< Mathayo 23 >

1 Kisha Yesu akauambia umati wa watu pamoja na wanafunzi wake,
Then, Jesus spake unto the multitudes and unto his disciples,
2 “Walimu wa Sheria na Mafarisayo wana mamlaka ya kufafanua Sheria ya Mose.
saying—Upon Moses’ seat, have sat down, the Scribes and the Pharisees:
3 Kwa hiyo shikeni na kutekeleza chochote watakachowaambieni. Lakini msiyaige matendo yao, maana hawatekelezi yale wanayoyahubiri.
All things, therefore, whatsoever they tell you, do and observe, —but, according to their works, do ye not, for they, say, and do not, perform.
4 Hufunga mizigo mizito na kuwatwika watu mabegani, lakini wao wenyewe hawataki kunyosha hata kidole wapate kuibeba.
But they bind together heavy burdens, and lay upon men’s shoulders, whereas, they, with their finger, are not willing to move them.
5 Wao hufanya matendo yao yote ili watu wawaone. Huvaa tepe zenye maandishi ya Sheria juu ya panda la uso na mikononi na hupanua pindo za makoti yao.
But, all their works, they do, to be gazed at, by men, —for they make broad their amulets, and make large their fringes,
6 Hupenda nafasi za heshima katika karamu na viti vya heshima katika masunagogi.
And dearly love the first couch in the chief meals, and the first seats in the synagogues,
7 Hupenda kusalimiwa kwa heshima sokoni na kupendelea kuitwa na watu: Mwalimu.
And the salutations in the market-places, and to be called by men, Rabbi.
8 Lakini ninyi msiitwe kamwe Mwalimu, maana mwalimu wenu ni mmoja tu, nanyi nyote ni ndugu.
But, ye, —do not be called Rabbi, —for, one, is your Teacher, and, all ye, are brethren;
9 Wala msimwite mtu yeyote Baba hapa duniani, maana Baba yenu ni mmoja tu aliye mbinguni.
And, father, be none of you called, upon the earth, for, one, is your Father, the Heavenly;
10 Wala msiitwe Viongozi, maana kiongozi wenu ni mmoja tu, ndiye Kristo.
Neither be called leaders, for, your leader, is one, the Christ;
11 Aliye mkubwa miongoni mwenu ni lazima awe mtumishi wenu.
And, the greatest of you, shall be to you, a minister;
12 Anayejikweza atashushwa, na anayejishusha atakwezwa.
And, whoever shall exalt himself, shall be, abased, and, whoever shall abase himself, shall be, exalted,
13 “Ole wenu walimu wa Sheria na Mafarisayo, wanafiki! Mnaufunga mlango wa Ufalme wa mbinguni mbele ya macho ya watu. Ninyi wenyewe hamwingii ndani, wala hamwaruhusu wanaotaka kuingia waingie.
But alas for you, Scribes and Pharisees, hypocrites; because ye are locking up the kingdom of the heavens before men, —for, ye, are not entering, neither, them who are entering, suffer ye to enter.
14 Ole wenu walimu wa Sheria na Mafarisayo, wanafiki! Mnawanyonya wajane na kujisingizia kuwa watu wema kwa kusali sala ndefu. Kwa sababu hiyo mtapata adhabu kali.
15 “Ole wenu walimu wa Sheria na Mafarisayo, wanafiki! Mnasafiri baharini na nchi kavu ili kumpata mtu mmoja afuate dini yenu. Mnapompata, mnamfanya astahili maradufu kwenda katika moto wa Jehanamu kuliko ninyi wenyewe. (Geenna g1067)
Alas for you, Scribes and Pharisees, hypocrites: because ye compass sea and dry land, to make one convert—and, when it is done, ye make him a son of gehenna, twofold more than ye. (Geenna g1067)
16 “Ole wenu viongozi vipofu! Ninyi mwasema ati mtu akiapa kwa Hekalu, kiapo hicho si kitu; lakini akiapa kwa dhahabu ya Hekalu, kiapo hicho kinamshika.
Alas for you, blind guides! that say—Whosoever shall swear by the Temple, it is, nothing, but, whosoever shall swear by the gold of the Temple, is bound:
17 Enyi vipofu wapumbavu! Kipi kilicho cha maana zaidi: dhahabu au Hekalu linalofanya hiyo dhahabu kuwa takatifu?
Foolish and blind! for which is, greater, The gold, or the Temple that hath hallowed the gold?
18 Tena mwasema ati mtu akiapa kwa madhabahu si kitu; lakini akiapa kwa zawadi iliyowekwa juu ya madhabahu, kiapo hicho humshika.
And, whosoever shall swear by the altar, it is, nothing, but, whosoever shall swear by the gift that is upon it, is bound:
19 Enyi vipofu! Ni kipi kilicho cha maana zaidi: ile zawadi, au madhabahu ambayo hufanya hiyo zawadi kuwa takatifu?
Blind! for which is greater, The gift, or the altar that halloweth the gift?
20 Anayeapa kwa madhabahu ameapa kwa hiyo madhabahu, na kwa chochote kilichowekwa juu yake.
He therefore that hath sworn by the altar, sweareth by it, and by all that is upon it;
21 Na anayeapa kwa Hekalu ameapa kwa hilo Hekalu na pia kwa yule akaaye ndani yake.
And, he that hath sworn by the Temple, sweareth by it, and by him who dwelleth therein;
22 Na anayeapa kwa mbingu ameapa kwa kiti cha enzi cha Mungu, na kwa huyo aketiye juu yake.
And, he that hath sworn by heaven, sweareth by the throne of God, and by him who sitteth thereupon.
