< Mathayo 6 >

1 “Jihadharini msije mkafanya matendo yenu mema mbele ya watu kusudi mwonekane nao. La sivyo, Baba yenu aliye mbinguni hatawapeni tuzo.
“Take heed not to do your kindness before men, to be seen by them, and if not—you have no reward from your Father who [is] in the heavens;
2 “Basi, unapomsaidia maskini, usijitangaze. Usifanye kama wanafiki wafanyavyo katika masunagogi na njiani ili watu wawasifu. Kweli nawaambieni, hao wamekwisha pata tuzo lao.
whenever, therefore, you may do kindness, you may not sound a trumpet before you as the hypocrites do, in the synagogues, and in the streets, that they may have glory from men; truly I say to you, they have their reward!
3 Lakini wewe unapomsaidia maskini, fanya hivyo kwamba hata rafiki yako asijue ufanyalo.
But you, doing kindness, do not let your left hand know what your right hand does,
4 Toa msaada wako kwa siri, na Baba yako aonaye yaliyofichika, atakutuza.
that your kindness may be in secret, and your Father who is seeing in secret will reward you Himself.
5 “Mnaposali, msifanye kama wanafiki. Wao hupenda kusimama na kusali katika masunagogi na katika pembe za njia ili watu wawaone. Kweli nawaambieni, hao wamekwisha pata tuzo lao.
And when you may pray, you will not be as the hypocrites, because they cherish to pray standing in the synagogues and in the corners of the broad places, that they may be seen of men; truly I say to you that they have their reward.
6 Lakini wewe unaposali, ingia chumbani mwako, funga mlango, kisha umwombe Baba yako asiyeonekana. Naye Baba yako aonaye yaliyofichika, atakutuza.
But you, when you may pray, go into your chamber, and having shut your door, pray to your Father who [is] in secret, and your Father who is seeing in secret will reward you.
7 “Mnaposali, msipayuke maneno kama watu wasiomjua Mungu. Wao hudhani kwamba Mungu atawasikiliza ati kwa sababu ya maneno mengi.
And—praying—you may not use vain repetitions like the nations, for they think that in their speaking much they will be heard,
8 Msiwe kama wao. Baba yenu anajua mnayoyahitaji hata kabla ya kumwomba.
therefore do not be like them, for your Father knows those things that you have need of before your asking Him;
9 Basi, hivi ndivyo mnavyopaswa kusali: Baba yetu uliye mbinguni: Jina lako litukuzwe.
therefore pray thus: Our Father who [is] in the heavens, hallowed be Your Name.
10 Ufalme wako ufike. Utakalo lifanyike duniani kama mbinguni.
Your kingdom come, Your will come to pass, as in Heaven also on the earth.
11 Utupe leo chakula chetu tunachohitaji.
Give us today our appointed bread.
12 Utusamehe makosa yetu, kama nasi tunavyowasamehe waliotukosea.
And forgive us our debts, as we also forgive our debtors.
13 Usitutie katika majaribu, lakini utuokoe na yule Mwovu. is Baadhi ya makala za zamani zina; Kwa kuwa ufalme ni wako, na nguvu, na utukufu, hata milele. Amina.
And may You not lead us into temptation, but deliver us from the evil [one], because Yours is the kingdom, and the power, and the glory—for all ages. Amen.
14 “Maana mkiwasamehe watu makosa yao, Baba yenu wa mbinguni atawasamehe ninyi pia.
For if you may forgive men their trespasses He also will forgive you—your Father who [is] in the heavens;
15 Lakini msipowasamehe watu makosa yao, naye Baba yenu hatawasamehe ninyi makosa yenu.
but if you may not forgive men their trespasses, neither will your Father forgive your trespasses.
16 “Mnapofunga, msiwe na huzuni kama wanafiki. Wao hukunja nyuso zao wapate kuonekana na watu kuwa wanafunga. Nawaambieni hakika, hao wamekwisha pata tuzo lao.
And when you may fast, do not be as the hypocrites, of sour countenances, for they disfigure their faces, that they may appear to men fasting; truly I say to you that they have their reward.
17 Wewe lakini unapofunga, paka kichwa chako mafuta, nawa uso wako,
But you, fasting, anoint your head, and wash your face,
18 ili mtu yeyote asijue kwamba unafunga, ila ujulikane tu kwa Baba yako asiyeonekana. Naye Baba yako aonaye yaliyofichika atakutuza.
that you may not appear to men fasting, but to your Father who [is] in secret, and your Father, who is seeing in secret, will reward you.
