< Ufunuo 15 >

1 Kisha nikaona ishara nyingine mbinguni, kubwa na ya kushangaza. Palikuwa hapo malaika saba wenye mabaa makubwa saba ya mwisho. Kwa mabaa hayo makubwa saba, ghadhabu ya Mungu imekamilishwa.
Vi outro grande e maravilhoso sinal no céu: sete anjos tendo as sete últimas pragas, pois nelas a ira de Deus está terminada.
2 Kisha nikaona kitu kama bahari ya kioo, imechanganywa na moto. Nikawaona pia wale watu waliomshinda yule mnyama na sanamu yake na ambaye jina lake lilitajwa kwa ile tarakimu. Watu hao walikuwa wamesimama kando ya hiyo bahari ya kioo, wakiwa na vinubi walivyopewa na Mungu.
Vi algo como um mar de vidro misturado com fogo, e aqueles que superaram a besta, sua imagem e o número de seu nome, de pé sobre o mar de vidro, tendo harpas de Deus.
3 Walikuwa wakiimba wimbo wa Mose, mtumishi wa Mungu, na wimbo wa Mwanakondoo: “Bwana Mungu Mwenye Uwezo, matendo yako ni makuu mno! Ewe Mfalme wa mataifa, njia zako ni za haki na za kweli!
Eles cantaram o canto de Moisés, o servo de Deus, e o canto do Cordeiro, dizendo, “Grandes e maravilhosas são suas obras, Senhor Deus, o Todo-Poderoso! Justos e verdadeiros são seus caminhos, seu rei das nações.
4 Bwana, ni nani asiyekucha wewe? Nani asiyelitukuza jina lako? Wewe peke yako ni Mtakatifu. Mataifa yote yatakujia na kukuabudu maana matendo yako ya haki yameonekana na wote.”
Quem não temeria você, Senhor, e glorificar seu nome? Pois você só é santo. Pois todas as nações virão e adorarão diante de vocês. Pois seus atos justos foram revelados”.
5 Baada ya hayo nikaona Hekalu limefunguliwa mbinguni, na ndani yake hema ionyeshayo kuwapo kwa Mungu.
Depois destas coisas eu olhei, e o templo do tabernáculo do testemunho no céu foi aberto.
6 Basi, wale malaika saba wenye mabaa saba wakatoka humo Hekaluni, wakiwa wamevaa nguo za kitani safi zenye kung'aa, na kanda za dhahabu vifuani mwao.
Os sete anjos que tinham as sete pragas saíram, vestidos com linho puro e brilhante, e usando faixas douradas ao redor de seu peito.
7 Kisha, mmojawapo wa vile viumbe vinne akawapa hao malaika saba mabakuli ya dhahabu yaliyojaa ghadhabu ya Mungu, aishiye milele na milele. (aiōn g165)
Um dos quatro seres vivos deu aos sete anjos sete taças de ouro cheias da ira de Deus, que vive para todo o sempre. (aiōn g165)
8 Hekalu likajaa moshi uliosababishwa na utukufu na nguvu ya Mungu, na hakuna mtu aliyeweza kuingia Hekaluni mpaka mwisho wa mabaa makubwa saba ya wale malaika saba.
O templo estava cheio de fumaça da glória de Deus e de seu poder. Ninguém pôde entrar no templo até que as sete pragas dos sete anjos estivessem terminadas.

< Ufunuo 15 >