu as de la constance, et tu as eu à souffrir à cause de mon nom, et tu n'as pas faibli.
4 Lakini ninayo hoja moja juu yako: wewe hunipendi tena sasa kama pale awali.
Mais je te reproche d'avoir abandonné ta charité première.
5 Basi, pakumbuke pale ulipokuwa kabla ya kuanguka, ukayaache madhambi yako, na kufanya kama ulivyofanya pale awali. La sivyo, naja kwako na kukiondoa kinara chako mahali pake.
Souviens-toi donc d'où tu es tombé, repens-toi, et pratique tes premières œuvres; sinon, je vais venir à toi, et j'ôterai ton candélabre de sa place, à moins que tu ne te repentes.
6 Lakini nakusifu juu ya kitu kimoja: wewe unayachukia wanayoyatenda Wanikolai kama ninavyoyachukia mimi.
Mais tu as en ta faveur de haïr les œuvres des Nicolaïtes, et moi aussi je les hais.
7 “Aliye na masikio, basi, na asikie yale Roho anayoyaambia makanisa! “Wale wanaoshinda nitawapa haki ya kula matunda ya mti wa uzima ulioko ndani ya bustani ya Mungu.
Que celui qui a une oreille entende ce que l'Esprit dit aux sept Églises: Au vainqueur je donnerai à manger de l'arbre de la vie, qui est dans le paradis de Dieu. »
8 “Kwa malaika wa kanisa la Smurna andika hivi: “Huu ndio ujumbe kutoka kwake yeye wa kwanza na wa mwisho, ambaye alikufa na akaishi tena.
« Écris aussi à l'ange de l'Église qui est dans Smyrne: Voici ce que dit le premier-né et le dernier, qui a été mort et il a vécu:
9 Najua taabu zako; najua pia umaskini wako, ingawaje kwa kweli wewe ni tajiri; najua kashfa walizokufanyia wale wanaojiita Wayahudi lakini si Wayahudi wa kweli, bali ni kundi lake Shetani.
Je connais ta tribulation et ton indigence (pourtant tu es riche), et les calomnies de ceux qui disent qu'ils sont Juifs, et ils ne le sont point, mais ils sont une synagogue de Satan.
10 Usiogope hata kidogo yale ambayo itakulazimu kuteseka. Sikiliza! Ibilisi anataka kuwajaribu kwa kuwatia baadhi yenu gerezani; nanyi mtapata dhiki kwa muda wa siku kumi. Muwe waaminifu hata mpaka kufa, nami nitawapeni taji ya uzima.
Ne crains point les souffrances que tu vas endurer. Voici, le diable va jeter quelques-uns de vous en prison, afin que vous soyez mis à l'épreuve, et que vous souffriez une persécution de dix jours. Sois fidèle jusques à la mort, et je te donnerai la couronne de vie.
11 “Aliye na masikio, basi, na asikie yale Roho anayoyaambia makanisa! “Wale wanaoshinda hawataumizwa na kifo cha pili.
Que celui qui a une oreille entende ce que l'Esprit dit aux Églises: Le vainqueur ne sera certainement point atteint par la seconde mort. »
12 “Kwa malaika wa kanisa la Pergamoni andika hivi: “Huu ndio ujumbe wake yeye aliye na upanga mkali wenye kuwili.
« Écris aussi à l'ange de l'Église qui est dans Pergame: Voici ce que dit celui qui tient le glaive acéré à deux tranchants:
13 Najua unakoishi: Wewe unaishi kwenye makao makuu ya Shetani! Lakini bado unashikilia jina langu; hukuikana imani yako kwangu hata siku zile Antipa shahidi wangu mwaminifu, alipouawa pale mahali anapoishi Shetani.
Je sais où tu habites, et que là se trouve le trône de Satan; cependant tu retiens mon nom, et tu n'as pas renié ma foi, même dans le temps d'Antipas, mon témoin, mon fidèle, qui a été mis à mort chez vous, là où habite Satan.
14 Lakini ninayo machache dhidi yako: baadhi yenu ni wafuasi wa Balaamu aliyemfundisha Balaki kuwatega wana wa Israeli wale vyakula vilivyotambikiwa sanamu za kufanya uzinzi.
Mais j'ai quelques reproches à te faire, car tu as là des gens qui retiennent la doctrine de Balaam, lequel enseignait au roi Balak, comme pierre d'achoppement devant les fils d'Israël, à manger des viandes offertes aux idoles, et à se livrer à l'impudicité.
15 Vivyo hivyo, wako pia miongoni mwenu watu wanaofuata mafundisho ya Wanikolai.
De même toi aussi tu as des gens qui retiennent d'une manière semblable la doctrine des Nicolaïtes.
