< Ufunuo 11 >

1 Kisha nikapewa mwanzi uliokuwa kama kijiti cha kupimia, nikaambiwa, “Inuka, ukalipime Hekalu la Mungu, madhabahu ya kufukizia ubani, na ukawahesabu watu wanaoabudu ndani ya Hekalu.
Foi-me dada uma palheta como uma vara. Alguém disse: “Levanta-te e mede o templo de Deus, e o altar, e aqueles que nele adoram”.
2 Lakini uache ukumbi ulio nje ya Hekalu; usiupime, maana huo umekabidhiwa watu wa mataifa mengine, ambao wataukanyanga mji Mtakatifu kwa muda wa miezi arobaini na miwili.
Deixe de fora a corte que está fora do templo, e não a meça, pois ela foi dada às nações. Eles pisarão a cidade santa por quarenta e dois meses.
3 Nami nitawatuma mashahidi wangu wawili ili watangaze ujumbe wa Mungu kwa muda huo wa siku elfu moja mia mbili na sitini wakiwa wamevaa mavazi ya magunia.”
Darei poder a minhas duas testemunhas, e elas profetizarão mil duzentos e sessenta dias, vestidas de pano de saco”.
4 Hao mashahidi wawili ni miti miwili ya Mizeituni na taa mbili zinazosimama mbele ya Bwana wa dunia.
Estas são as duas oliveiras e os dois candeeiros, de pé diante do Senhor da Terra.
5 Kama mtu akijaribu kuwadhuru, moto hutoka kinywani mwao na kuwaangamiza adui zao; na kila mtu atakayejaribu kuwadhuru atakufa namna hiyo.
Se alguém desejar prejudicá-los, o fogo sai de sua boca e devora seus inimigos. Se alguém deseja fazer-lhes mal, deve ser morto desta forma.
6 Hao wanayo mamlaka ya kufunga anga, mvua isinyeshe wakati wanapotangaza ujumbe wa Mungu. Tena wanayo mamlaka ya kuzigeuza chemchemi zote za maji ziwe damu, na ya kusababisha maafa ya kila namna duniani kila mara wapendavyo.
Estes têm o poder de calar o céu, para que não chova durante os dias de sua profecia. Eles têm poder sobre as águas, para transformá-las em sangue e para atingir a terra com cada praga, tantas vezes quantas desejarem.
7 Lakini wakisha maliza kutangaza ujumbe huo, mnyama atokaye shimoni kuzimu atapigana nao, atawashinda na kuwaua. (Abyssos g12)
Quando tiverem terminado seu testemunho, a besta que sai do abismo fará guerra com eles, os vencerá e os matará. (Abyssos g12)
8 Maiti zao zitabaki katika barabara za mji mkuu ambapo Bwana wao alisulubiwa; jina la kupanga la mji huo ni Sodoma au Misri.
Seus corpos mortos estarão na rua da grande cidade, que espiritualmente é chamada Sodoma e Egito, onde também seu Senhor foi crucificado.
9 Watu wa kila kabila, lugha, taifa na rangi wataziangalia maiti hizo kwa muda wa siku tatu na nusu, na hawataruhusu zizikwe.
Entre os povos, tribos, línguas e nações, as pessoas olharão seus cadáveres por três dias e meio, e não permitirão que seus corpos mortos sejam depositados em um túmulo.
10 Watu waishio duniani watafurahia kifo cha hao wawili. Watafanya sherehe na kupelekeana zawadi maana manabii hawa wawili walikuwa wamewasumbua mno watu wa dunia.
Aqueles que habitam sobre a terra se alegrarão por eles, e ficarão felizes. Darão presentes um ao outro, porque estes dois profetas atormentaram aqueles que habitam sobre a terra.
11 Lakini baada ya zile siku tatu na nusu pumzi ya uhai kutoka kwa Mungu iliwaingia, nao wakasimama; wote waliowaona wakaingiwa na hofu kuu.
Depois dos três dias e meio, o sopro de vida de Deus entrou neles, e eles ficaram de pé. Um grande medo caiu sobre aqueles que os viram.
12 Kisha hao manabii wawili wakasikia sauti kubwa kutoka mbinguni ikiwaambia, “Njoni hapa juu!” Nao wakapanda juu mbinguni katika wingu, maadui wao wakiwa wanawatazama.
Ouvi uma voz alta do céu dizendo a eles: “Subam aqui”! Eles subiram ao céu em uma nuvem, e seus inimigos os viram.
13 Wakati huohuo, kukatokea tetemeko kubwa la ardhi, sehemu moja ya kumi ya ardhi ikaharibiwa. Watu elfu saba wakauawa kwa tetemeko hilo la ardhi. Watu waliosalia wakaogopa sana, wakamtukuza Mungu wa mbinguni.
Naquele dia, houve um grande terremoto, e um décimo da cidade caiu. Sete mil pessoas morreram no terremoto, e as demais ficaram aterrorizadas e deram glória ao Deus do céu.
14 Maafa ya pili yamepita; lakini tazama! Maafa ya tatu yanafuata hima.
O segundo infortúnio é passado. Eis que o terceiro infortúnio vem rapidamente.
15 Kisha malaika wa saba akapiga tarumbeta yake. Na sauti kuu zikasikika mbinguni zikisema, “Sasa utawala juu ya ulimwengu ni wa Bwana wetu na Kristo wake. Naye atatawala milele na milele!” (aiōn g165)
O sétimo anjo soou, e grandes vozes no céu se seguiram, dizendo: “O reino do mundo se tornou o Reino de nosso Senhor e de seu Cristo”. Ele reinará para todo o sempre”. (aiōn g165)
16 Kisha wale wazee ishirini na wanne walioketi mbele ya Mungu katika viti vyao vya enzi, wakaanguka kifudifudi, wakamwabudu Mungu,
Os vinte e quatro anciãos, que se sentam em seus tronos diante do trono de Deus, caíram sobre seus rostos e adoraram a Deus,
17 wakisema: “Bwana Mungu Mwenye uwezo, uliyeko na uliyekuwako! Tunakushukuru, maana umetumia nguvu yako kuu ukaanza kutawala!
dizendo: “Nós lhe damos graças, Senhor Deus, o Todo-Poderoso, aquele que é e que foi, porque você tomou seu grande poder e reinou.
18 Watu wa mataifa waliwaka hasira, maana wakati wa ghadhabu yako umefika, wakati wa kuwahukumu wafu. Ndio wakati wa kuwatuza watumishi wako manabii, watu wako na wote wanaolitukuza jina lako, wakubwa kwa wadogo. Ni wakati wa kuwaangamiza wale wanaoangamiza dunia.”
As nações se enfureceram, e veio a tua ira, assim como a hora de julgar os mortos, e de dar a teus servos os profetas, sua recompensa, assim como aos santos e aos que temem teu nome, aos pequenos e aos grandes, e de destruir os que destroem a terra”.
19 Hekalu la Mungu mbinguni likafunguliwa, na Sanduku la Agano lake likaonekana Hekaluni mwake. Kisha kukatokea umeme, sauti, ngurumo, tetemeko la ardhi, na mvua kubwa ya mawe.
O templo de Deus que está no céu foi aberto, e a arca do pacto do Senhor foi vista em seu templo. Seguiram-se relâmpagos, sons, trovões, um terremoto e um grande granizo.

< Ufunuo 11 >