< Filemoni 1 >

1 Mimi Paulo, mfungwa kwa ajili ya Kristo Yesu, na ndugu Timotheo, ninakuandikia wewe Filemoni mpendwa, mfanyakazi mwenzetu
Pablo, prisionero de Jesucristo, y Timoteo nuestro hermano, a Filemón, nuestro querido ayudante en la fe,
2 na kanisa linalokutana nyumbani kwako, na wewe dada Afia, na askari mwenzetu Arkupo.
Y a Apia, nuestra hermana, y a Arquipo, nuestro hermano en el ejército de Dios, y a la iglesia en tu casa.
3 Tunawatakieni neema na amani kutoka kwa Mungu Baba yetu, na kwa Bwana yesu Kristo.
Gracia y paz a ustedes de parte de Dios nuestro Padre y del Señor Jesucristo.
4 Kila wakati ninaposali nakukumbuka wewe Filemoni, na kumshukuru Mungu
Alabaré a Dios en todo tiempo y oraré por ti,
5 maana nasikia habari za imani yako kwa Bwana wetu Yesu na upendo wako kwa watu wote wa Mungu.
Escuchando el amor y la fe que tienes para el Señor Jesús y para todos los santos;
6 Naomba ili imani hiyo unayoshiriki pamoja nasi ikuwezeshe kuwa na ujuzi mkamilifu zaidi wa baraka zote tunazopata katika kuungana kwetu na Kristo.
Para que la fe que tienes en común con ellos obre con poder, en el conocimiento de todo lo bueno que hay en ti, para Cristo.
7 Ndugu, upendo wako yameniletea furaha kubwa na kunipa moyo sana! Nawe umeichangamsha mioyo ya watu wa Mungu.
Porque tuve gran gozo y consuelo en tu amor, porque los corazones de los santos se han fortalecido por medio de ti, hermano.
8 Kwa sababu hiyo, ningeweza, kwa uhodari kabisa, nikiwa ndugu yako katika Kristo, kukuamuru ufanye unachopaswa kufanya.
Y así, aunque podría, en nombre de Cristo, darte órdenes de hacer lo correcto,
9 Lakini kwa sababu ya upendo, ni afadhali zaidi nikuombe. Nafanya hivi ingawa mimi ni Paulo, balozi wa Kristo Yesu, na sasa pia mfungwa kwa ajili yake.
Aún así, por amor, en lugar de una orden, te hago una petición, yo, Pablo, un anciano y ahora un prisionero de Cristo Jesús.
10 Basi, ninalo ombi moja kwako kuhusu mwanangu Onesimo, ambaye ni mwanangu katika Kristo kwani nimekuwa baba yake nikiwa kifungoni.
Mi petición es para mi hijo Onésimo, el hijo de mis cadenas,
11 Ni Onesimo yuleyule ambaye wakati mmoja alikuwa hakufai kitu, lakini sasa ananifaa mimi na wewe pia.
Que en el pasado no te servía de nada, pero que ahora te beneficia a ti y a mí:
12 Sasa namrudisha kwako, naye ni kama moyo wangu mimi mwenyewe.
A quien he enviado a ti, tu, pues, recíbele como a mi mismo:
13 Ningependa akae nami hapa anisaidie badala yako wakati niwapo kifungoni kwa sababu ya Habari Njema.
Aunque mi deseo era mantenerlo conmigo, ser mi siervo en las cadenas de las buenas nuevas, en tu lugar:
14 Lakini sitafanya chochote bila kibali chako. Sipendi kukulazimisha unisaidie, kwani wema wako unapaswa kutokana na hiari yako wewe mwenyewe na si kwa kulazimika.
Pero sin tu aprobación no haría nada; para que tus buenas obras no sean forzadas, sino hechas libremente desde tu corazón.
15 Labda Onesimo aliondoka kwako kwa kitambo tu, kusudi uweze tena kuwa naye daima. (aiōnios g166)
Porque es posible que por esta razón él se separó de ti por un tiempo, para que puedas recibirlo para siempre; (aiōnios g166)
16 Na sasa yeye si mtumwa tu, ila ni bora zaidi ya mtumwa: yeye ni ndugu yetu mpenzi. Na wa maana sana kwangu mimi, na kwako atakuwa wa maana zaidi kama mtumwa na kama ndugu katika Bwana.
Ya no como siervo, sino más que como siervo, como hermano, muy querido para mí especialmente, pero mucho más para ti, tanto en la carne como en el Señor.
17 Basi, ikiwa wanitambua mimi kuwa mwenzako, mpokee tena kama vile ungenipokea mimi mwenyewe.
Si luego me llevas a ser tu amigo y hermano, acéptalo como a mí mismo.
18 Kama alikuwa amekukosea kitu, au alikuwa na deni lako, basi, unidai mimi.
Si él te ha hecho algo malo o está en deuda contigo por algo, póngalo en mi cuenta.
19 Naandika jambo hili kwa mkono wangu mwenyewe: Mimi Paulo nitalipa! (Tena sina haja ya kusema kwamba wewe unalo deni kwangu la nafsi yako.)
Yo, Pablo, escribiéndolo yo mismo, te digo: te pagaré; y no te digo que estás en deuda conmigo, por tu propia vida.
20 Haya, basi, ndugu yangu, nifanyie jambo hilo kwa ajili ya jina la Bwana; burudisha moyo wangu kama ndugu katika Kristo.
Así que hermano, como cristiano se generoso conmigo en él Señor: consuela mi corazón en Cristo.
21 Naandika nikitumaini kwamba utanikubalia ombi langu; tena najua kwamba utafanya hata zaidi ya haya ninayokuomba.
Estoy seguro de que harás mi deseo, te escribo, sabiendo que harás incluso más de lo que digo.
22 Pamoja na hayo, nitayarishie chumba kwani natumaini kwamba kwa sala zenu, Mungu atanijalia niwatembeleeni.
Y prepárame una habitación; porque espero que a través de sus oraciones pueda venir a ustedes.
23 Epafra, mfungwa mwenzangu kwa ajili ya Kristo Yesu, anakusalimu.
Epafras, mi hermano, prisionero en Cristo Jesús, te envía saludos;
24 Nao akina Marko, Aristarko, Dema na Luka, wafanyakazi wenzangu, wanakusalimu.
Y también Marcos, Aristarco, Demas y Lucas, mis hermanos trabajadores.
25 Nawatakieni ninyi nyote neema ya Bwana wetu Yesu Kristo.
La gracia de nuestro Señor Jesucristo sea derramada sobre ustedes. Amen.

< Filemoni 1 >