< Ufunuo 18 >

1 Baada ya hayo, nilimwona malaika mwingine akishuka kutoka mbinguni. Alikuwa na uwezo mkuu, na dunia ikamulikwa na mng'ao wake.
And after these things I saw another angel come down from heaven, having great power; and the earth was enlightened with his glory.
2 Basi, akapaaza sauti kwa nguvu akisema, “Umeanguka; Babuloni mkuu umeanguka! Sasa umekuwa makao ya mashetani na pepo wachafu; umekuwa makao ya ndege wachafu na wa kuchukiza mno.
And he cried with vehemence, and with a loud voice, saying, Babylon the great is fallen, is fallen, and is become the habitation of demons, a den of impure spirits, and a cage for every unclean and hateful bird.
3 Maana mataifa yote yalileweshwa kwa divai kali ya uzinzi wake, nao wafalme wa dunia wamefanya uzinzi naye. Nao wafanyabiashara wa dunia wametajirika kutokana na anasa zake zisizo na kipimo.”
For all nations have drunk of the wine of her furious whoredom, and the kings of the earth have committed whoredom with her, and the merchants of the earth are grown rich by the abundance of her luxury.
4 Kisha nikasikia sauti nyingine kutoka mbinguni ikisema, “Watu wangu, ondokeni kwake, ili msishirikiane naye katika dhambi zake, msije mkaipata adhabu yake.
And I heard another voice from heaven, saying, Come out from her, my people, that ye be not partakers of her sins, and that ye may not suffer by her plagues:
5 Kwa maana dhambi zake zimekuwa nyingi mno, zimelundikana mpaka mbinguni, na Mungu ameyakumbuka maovu yake.
for her sins have reached unto heaven, and God hath remembered her iniquities.
6 Mtendeeni kama alivyowatendea ninyi; mlipeni mara mbili kwa yale aliyoyatenda. Jazeni kikombe chake kwa kinywaji kikali mara mbili zaidi ya kile alichowapeni.
Give to her as she hath given to you, and repay her double according to her works: in the cup, which she hath mixed, mix for her double.
7 Mpeni mateso na uchungu kadiri ya kujigamba kwake, na kuishi kwake kwa anasa. Maana anajisemea moyoni: Ninaketi hapa; mimi ni malkia. Mimi si mjane, wala sitapatwa na uchungu!
As much as she hath glorified herself and indulged to luxury, so much torment and sorrow give her; because she saith in her heart, I sit as a queen, I am not a widow, and I shall see no sorrow.
8 Kwa sababu hiyo mabaa yake yatampata kwa siku moja: ugonjwa, huzuni na njaa. Atachomwa moto, maana Bwana Mungu mwenye kumhukumu ni Mwenye Uwezo.”
Therefore in one day shall her plagues come, even death and mourning and famine; and she shall be burnt with fire: for strong is the Lord God who judgeth her.
9 Wafalme wa Dunia waliofanya uzinzi naye na kuishi naye maisha ya anasa wataomboleza na kulia wakati watakapoona moshi wa mji huo unaoteketea.
And the kings of the earth, who have committed lewdness and lived luxuriously with her, shall bemoan her and lament for her, when they see the smoke of her burning;
10 Wanasimama kwa mbali kwa sababu ya kuogopa mateso yake, na kusema, “Ole! Ole kwako Babuloni, mji maarufu na wenye nguvu! Kwa muda wa saa moja tu adhabu yako imekupata.”
standing afar off for fear of her torment, saying, Alas, alas, the great city Babylon, that powerful city! for in one hour is thy judgement come.
11 Wafanyabiashara wa dunia watalia na kumfanyia matanga, maana hakuna mtu anayenunua tena bidhaa zao;
And the merchants of the earth shall bewail and mourn over her, because no one will buy their merchandize any more:
12 hakuna tena wa kununua dhahabu yao, fedha, mawe ya thamani na lulu, kitani na nguo za rangi ya zambarau, hariri na nguo nyekundu; vyombo vya kila aina ya miti ya pekee, vyombo vya pembe za ndovu, vya miti ya thamani kubwa, vya shaba, chuma na marmari;
the lading of gold, and silver, and precious stones, and pearl, and fine linen, and purple, and silk, and all sorts of thyine wood, and vessels of ivory, and of the most precious wood, and of brass, and iron, and marble;
13 mdalasini, viungo, ubani, manemane, udi, divai, mafuta, unga na ngano, ng'ombe na kondoo, farasi na magari ya kukokotwa, watumwa wao na hata maisha ya watu.
and their cinnamon, and perfumes, and sweet ointment, and incense, and wine, and oil, and fine flour, and wheat, and cattle, and sheep, and horses, and chariots, and slaves, yea and the souls of men.
