< Mathayo 27 >
1 Kulipopambazuka, makuhani wakuu wote na wazee wa watu walifanya mashauri juu ya Yesu wapate kumwua.
When morning came all the High Priests and the Elders of the people consulted together against Jesus to put Him to death;
2 Wakamfunga pingu, wakamchukua, wakamkabidhi kwa Pilato, mkuu wa mkoa.
and binding Him they led Him away and handed Him over to Pilate the Governor.
3 Hapo, Yuda ambaye ndiye aliyemsaliti, alipoona kwamba wamekwisha mhukumu Yesu, akajuta, akawarudishia makuhani wakuu zile sarafu thelathini za fedha.
Then when Judas, who had betrayed Him, saw that He was condemned, smitten with remorse he brought back the thirty shekels to the High Priests and Elders
4 Akawaambia, “Nimekosa kwa kumtoa mtu asiye na hatia auawe.” Lakini wao wakasema, “Yatuhusu nini sisi? Hilo ni shauri lako.”
and said, "I have sinned, in betraying to death one who is innocent." "What does that matter to us?" they replied; it is your business."
5 Naye akazitupa zile fedha Hekaluni, akatoka nje, akaenda akajinyonga.
Flinging the shekels into the Sanctuary he left the place, and went and hanged himself.
6 Makuhani wakuu wakazichukua zile fedha, wakasema, “Haifai kuziweka katika hazina ya Hekalu kwa maana ni fedha za damu.”
When the High Priests had gathered up the money they said, "It is illegal to put it into the Treasury, because it is the price of blood."
7 Basi, wakashauriana, wakazitumia kununua shamba la mfinyanzi liwe mahali pa kuzika wageni.
So after consulting together they spent the money in the purchase of the Potter's Field as a burial place for people not belonging to the city;
8 Ndiyo maana mpaka leo shamba hilo linaitwa Shamba la Damu.
for which reason that piece of ground received the name, which it still bears, of 'the Field of Blood.'
9 Hivyo maneno ya nabii Yeremia yakatimia: “Walizichukua sarafu thelathini za fedha, thamani ya yule ambaye watu wa Israeli walipanga bei,
Then were fulfilled the words spoken by the Prophet Jeremiah, "And I took the thirty shekels, the price of the prized one on whom Israelites had set a price,
10 wakanunua nazo shamba la mfinyanzi, kama Bwana alivyoniagiza.”
and gave them for the potter's field, as the Lord directed me."
11 Yesu alisimamishwa mbele ya mkuu wa mkoa. Basi, mkuu wa mkoa akamwuliza, “Je, wewe ndiwe Mfalme wa Wayahudi?” Yesu akamwambia, “Wewe umesema.”
Meanwhile Jesus was brought before the Governor, and the latter put the question, "Are you the King of the Jews?" "I am their King," He answered.
12 Lakini makuhani wakuu na wazee walipokuwa wanamshtaki, hakujibu neno.
When however the High Priests and the Elders kept bringing their charges against Him, He said not a word in reply.
13 Hivyo Pilato akamwuliza, “Je, husikii mashtaka hayo yote wanayotoa juu yako?”
"Do you not hear," asked Pilate, "what a mass of evidence they are bringing against you?"
14 Lakini Yesu hakumjibu hata neno moja; hata huyo mkuu wa mkoa akashangaa sana.
But He made no reply to a single accusation, so that the Governor was greatly astonished.
15 Ilikuwa kawaida wakati wa Sikukuu ya Pasaka mkuu wa mkoa kuwafungulia Wayahudi mfungwa mmoja waliyemtaka.
"Now it was the Governor's custom at the Festival to release some one prisoner, whomsoever the populace desired;
16 Wakati huo kulikuwa na mfungwa mmoja, jina lake Baraba.
and at this time they had a notorious prisoner called Barabbas.
17 Hivyo, watu walipokusanyika pamoja, Pilato akawauliza, “Mwataka nimfungue yupi kati ya wawili hawa, Baraba ama Yesu aitwae Kristo?”
