< Ufunuo 2 >

1 “Kwa malaika wa kanisa la Efeso andika hivi: “Huu ndio ujumbe kutoka kwake yeye ashikaye nyota saba katika mkono wake wa kulia, na ambaye hutembea katikati ya vinara saba vya taa vya dhahabu.
“To the angel of the church in Ephesus write: ‘These are the words of him who holds the seven stars in his right hand and who walks among the seven golden lampstands:
2 Najua mambo yako yote; najua bidii yako na uvumilivu wako. Najua kwamba huwezi kuwavumilia watu waovu, na kwamba umewapima wale wanaojisemea kuwa mitume na kumbe sio, ukagundua kwamba ni waongo.
I know yoʋr works, yoʋr labor, and yoʋr endurance. I know that yoʋ cannot tolerate those who are evil, and that yoʋ have tested those who declare themselves to be apostles but are not, and have found them to be false.
3 Wewe unayo saburi, umestahimili taabu nyingi kwa ajili ya jina langu, wala hukuvunjika moyo.
Yoʋ have persevered and endured hardships for the sake of my name, and have not grown weary.
4 Lakini ninayo hoja moja juu yako: wewe hunipendi tena sasa kama pale awali.
But I have this against yoʋ: Yoʋ have left yoʋr first love.
5 Basi, pakumbuke pale ulipokuwa kabla ya kuanguka, ukayaache madhambi yako, na kufanya kama ulivyofanya pale awali. La sivyo, naja kwako na kukiondoa kinara chako mahali pake.
Therefore, remember where yoʋ have fallen from; repent and do the works yoʋ did at first. If yoʋ do not repent, I will come to yoʋ quickly and remove yoʋr lampstand from its place.
6 Lakini nakusifu juu ya kitu kimoja: wewe unayachukia wanayoyatenda Wanikolai kama ninavyoyachukia mimi.
Yet yoʋ do have this: Yoʋ hate the works of the Nicolaitans, which I also hate.
7 “Aliye na masikio, basi, na asikie yale Roho anayoyaambia makanisa! “Wale wanaoshinda nitawapa haki ya kula matunda ya mti wa uzima ulioko ndani ya bustani ya Mungu.
He who has an ear, let him hear what the Spirit is saying to the churches. To him who overcomes I will give the right to eat of the tree of life, which is in the paradise of my God.’
8 “Kwa malaika wa kanisa la Smurna andika hivi: “Huu ndio ujumbe kutoka kwake yeye wa kwanza na wa mwisho, ambaye alikufa na akaishi tena.
“To the angel of the church in Smyrna write: ‘These are the words of the first and the last, who was dead and came to life:
9 Najua taabu zako; najua pia umaskini wako, ingawaje kwa kweli wewe ni tajiri; najua kashfa walizokufanyia wale wanaojiita Wayahudi lakini si Wayahudi wa kweli, bali ni kundi lake Shetani.
I know yoʋr works, yoʋr tribulation, and yoʋr poverty—yet yoʋ are rich! I know the slander of those who declare themselves to be Jews and are not, but are a synagogue of Satan.
10 Usiogope hata kidogo yale ambayo itakulazimu kuteseka. Sikiliza! Ibilisi anataka kuwajaribu kwa kuwatia baadhi yenu gerezani; nanyi mtapata dhiki kwa muda wa siku kumi. Muwe waaminifu hata mpaka kufa, nami nitawapeni taji ya uzima.
Do not be afraid of what yoʋ are about to suffer. Behold, the devil is about to throw some of you into prison so that you may be tested, and you will have tribulation for ten days. Be faithful, even to the point of death, and I will give yoʋ the crown of life.
11 “Aliye na masikio, basi, na asikie yale Roho anayoyaambia makanisa! “Wale wanaoshinda hawataumizwa na kifo cha pili.
He who has an ear, let him hear what the Spirit is saying to the churches. He who overcomes will certainly not be harmed by the second death.’
12 “Kwa malaika wa kanisa la Pergamoni andika hivi: “Huu ndio ujumbe wake yeye aliye na upanga mkali wenye kuwili.
“To the angel of the church in Pergamum write: ‘These are the words of him who has the sharp two-edged sword:
13 Najua unakoishi: Wewe unaishi kwenye makao makuu ya Shetani! Lakini bado unashikilia jina langu; hukuikana imani yako kwangu hata siku zile Antipa shahidi wangu mwaminifu, alipouawa pale mahali anapoishi Shetani.
I know yoʋr works and where yoʋ dwell, where Satan's throne is. Yet yoʋ hold fast to my name, and yoʋ did not deny my faith in the days when Antipas was my faithful witness, who was killed among you, where Satan dwells.