14 Wafanyabiashara wanamwambia: “Faida yote uliyotazamia imetoweka, na utajiri na fahari vimekuponyoka; hutaweza kuvipata tena!”
And the fruits, which thy soul longed after, are gone from thee, and all thy delicate and splendid things are departed, and thou shalt find them no more.
15 Wafanya biashara waliotajirika kutokana na mji huo, watasimama mbali kwa sababu ya hofu ya mateso yake, watalalamika na kuomboleza,
The merchants of these things, who grew rich by their trade with her, shall stand afar off for fear of her torment, weeping and mourning,
16 wakisema, “Ole! Ole kwa mji huu mkuu. Ulizoea kuvalia nguo za kitani, za rangi ya zambarau na nyekundu, na kujipamba kwa dhahabu, mawe ya thamani na lulu!
and saying, Alas, alas, the great city, that was clothed in fine linen, and purple, and scarlet, and adorned with gold, and precious stones, and pearls!
17 Kwa saa moja tu utajiri wako umetoweka!” Halafu manahodha wote na wasafiri wao, wanamaji na wote wanaofanya kazi baharini, walisimama kwa mbali,
for in one hour is so great wealth laid waste. And every pilot, and all on board the ships, and the mariners, and all that traffic by sea, stood afar off,
18 na walipouona moshi wa moto ule uliouteketeza, wakalia kwa sauti: “Hakujapata kuwako mji kama mji huu mkuu!”
and cried out, when they saw the smoke of her burning, saying, What city is like to this great city?
19 Wakajimwagia vumbi juu ya vichwa vyao wakilia kwa sauti na kuomboleza: “Ole! Ole kwako mji mkuu! Ni mji ambamo wote wenye meli zisafirizo baharini walitajirika kutokana na utajiri wake. Kwa muda wa saa moja tu umepoteza kila kitu!”
And they threw dust on their heads, and cried out, weeping and moaning, saying, Alas, alas, that great city, in which all that had ships at sea were enriched by her sumptuous expences! for in one hour she is become desolate.
20 Furahi ee mbingu, kwa sababu ya uharibifu wake. Furahini watu wa Mungu, mitume na manabii! Kwa maana Mungu ameuhukumu kwa sababu ya mambo uliyowatenda ninyi!
Rejoice over her, O heaven, and ye holy apostles and prophets, for God hath avenged you on her.
21 Kisha malaika mmoja mwenye nguvu sana akainua jiwe mfano wa jiwe kubwa la kusagia, akalitupa baharini akisema, “Ndivyo, Babuloni atakavyotupwa na kupotea kabisa.
And a mighty angel took up a stone like a great milstone, and cast it into the sea, saying, Thus shall the great city Babylon be thrown down with violence, and never be found more.
22 Sauti za vinubi za muziki, sauti za wapiga filimbi na tarumbeta hazitasikika tena ndani yako. Hakuna fundi wa namna yoyote ile atakayepatikana tena ndani yako; wala sauti ya jiwe la kusagia haitasikika tena ndani yako.
And the voice of harpers, and musicians, and pipers, and trumpeters, shall be heard in thee no more: and no artist of any art whatsoever shall be found in thee any more; and the sound of a milstone shall be heard in thee no more.
23 Mwanga wa taa hautaonekana tena ndani yako; sauti za bwana arusi na bibi arusi hazitasikika tena ndani yako. Wafanyabiashara wako walikuwa wakuu duniani, na kwa uchawi wako mataifa yote yalipotoshwa!”
And the light of a candle shall be seen in thee no more; and the voice of the bridegroom and bride shall be heard no more in thee: for thy merchants were the great men of the earth, and by thy sorceries were all nations deceived.
24 Mji huo uliadhibiwa kwani humo mlipatikana damu ya manabii, damu ya watu wa Mungu na damu ya watu wote waliouawa duniani.
And herein was found the blood of prophets and saints, and of all that were slain upon the earth.

< Ufunuo 18 >