So when they were now assembled Pilate appealed to them. "Whom shall I release to you," he said, "Barabbas, or Jesus the so-called Christ?"
18 Alisema hivyo maana alijua wazi kwamba walimleta kwake kwa sababu ya wivu.
For he knew that it was from envious hatred that Jesus had been brought before him.
19 Pilato alipokuwa amekaa katika kiti cha hukumu, mke wake akampelekea ujumbe: “Usijitie katika shauri la mtu huyu mwema, maana leo nimeteseka sana katika ndoto kwa sababu yake.”
While he was sitting on the tribunal a message came to him from his wife. "Have nothing to do with that innocent man," she said, "for during the night I have suffered terribly in a dream through him."
20 Lakini makuhani wakuu na wazee wakawashawishi watu waombe Baraba afunguliwe na Yesu auawe.
The High Priests, however, and the Elders urged the crowd to ask for Barabbas and to demand the death of Jesus.
21 Mkuu wa mkoa akawauliza, “Ni yupi kati ya hawa wawili mnayetaka nimfungue?” Wakamjibu, “Baraba!”
So when the Governor a second time asked them, "Which of the two shall I release to you?" --they cried, "Barabbas!"
22 Pilato akawauliza, “Sasa, nifanye nini na Yesu aitwaye Kristo?” Wote wakasema, “Asulubiwe!”
"What then," said Pilate, "shall I do with Jesus, the so-called Christ?" With one voice they shouted, "Let him be crucified!"
23 Pilato akauliza, “Kwa nini? Amefanya kosa gani?” Wao wakazidi kupaaza sauti: “Asulubiwe!”
"Why, what crime has he committed?" asked Pilate. But they kept on furiously shouting, "Let him be crucified!"
24 Basi, Pilato alipotambua kwamba hafanikiwi chochote na kwamba maasi yalikuwa yanaanza, alichukua maji, akanawa mikono mbele ya ule umati wa watu, akasema, “Mimi sina lawama juu ya kifo cha mtu huyu; shauri lenu wenyewe.”
So when he saw that he could gain nothing, but that on the contrary there was a riot threatening, he called for water and washed his hands in sight of them all, saying, "I am not responsible for this murder: you must answer for it."
25 Watu wote wakasema, “Damu yake na iwe juu yetu na juu ya watoto wetu!”
"His blood," replied all the people, "be on us and on our children!"
26 Hapo Pilato akawafungulia Baraba kutoka gerezani, lakini akamtoa Yesu asulubiwe.
Then he released Barabbas to them, but Jesus he ordered to be scourged, and gave Him up to be crucified.
27 Kisha askari wa mkuu wa mkoa wakamwingiza Yesu ndani ya ikulu, wakamkusanyikia kikosi kizima.
Then the Governor's soldiers took Jesus into the Praetorium, and called together the whole battalion to make sport of Him.
28 Wakamvua nguo zake, wakamvika joho la rangi nyekundu.
Stripping off His garments, they put on Him a general's short crimson cloak.
29 Kisha wakasokota taji ya miiba, wakamvika kichwani, wakamwekea pia mwanzi katika mkono wake wa kulia. Wakapiga magoti mbele yake, wakamdhihaki wakisema, “Shikamoo mfalme wa Wayahudi!”
They twisted a wreath of thorny twigs and put it on His head, and they put a sceptre of cane in His right hand, and kneeling to Him they shouted in mockery, "Long live the King of the Jews!"
30 Wakamtemea mate, wakauchukua ule mwanzi, wakampiga nao kichwani.
Then they spat upon Him, and taking the cane they repeatedly struck Him on the head with it.
31 Baada ya kumdhihaki, wakamvua lile joho, wakamvika nguo zake, kisha wakampeleka kumsulubisha.
At last, having finished their sport, they took off the cloak, clothed Him again in His own garments, and led Him away for crucifixion.
32 Walipokuwa wakienda, wakamkuta mtu mmoja jina lake Simoni, mwenyeji wa Kurene, wakamlazimisha kuuchukua msalaba wake Yesu.