19 “Msijiwekee hazina hapa duniani ambako nondo na kutu huharibu, na wezi huingia na kuiba.
Do not treasure up to yourselves treasures on the earth, where moth and rust disfigure, and where thieves break through and steal,
20 Jiwekeeni hazina mbinguni ambako nondo na kutu hawawezi kuiharibu, wala wezi hawaingii wakaiba.
but treasure up to yourselves treasures in Heaven, where neither moth nor rust disfigure, and where thieves do not break through nor steal,
21 Maana pale ilipo hazina yako, ndipo pia utakapokuwa moyo wako.
for where your treasure is, there will your heart be also.
22 “Jicho ni taa ya mwili. Kama jicho lako ni zima, mwili wako wote utakuwa katika mwanga.
The lamp of the body is the eye, if, therefore, your eye may be perfect, all your body will be enlightened,
23 Lakini ikiwa jicho lako ni bovu, mwili wako wote utakuwa katika giza. Basi, ikiwa mwanga ulioko ndani yako ni giza, basi, hilo ni giza la kutisha mno.
but if your eye may be evil, all your body will be dark; if, therefore, the light that [is] in you is darkness—the darkness, how great!
24 “Hakuna mtu awezaye kutumikia mabwana wawili. Maana atamchukia mmoja na kumpenda huyo wa pili; au ataambatana na mmoja na kumdharau huyo mwingine. Hamwezi kumtumikia Mungu na mali pamoja.
None is able to serve two lords, for either he will hate the one and love the other, or he will hold to the one, and despise the other; you are not able to serve God and wealth.
25 “Ndiyo maana nawaambieni, msiwe na wasiwasi juu ya chakula na kinywaji mnavyohitaji ili kuishi, wala juu ya mavazi mnayohitaji kwa ajili ya miili yenu. Je, maisha ni chakula tu au zaidi? Na mwili, je, si zaidi ya mavazi?
Because of this I say to you, do not be anxious for your life, what you may eat, and what you may drink, nor for your body, what you may put on. Is not life more than nourishment, and the body than clothing?
26 Waangalieni ndege wa mwituni: hawapandi, hawavuni, wala hawana ghala yoyoye. Hata hivyo, Baba yenu wa mbinguni huwalisha. Je, ninyi si wa thamani kuliko hao?
Look to the birds of the sky, for they do not sow, nor reap, nor gather into storehouses, and your heavenly Father nourishes them; are you not much better than they?
27 Ni nani miongoni mwenu kwa kuwa na wasiwasi sana anaweza kuuongeza muda wa maisha yake?
And who of you, being anxious, is able to add to his age one cubit?
28 “Na kuhusu mavazi, ya nini kuwa na wasiwasi? Tazameni maua ya porini jinsi yanavyostawi. Hayafanyi kazi wala hayasokoti.
And why are you anxious about clothing? Consider well the lilies of the field; how do they grow? They do not labor, nor do they spin;
29 Lakini nawaambieni, hata Solomoni mwenyewe na fahari zake zote hakupata kuvikwa vizuri kama ua mojawapo.
and I say to you that not even Solomon in all his glory was clothed as one of these.
30 Ikiwa basi Mungu hulivika hivyo jani la shambani ambalo leo liko na kesho latupwa motoni, je, hatafanya zaidi kwenu ninyi? Enyi watu wenye imani haba!
And if the herb of the field, that today is, and tomorrow is cast into the furnace, God so clothes—not much more you, O you of little faith?
31 “Basi, msiwe na wasiwasi: Tutakula nini, tutakunywa nini, tutavaa nini!
Therefore you may not be anxious, saying, What may we eat? Or, What may we drink? Or, [With] what may we be clothed?
32 Maana hayo yote yanahangaikiwa na watu wasiomjua Mungu. Baba yenu wa mbinguni anajua kwamba mnahitaji vitu hivyo vyote.
For the nations seek for all these, for your heavenly Father knows that you have need of all these;
33 Bali, zingatieni kwanza Ufalme wa Mungu na matakwa yake, na hayo mengine yote mtapewa kwa ziada.
but seek first the Kingdom of God and His righteousness, and all these will be added to you.
34 Basi, msiwe na wasiwasi juu ya kesho; kesho inayo yake. Matatizo ya siku moja yanawatosheni kwa siku hiyo.
Therefore do not be anxious for tomorrow, for tomorrow will be anxious for its own things; sufficient for the day [is] the evil of it.”

< Mathayo 6 >