16 Basi, achana na madhambi yako. La sivyo, nitakuja kwako upesi na kupigana na watu hao kwa upanga utokao kinywani mwangu.
Repens-toi donc, sinon je vais promptement venir à toi, et je combattrai contre eux avec le glaive qui sort de ma bouche.
17 “Aliye na masikio, basi, na asikie yale Roho anayoyaambia makanisa! “Wale wanaoshinda nitawapa ile mana iliyofichika. Nitawapa pia jiwe jeupe lililoandikwa jina jipya ambalo hakuna mtu aliyelijua isipokuwa tu wale wanaolipokea.
Que celui qui a une oreille entende ce que l'Esprit dit aux Églises: Au vainqueur je donnerai de la manne cachée, et je lui donnerai un caillou blanc, et sur ce caillou est écrit un nouveau nom, que personne ne connaît, sinon celui qui le reçoit. »
18 “Kwa malaika wa kanisa la Thuatira andika hivi: “Huu ndio ujumbe wa Mwana wa Mungu, ambaye macho yake yametameta kama moto, na miguu yake inang'aa kama shaba iliyosuguliwa.
« Écris aussi à l'ange qui est dans Thyatire: Voici ce que dit le fils de Dieu, celui qui a les yeux comme une flamme de feu, et dont les pieds sont semblables à de l'airain brillant:
19 Najua mambo yako yote. Najua upendo wako, imani yako, utumishi wako na uvumilivu wako. Wewe unafanya vizuri zaidi sasa kuliko pale awali.
Je connais tes œuvres et ta charité et ta foi et ton service et ta constance, et tes dernières œuvres plus nombreuses que les premières.
20 Lakini nina hoja moja juu yako: wewe unamvumilia yule mwanamke Yezabeli anayejiita nabii wa Mungu. Yeye huwafundisha na kuwapotosha watumishi wangu wafanye uzinzi na kula vyakula vilivyotambikiwa sanamu.
Mais je te reproche de laisser faire ta femme, la Jésabel qui se dit prophétesse, et elle instruit et entraîne mes esclaves à se livrer à l'impudicité et à manger des viandes offertes aux idoles.
21 Nimempa muda wa kutubu dhambi zake, lakini hataki kuachana na uzinzi wake.
Et je lui ai donné du temps afin qu'elle se repentît, et elle n'a pas voulu se repentir de son impudicité.
22 Sikiliza! Sasa namtupa kitandani ambapo yeye pamoja na wote waliofanya uzinzi naye watapatwa na mateso makali. Naam, nitafanya hivyo, kama wasipotubu matendo yao mabaya waliyotenda naye.
Voici, je vais la jeter en prison, et ses complices adultères dans une grande tribulation, à moins qu'ils ne se repentent de leurs œuvres;
23 Tena nitawaua wafuasi wake, ili makanisa yote yatambue kwamba mimi ndiye ninayechunguza mioyo na fikira za watu.
je ferai mourir de mort ses enfants, et toutes les Églises sauront que c'est moi qui suis celui qui sonde les reins et les cœurs, et je vous rendrai à chacun selon vos œuvres.
24 “Lakini ninyi wengine mlioko huko Thuatira ambao hamfuati mafundisho yake Yezabeli, na ambao hamkujifunza kile wanachokiita Siri ya Shetani, nawaambieni kwamba sitawapeni mzigo mwingine.
Mais je vous le déclare, à vous tous autres de Thyatire qui ne suivez pas cette doctrine, étant de ceux qui n'ont pas connu ce qu'ils appellent les profondeurs de Satan: je ne vous impose point d'autre fardeau.
25 Lazima mzingatie yale mliyo nayo sasa mpaka nitakapokuja.
Seulement ce que vous avez, retenez-le jusques à ce que je vienne.
26 “Wanaoshinda, na wale watakaozingatia mpaka mwisho kutenda ninayotaka, nitawapa mamlaka juu ya mataifa.
Et le vainqueur, et celui qui observe jusques à la fin mes œuvres, je lui donnerai autorité sur les nations,
27 Naam, nitawapa uwezo uleule nilioupokea kwa Baba: yaani, watayatawala mataifa kwa fimbo ya chuma na kuyavunjavunja kama chombo cha udongo.
et il les paîtra avec une verge de fer, comme sont brisés les vases d'argile. De même que moi de mon côté je l'ai reçue de mon Père,
28 Tena nitawapa nyota ya asubuhi.
je lui donnerai l'étoile matinale.
29 “Aliye na masikio, basi, na ayasikie yale Roho anayoyaambia makanisa!
Que celui qui a une oreille entende ce que l'Esprit dit aux Églises. »