< Mathayo 6 >
1 “Jihadharini msije mkafanya matendo yenu mema mbele ya watu kusudi mwonekane nao. La sivyo, Baba yenu aliye mbinguni hatawapeni tuzo.
Take heed that all of you do not your alms before men, to be seen of them: otherwise all of you have no reward of your Father which is in heaven.
2 “Basi, unapomsaidia maskini, usijitangaze. Usifanye kama wanafiki wafanyavyo katika masunagogi na njiani ili watu wawasifu. Kweli nawaambieni, hao wamekwisha pata tuzo lao.
Therefore when you do your alms, do not sound a trumpet before you, as the hypocrites do in the synagogues and in the streets, that they may have glory of men. Verily I say unto you, They have their reward.
3 Lakini wewe unapomsaidia maskini, fanya hivyo kwamba hata rafiki yako asijue ufanyalo.
But when you do alms, let not your left hand know what your right hand does:
4 Toa msaada wako kwa siri, na Baba yako aonaye yaliyofichika, atakutuza.
That your alms may be in secret: and your Father which sees in secret himself shall reward you openly.
5 “Mnaposali, msifanye kama wanafiki. Wao hupenda kusimama na kusali katika masunagogi na katika pembe za njia ili watu wawaone. Kweli nawaambieni, hao wamekwisha pata tuzo lao.
And when you pray, you shall not be as the hypocrites are: for they love to pray standing in the synagogues and in the corners of the streets, that they may be seen of men. Verily I say unto you, They have their reward.
6 Lakini wewe unaposali, ingia chumbani mwako, funga mlango, kisha umwombe Baba yako asiyeonekana. Naye Baba yako aonaye yaliyofichika, atakutuza.
But you, when you pray, enter into your closet, and when you have shut your door, pray to your Father which is in secret; and your Father which sees in secret shall reward you openly.
7 “Mnaposali, msipayuke maneno kama watu wasiomjua Mungu. Wao hudhani kwamba Mungu atawasikiliza ati kwa sababu ya maneno mengi.
But when all of you pray, use not vain repetitions, as the heathen do: for they think that they shall be heard for their much speaking.
8 Msiwe kama wao. Baba yenu anajua mnayoyahitaji hata kabla ya kumwomba.
Be not all of you therefore like unto them: for your Father knows what things all of you have need of, before all of you ask him.
9 Basi, hivi ndivyo mnavyopaswa kusali: Baba yetu uliye mbinguni: Jina lako litukuzwe.
After this manner therefore pray all of you: Our Father which are in heaven, Hallowed be your name.
10 Ufalme wako ufike. Utakalo lifanyike duniani kama mbinguni.
Your kingdom come, Your will be done in earth, as it is in heaven.
11 Utupe leo chakula chetu tunachohitaji.
Give us this day our daily bread.
12 Utusamehe makosa yetu, kama nasi tunavyowasamehe waliotukosea.
And forgive us our debts, as we forgive our debtors.
13 Usitutie katika majaribu, lakini utuokoe na yule Mwovu. is Baadhi ya makala za zamani zina; Kwa kuwa ufalme ni wako, na nguvu, na utukufu, hata milele. Amina.
And lead us not into temptation, but deliver us from evil: For your is the kingdom, and the power, and the glory, for ever. Amen.
14 “Maana mkiwasamehe watu makosa yao, Baba yenu wa mbinguni atawasamehe ninyi pia.
For if all of you forgive men their trespasses, your heavenly Father will also forgive you:
15 Lakini msipowasamehe watu makosa yao, naye Baba yenu hatawasamehe ninyi makosa yenu.
But if all of you forgive not men their trespasses, neither will your Father forgive your trespasses.
16 “Mnapofunga, msiwe na huzuni kama wanafiki. Wao hukunja nyuso zao wapate kuonekana na watu kuwa wanafunga. Nawaambieni hakika, hao wamekwisha pata tuzo lao.
Moreover when all of you fast, be not, as the hypocrites, of a sad countenance: for they disfigure their faces, that they may appear unto men to fast. Verily I say unto you, They have their reward.
17 Wewe lakini unapofunga, paka kichwa chako mafuta, nawa uso wako,
But you, when you fast, anoint your head, and wash your face;
18 ili mtu yeyote asijue kwamba unafunga, ila ujulikane tu kwa Baba yako asiyeonekana. Naye Baba yako aonaye yaliyofichika atakutuza.
That you appear not unto men to fast, but unto your Father which is in secret: and your Father, which sees in secret, shall reward you openly.
