< Mathayo 8 >

1 Yesu aliposhuka kutoka mlimani, makundi mengi ya watu yalimfuata.
Quand il descendit de la montagne, de grandes troupes le suivirent.
2 Basi, akaja mtu mmoja mwenye ukoma, akamsujudia akisema, “Bwana, ukitaka, waweza kunitakasa!”
Survint un lépreux qui s'approcha et se prosterna. devant lui: «Seigneur, dit-il, si tu le veux, tu peux me guérir.»
3 Yesu akanyosha mkono wake, akamgusa na kusema, “Nataka! Takasika.” Mara huyo mtu akapona ukoma wake.
Jésus étendit la main, le toucha et dit: «Je le veux, sois guéri»; et à l'instant il fut guéri de sa lèpre.
4 Kisha Yesu akamwambia, “Sikiliza, usimwambie mtu yeyote, ila nenda ukajionyeshe kwa kuhani, na ukatoe sadaka iliyoamriwa na Mose kuwathibitishia kwamba umepona.”
Jésus ajouta: «Garde-toi de parler de ceci à personne; mais va te montrer au prêtre et offre le don prescrit par Moïse; que ce leur soit un témoignage.»
5 Yesu alipokuwa anaingia mjini Kafarnaumu, ofisa mmoja Mroma alimwendea, akamsihi
Comme il entrait dans Capharnaüm, un centurion s'approcha de lui, lui adressant cette prière:
6 akisema, “Mheshimiwa, mtumishi wangu amelala nyumbani, mgonjwa wa kupooza na anaumwa sana.”
Seigneur, mon serviteur est dans ma maison, étendu sur son lit, paralytique et en proie à de cruelles souffrances.»
7 Yesu akamwambia, “Nitakuja kumponya.”
Jésus lui répondit: «J'irai, et je le guérirai.»
8 Huyo ofisa akamwambia, “Mheshimiwa, sistahili uingie nyumbani mwangu. Lakini sema tu neno, na mtumishi wangu atapona.
Alors le centurion reprit: «Seigneur, je ne suis pas digne que tu entres sous mon toit, mais donne seulement un ordre et mon serviteur sera guéri.
9 Maana, hata mimi niliye mtu chini ya mamlaka ya wengine, ninao askari chini yangu. Namwambia mmoja, Nenda! naye huenda; na mwingine, Njoo! naye huja; na mtumishi wangu, Fanya kitu hiki! naye hufanya.”
Car moi (qui ne suis pourtant qu'un subordonné) j'ai sous mes ordres des soldats, et si je dis à l'un: «va-t'en» — il s'en va; à l'autre: «viens» — il vient; à mon esclave: «fais cela — il le fait.»
10 Yesu aliposikia hayo, alistaajabu, akawaambia watu waliokuwa wanamfuata, “Kweli nawaambieni, sijapata kumwona mtu yeyote katika Israeli aliye na imani kama hii.
Jésus fut dans l'admiration de ce langage; et s'adressant à ceux qui le suivaient: «Je vous le dis en vérité, chez personne, même en Israël, je n'ai trouvé une foi aussi grande?
11 Basi, nawaambieni kwamba watu wengi watakuja kutoka mashariki na magharibi, nao wataketi karamuni pamoja na Abrahamu, Isaka na Yakobo katika Ufalme wa mbinguni.
Je vous déclare que plusieurs viendront de l'Orient et de l'Occident et se mettront à table avec Abraham, Isaac et Jacob dans le Royaume des cieux,
12 Lakini wale ambao wangalipaswa kuwa katika Ufalme huo watatupwa nje, gizani, ambako watalia na kusaga meno.”
tandis que les fils du Royaume seront jetés dehors dans les ténèbres. Là seront les pleurs et le grincement des dents.»
13 Kisha Yesu akamwambia huyo ofisa Mroma, “Nenda nyumbani; na iwe kama ulivyoamini.” Na mtumishi wake akapona saa ileile.
Ensuite Jésus dit au centurion; «Va et qu'il te soit fait comme tu as cru.» Et, à cette heure même, le serviteur fut guéri.
14 Yesu alifika nyumbani kwa Petro, akamkuta mama mkwe wa Petro amelala kitandani, ana homa kali.
Arrivé à la maison de Pierre, Jésus vit la belle-mère de celui-ci, couchée; elle avait la fièvre.
15 Basi, Yesu akamgusa huyo mama mkono, na homa ikamwacha; akasimama, akamtumikia.
Il lui toucha la main et la fièvre disparut; aussi se leva-t-elle et se mit-elle à les servir.
16 Ilipokuwa jioni, walimletea watu wengi waliokuwa wamepagawa na pepo; naye, kwa kusema neno tu, akawafukuza hao pepo. Aliwaponya pia watu wote waliokuwa wagonjwa.
Le soir venu, on lui apporta beaucoup de démoniaques, et d'un mot il chassait les Esprits. Il guérit aussi tous ceux qui étaient malades,
17 Alifanya hivyo ili yale aliyosema nabii Isaya yatimie: “Yeye mwenyewe ameondoa udhaifu wetu, ameyachukua magonjwa yetu.”
afin que fût accompli ce qu'avait annoncé le prophète Ésaïe disant: «C'est lui qui a pris nos infirmités et porté nos maladies.»