Going out they met a Cyrenaean named Simon; whom they compelled to carry His cross,
33 Walipofika mahali paitwapo Golgotha, maana yake, “Mahali pa Fuvu la kichwa,”
and so they came to a place called Golgotha, which means 'Skull-ground.'
34 wakampa mchanganyiko wa divai na nyongo. Lakini Yesu alipoonja akakataa kunywa.
Here they gave Him a mixture of wine and gall to drink, but having tasted it He refused to drink it.
35 Walimsulubisha, kisha wakagawana mavazi yake kwa kuyapigia kura.
After crucifying Him, they divided His garments among them by lot,
36 Wakaketi, wakawa wanamchunga.
and sat down there on guard.
37 Juu ya kichwa chake wakaweka shtaka dhidi yake lilioandikwa, “Huyu ni Yesu, Mfalme wa Wayahudi.”
Over His head they placed a written statement of the charge against Him: THIS IS JESUS THE KING OF THE JEWS.
38 Wanyang'anyi wawili walisulubishwa pia pamoja naye, mmoja upande wa kushoto na mwingine upande wa kulia.
At the same time two robbers were crucified with Him, one at His right hand and the other at His left.
39 Watu waliokuwa wanapita mahali hapo walimtukana wakitikisa vichwa vyao na kusema,
And the passers-by reviled Him. They shook their heads at Him
40 “Wewe! Si ulijidai kulivunja Hekalu na kulijenga kwa siku tatu? Sasa jiokoe mwenyewe. Kama wewe ni Mwana wa Mungu, basi shuka msalabani!”
and said, "You who would pull down the Sanctuary and build a new one within three days, save yourself. If you are God's Son, come down from the cross."
41 Hali kadhalika na makuhani wakuu pamoja na walimu wa Sheria na wazee walimdhihaki wakisema,
In like manner the High Priests also, together with the Scribes and the Elders, taunted Him.
42 “Aliwaokoa wengine, lakini kujiokoa mwenyewe hawezi! Eti yeye ni mfalme wa Wayahudi! Basi, sasa na ashuke msalabani, nasi tutamwamini.
"He saved others," they said, "himself he cannot save! He is the King of Israel! Let him now come down from the cross, and we will believe in him.
43 Alimtumainia Mungu na kusema eti yeye ni Mwana wa Mungu; basi, Mungu na amwokoe kama anamtaka.”
His trust is in God: let God deliver him now, if He will have him; for he said, 'I am God's Son.'"
44 Hali kadhalika na wale waliosulubiwa pamoja naye wakamtukana.
Insults of the same kind were heaped on Him even by the robbers who were being crucified with Him.
45 Tangu saa sita mchana mpaka saa tisa, nchi yote ikawa katika giza.
Now from noon until three o'clock in the afternoon there was darkness over the whole land;
46 Mnamo saa tisa Yesu akalia kwa sauti kubwa, “Eli, Eli, lema sabakthani?” Maana yake, “Mungu wangu, Mungu wangu, mbona umeniacha?”
but about three o'clock Jesus cried out in a loud voice, "Eli, Eli, lama sabachthani?" that is to say, "My God, My God, why hast Thou forsaken me?"
47 Lakini wale waliosimama pale waliposikia hivyo wakasema, “Anamwita Eliya.”
"The man is calling for Elijah," said some of the bystanders.
48 Mmoja wao akakimbia, akachukua sifongo, akaichovya katika siki, akaiweka juu ya mwanzi, akampa anywe.
One of them ran forthwith, and filling a sponge with sour wine put it on the end of a cane and offered it Him to drink;
49 Wengine wakasema, “Acha tuone kama Eliya anakuja kumwokoa.”
while the rest said, "Let us see whether Elijah is coming to deliver him."
50 Basi, Yesu akalia tena kwa sauti kubwa, akakata roho.
But Jesus uttered another loud cry and then yielded up His spirit.
