< Mathayo 27 >

1 Kulipopambazuka, makuhani wakuu wote na wazee wa watu walifanya mashauri juu ya Yesu wapate kumwua.
Now when morning had come, all the chief priests and the elders of the people took counsel against Jesus to put him to death:
2 Wakamfunga pingu, wakamchukua, wakamkabidhi kwa Pilato, mkuu wa mkoa.
and they bound him, and led him away, and delivered him to Pilate, the governor.
3 Hapo, Yuda ambaye ndiye aliyemsaliti, alipoona kwamba wamekwisha mhukumu Yesu, akajuta, akawarudishia makuhani wakuu zile sarafu thelathini za fedha.
Then Judas, who betrayed him, when he saw that Jesus was condemned, felt remorse, and returned the thirty pieces of silver to the chief priests and elders,
4 Akawaambia, “Nimekosa kwa kumtoa mtu asiye na hatia auawe.” Lakini wao wakasema, “Yatuhusu nini sisi? Hilo ni shauri lako.”
saying, "I have sinned in that I betrayed innocent blood." But they said, "What is that to us? You see to it."
5 Naye akazitupa zile fedha Hekaluni, akatoka nje, akaenda akajinyonga.
He threw down the pieces of silver in the sanctuary, and departed. He went away and hanged himself.
6 Makuhani wakuu wakazichukua zile fedha, wakasema, “Haifai kuziweka katika hazina ya Hekalu kwa maana ni fedha za damu.”
The chief priests took the pieces of silver, and said, "It's not lawful to put them into the treasury, since it is the price of blood."
7 Basi, wakashauriana, wakazitumia kununua shamba la mfinyanzi liwe mahali pa kuzika wageni.
They took counsel, and bought the potter's field with them, to bury strangers in.
8 Ndiyo maana mpaka leo shamba hilo linaitwa Shamba la Damu.
Therefore that field was called "The Field of Blood" to this day.
9 Hivyo maneno ya nabii Yeremia yakatimia: “Walizichukua sarafu thelathini za fedha, thamani ya yule ambaye watu wa Israeli walipanga bei,
Then that which was spoken through Jeremiah the prophet was fulfilled, saying, "They took the thirty pieces of silver, the price of him upon whom a price had been set, whom some of the children of Israel priced,
10 wakanunua nazo shamba la mfinyanzi, kama Bwana alivyoniagiza.”
and they gave them for the potter's field, as the Lord commanded me."
11 Yesu alisimamishwa mbele ya mkuu wa mkoa. Basi, mkuu wa mkoa akamwuliza, “Je, wewe ndiwe Mfalme wa Wayahudi?” Yesu akamwambia, “Wewe umesema.”
Now Jesus stood before the governor: and the governor asked him, saying, "Are you the King of the Jews?" Jesus said to him, "You say so."
12 Lakini makuhani wakuu na wazee walipokuwa wanamshtaki, hakujibu neno.
When he was accused by the chief priests and elders, he answered nothing.
13 Hivyo Pilato akamwuliza, “Je, husikii mashtaka hayo yote wanayotoa juu yako?”
Then Pilate said to him, "Do you not hear how many things they testify against you?"
14 Lakini Yesu hakumjibu hata neno moja; hata huyo mkuu wa mkoa akashangaa sana.
He gave him no answer, not even one word, so that the governor was greatly amazed.
15 Ilikuwa kawaida wakati wa Sikukuu ya Pasaka mkuu wa mkoa kuwafungulia Wayahudi mfungwa mmoja waliyemtaka.
Now at the feast the governor was accustomed to release to the crowd one prisoner, whom they desired.
16 Wakati huo kulikuwa na mfungwa mmoja, jina lake Baraba.
They had then a notable prisoner, called Barabbas.
17 Hivyo, watu walipokusanyika pamoja, Pilato akawauliza, “Mwataka nimfungue yupi kati ya wawili hawa, Baraba ama Yesu aitwae Kristo?”