18 Yesu alipoona kundi la watu limemzunguka, aliwaamuru wanafunzi wake waende ng'ambo ya ziwa.
Voyant de nombreuses troupes autour de lui, Jésus donna l'ordre de passer sur l'autre rive.
19 Mwalimu mmoja wa Sheria akamwendea, akamwambia, “Mwalimu, mimi nitakufuata kokote uendako.”
Alors un Scribe, s'avançant, lui dit: «Maître, je te suivrai partout où tu iras.»
20 Yesu akamjibu, “Mbweha wana mapango, na ndege wana viota; lakini Mwana wa Mtu hana mahali pa kupumzikia.”
Jésus lui répond: «Les renards ont des tanières et les oiseaux du ciel ont des nids; mais le Fils de l'homme n'a pas où reposer sa tête.»
21 Kisha mtu mwingine miongoni mwa wanafunzi wake akamwambia, “Bwana, niruhusu kwanza niende nikamzike baba yangu.”
«Seigneur, lui dit un autre des disciples, permets-moi d'aller d'abord ensevelir mon père.»
22 Lakini Yesu akamwambia, “Nifuate! Waache wafu wazike wafu wao.”
«Suis-moi! Lui répond Jésus, et laisse les morts ensevelir leurs morts!»
23 Yesu alipanda mashua, na wanafunzi wake wakaenda pamoja naye.
Il monta dans la barque, suivi de ses disciples.
24 Ghafla, dhoruba kali ikatokea ziwani, hata mawimbi yakaanza kuifunika mashua. Yesu alikuwa amelala usingizi.
Soudain une grande tempête s'éleva sur la mer, à tel point que la barque était couverte par les vagues. Lui, il dormait.
25 Wanafunzi wakamwendea, wakamwamsha wakisema, “Bwana, tuokoe, tunaangamia!”
Les disciples s'approchèrent de lui et le réveillèrent. «Sauve-nous, Seigneur, lui dirent-ils, nous périssons!»
26 Yesu akawaambia, “Enyi watu wenye imani haba; mbona mnaogopa?” Basi, akainuka, akazikemea pepo na mawimbi; kukawa shwari kabisa.
Il leur répondit: «Pourquoi vous effrayez-vous, hommes de peu de foi?» Alors il se leva, fit des menaces aux vents et à la mer, et il se fit un grand calme.
27 Watu wakashangaa, wakasema, “Ni mtu wa namna gani huyu? Hata pepo na mawimbi vinamtii!”
Ces hommes dirent alors remplis d'admiration: «Qui est-il pour que lui obéissent et les vents et la mer?»
28 Yesu alifika katika nchi ya Wagerasi, ng'ambo ya ziwa, na huko watu wawili waliopagawa na pepo wakakutana naye wakitokea makaburini. Watu hawa walikuwa wenye kutisha mno, hata hakuna mtu aliyethubutu kupita katika njia hiyo.
Quand il fut arrivé à l'autre bord, dans le pays des Gadaréniens, vinrent à sa rencontre deux démoniaques, sortant des sépulcres. Ils étaient si dangereux que personne n'osait passer par ce chemin.
29 Nao wakaanza kupiga kelele, “Una shauri gani nasi, wewe Mwana wa Mungu? Je, umekuja kututesa kabla ya wakati wake?”
Qu'y a-t-il entre nous et toi, fils de Dieu?» se mirent-ils à crier. «Es-tu venu ici pour nous torturer avant le temps.»
30 Karibu na mahali hapo kulikuwa na nguruwe wengi wakichungwa.
Or, il y avait, dans l'éloignement, un nombreux troupeau de pourceaux qui paissaient.
31 Basi, hao pepo wakamsihi, “Ikiwa utatutoa, basi uturuhusu tuwaingie nguruwe wale.”
Les démons lui adressaient cette demande: «Si tu nous chasses, envoie-nous dans ce troupeau de pourceaux.»
32 Yesu akawaambia, “Haya, nendeni.” Hapo wakawatoka watu hao, wakawaingia nguruwe. Kundi lote la nguruwe likaporomoka kwenye ule mteremko mkali, likatumbukia ziwani; nguruwe wote wakafa maji.
«Allez!» leur dit Jésus. Alors ils partirent et entrèrent dans les pourceaux; et voilà que, d'une course impétueuse, le troupeau tout entier se précipita dans la mer et périt dans les flots.
33 Wachungaji wa hao nguruwe walikimbia, wakaenda mjini. Huko walitoa habari zote na mambo yaliyowapata wale watu waliokuwa wamepagawa.
Les gardeurs prirent la fuite; ils allèrent à la ville tout raconter, et ce qui était arrivé aux démoniaques.
34 Basi, watu wote katika mji ule walitoka, wakamwendea Yesu; na walipomwona, wakamsihi aondoke katika nchi yao.
Là dessus, la ville entière sortit au devant de Jésus, et, quand ces gens le virent ils le prièrent de s'éloigner de leur pays.

< Mathayo 8 >