< Mathayo 27 >

1 Kulipopambazuka, makuhani wakuu wote na wazee wa watu walifanya mashauri juu ya Yesu wapate kumwua.
晨,眾司祭長和民間的長老就決意陷害耶穌,要把衪處死,
2 Wakamfunga pingu, wakamchukua, wakamkabidhi kwa Pilato, mkuu wa mkoa.
遂把衪捆綁了,解送給總督比拉多。
3 Hapo, Yuda ambaye ndiye aliyemsaliti, alipoona kwamba wamekwisha mhukumu Yesu, akajuta, akawarudishia makuhani wakuu zile sarafu thelathini za fedha.
那時,那出賣耶穌的猶達斯見衪已被判決,就後悔了,把那三十塊銀錢,退還給司祭長和長老
4 Akawaambia, “Nimekosa kwa kumtoa mtu asiye na hatia auawe.” Lakini wao wakasema, “Yatuhusu nini sisi? Hilo ni shauri lako.”
說:「我出賣了無辜的血,犯了罪了!」他們卻說:「這與我們何干? 是你自己的事 !」
5 Naye akazitupa zile fedha Hekaluni, akatoka nje, akaenda akajinyonga.
於是他把那些錢扔在聖所裏,就退出來,上吊死了。
6 Makuhani wakuu wakazichukua zile fedha, wakasema, “Haifai kuziweka katika hazina ya Hekalu kwa maana ni fedha za damu.”
司祭長拿了那銀錢說:「這是血價,不可放入獻儀箱內。」
7 Basi, wakashauriana, wakazitumia kununua shamba la mfinyanzi liwe mahali pa kuzika wageni.
他們商議後,就用那銀錢買了陶工的田地,作為埋葬外鄉人用。
8 Ndiyo maana mpaka leo shamba hilo linaitwa Shamba la Damu.
為此直到今日稱那塊地為「血田」。
9 Hivyo maneno ya nabii Yeremia yakatimia: “Walizichukua sarafu thelathini za fedha, thamani ya yule ambaye watu wa Israeli walipanga bei,
這就應驗了耶肋米亞先知所說的話:『他們拿了三十塊銀錢,即以色列子民為被賣的人所定的價錢,
10 wakanunua nazo shamba la mfinyanzi, kama Bwana alivyoniagiza.”
用這錢買了陶工的那塊田,如上主所吩咐我的。』
11 Yesu alisimamishwa mbele ya mkuu wa mkoa. Basi, mkuu wa mkoa akamwuliza, “Je, wewe ndiwe Mfalme wa Wayahudi?” Yesu akamwambia, “Wewe umesema.”
耶穌站在總督面前,總督便審問衪說:「你是猶太人的君王嗎? 」耶穌回答說:「你說的是。」
12 Lakini makuhani wakuu na wazee walipokuwa wanamshtaki, hakujibu neno.
當司祭長和長老控告衪時,衪什麼也不回答。
13 Hivyo Pilato akamwuliza, “Je, husikii mashtaka hayo yote wanayotoa juu yako?”
於是比拉多對衪說:「你沒有聽見他們提出多少證據告你嗎? 」
14 Lakini Yesu hakumjibu hata neno moja; hata huyo mkuu wa mkoa akashangaa sana.
耶穌連一話也沒有回答他,以至總督大為驚異。
15 Ilikuwa kawaida wakati wa Sikukuu ya Pasaka mkuu wa mkoa kuwafungulia Wayahudi mfungwa mmoja waliyemtaka.
每逢節日,總督慣常給民眾釋放一個他們願意釋放的囚犯。
16 Wakati huo kulikuwa na mfungwa mmoja, jina lake Baraba.
那時正有一個出名的囚犯,名叫巴辣巴。
17 Hivyo, watu walipokusanyika pamoja, Pilato akawauliza, “Mwataka nimfungue yupi kati ya wawili hawa, Baraba ama Yesu aitwae Kristo?”
