< Ufunuo 14 >
1 Kisha nikaona mlima Sioni, na Mwanakondoo amesimama juu yake; pamoja naye walikuwa watu mia moja arobaini na nne elfu ambao juu ya paji za nyuso zao walikuwa wameandikwa jina la Mwanakondoo na jina la Baba yake.
Je regardai, et je vis l'Agneau qui se tenait sur la montagne de Sion, et avec lui cent quarante-quatre mille personnes, qui avaient son nom et le nom de son Père écrits sur leurs fronts.
2 Basi, nikasikia sauti kutoka mbinguni, sauti iliyokuwa kama sauti ya maji mengi na kama sauti ya ngurumo kubwa. Sauti niliyosikia ilikuwa kama sauti ya wachezaji muziki wakipiga vinubi vyao.
Puis j'entendis une voix qui venait du ciel, semblable au bruit des grosses eaux et au bruit d'un grand tonnerre; et la voix que j'entendis était comme le son des harpes touchées par des harpistes:
3 Walikuwa wanaimba wimbo mpya mbele ya kiti cha enzi na mbele ya wale viumbe hai wanne na wale wazee. Hakuna mtu aliyeweza kujifunza wimbo huo isipokuwa hao watu mia moja arobaini na nne elfu waliokombolewa duniani.
ils chantent un cantique nouveau devant le trône et devant les quatre animaux et les vieillards. Et personne ne pouvait apprendre ce cantique, si ce n'est les cent quarante-quatre mille, qui ont été rachetés de la terre.
4 Watu hao ndio wale waliojiweka safi kwa kutoonana kimwili na wanawake, nao ni mabikira. Wao humfuata Mwanakondoo kokote aendako. Wamekombolewa kutoka miongoni mwa binadamu wengine, wakawa wa kwanza kutolewa kwa Mungu na kwa Mwanakondoo.
Ceux-là ne se sont point souillés avec des femmes; car ils sont vierges. Ceux-là suivent l'Agneau partout où il va. Ils ont été rachetés parmi les hommes, comme des prémices consacrées à Dieu et à l'Agneau;
5 Hawakupata kamwe kuwa waongo; hawana hatia yoyote.
et dans leur bouche, il ne s'est point trouvé de mensonge, car ils sont sans tache.
6 Kisha nikamwona malaika mwingine anaruka juu angani akiwa na Habari Njema ya milele ya Mungu, aitangaze kwa watu wote waishio duniani, kwa mataifa yote, makabila yote, watu wa lugha zote na rangi zote. (aiōnios )
Après cela, je vis un autre ange, qui volait au milieu du ciel, portant l'Évangile éternel, pour l'annoncer à ceux qui habitent sur la terre, à toute nation, à toute tribu, à toute langue et à tout peuple. (aiōnios )
7 Akasema kwa sauti kubwa, “Mcheni Mungu na kumtukuza! Maana saa imefika ya kutoa hukumu yake. Mwabuduni yeye aliyeumba mbingu na nchi, bahari na chemchemi za maji.”
Il disait d'une voix forte: Craignez Dieu, et donnez-lui gloire; car l'heure de son jugement est venue. Adorez Celui qui a fait le ciel, la terre, la mer et les sources d'eaux!
8 Malaika wa pili alimfuata huyo wa kwanza akisema, “Ameanguka! Naam, Babuloni mkuu ameanguka! Babuloni ambaye aliwapa mataifa yote wainywe divai yake—divai kali ya uzinzi wake!”
Un autre ange, un second, le suivit, qui disait: Elle est tombée, elle est tombée, Babylone la grande, qui a abreuvé toutes les nations du vin de son impudicité effrénée.
9 Na malaika wa tatu aliwafuata hao wawili akisema kwa sauti kubwa, “Yeyote anayemwabudu yule mnyama na sanamu yake na kukubali kutiwa alama yake juu ya paji la uso wake au juu ya mkono wake,
Un autre ange, un troisième, les suivit, disant d'une voix forte: Si quelqu'un adore la bête et son image, et qu'il en prenne la marque sur le front ou sur la main,
10 yeye mwenyewe atakunywa divai ya ghadhabu ya Mungu, ambayo imemiminwa katika kikombe cha ghadhabu yake bila kuchanganywa na maji. Mtu huyo atateseka ndani ya moto na kiberiti mbele ya malaika watakatifu na mbele ya Mwanakondoo.
il boira, lui aussi, du vin du courroux de Dieu, versé pur dans la coupe de sa colère, et il sera tourmenté dans le feu et le soufre, en présence des saints anges et en présence de l'Agneau.
