< Ufunuo 14 >
1 Kisha nikaona mlima Sioni, na Mwanakondoo amesimama juu yake; pamoja naye walikuwa watu mia moja arobaini na nne elfu ambao juu ya paji za nyuso zao walikuwa wameandikwa jina la Mwanakondoo na jina la Baba yake.
And I looked, and behold, a Lamb stood on mount Zion; and with him the number of a hundred and forty and four thousand, having his name and the name of his Father written upon their foreheads.
2 Basi, nikasikia sauti kutoka mbinguni, sauti iliyokuwa kama sauti ya maji mengi na kama sauti ya ngurumo kubwa. Sauti niliyosikia ilikuwa kama sauti ya wachezaji muziki wakipiga vinubi vyao.
And I heard a sound from heaven, as the sound of many waters, and as the sound of great thunder; and the sound which I heard, was like that of harpers striking on their harps.
3 Walikuwa wanaimba wimbo mpya mbele ya kiti cha enzi na mbele ya wale viumbe hai wanne na wale wazee. Hakuna mtu aliyeweza kujifunza wimbo huo isipokuwa hao watu mia moja arobaini na nne elfu waliokombolewa duniani.
And they sang a new song before the throne, and before the four Animals and the Elders: and no one was able to learn that song, except the hundred and forty and four thousand who were redeemed from the earth.
4 Watu hao ndio wale waliojiweka safi kwa kutoonana kimwili na wanawake, nao ni mabikira. Wao humfuata Mwanakondoo kokote aendako. Wamekombolewa kutoka miongoni mwa binadamu wengine, wakawa wa kwanza kutolewa kwa Mungu na kwa Mwanakondoo.
These are they who have not defiled themselves with women, for they are virgins. These are they who followed the Lamb, whithersoever he went. These have been redeemed by Jesus from among men, the first fruits to God and the Lamb.
5 Hawakupata kamwe kuwa waongo; hawana hatia yoyote.
And in their mouth was found, no falsehood; for they are without faults.
6 Kisha nikamwona malaika mwingine anaruka juu angani akiwa na Habari Njema ya milele ya Mungu, aitangaze kwa watu wote waishio duniani, kwa mataifa yote, makabila yote, watu wa lugha zote na rangi zote. (aiōnios )
And I saw another angel flying in heaven: and with blood, he had the everlasting gospel, to proclaim to dwellers on the earth, and to every nation and tribe and tongue and people; (aiōnios )
7 Akasema kwa sauti kubwa, “Mcheni Mungu na kumtukuza! Maana saa imefika ya kutoa hukumu yake. Mwabuduni yeye aliyeumba mbingu na nchi, bahari na chemchemi za maji.”
saying with a loud voice, Worship God, and give glory to him; because the hour of his judgment is come; and adore ye Him, who made heaven and earth, and the sea, and the fountains of water.
8 Malaika wa pili alimfuata huyo wa kwanza akisema, “Ameanguka! Naam, Babuloni mkuu ameanguka! Babuloni ambaye aliwapa mataifa yote wainywe divai yake—divai kali ya uzinzi wake!”
And another, a second angel followed him, saying: Fallen, fallen is Babylon the great, which made all nations drink of the wine of the rage of her whoredom.
9 Na malaika wa tatu aliwafuata hao wawili akisema kwa sauti kubwa, “Yeyote anayemwabudu yule mnyama na sanamu yake na kukubali kutiwa alama yake juu ya paji la uso wake au juu ya mkono wake,
And another, a third angel followed them, saying with a loud voice: If any man shall worship the beast of prey and its image, and shall receive its mark upon his forehead or on his hand,
10 yeye mwenyewe atakunywa divai ya ghadhabu ya Mungu, ambayo imemiminwa katika kikombe cha ghadhabu yake bila kuchanganywa na maji. Mtu huyo atateseka ndani ya moto na kiberiti mbele ya malaika watakatifu na mbele ya Mwanakondoo.
he also shall drink of the wine of the wrath of God, which is poured undiluted into the cup of his indignation, and shall be tormented with fire and sulphur, before the holy angels, and before the throne.
11 Moshi wa moto unaowatesa kupanda juu milele na milele. Watu hao waliomwabudu huyo mnyama na sanamu yake, na kutiwa alama ya jina lake, hawatakuwa na nafuu yoyote usiku na mchana.” (aiōn )
And the smoke of their torment ascendeth up for ever and ever; and there is no rest, by day or by night, to those that worship the beast of prey and its image. (aiōn )
12 Kutokana na hayo, ni lazima watu wa Mungu, yaani watu wanaotii amri ya Mungu na kumwamini Yesu, wawe na uvumilivu.
Here is the patience of the saints, who keep the commandments of God, and the faith of Jesus.
13 Kisha nikasikia sauti kutoka mbinguni ikisema, “Andika! Heri watu ambao tangu sasa wanakufa wakiwa wameungana na Bwana.” Naye Roho asema, “Naam! Watapumzika kutoka taabu zao; maana matunda ya jasho lao yatawafuata.”
And I heard a voice from heaven, saying: Write, Blessed are the dead that die in the Lord, henceforth: yes, saith the Spirit, that they may rest from their toils; for their deeds do accompany them.
14 Kisha nikatazama, na kumbe palikuwapo wingu jeupe hapo. Na juu ya wingu hilo kulikuwa na kiumbe kama mtu. Alikuwa amevaa taji ya dhahabu kichwani, na kushika mundu mkononi mwake.
And I looked, and lo, a white cloud; and upon the cloud sat one who was like the Son of man; and on his head was a crown of gold, and in his hand a sharp sickle.
15 Kisha malaika mwingine akatoka Hekaluni, na kwa sauti kubwa akamwambia yule aliyekuwa amekaa juu ya wingu, “Tafadhali, tumia mundu wako ukavune mavuno, maana wakati wa mavuno umefika; mavuno ya dunia yameiva.”
And another angel came out of the temple, crying with a loud voice, to him that sat on the cloud.
16 Basi, yule aliyekuwa amekaa juu ya wingu akautupa mundu wake duniani, na mavuno ya dunia yakavunwa.
And he thrust his sickle over the earth; and the earth was reaped.
17 Kisha malaika mwingine akatoka katika Hekalu mbinguni akiwa na mundu wenye makali.
And another angel came out of the temple that is in heaven, having also a sharp sickle.
18 Kisha malaika mwingine msimamizi wa moto, akatoka madhabahuni akamwambia kwa sauti kubwa yule malaika mwenye mundu wenye makali, “Nawe tia huo mundu wako mkali, ukakate vichala vya mizabibu ya dunia, maana zabibu zake zimeiva!”
And another angel came out from the altar, having authority over fire. And he cried with a loud voice, to him who had the sharp sickle, saying: Thrust in thy sickle which is sharp, and gather the clusters of the vineyard of the earth, because the grapes of the earth are ripe.
19 Basi, malaika huyo akautupa mundu wake duniani, akakata zabibu za dunia, akazitia ndani ya chombo kikubwa cha kukamulia zabibu, chombo cha ghadhabu ya Mungu.
And the angel thrust in his sickle on the earth, and gathered the vintage of the earth, and cast it into the wine-press of the wrath of the great God.
20 Zabibu zikakamuliwa ndani ya hilo shinikizo lililoko nje ya mji, na damu ikatoka katika shinikizo hilo mtiririko mrefu kiasi cha mita mia tatu na kina chake kiasi cha mita mia mbili.
And the wine-press was trodden, up to the horses' bridles, for a thousand and six hundred furlongs.