當他們聚集在一起時,比拉多對他們說:「你們願意我給你們釋放那一個? 巴辣巴,或是那稱為默西亞的耶穌? 」
18 Alisema hivyo maana alijua wazi kwamba walimleta kwake kwa sababu ya wivu.
原來他知道,他們是由於嫉妒才把衪解送來的。
19 Pilato alipokuwa amekaa katika kiti cha hukumu, mke wake akampelekea ujumbe: “Usijitie katika shauri la mtu huyu mwema, maana leo nimeteseka sana katika ndoto kwa sababu yake.”
比拉多正坐堂時,他的妻子差人到他跟前說:「你千萬不要干涉那義人的事,因為我為他,今天在夢中受了許多苦。
20 Lakini makuhani wakuu na wazee wakawashawishi watu waombe Baraba afunguliwe na Yesu auawe.
司祭長和長老卻說服了民眾,叫他們要巴拉巴,而除掉耶穌。
21 Mkuu wa mkoa akawauliza, “Ni yupi kati ya hawa wawili mnayetaka nimfungue?” Wakamjibu, “Baraba!”
總又向他們發言說:「這兩個人中,你們願意我給你們釋放那一個? 」他們說:「巴拉巴。」
22 Pilato akawauliza, “Sasa, nifanye nini na Yesu aitwaye Kristo?” Wote wakasema, “Asulubiwe!”
比拉多對他們說:「那麼,對於那稱為默西亞的耶穌我該怎麼辦? 」眾人答說:「該釘他在十字架上。」
23 Pilato akauliza, “Kwa nini? Amefanya kosa gani?” Wao wakazidi kupaaza sauti: “Asulubiwe!”
總督問說:「他究竟做了什麼惡事?」他們越發喊說:「該釘他在十字架上。」
24 Basi, Pilato alipotambua kwamba hafanikiwi chochote na kwamba maasi yalikuwa yanaanza, alichukua maji, akanawa mikono mbele ya ule umati wa watu, akasema, “Mimi sina lawama juu ya kifo cha mtu huyu; shauri lenu wenyewe.”
比拉多見事毫無進展,反而更為混亂,就拿水,看民眾洗手說:「對這義人的血,我是無罪的,你們自己負責吧? 」
25 Watu wote wakasema, “Damu yake na iwe juu yetu na juu ya watoto wetu!”
全體百姓回答說:「他的血歸在我們和我們的子孫身上!」
26 Hapo Pilato akawafungulia Baraba kutoka gerezani, lakini akamtoa Yesu asulubiwe.
於是比拉多給他們釋放了巴拉巴;至於耶穌,把衪鞭打了以後,交給人釘在十字架上。
27 Kisha askari wa mkuu wa mkoa wakamwingiza Yesu ndani ya ikulu, wakamkusanyikia kikosi kizima.
那時,總督的兵士把耶穌帶到總督府內,召集了全隊圍著衪,
28 Wakamvua nguo zake, wakamvika joho la rangi nyekundu.
脫去了衪的衣服,給衪披上一件紫紅的外氅;
29 Kisha wakasokota taji ya miiba, wakamvika kichwani, wakamwekea pia mwanzi katika mkono wake wa kulia. Wakapiga magoti mbele yake, wakamdhihaki wakisema, “Shikamoo mfalme wa Wayahudi!”
又用荊棘編了一個茨冠,戴在衪頭上,拿一根蘆葦放在衪右手裏;然後跪在衪前,戲弄衪說:「猶太人的君王,萬歲!」
30 Wakamtemea mate, wakauchukua ule mwanzi, wakampiga nao kichwani.
隨後向衪吐唾沬,拿起蘆葦來敲衪的頭。
31 Baada ya kumdhihaki, wakamvua lile joho, wakamvika nguo zake, kisha wakampeleka kumsulubisha.
戲弄完了,就給衪脫去外氅,又給衪穿上衪自己的衣服,帶衪去釘在十字架上。
32 Walipokuwa wakienda, wakamkuta mtu mmoja jina lake Simoni, mwenyeji wa Kurene, wakamlazimisha kuuchukua msalaba wake Yesu.