23 Ole wenu walimu wa Sheria na Mafarisayo, wanafiki! Mnatoza watu zaka, hata juu ya majani yenye harufu nzuri, bizari na jira, na huku mnaacha mambo muhimu ya Sheria kama vile haki, huruma na imani. Haya ndiyo hasa mliyopaswa kuyazingatia bila kusahau yale mengine.
Alas for you, Scribes and Pharisees, hypocrites; because ye tithe the mint and the anise and the cummin, —and have dismissed the weightier matters of the law—the justice, the mercy, and the faith; whereas, these, it was binding, to do, and, those, not to, dismiss.
24 Viongozi vipofu! Mnatoa nzi katika kinywaji, lakini mnameza ngamia!
Blind guides! Straining out the gnat, but, the camel, swallowing.
25 “Ole wenu walimu wa Sheria na Mafarisayo, wanafiki! Mnasafisha kikombe na bakuli kwa nje, lakini ndani mnaacha kumejaa vitu mlivyopata kwa unyang'anyi na uchoyo.
Alas for you, Scribes and Pharisees, hypocrites; because ye cleanse the outside of the cup and of the dish, —while, within, they are full of plunder and intemperance.
26 Mfarisayo kipofu! Kisafishe kikombe ndani kwanza na nje kutakuwa safi pia.
Blind Pharisee! cleanse, first, the inside, of the cup [and of the dish], that, the outside thereof, may become, clean.
27 “Ole wenu walimu wa Sheria na Mafarisayo, wanafiki! Mko kama makaburi yaliyopakwa chokaa ambayo kwa nje yanaonekana kuwa mazuri, lakini ndani yamejaa mifupa ya maiti na kila namna ya uchafu.
Alas for you, Scribes and Pharisees, hypocrites; because ye make yourselves like sepulchres whitewashed, which, outside, indeed, appear, beautiful, but, within, are full, of dead men’s bones and all uncleanness, —
28 Hali kadhalika ninyi mnaonekana na watu kwa nje kuwa wema, lakini kwa ndani mmejaa unafiki na uovu.
Thus, ye also, outside, indeed, appear to men, righteous, but, within, are full, of hypocrisy and lawlessness.
29 “Ole wenu walimu wa Sheria na Mafarisayo, wanafiki! Mnajenga makaburi ya manabii na kuyapamba makaburi ya watu wema.
Alas for you, Scribes and Pharisees, hypocrites; because ye build the sepulchres of the prophets, and adorn the monuments of the righteous,
30 Mwasema: Kama sisi tungaliishi nyakati za wazee wetu hatungalishirikiana nao katika mauaji ya manabii!
and say—If we had been in the days of our fathers, we would not have been their partners in the blood of the prophets:
31 Hivyo mnathibitisha ninyi wenyewe kwamba ninyi ni watoto wa watu waliowaua manabii.
So that ye bear witness against yourselves, that ye are, sons, of them who murdered the prophets.
32 Haya, kamilisheni ile kazi wazee wenu waliyoianza!
And, ye, fill ye up the measure of your fathers!
33 Enyi kizazi cha nyoka wenye sumu! Mnawezaje kuiepa hukumu ya moto wa Jehanamu? (Geenna g1067)
Serpents! broods of vipers! how should ye flee from the judgment of gehenna? (Geenna g1067)
34 Ndiyo maana mimi ninawapelekea ninyi manabii, watu wenye hekima na walimu; mtawaua na kuwasulubisha baadhi yao, na wengine mtawapiga viboko katika masunagogi yenu na kuwasaka katika kila mji.
For this cause, lo! I, send unto you, prophets and wise men and scribes, —some from among them, ye will slay and crucify, And some from among them ye will—scourge in your synagogues, and pursue from city to city:
35 Hivyo lawama yote itawapateni kwa ajili ya damu yote ya watu wema iliyomwagwa juu ya ardhi. Naam, tangu kuuawa kwa Abeli ambaye hakuwa na hatia, mpaka kuuawa kwa Zakariya, mwana wa Barakia, ambaye mlimuua Hekaluni kati ya patakatifu na madhabahu.
That there may come upon you—all righteous blood poured out upon the earth, from the blood of Abel the righteous, unto the blood of Zachariah, son of Barachiah, whom ye murdered between the Temple and the altar.
36 Nawaambieni kweli, kizazi hiki kitapata adhabu kwa sababu ya mambo haya.
Verily, I say unto you—All these things, will have come, upon this generation.
37 “Yerusalemu, Ee Yerusalemu! Unawaua manabii na kuwapiga mawe wale waliotumwa kwako. Mara ngapi nimejaribu kuwakusanya watoto wako kwangu, kama vile kuku anavyokusanya vifaranga vyake chini ya mabawa yake, lakini hukutaka.
Jerusalem! Jerusalem! that slayeth the prophets, and stoneth them that have been sent unto her, —how often, would I have gathered thy children, like as a hen gathereth her chickens under her wings, —and ye would not!
38 Haya basi, nyumba yako itaachwa mahame.
Lo! your house is left to you;
39 Nakwambia kweli, hutaniona tena mpaka wakati utakaposema: Abarikiwe huyo ajaye kwa jina la Bwana.”
For I say unto you—in no wise, may ye see me, henceforth, until ye say, Blessed, is he that cometh, in the name of the Lord!

< Mathayo 23 >