14 Lakini ninayo machache dhidi yako: baadhi yenu ni wafuasi wa Balaamu aliyemfundisha Balaki kuwatega wana wa Israeli wale vyakula vilivyotambikiwa sanamu za kufanya uzinzi.
But I have a few things against yoʋ: Yoʋ have some there who hold to the teaching of Balaam, who taught Balak to put a stumbling block before the sons of Israel and to eat food sacrificed to idols and commit fornication.
15 Vivyo hivyo, wako pia miongoni mwenu watu wanaofuata mafundisho ya Wanikolai.
In the same way, yoʋ also have some who hold to the teaching of the Nicolaitans.
16 Basi, achana na madhambi yako. La sivyo, nitakuja kwako upesi na kupigana na watu hao kwa upanga utokao kinywani mwangu.
Therefore repent. Otherwise, I will come to yoʋ quickly and make war against them with the sword of my mouth.
17 “Aliye na masikio, basi, na asikie yale Roho anayoyaambia makanisa! “Wale wanaoshinda nitawapa ile mana iliyofichika. Nitawapa pia jiwe jeupe lililoandikwa jina jipya ambalo hakuna mtu aliyelijua isipokuwa tu wale wanaolipokea.
He who has an ear, let him hear what the Spirit is saying to the churches. To him who overcomes I will give some of the hidden manna. I will also give him a white stone, and on the stone will be written a new name that no one knows except the one who receives it.’
18 “Kwa malaika wa kanisa la Thuatira andika hivi: “Huu ndio ujumbe wa Mwana wa Mungu, ambaye macho yake yametameta kama moto, na miguu yake inang'aa kama shaba iliyosuguliwa.
“To the angel of the church in Thyatira write: ‘These are the words of the Son of God, whose eyes are like a flame of fire and whose feet are like burnished bronze:
19 Najua mambo yako yote. Najua upendo wako, imani yako, utumishi wako na uvumilivu wako. Wewe unafanya vizuri zaidi sasa kuliko pale awali.
I know yoʋr works, yoʋr love and faith, yoʋr service and endurance, and that yoʋr latter works are greater than the ones yoʋ did at first.
20 Lakini nina hoja moja juu yako: wewe unamvumilia yule mwanamke Yezabeli anayejiita nabii wa Mungu. Yeye huwafundisha na kuwapotosha watumishi wangu wafanye uzinzi na kula vyakula vilivyotambikiwa sanamu.
But I have this against yoʋ: Yoʋ tolerate yoʋr wife Jezebel, who calls herself a prophetess while teaching and seducing my servants to commit fornication and eat food sacrificed to idols.
21 Nimempa muda wa kutubu dhambi zake, lakini hataki kuachana na uzinzi wake.
I gave her time to repent, but she refuses to repent of her fornication.
22 Sikiliza! Sasa namtupa kitandani ambapo yeye pamoja na wote waliofanya uzinzi naye watapatwa na mateso makali. Naam, nitafanya hivyo, kama wasipotubu matendo yao mabaya waliyotenda naye.
Behold, I will throw her onto a sickbed, and those who commit adultery with her I will throw into great tribulation, unless they repent from her works.
23 Tena nitawaua wafuasi wake, ili makanisa yote yatambue kwamba mimi ndiye ninayechunguza mioyo na fikira za watu.
I will strike her children dead. Then all the churches will know that I am he who searches minds and hearts, and I will give to each of you according to your works.
24 “Lakini ninyi wengine mlioko huko Thuatira ambao hamfuati mafundisho yake Yezabeli, na ambao hamkujifunza kile wanachokiita Siri ya Shetani, nawaambieni kwamba sitawapeni mzigo mwingine.
But to the rest of you who are in Thyatira, who do not hold to this teaching and have not learned what some call the deep things of Satan—to you I say: I place no further burden upon you.
25 Lazima mzingatie yale mliyo nayo sasa mpaka nitakapokuja.
Only hold fast to what you have until I come.
26 “Wanaoshinda, na wale watakaozingatia mpaka mwisho kutenda ninayotaka, nitawapa mamlaka juu ya mataifa.
To him who overcomes and keeps my works to the end, I will give authority over the nations,
27 Naam, nitawapa uwezo uleule nilioupokea kwa Baba: yaani, watayatawala mataifa kwa fimbo ya chuma na kuyavunjavunja kama chombo cha udongo.
and he will rule them with a rod of iron; like earthen vessels they will be shattered, just as I have received authority from my Father.
28 Tena nitawapa nyota ya asubuhi.
I will also give him the morning star.
29 “Aliye na masikio, basi, na ayasikie yale Roho anayoyaambia makanisa!
He who has an ear, let him hear what the Spirit is saying to the churches.’

< Ufunuo 2 >