< Ufunuo 2 >

1 “Kwa malaika wa kanisa la Efeso andika hivi: “Huu ndio ujumbe kutoka kwake yeye ashikaye nyota saba katika mkono wake wa kulia, na ambaye hutembea katikati ya vinara saba vya taa vya dhahabu.
To the angel of the church which is at Ephesus write: These things saith he who holdeth all things, and the seven stars, in his right hand; he that walketh in the midst of the seven candlesticks of gold;
2 Najua mambo yako yote; najua bidii yako na uvumilivu wako. Najua kwamba huwezi kuwavumilia watu waovu, na kwamba umewapima wale wanaojisemea kuwa mitume na kumbe sio, ukagundua kwamba ni waongo.
I know thy works, and thy toil, and thy patience, and that thou canst not endure the wicked; and thou hast tried them who say they are legates, and are not; and thou hast found them liars.
3 Wewe unayo saburi, umestahimili taabu nyingi kwa ajili ya jina langu, wala hukuvunjika moyo.
And thou hast had patience, and hast borne the burden, on account of my name, and hast not fainted.
4 Lakini ninayo hoja moja juu yako: wewe hunipendi tena sasa kama pale awali.
Yet I have a charge against thee, on account of thy former love, which thou hast left.
5 Basi, pakumbuke pale ulipokuwa kabla ya kuanguka, ukayaache madhambi yako, na kufanya kama ulivyofanya pale awali. La sivyo, naja kwako na kukiondoa kinara chako mahali pake.
Therefore remember whence thou hast fallen; and repent, and do the former works: or if not, I will come to thee quickly, and I will remove thy candlestick from its place, except thou repent.
6 Lakini nakusifu juu ya kitu kimoja: wewe unayachukia wanayoyatenda Wanikolai kama ninavyoyachukia mimi.
But this thou hast, that thou hatest the deeds of the Nicolaitans, which I also hate.
7 “Aliye na masikio, basi, na asikie yale Roho anayoyaambia makanisa! “Wale wanaoshinda nitawapa haki ya kula matunda ya mti wa uzima ulioko ndani ya bustani ya Mungu.
He that hath ears, let him hear what the Spirit saith to the churches. To him who is victorious, will I give to eat of the tree of life which is in the paradise of my God.
8 “Kwa malaika wa kanisa la Smurna andika hivi: “Huu ndio ujumbe kutoka kwake yeye wa kwanza na wa mwisho, ambaye alikufa na akaishi tena.
And to the angel of the church which is at Smyrna, write: These things saith the First and the Last, he who was dead, and liveth.
9 Najua taabu zako; najua pia umaskini wako, ingawaje kwa kweli wewe ni tajiri; najua kashfa walizokufanyia wale wanaojiita Wayahudi lakini si Wayahudi wa kweli, bali ni kundi lake Shetani.
I know thy works, and the affliction, and the poverty, (yet thou art rich; ) and the railing which is from them who say they are Jews, and they are not, but are of the congregation of Satan.
10 Usiogope hata kidogo yale ambayo itakulazimu kuteseka. Sikiliza! Ibilisi anataka kuwajaribu kwa kuwatia baadhi yenu gerezani; nanyi mtapata dhiki kwa muda wa siku kumi. Muwe waaminifu hata mpaka kufa, nami nitawapeni taji ya uzima.
Be not terrified at any of the things thou art to suffer. For lo, the Accuser will throw some of you into custody, that ye may be tried; and there will be trouble to you ten days. Be faithful unto death, and I will give thee the crown of life.
11 “Aliye na masikio, basi, na asikie yale Roho anayoyaambia makanisa! “Wale wanaoshinda hawataumizwa na kifo cha pili.
He that hath ears, let him hear what the Spirit saith to the churches. He that is victorious, shall not be harmed by the second death.
12 “Kwa malaika wa kanisa la Pergamoni andika hivi: “Huu ndio ujumbe wake yeye aliye na upanga mkali wenye kuwili.
And to the angel of the church at Pergamos, write: Thus saith he who hath the sharp two-edged sword;
13 Najua unakoishi: Wewe unaishi kwenye makao makuu ya Shetani! Lakini bado unashikilia jina langu; hukuikana imani yako kwangu hata siku zile Antipa shahidi wangu mwaminifu, alipouawa pale mahali anapoishi Shetani.
I know thy works, and where thou dwellest, even where the throne of Satan is: and thou holdest fast my name, and hast not denied the faith of me, in those days when my faithful witness, who was slain among you, was made a spectacle where Satan dwelleth.