11 Moshi wa moto unaowatesa kupanda juu milele na milele. Watu hao waliomwabudu huyo mnyama na sanamu yake, na kutiwa alama ya jina lake, hawatakuwa na nafuu yoyote usiku na mchana.” (aiōn )
Et la fumée de leur tourment monte aux siècles des siècles. Jour et nuit, il n'y aura aucun repos, ni pour ceux qui adorent la bête et son image, ni pour ceux qui prennent la marque de son nom. (aiōn )
12 Kutokana na hayo, ni lazima watu wa Mungu, yaani watu wanaotii amri ya Mungu na kumwamini Yesu, wawe na uvumilivu.
Ici se montre la patience des saints: ils gardent les commandements de Dieu et la foi en Jésus.
13 Kisha nikasikia sauti kutoka mbinguni ikisema, “Andika! Heri watu ambao tangu sasa wanakufa wakiwa wameungana na Bwana.” Naye Roho asema, “Naam! Watapumzika kutoka taabu zao; maana matunda ya jasho lao yatawafuata.”
J'entendis une voix venant du ciel, qui disait: Écris: Heureux, dès à présent, les morts qui meurent dans le Seigneur! Oui, dit l'Esprit; car ils se reposent de leurs travaux, et leurs oeuvres les suivent.
14 Kisha nikatazama, na kumbe palikuwapo wingu jeupe hapo. Na juu ya wingu hilo kulikuwa na kiumbe kama mtu. Alikuwa amevaa taji ya dhahabu kichwani, na kushika mundu mkononi mwake.
Je regardai, et je vis une nuée blanche, et sur cette nuée était assis quelqu'un qui ressemblait à un fils d'homme: il avait sur la tête une couronne d'or, et à la main une faucille tranchante.
15 Kisha malaika mwingine akatoka Hekaluni, na kwa sauti kubwa akamwambia yule aliyekuwa amekaa juu ya wingu, “Tafadhali, tumia mundu wako ukavune mavuno, maana wakati wa mavuno umefika; mavuno ya dunia yameiva.”
Un autre ange sortit du temple, criant d'une voix forte à celui qui était assis sur la nuée: Lance ta faucille et moissonne; car le temps de moissonner est venu, la moisson de la terre est mûre.
16 Basi, yule aliyekuwa amekaa juu ya wingu akautupa mundu wake duniani, na mavuno ya dunia yakavunwa.
Alors celui qui était assis sur la nuée lança sa faucille sur la terre, et la terre fut moissonnée.
17 Kisha malaika mwingine akatoka katika Hekalu mbinguni akiwa na mundu wenye makali.
Un autre ange sortit du temple qui est dans le ciel, tenant, lui aussi, une faucille tranchante.
18 Kisha malaika mwingine msimamizi wa moto, akatoka madhabahuni akamwambia kwa sauti kubwa yule malaika mwenye mundu wenye makali, “Nawe tia huo mundu wako mkali, ukakate vichala vya mizabibu ya dunia, maana zabibu zake zimeiva!”
Un autre ange qui avait pouvoir sur le feu, sortit de l'autel. Il cria, d'une voix forte, à celui qui tenait la faucille tranchante, et il lui dit: Lance ta faucille tranchante, et vendange les grappes de la vigne de la terre; car ses raisins sont mûrs.
19 Basi, malaika huyo akautupa mundu wake duniani, akakata zabibu za dunia, akazitia ndani ya chombo kikubwa cha kukamulia zabibu, chombo cha ghadhabu ya Mungu.
L'ange lança sa faucille sur la terre et vendangea la vigne de la terre; et il jeta la vendange dans la grande cuve de la colère de Dieu.
20 Zabibu zikakamuliwa ndani ya hilo shinikizo lililoko nje ya mji, na damu ikatoka katika shinikizo hilo mtiririko mrefu kiasi cha mita mia tatu na kina chake kiasi cha mita mia mbili.
La cuve fut foulée hors de la ville; et de la cuve il sortit du sang qui montait jusqu'aux freins des chevaux, sur un espace de mille six cents stades.