< Mathayo 8 >
1 Yesu aliposhuka kutoka mlimani, makundi mengi ya watu yalimfuata.
耶穌從山上下來,有許多群眾跟隨衪。
2 Basi, akaja mtu mmoja mwenye ukoma, akamsujudia akisema, “Bwana, ukitaka, waweza kunitakasa!”
看,有一個癩病人前來叩拜耶穌說:「主!你若願意,就能潔淨我。」
3 Yesu akanyosha mkono wake, akamgusa na kusema, “Nataka! Takasika.” Mara huyo mtu akapona ukoma wake.
耶穌就伸手撫摸他說:「我願意,你潔淨了吧 !」他的癩病立刻就潔淨了。
4 Kisha Yesu akamwambia, “Sikiliza, usimwambie mtu yeyote, ila nenda ukajionyeshe kwa kuhani, na ukatoe sadaka iliyoamriwa na Mose kuwathibitishia kwamba umepona.”
耶穌對他說:「小心,不要對任何人說!但去叫司祭檢驗你,獻上梅瑟所規定的禮物,給他們當作證據。」
5 Yesu alipokuwa anaingia mjini Kafarnaumu, ofisa mmoja Mroma alimwendea, akamsihi
耶穌進了葛法翁,有一位百夫長來到衪跟前,求衪說:
6 akisema, “Mheshimiwa, mtumishi wangu amelala nyumbani, mgonjwa wa kupooza na anaumwa sana.”
「主!我的僕人癱瘓了;躺在家裏;疼痛得很厲害。」
7 Yesu akamwambia, “Nitakuja kumponya.”
耶穌對他說:「我去治好他。」
8 Huyo ofisa akamwambia, “Mheshimiwa, sistahili uingie nyumbani mwangu. Lakini sema tu neno, na mtumishi wangu atapona.
百夫長答說:「主!我不堪當你到我舍下來,你只要說一句話,我的僕人就會好的。
9 Maana, hata mimi niliye mtu chini ya mamlaka ya wengine, ninao askari chini yangu. Namwambia mmoja, Nenda! naye huenda; na mwingine, Njoo! naye huja; na mtumishi wangu, Fanya kitu hiki! naye hufanya.”
因為我雖是屬人權下的人,佰是我也巾士兵屬我權下;我對這個說:你去,他就去;對另一個說:你來,他就來;對我的奴僕說:你作這個,他就作。」
10 Yesu aliposikia hayo, alistaajabu, akawaambia watu waliokuwa wanamfuata, “Kweli nawaambieni, sijapata kumwona mtu yeyote katika Israeli aliye na imani kama hii.
耶穌聽了,非常詑異,就對跟隨的人說:「我實在告訴你們:在以色列我從未見過一個人,有這樣大的信心。
11 Basi, nawaambieni kwamba watu wengi watakuja kutoka mashariki na magharibi, nao wataketi karamuni pamoja na Abrahamu, Isaka na Yakobo katika Ufalme wa mbinguni.
我給你們說:將有許多人從東方和西,方來,同亞巴郎、依撒各和亞各伯在天國裏一起坐席;
12 Lakini wale ambao wangalipaswa kuwa katika Ufalme huo watatupwa nje, gizani, ambako watalia na kusaga meno.”
本國的子民,反要被驅逐到外邊黑暗裏;那裏要有哀號和切齒。」
13 Kisha Yesu akamwambia huyo ofisa Mroma, “Nenda nyumbani; na iwe kama ulivyoamini.” Na mtumishi wake akapona saa ileile.
耶穌遂對百夫長說:「你回去,就照你所信的,給你成就吧!」僕人就在那時痊癒了。
14 Yesu alifika nyumbani kwa Petro, akamkuta mama mkwe wa Petro amelala kitandani, ana homa kali.
耶穌來到伯多碌家裏,看伯多碌的岳母躺著發燒,
15 Basi, Yesu akamgusa huyo mama mkono, na homa ikamwacha; akasimama, akamtumikia.
就摸了她的手,熱症就從她身上退了。她便起來,伺候衪。
16 Ilipokuwa jioni, walimletea watu wengi waliokuwa wamepagawa na pepo; naye, kwa kusema neno tu, akawafukuza hao pepo. Aliwaponya pia watu wote waliokuwa wagonjwa.
到了晚上,人們給衪送來了許多附魔的人,衪一句話就驅逐了惡神;治好了一切有的人。
17 Alifanya hivyo ili yale aliyosema nabii Isaya yatimie: “Yeye mwenyewe ameondoa udhaifu wetu, ameyachukua magonjwa yetu.”