When therefore they were gathered together, Pilate said to them, "Whom do you want me to release to you? Barabbas, or Jesus, who is called Christ?"
18 Alisema hivyo maana alijua wazi kwamba walimleta kwake kwa sababu ya wivu.
For he knew that because of envy they had delivered him up.
19 Pilato alipokuwa amekaa katika kiti cha hukumu, mke wake akampelekea ujumbe: “Usijitie katika shauri la mtu huyu mwema, maana leo nimeteseka sana katika ndoto kwa sababu yake.”
While he was sitting on the judgment seat, his wife sent to him, saying, "Have nothing to do with that righteous man, for I have suffered many things this day in a dream because of him."
20 Lakini makuhani wakuu na wazee wakawashawishi watu waombe Baraba afunguliwe na Yesu auawe.
Now the chief priests and the elders persuaded the crowds to ask for Barabbas, and destroy Jesus.
21 Mkuu wa mkoa akawauliza, “Ni yupi kati ya hawa wawili mnayetaka nimfungue?” Wakamjibu, “Baraba!”
But the governor answered them, "Which of the two do you want me to release to you?" They said, "Barabbas."
22 Pilato akawauliza, “Sasa, nifanye nini na Yesu aitwaye Kristo?” Wote wakasema, “Asulubiwe!”
Pilate said to them, "What then should I do with Jesus, who is called Christ?" They all said, "Let him be crucified."
23 Pilato akauliza, “Kwa nini? Amefanya kosa gani?” Wao wakazidi kupaaza sauti: “Asulubiwe!”
But he said, "Why? What evil has he done?" But they shouted all the louder, saying, "Let him be crucified."
24 Basi, Pilato alipotambua kwamba hafanikiwi chochote na kwamba maasi yalikuwa yanaanza, alichukua maji, akanawa mikono mbele ya ule umati wa watu, akasema, “Mimi sina lawama juu ya kifo cha mtu huyu; shauri lenu wenyewe.”
So Pilate, seeing that nothing was being gained, but rather that a disturbance was starting, took water and he washed his hands before the crowd, saying, "I am innocent of the blood of this righteous man. You see to it."
25 Watu wote wakasema, “Damu yake na iwe juu yetu na juu ya watoto wetu!”
All the people answered, "May his blood be on us, and on our children."
26 Hapo Pilato akawafungulia Baraba kutoka gerezani, lakini akamtoa Yesu asulubiwe.
Then he released to them Barabbas, but Jesus he flogged and delivered to be crucified.
27 Kisha askari wa mkuu wa mkoa wakamwingiza Yesu ndani ya ikulu, wakamkusanyikia kikosi kizima.
Then the governor's soldiers took Jesus into the Praetorium, and gathered the whole garrison together against him.
28 Wakamvua nguo zake, wakamvika joho la rangi nyekundu.
They stripped him, and put a scarlet robe on him.
29 Kisha wakasokota taji ya miiba, wakamvika kichwani, wakamwekea pia mwanzi katika mkono wake wa kulia. Wakapiga magoti mbele yake, wakamdhihaki wakisema, “Shikamoo mfalme wa Wayahudi!”
They braided a crown of thorns and put it on his head, and a reed in his right hand; and they kneeled down before him, and mocked him, saying, "Greetings, King of the Jews."
30 Wakamtemea mate, wakauchukua ule mwanzi, wakampiga nao kichwani.
They spat on him, and took the reed and struck him on the head.
31 Baada ya kumdhihaki, wakamvua lile joho, wakamvika nguo zake, kisha wakampeleka kumsulubisha.
When they had mocked him, they took the robe off of him, and put his clothes on him, and led him away to crucify him.
32 Walipokuwa wakienda, wakamkuta mtu mmoja jina lake Simoni, mwenyeji wa Kurene, wakamlazimisha kuuchukua msalaba wake Yesu.
As they came out, they found a man of Cyrene, Simon by name, and they compelled him to go with them, that he might carry his cross.