51 Hapo pazia la Hekalu likapasuka vipande viwili, toka juu mpaka chini; nchi ikatetemeka; miamba ikapasuka;
Immediately the curtain of the Sanctuary was torn in two from top to bottom: the earth quaked; the rocks split;
52 makaburi yakafunguka na watu wengi wa Mungu waliokufa wakafufuliwa;
the tombs opened; and many of God's people who were asleep in death awoke.
53 nao, baada ya kufufuka kwake, wakatoka makaburini, wakaingia katika Mji Mtakatifu, wakaonekana na watu wengi.
And coming out of their tombs after Christ's resurrection they entered the holy city and showed themselves to many.
54 Basi, jemadari na wale waliokuwa wakimlinda Yesu walipoona tetemeko la ardhi na yale mambo yaliyotukia, wakaogopa sana, wakasema, “Hakika mtu huyu alikuwa Mwana wa Mungu.”
As for the Captain and the soldiers who were with Him keeping guard over Jesus, when they witnessed the earthquake and the other occurrences they were filled with terror, and exclaimed, "Assuredly he was God's Son."
55 Mahali hapo walikuwapo wanawake wengi wakitazama kwa mbali. Hao ndio wale waliomfuata Yesu kutoka Galilaya wakimtumikia.
And there were a number of women there looking on from a distance, who had followed Jesus from Galilee ministering to His necessities;
56 Miongoni mwao walikuwa Maria Magdalene, Maria mama yao Yakobo na Yosefu, pamoja na mama yao wana wa Zebedayo.
among them being Mary of Magdala, Mary the mother of James and Joses, and the mother of the sons of Zabdi.
57 Ilipokuwa jioni, akaja mtu mmoja tajiri mwenyeji wa Armathaya, jina lake Yosefu. Yeye pia alikuwa mwanafunzi wa Yesu.
Towards sunset there came a wealthy inhabitant of Arimathaea, named Joseph, who himself also had become a disciple of Jesus.
58 Akamwendea Pilato, akaomba apewe mwili wa Yesu. Basi, Pilato akaamuru apewe.
He went to Pilate and begged to have the body of Jesus, and Pilate ordered it to be given to him.
59 Yosefu akauchukua ule mwili akauzungushia sanda safi ya kitani,
So Joseph took the body and wrapped it in a clean sheet of fine linen.
60 akauweka ndani ya kaburi lake jipya alilokuwa amelichonga katika mwamba. Kisha akavingirisha jiwe kubwa mbele ya mlango wa kaburi, akaenda zake.
He then laid it in his own new tomb which he had hewn in the solid rock, and after rolling a great stone against the door of the tomb he went home.
61 Maria Magdalene na yule Maria mwingine walikuwa wameketi kulielekea kaburi.
Mary of Magdala and the other Mary were both present there, sitting opposite to the sepulchre.
62 Kesho yake, yaani siku iliyofuata ile ya Maandalio, makuhani wakuu na Mafarisayo walimwendea Pilato,
On the next day, the day after the Preparation, the High Priests and the Pharisees came in a body to Pilate.
63 Wakasema, “Mheshimiwa, tunakumbuka kwamba yule mdanganyifu alisema kabla ya kufa ati, Baada ya siku tatu nitafufuka.
"Sir," they said, "we recollect that during his lifetime that impostor pretended that after two days he was to rise to life again.
64 Kwa hiyo amuru kaburi lilindwe mpaka siku ya tatu ili wanafunzi wake wasije wakamwiba na kuwaambia watu kwamba amefufuka. Uongo huu wa mwisho utakuwa mbaya kuliko ule wa awali.”
So give orders for the sepulchre to be securely guarded till the third day, for fear his disciples should come by night and steal the body, and then tell the people that he has come back to life; and so the last imposture will be more serious than the first."
65 Pilato akawaambia, “Haya, mnao walinzi; nendeni mkalinde kadiri mjuavyo.”
"You can have a guard," said Pilate: "go and make all safe, as best you can."
66 Basi, wakaenda, wakalilinda kaburi, wakatia mhuri juu ya lile jiwe na kuacha hapo askari walinzi.
So they went and made the sepulchre secure, sealing the stone besides setting the guard.