他們出來時,遇見一個基勒乃人,名叫西滿,就強迫他背耶穌的十字架。
33 Walipofika mahali paitwapo Golgotha, maana yake, “Mahali pa Fuvu la kichwa,”
到了一個名哥耳哥達的地方,即稱為「髑髏」的地方,
34 wakampa mchanganyiko wa divai na nyongo. Lakini Yesu alipoonja akakataa kunywa.
休們酒就拿苦艾調和的酒給衪喝;衪只嘗了嘗,卻不願意喝。
35 Walimsulubisha, kisha wakagawana mavazi yake kwa kuyapigia kura.
他們把衪釘在十字架上以後,就拈鬮分了衪的衣服;
36 Wakaketi, wakawa wanamchunga.
然後坐在那看守衪。
37 Juu ya kichwa chake wakaweka shtaka dhidi yake lilioandikwa, “Huyu ni Yesu, Mfalme wa Wayahudi.”
在衪的頭上,巿放了衪的罪狀牌,寫著說:「這是猶太人的君王。」
38 Wanyang'anyi wawili walisulubishwa pia pamoja naye, mmoja upande wa kushoto na mwingine upande wa kulia.
當時與衪一起被釘在十字架上的,還有兩個強盜:一個在右邊,一個在左邊。
39 Watu waliokuwa wanapita mahali hapo walimtukana wakitikisa vichwa vyao na kusema,
路過的人都搖頭辱罵衪說:
40 “Wewe! Si ulijidai kulivunja Hekalu na kulijenga kwa siku tatu? Sasa jiokoe mwenyewe. Kama wewe ni Mwana wa Mungu, basi shuka msalabani!”
「你這拆毀聖殿而三日內重建起來的,救你自己吧! 如果你是天主子,從十字架上下來!」
41 Hali kadhalika na makuhani wakuu pamoja na walimu wa Sheria na wazee walimdhihaki wakisema,
司祭長和經師與長老們也同樣戲弄說:
42 “Aliwaokoa wengine, lakini kujiokoa mwenyewe hawezi! Eti yeye ni mfalme wa Wayahudi! Basi, sasa na ashuke msalabani, nasi tutamwamini.
「他救了別人,卻救不了自己;他既是以色列君王:如今從十架上下來吧!我們就信他。
43 Alimtumainia Mungu na kusema eti yeye ni Mwana wa Mungu; basi, Mungu na amwokoe kama anamtaka.”
他既信賴天主,天主如喜歡他,如今就該救他,因為他說過:我是天主子。」
44 Hali kadhalika na wale waliosulubiwa pamoja naye wakamtukana.
同衪一起釘在十字架上的強盜,也這樣譏誚衪。
45 Tangu saa sita mchana mpaka saa tisa, nchi yote ikawa katika giza.
從第六時辰起,直到第九時辰,遍地都黑暗了。
46 Mnamo saa tisa Yesu akalia kwa sauti kubwa, “Eli, Eli, lema sabakthani?” Maana yake, “Mungu wangu, Mungu wangu, mbona umeniacha?”
約莫第九辰,耶穌大聲喊說:「厄里,厄里,肋瑪撒巴黑塔尼!」就是說:「我的天主,我的天主,你為什麼捨棄了我?」
47 Lakini wale waliosimama pale waliposikia hivyo wakasema, “Anamwita Eliya.”
站在那裏的人中,有幾個聽見了就說:「這人呼喚厄里亞呢!」
48 Mmoja wao akakimbia, akachukua sifongo, akaichovya katika siki, akaiweka juu ya mwanzi, akampa anywe.
他們中遂有一個立刻跑去,拿了海綿,浸滿醋,綁在蘆葦上,遞給衪喝。
49 Wengine wakasema, “Acha tuone kama Eliya anakuja kumwokoa.”
其餘的卻說:「等一等,我們看,是否厄里亞來救他! 」
50 Basi, Yesu akalia tena kwa sauti kubwa, akakata roho.
耶穌又大喊一聲,遂交付了靈魂。
51 Hapo pazia la Hekalu likapasuka vipande viwili, toka juu mpaka chini; nchi ikatetemeka; miamba ikapasuka;
看,聖所的帳幔,從上到下分裂為二,大地震動,岩石崩裂,
52 makaburi yakafunguka na watu wengi wa Mungu waliokufa wakafufuliwa;
墳墓自開,許多長眠的聖者的身體復活了。
53 nao, baada ya kufufuka kwake, wakatoka makaburini, wakaingia katika Mji Mtakatifu, wakaonekana na watu wengi.