33 Walipofika mahali paitwapo Golgotha, maana yake, “Mahali pa Fuvu la kichwa,”
They came to a place called "Golgotha," that is to say, "The place of a skull."
34 wakampa mchanganyiko wa divai na nyongo. Lakini Yesu alipoonja akakataa kunywa.
They gave him wine to drink mixed with gall. When he had tasted it, he would not drink.
35 Walimsulubisha, kisha wakagawana mavazi yake kwa kuyapigia kura.
When they had crucified him, they divided his clothing among themselves, casting a lot, that it might be fulfilled which was spoken by the prophet: 'They divided my clothes among themselves, and for my clothing they cast a lot.'
36 Wakaketi, wakawa wanamchunga.
And they sat and watched him there.
37 Juu ya kichwa chake wakaweka shtaka dhidi yake lilioandikwa, “Huyu ni Yesu, Mfalme wa Wayahudi.”
They set up over his head the accusation against him written, "THIS IS JESUS, THE KING OF THE JEWS."
38 Wanyang'anyi wawili walisulubishwa pia pamoja naye, mmoja upande wa kushoto na mwingine upande wa kulia.
Then there were two robbers crucified with him, one on his right hand and one on the left.
39 Watu waliokuwa wanapita mahali hapo walimtukana wakitikisa vichwa vyao na kusema,
Those who passed by blasphemed him, wagging their heads,
40 “Wewe! Si ulijidai kulivunja Hekalu na kulijenga kwa siku tatu? Sasa jiokoe mwenyewe. Kama wewe ni Mwana wa Mungu, basi shuka msalabani!”
and saying, "You who destroy the temple, and build it in three days, save yourself. If you are the Son of God, come down from the cross."
41 Hali kadhalika na makuhani wakuu pamoja na walimu wa Sheria na wazee walimdhihaki wakisema,
Likewise the chief priests also mocking, with the scribes, and the elders, said,
42 “Aliwaokoa wengine, lakini kujiokoa mwenyewe hawezi! Eti yeye ni mfalme wa Wayahudi! Basi, sasa na ashuke msalabani, nasi tutamwamini.
"He saved others, but he cannot save himself. If he is the King of Israel, let him come down from the cross now, and we will believe in him.
43 Alimtumainia Mungu na kusema eti yeye ni Mwana wa Mungu; basi, Mungu na amwokoe kama anamtaka.”
He trusts in God. Let God deliver him now, if he wants him; for he said, 'I am the Son of God.'"
44 Hali kadhalika na wale waliosulubiwa pamoja naye wakamtukana.
The robbers also who were crucified with him insulted him in the same way.
45 Tangu saa sita mchana mpaka saa tisa, nchi yote ikawa katika giza.
Now from noon until three in the afternoon there was darkness over all the land.
46 Mnamo saa tisa Yesu akalia kwa sauti kubwa, “Eli, Eli, lema sabakthani?” Maana yake, “Mungu wangu, Mungu wangu, mbona umeniacha?”
Then at about three in the afternoon Jesus called out with a loud voice, saying, "Eli, Eli, lema shabachthani?" That is, "My God, my God, why have you forsaken me?"
47 Lakini wale waliosimama pale waliposikia hivyo wakasema, “Anamwita Eliya.”
Some of them who stood there, when they heard it, said, "This man is calling Elijah."
48 Mmoja wao akakimbia, akachukua sifongo, akaichovya katika siki, akaiweka juu ya mwanzi, akampa anywe.
Immediately one of them ran, and took a sponge, and filled it with vinegar, and put it on a reed, and gave him a drink.
49 Wengine wakasema, “Acha tuone kama Eliya anakuja kumwokoa.”
The rest said, "Let him be. Let us see whether Elijah comes to save him."
50 Basi, Yesu akalia tena kwa sauti kubwa, akakata roho.
And Jesus cried out again with a loud voice, and yielded up his spirit.
51 Hapo pazia la Hekalu likapasuka vipande viwili, toka juu mpaka chini; nchi ikatetemeka; miamba ikapasuka;
And look, the veil of the temple was torn in two from the top to the bottom. The earth quaked and the rocks were split.