14 Lakini ninayo machache dhidi yako: baadhi yenu ni wafuasi wa Balaamu aliyemfundisha Balaki kuwatega wana wa Israeli wale vyakula vilivyotambikiwa sanamu za kufanya uzinzi.
Yet I have a small charge against thee. Thou hast there them who hold the doctrine of Balaam, who taught Balak to throw a stumbling-block before the children of Israel, that they might eat the sacrifices of idols, and might commit whoredom.
15 Vivyo hivyo, wako pia miongoni mwenu watu wanaofuata mafundisho ya Wanikolai.
So also thou hast them who hold the doctrine of the Nicolaitans. In like manner, repent thou.
16 Basi, achana na madhambi yako. La sivyo, nitakuja kwako upesi na kupigana na watu hao kwa upanga utokao kinywani mwangu.
Or if not, I will come to thee quickly, and I will war upon them with the sword of my mouth.
17 “Aliye na masikio, basi, na asikie yale Roho anayoyaambia makanisa! “Wale wanaoshinda nitawapa ile mana iliyofichika. Nitawapa pia jiwe jeupe lililoandikwa jina jipya ambalo hakuna mtu aliyelijua isipokuwa tu wale wanaolipokea.
He that hath ears, let him hear what the Spirit saith to the churches. To him that is victorious, will I give to eat of the hidden manna; and I will give him a white counter, and upon the counter a new name written, which no one knoweth but he that receiveth it.
18 “Kwa malaika wa kanisa la Thuatira andika hivi: “Huu ndio ujumbe wa Mwana wa Mungu, ambaye macho yake yametameta kama moto, na miguu yake inang'aa kama shaba iliyosuguliwa.
And to the angel of the church at Thyatira, write: These things saith the Son of God, who hath his eyes like a flame of fire, and his feet like fine brass:
19 Najua mambo yako yote. Najua upendo wako, imani yako, utumishi wako na uvumilivu wako. Wewe unafanya vizuri zaidi sasa kuliko pale awali.
I know thy works, and love, and faith, and service, and also thy patience; and that these thy latter works are more than the former.
20 Lakini nina hoja moja juu yako: wewe unamvumilia yule mwanamke Yezabeli anayejiita nabii wa Mungu. Yeye huwafundisha na kuwapotosha watumishi wangu wafanye uzinzi na kula vyakula vilivyotambikiwa sanamu.
But I have a charge against thee, because thou sufferest thy woman Jezabel, who saith she is a prophetess, and teacheth, and seduceth my servants to whoredom, and to eating of the sacrifices of idols.
21 Nimempa muda wa kutubu dhambi zake, lakini hataki kuachana na uzinzi wake.
And I gave her a season for repentance, and she is not disposed to repent of her whoredom.
22 Sikiliza! Sasa namtupa kitandani ambapo yeye pamoja na wote waliofanya uzinzi naye watapatwa na mateso makali. Naam, nitafanya hivyo, kama wasipotubu matendo yao mabaya waliyotenda naye.
Behold, I will cast her upon a bed, and them who commit adultery with her into great affliction, unless they repent of their deeds.
23 Tena nitawaua wafuasi wake, ili makanisa yote yatambue kwamba mimi ndiye ninayechunguza mioyo na fikira za watu.
And her children will I slay with death: and all the churches shall know, that I am he who searcheth reins and hearts; and I will render to each of you according to your works.
24 “Lakini ninyi wengine mlioko huko Thuatira ambao hamfuati mafundisho yake Yezabeli, na ambao hamkujifunza kile wanachokiita Siri ya Shetani, nawaambieni kwamba sitawapeni mzigo mwingine.
And I say to you, to the rest that are in Thyatira, to all them who have not received this doctrine, the men who have not known the profound things of Satan, as they say; I lay no other burden upon you:
25 Lazima mzingatie yale mliyo nayo sasa mpaka nitakapokuja.
but, what ye have, hold fast until I come.
26 “Wanaoshinda, na wale watakaozingatia mpaka mwisho kutenda ninayotaka, nitawapa mamlaka juu ya mataifa.
And to him that is victorious, and to him that observeth my works unto the end, to him will I give authority, over the nations;
27 Naam, nitawapa uwezo uleule nilioupokea kwa Baba: yaani, watayatawala mataifa kwa fimbo ya chuma na kuyavunjavunja kama chombo cha udongo.
and he shall rule them with a rod of iron; and like vessels of pottery, shall they be broken: as I also have received of my Father.
28 Tena nitawapa nyota ya asubuhi.
And I will give him the morning star.
29 “Aliye na masikio, basi, na ayasikie yale Roho anayoyaambia makanisa!
He that hath ears, let him hear what the Spirit saith to the churches.

< Ufunuo 2 >