在耶穌復活後,他們由墳墓出來,進入聖城,發現給許多人。
54 Basi, jemadari na wale waliokuwa wakimlinda Yesu walipoona tetemeko la ardhi na yale mambo yaliyotukia, wakaogopa sana, wakasema, “Hakika mtu huyu alikuwa Mwana wa Mungu.”
百夫長和同衪一起看守耶穌的人,一見地動和所發生的事,就非常害怕說:「這人真是天主子。」
55 Mahali hapo walikuwapo wanawake wengi wakitazama kwa mbali. Hao ndio wale waliomfuata Yesu kutoka Galilaya wakimtumikia.
有許多婦女在那裏從遠處觀望,她們從加利肋亞就跟隨了耶穌為服事衪。
56 Miongoni mwao walikuwa Maria Magdalene, Maria mama yao Yakobo na Yosefu, pamoja na mama yao wana wa Zebedayo.
其中有瑪利亞瑪達肋納,雅各伯和若瑟的母親瑪利亞與載伯達兒子的母親。
57 Ilipokuwa jioni, akaja mtu mmoja tajiri mwenyeji wa Armathaya, jina lake Yosefu. Yeye pia alikuwa mwanafunzi wa Yesu.
到了傍晚,來了一個阿黎瑪特雅的富人,名叫若瑟,他也是耶穌的門徒。
58 Akamwendea Pilato, akaomba apewe mwili wa Yesu. Basi, Pilato akaamuru apewe.
這人去見比拉多請求耶穌的遺體,比拉多就下令交給他。
59 Yosefu akauchukua ule mwili akauzungushia sanda safi ya kitani,
若瑟領了耶穌的遺體,就用潔白的殮布將衪包好,
60 akauweka ndani ya kaburi lake jipya alilokuwa amelichonga katika mwamba. Kisha akavingirisha jiwe kubwa mbele ya mlango wa kaburi, akaenda zake.
安放在為自己於岩石間所鑿的新墓穴內;並把一塊大石滾到墓口,就走了。
61 Maria Magdalene na yule Maria mwingine walikuwa wameketi kulielekea kaburi.
在那裏還有瑪利亞瑪達肋納和另外一個瑪利亞,對著墳墓坐著。
62 Kesho yake, yaani siku iliyofuata ile ya Maandalio, makuhani wakuu na Mafarisayo walimwendea Pilato,
第二天,即預備日以後的那天,司祭長和法利賽人同來見比拉多
63 Wakasema, “Mheshimiwa, tunakumbuka kwamba yule mdanganyifu alisema kabla ya kufa ati, Baada ya siku tatu nitafufuka.
說:「大人,我們記得那個騙子活著的時候曾說過:三天以後我要復活。
64 Kwa hiyo amuru kaburi lilindwe mpaka siku ya tatu ili wanafunzi wake wasije wakamwiba na kuwaambia watu kwamba amefufuka. Uongo huu wa mwisho utakuwa mbaya kuliko ule wa awali.”
為此,請你下令,把守墳墓直到第三天;怕他的門徒來了,把他偷去,而對百姓說:他從死人中復活了。那最後的騙局,就比以前的更壞了!」
65 Pilato akawaambia, “Haya, mnao walinzi; nendeni mkalinde kadiri mjuavyo.”
比拉多對他們說:「你們可得一隊衛兵;你們去,照你們所知道的,好好看守。」
66 Basi, wakaenda, wakalilinda kaburi, wakatia mhuri juu ya lile jiwe na kuacha hapo askari walinzi.
他們就去,在石頭上加了封條,派駐兵把守墳墓。

< Mathayo 27 >