52 makaburi yakafunguka na watu wengi wa Mungu waliokufa wakafufuliwa;
The tombs were opened, and many bodies of the saints who had fallen asleep were raised;
53 nao, baada ya kufufuka kwake, wakatoka makaburini, wakaingia katika Mji Mtakatifu, wakaonekana na watu wengi.
and coming out of the tombs after his resurrection, they entered into the holy city and appeared to many.
54 Basi, jemadari na wale waliokuwa wakimlinda Yesu walipoona tetemeko la ardhi na yale mambo yaliyotukia, wakaogopa sana, wakasema, “Hakika mtu huyu alikuwa Mwana wa Mungu.”
Now the centurion, and those who were with him watching Jesus, when they saw the earthquake, and the things that were done, feared exceedingly, saying, "Truly this was the Son of God."
55 Mahali hapo walikuwapo wanawake wengi wakitazama kwa mbali. Hao ndio wale waliomfuata Yesu kutoka Galilaya wakimtumikia.
Many women were there watching from afar, who had followed Jesus from Galilee, serving him.
56 Miongoni mwao walikuwa Maria Magdalene, Maria mama yao Yakobo na Yosefu, pamoja na mama yao wana wa Zebedayo.
Among them were Mary Magdalene, Mary the mother of James and Joseph, and the mother of the sons of Zebedee.
57 Ilipokuwa jioni, akaja mtu mmoja tajiri mwenyeji wa Armathaya, jina lake Yosefu. Yeye pia alikuwa mwanafunzi wa Yesu.
When evening had come, a rich man from Arimathea, named Joseph, who himself was also Jesus' disciple came.
58 Akamwendea Pilato, akaomba apewe mwili wa Yesu. Basi, Pilato akaamuru apewe.
This man went to Pilate, and asked for the body of Jesus. Then Pilate commanded that it be released.
59 Yosefu akauchukua ule mwili akauzungushia sanda safi ya kitani,
Joseph took the body, and wrapped it in a clean linen cloth,
60 akauweka ndani ya kaburi lake jipya alilokuwa amelichonga katika mwamba. Kisha akavingirisha jiwe kubwa mbele ya mlango wa kaburi, akaenda zake.
and placed it in his own new tomb, which he had cut out in the rock, and he rolled a great stone to the door of the tomb, and departed.
61 Maria Magdalene na yule Maria mwingine walikuwa wameketi kulielekea kaburi.
Mary Magdalene was there, and the other Mary, sitting opposite the tomb.
62 Kesho yake, yaani siku iliyofuata ile ya Maandalio, makuhani wakuu na Mafarisayo walimwendea Pilato,
Now on the next day, which was the day after the Preparation Day, the chief priests and the Pharisees were gathered together to Pilate,
63 Wakasema, “Mheshimiwa, tunakumbuka kwamba yule mdanganyifu alisema kabla ya kufa ati, Baada ya siku tatu nitafufuka.
saying, "Sir, we remember what that deceiver said while he was still alive: 'After three days I will rise again.'
64 Kwa hiyo amuru kaburi lilindwe mpaka siku ya tatu ili wanafunzi wake wasije wakamwiba na kuwaambia watu kwamba amefufuka. Uongo huu wa mwisho utakuwa mbaya kuliko ule wa awali.”
Command therefore that the tomb be made secure until the third day, lest perhaps his disciples come and steal him away, and tell the people, 'He is risen from the dead;' and the last deception will be worse than the first."
65 Pilato akawaambia, “Haya, mnao walinzi; nendeni mkalinde kadiri mjuavyo.”
Pilate said to them, "You have a guard. Go, make it as secure as you can."
66 Basi, wakaenda, wakalilinda kaburi, wakatia mhuri juu ya lile jiwe na kuacha hapo askari walinzi.
So they went with the guard and made the tomb secure, sealing the stone.

< Mathayo 27 >