這樣,就應驗了那藉依撒依亞先知所說的話:『衪承受我們的脆弱,擔荷了我你的疾病。』
18 Yesu alipoona kundi la watu limemzunguka, aliwaamuru wanafunzi wake waende ng'ambo ya ziwa.
耶穌看見許多群眾圍著自己,就吩咐往對岸去。
19 Mwalimu mmoja wa Sheria akamwendea, akamwambia, “Mwalimu, mimi nitakufuata kokote uendako.”
有一位經師前來,對衪說:「師傅,你不論往那裏去,我要跟隨你。」
20 Yesu akamjibu, “Mbweha wana mapango, na ndege wana viota; lakini Mwana wa Mtu hana mahali pa kupumzikia.”
耶穌給他說:「狐狸有穴,天上飛鳥有巢,但是人子卻沒有枕頭的地方。」
21 Kisha mtu mwingine miongoni mwa wanafunzi wake akamwambia, “Bwana, niruhusu kwanza niende nikamzike baba yangu.”
門徒中有一個對衪說:「主,請許我先去埋葬我的父親。」
22 Lakini Yesu akamwambia, “Nifuate! Waache wafu wazike wafu wao.”
耶穌對他說:「你跟隨我罷!任憑死人去埋葬死人!」
23 Yesu alipanda mashua, na wanafunzi wake wakaenda pamoja naye.
耶穌上了船,他的門徒跟隨著牠。
24 Ghafla, dhoruba kali ikatokea ziwani, hata mawimbi yakaanza kuifunika mashua. Yesu alikuwa amelala usingizi.
忽然海裏起了大震盪,以致那船為浪所掩蓋,耶穌卻睡著了。
25 Wanafunzi wakamwendea, wakamwamsha wakisema, “Bwana, tuokoe, tunaangamia!”
他們遂前來喚醒牠說:「主!救命啊!我們要喪亡了。」
26 Yesu akawaambia, “Enyi watu wenye imani haba; mbona mnaogopa?” Basi, akainuka, akazikemea pepo na mawimbi; kukawa shwari kabisa.
耶穌對他捫說:「小信德的人啊!你們為什麼膽怯﹖」就起來叱責風和海,遂大為平靜。
27 Watu wakashangaa, wakasema, “Ni mtu wa namna gani huyu? Hata pepo na mawimbi vinamtii!”
那些人驚訝說:「這是怎麼的一個人呢﹖竟連風和海也聽從牠!」
28 Yesu alifika katika nchi ya Wagerasi, ng'ambo ya ziwa, na huko watu wawili waliopagawa na pepo wakakutana naye wakitokea makaburini. Watu hawa walikuwa wenye kutisha mno, hata hakuna mtu aliyethubutu kupita katika njia hiyo.
耶穌來到對岸加達辣人的地方,有兩個附魔的人從墳墓裏走出,向牠走來;他們異常兇猛,以致沒有人能從那條路上經過。
29 Nao wakaanza kupiga kelele, “Una shauri gani nasi, wewe Mwana wa Mungu? Je, umekuja kututesa kabla ya wakati wake?”
他門喊說:「天主子,我們與你有什麼相干﹖時期還沒有到,你就來這裏苦害我捫嗎﹖」
30 Karibu na mahali hapo kulikuwa na nguruwe wengi wakichungwa.
離他們很遠,有一大群豬正在牧放。
31 Basi, hao pepo wakamsihi, “Ikiwa utatutoa, basi uturuhusu tuwaingie nguruwe wale.”
魔鬼懇求耶穌說:「你若驅逐我捫,就趕我們進入豬群吧!」
32 Yesu akawaambia, “Haya, nendeni.” Hapo wakawatoka watu hao, wakawaingia nguruwe. Kundi lote la nguruwe likaporomoka kwenye ule mteremko mkali, likatumbukia ziwani; nguruwe wote wakafa maji.
耶穌對他們說:「去吧!」魔鬼就出來進入豬內;忽然全群豬從山崖上直衝入海,死在水裹。
33 Wachungaji wa hao nguruwe walikimbia, wakaenda mjini. Huko walitoa habari zote na mambo yaliyowapata wale watu waliokuwa wamepagawa.
放豬的便逃走,來到城裏,把這一切和附魔人的事都報告了。
34 Basi, watu wote katika mji ule walitoka, wakamwendea Yesu; na walipomwona, wakamsihi aondoke katika nchi yao.
全城的人就出來會見耶穌,一見了衪,就求衪離開他們的境界。