< Mathayo 28 >
1 Baada ya Sabato, karibu na mapambazuko ya siku ile ya Jumapili, Maria Magdalene na yule Maria mwingine walikwenda kutazama lile kaburi.
日既過,一週的第一天,天快亮時,瑪利亞瑪達肋納和另一個瑪利亞來看墳墓。
2 Ghafla kutatokea tetemeko kubwa la nchi; malaika wa Bwana alishuka kutoka mbinguni, akalivingirisha lile jiwe, akalikalia.
忽然發生了大地震,因為上主的天使從上天降來,上前把石頭滾開,坐在上面。
3 Alionekana kama umeme na mavazi yake yalikuwa meupe kama theluji.
他的容貌好像閃電,他的衣服潔白如雪。
4 Walinzi wa lile kaburi wakatetemeka kwa hofu kubwa, hata wakawa kama wamekufa.
看守的人由於怕衪,嚇得打顫,變得好像死人一樣。
5 Lakini yule malaika akawaambia wale wanawake, “Ninyi msiogope! Najua kwamba mnamtafuta Yesu aliyesulubiwa.
天使對婦女說道:「妳們不要害怕!我知道妳們尋找被釘死的耶穌。
6 Hayupo hapa maana amefufuka kama alivyosema. Njoni mkaone mahali alipokuwa amelala.
衪不在這裏,因為衪已經照衪所說的復活了。妳們來看看安放過衪的地方;
7 Basi, nendeni upesi mkawaambie wanafunzi wake kwamba amefufuka kutoka wafu, na sasa anawatangulieni kule Galilaya; huko mtamwona. Haya, mimi nimekwisha waambieni.”
並且快去對衪的門徒說:衪已經由死者中復活了。看,衪在你們以先往加利肋亞去,在那裏你們要看見衪。看,我已經告訴了妳們。」
8 Wakiwa wenye hofu na furaha kubwa, hao wanawake walitoka upesi kaburini, wakakimbia kwenda kuwaambia wanafunzi wake.
她們趕快離開墳墓,又恐懼又異常喜樂,去報告衪的門徒。
9 Mara, Yesu akakutana nao, akawasalimu: “Salamu.” Hao wanawake wakamwendea, wakapiga magoti mbele yake, wakashika miguu yake.
忽然,耶穌迎上妳們說:「願妳們平安!」好們遂上前抱住耶穌的腳,朝拜了衪。
10 Kisha Yesu akawaambia, “Msiogope! Nendeni mkawaambie ndugu zangu waende Galilaya, na huko wataniona.”
耶穌對你們說:「不要害怕!妳們去,報告我的兄弟,叫他們往加利肋亞去,他們要在那裏看見我。」
11 Wale wanawake walipokuwa wanakwenda zao, baadhi ya walinzi wa lile kaburi walikwenda mjini kutoa taarifa kwa makuhani wakuu juu ya mambo yote yaliyotukia.
當婦女離去的時候,有幾個看守的兵士來到城裏,把所發生的事,全告訴了司祭長。
12 Basi, wakakutana pamoja na wazee, na baada ya kushauriana, wakawapa wale askari kiasi kikubwa cha fedha
司祭長就同長老聚會商議之後,給了兵士許多錢,
13 wakisema, “Ninyi mtasema hivi: Wanafunzi wake walikuja usiku, wakamwiba sisi tukiwa tumelala.
囑咐他們說:「你們就說:我們睡覺的時候,他的門徒夜間來了,把他偷去了。
14 Na kama mkuu wa mkoa akijua jambo hili, sisi tutasema naye na kuhakikisha kuwa ninyi hamtapata matatizo.”
如果這事為總督聽見,有我們說好話,保營你們無事。」
15 Wale walinzi wakazichukua zile fedha, wakafanya kama walivyofundishwa. Habari hiyo imeenea kati ya Wayahudi mpaka leo.
兵士拿了銀錢,就照他們所囑咐的做了。這消息就在猶太人間傳揚開了,一直到今天。
16 Wale wanafunzi kumi na mmoja walikwenda Galilaya kwenye ule mlima aliowaagiza Yesu.
十一個門徒就往加利肋亞,到耶穌給他們所指定的山上去了。
17 Walipomwona, wakamwabudu, ingawa wengine walikuwa na mashaka.
他們一看見衪,就朝拜了衪,雖然有人還心中疑惑。
18 Yesu akaja karibu, akawaambia, “Nimepewa mamlaka yote mbinguni na duniani.
耶穌便上前對他們說:「天上地下的一切權柄都交給了我,
19 Nendeni basi, mkawafanye watu wa mataifa yote wawe wanafunzi wangu; mkiwabatiza kwa jina la Baba, na la Mwana, na la Roho Mtakatifu.
所以你們要去使萬民成為門徒,因父及子及聖神之名給他們授洗
20 Wafundisheni kushika maagizo yote niliyowapeni. Nami nipo pamoja nanyi siku zote; naam, mpaka mwisho wa nyakati.” (aiōn )
教訓他們遵守我所份咐你們的一切。看,我同你們天天在一起,直到今世的終結。」 (aiōn )