19 “Msijiwekee hazina hapa duniani ambako nondo na kutu huharibu, na wezi huingia na kuiba.
Lay not up for yourselves treasures upon earth, where moth and rust does corrupt, and where thieves break through and steal:
20 Jiwekeeni hazina mbinguni ambako nondo na kutu hawawezi kuiharibu, wala wezi hawaingii wakaiba.
But lay up for yourselves treasures in heaven, where neither moth nor rust does corrupt, and where thieves do not break through nor steal:
21 Maana pale ilipo hazina yako, ndipo pia utakapokuwa moyo wako.
For where your treasure is, there will your heart be also.
22 “Jicho ni taa ya mwili. Kama jicho lako ni zima, mwili wako wote utakuwa katika mwanga.
The light of the body is the eye: if therefore your eye be single, your whole body shall be full of light.
23 Lakini ikiwa jicho lako ni bovu, mwili wako wote utakuwa katika giza. Basi, ikiwa mwanga ulioko ndani yako ni giza, basi, hilo ni giza la kutisha mno.
But if your eye be evil, your whole body shall be full of darkness. If therefore the light that is in you be darkness, how great is that darkness!
24 “Hakuna mtu awezaye kutumikia mabwana wawili. Maana atamchukia mmoja na kumpenda huyo wa pili; au ataambatana na mmoja na kumdharau huyo mwingine. Hamwezi kumtumikia Mungu na mali pamoja.
No man can serve two masters: for either he will hate the one, and love the other; or else he will hold to the one, and despise the other. All of you cannot serve God and mammon.
25 “Ndiyo maana nawaambieni, msiwe na wasiwasi juu ya chakula na kinywaji mnavyohitaji ili kuishi, wala juu ya mavazi mnayohitaji kwa ajili ya miili yenu. Je, maisha ni chakula tu au zaidi? Na mwili, je, si zaidi ya mavazi?
Therefore I say unto you, Take no thought for your life, what all of you shall eat, or what all of you shall drink; nor yet for your body, what all of you shall put on. Is not the life more than food, and the body than raiment?
26 Waangalieni ndege wa mwituni: hawapandi, hawavuni, wala hawana ghala yoyoye. Hata hivyo, Baba yenu wa mbinguni huwalisha. Je, ninyi si wa thamani kuliko hao?
Behold the fowls of the air: for they sow not, neither do they reap, nor gather into barns; yet your heavenly Father feeds them. Are all of you not much better than they?
27 Ni nani miongoni mwenu kwa kuwa na wasiwasi sana anaweza kuuongeza muda wa maisha yake?
Which of you by taking thought can add one cubit unto his stature?
28 “Na kuhusu mavazi, ya nini kuwa na wasiwasi? Tazameni maua ya porini jinsi yanavyostawi. Hayafanyi kazi wala hayasokoti.
And why take all of you thought for raiment? Consider the lilies of the field, how they grow; they toil not, neither do they spin:
29 Lakini nawaambieni, hata Solomoni mwenyewe na fahari zake zote hakupata kuvikwa vizuri kama ua mojawapo.
And yet I say unto you, That even Solomon in all his glory was not arrayed like one of these.
30 Ikiwa basi Mungu hulivika hivyo jani la shambani ambalo leo liko na kesho latupwa motoni, je, hatafanya zaidi kwenu ninyi? Enyi watu wenye imani haba!
Wherefore, if God so clothe the grass of the field, which to day is, and tomorrow is cast into the oven, shall he not much more clothe you, O all of you of little faith?
31 “Basi, msiwe na wasiwasi: Tutakula nini, tutakunywa nini, tutavaa nini!
Therefore take no thought, saying, What shall we eat? or, What shall we drink? or, Wherewithal shall we be clothed?
32 Maana hayo yote yanahangaikiwa na watu wasiomjua Mungu. Baba yenu wa mbinguni anajua kwamba mnahitaji vitu hivyo vyote.
(For after all these things do the Gentiles seek: ) for your heavenly Father knows that all of you have need of all these things.
33 Bali, zingatieni kwanza Ufalme wa Mungu na matakwa yake, na hayo mengine yote mtapewa kwa ziada.
But seek all of you first the kingdom of God, and his righteousness; and all these things shall be added unto you.
34 Basi, msiwe na wasiwasi juu ya kesho; kesho inayo yake. Matatizo ya siku moja yanawatosheni kwa siku hiyo.
Take therefore no thought for the next day: for the next day shall take thought for the things of itself. Sufficient unto the day is the evil thereof.