< Mathayo 23 >
1 Kisha Yesu akauambia umati wa watu pamoja na wanafunzi wake,
Then spake Iesus to the multitude, and to his disciples,
2 “Walimu wa Sheria na Mafarisayo wana mamlaka ya kufafanua Sheria ya Mose.
Saying, The Scribes and the Pharises sit in Moses seate.
3 Kwa hiyo shikeni na kutekeleza chochote watakachowaambieni. Lakini msiyaige matendo yao, maana hawatekelezi yale wanayoyahubiri.
All therefore whatsoeuer they bid you obserue, that obserue and doe: but after their workes doe not: for they say, and doe not.
4 Hufunga mizigo mizito na kuwatwika watu mabegani, lakini wao wenyewe hawataki kunyosha hata kidole wapate kuibeba.
For they binde heauie burdens, and grieuous to be borne, and lay them on mens shoulders, but they themselues will not moue them with one of their fingers.
5 Wao hufanya matendo yao yote ili watu wawaone. Huvaa tepe zenye maandishi ya Sheria juu ya panda la uso na mikononi na hupanua pindo za makoti yao.
All their workes they doe for to be seene of men: for they make their phylacteries broad, and make long the frindges of their garments,
6 Hupenda nafasi za heshima katika karamu na viti vya heshima katika masunagogi.
And loue the chiefe place at feastes, and to haue the chiefe seates in the assemblies,
7 Hupenda kusalimiwa kwa heshima sokoni na kupendelea kuitwa na watu: Mwalimu.
And greetings in the markets, and to be called of men, Rabbi, Rabbi.
8 Lakini ninyi msiitwe kamwe Mwalimu, maana mwalimu wenu ni mmoja tu, nanyi nyote ni ndugu.
But be not ye called, Rabbi: for one is your doctour, to wit, Christ, and all ye are brethren.
9 Wala msimwite mtu yeyote Baba hapa duniani, maana Baba yenu ni mmoja tu aliye mbinguni.
And call no man your father vpon the earth: for there is but one, your father which is in heauen.
10 Wala msiitwe Viongozi, maana kiongozi wenu ni mmoja tu, ndiye Kristo.
Be not called doctours: for one is your doctour, euen Christ.
11 Aliye mkubwa miongoni mwenu ni lazima awe mtumishi wenu.
But he that is greatest among you, let him be your seruant.
12 Anayejikweza atashushwa, na anayejishusha atakwezwa.
For whosoeuer will exalt himselfe, shall be brought lowe: and whosoeuer will humble himselfe, shalbe exalted.
13 “Ole wenu walimu wa Sheria na Mafarisayo, wanafiki! Mnaufunga mlango wa Ufalme wa mbinguni mbele ya macho ya watu. Ninyi wenyewe hamwingii ndani, wala hamwaruhusu wanaotaka kuingia waingie.
Wo therefore be vnto you, Scribes and Pharises, hypocrites, because ye shut vp the kingdome of heauen before men: for ye your selues go not in, neither suffer ye them that would enter, to come in.
14 Ole wenu walimu wa Sheria na Mafarisayo, wanafiki! Mnawanyonya wajane na kujisingizia kuwa watu wema kwa kusali sala ndefu. Kwa sababu hiyo mtapata adhabu kali.
Wo be vnto you, Scribes and Pharises, hypocrites: for ye deuoure widowes houses, euen vnder a colour of long prayers: wherefore ye shall receiue the greater damnation.
15 “Ole wenu walimu wa Sheria na Mafarisayo, wanafiki! Mnasafiri baharini na nchi kavu ili kumpata mtu mmoja afuate dini yenu. Mnapompata, mnamfanya astahili maradufu kwenda katika moto wa Jehanamu kuliko ninyi wenyewe. (Geenna )
Wo be vnto you, Scribes and Pharises, hypocrites: for ye compasse sea and land to make one of your profession: and when he is made, ye make him two folde more the childe of hell, then you your selues. (Geenna )
16 “Ole wenu viongozi vipofu! Ninyi mwasema ati mtu akiapa kwa Hekalu, kiapo hicho si kitu; lakini akiapa kwa dhahabu ya Hekalu, kiapo hicho kinamshika.
Wo be vnto you blinde guides, which say, Whosoeuer sweareth by the Temple, it is nothing: but whosoeuer sweareth by the golde of the Temple, he offendeth.
17 Enyi vipofu wapumbavu! Kipi kilicho cha maana zaidi: dhahabu au Hekalu linalofanya hiyo dhahabu kuwa takatifu?
Ye fooles and blinde, whether is greater, the golde, or the Temple that sanctifieth the golde?
18 Tena mwasema ati mtu akiapa kwa madhabahu si kitu; lakini akiapa kwa zawadi iliyowekwa juu ya madhabahu, kiapo hicho humshika.
And whosoeuer sweareth by the altar, it is nothing: but whosoeuer sweareth by the offering that is vpon it, offendeth.
19 Enyi vipofu! Ni kipi kilicho cha maana zaidi: ile zawadi, au madhabahu ambayo hufanya hiyo zawadi kuwa takatifu?
Ye fooles and blinde, whether is greater, the offering, or the altar which sanctifieth the offering?
20 Anayeapa kwa madhabahu ameapa kwa hiyo madhabahu, na kwa chochote kilichowekwa juu yake.
Whosoeuer therefore sweareth by the altar, sweareth by it, and by all things thereon.
21 Na anayeapa kwa Hekalu ameapa kwa hilo Hekalu na pia kwa yule akaaye ndani yake.
And whosoeuer sweareth by the Temple, sweareth by it, and by him that dwelleth therein.
22 Na anayeapa kwa mbingu ameapa kwa kiti cha enzi cha Mungu, na kwa huyo aketiye juu yake.
And he that sweareth by heauen, sweareth by the throne of God, and by him that sitteth thereon.
23 Ole wenu walimu wa Sheria na Mafarisayo, wanafiki! Mnatoza watu zaka, hata juu ya majani yenye harufu nzuri, bizari na jira, na huku mnaacha mambo muhimu ya Sheria kama vile haki, huruma na imani. Haya ndiyo hasa mliyopaswa kuyazingatia bila kusahau yale mengine.
Wo be to you, Scribes and Pharises, hypocrites: for ye tithe mynt, and annyse, and cummyn, and leaue the weightier matters of the law, as iudgement, and mercy and fidelitie. These ought ye to haue done, and not to haue left the other.
24 Viongozi vipofu! Mnatoa nzi katika kinywaji, lakini mnameza ngamia!
Ye blinde guides, which straine out a gnat, and swallowe a camell.
25 “Ole wenu walimu wa Sheria na Mafarisayo, wanafiki! Mnasafisha kikombe na bakuli kwa nje, lakini ndani mnaacha kumejaa vitu mlivyopata kwa unyang'anyi na uchoyo.
Wo be to you, Scribes and Pharises, hypocrites: for ye make cleane the vtter side of the cup, and of the platter: but within they are ful of briberie and excesse.
26 Mfarisayo kipofu! Kisafishe kikombe ndani kwanza na nje kutakuwa safi pia.
Thou blinde Pharise, cleanse first the inside of the cup and platter, that the outside of them may be cleane also.
27 “Ole wenu walimu wa Sheria na Mafarisayo, wanafiki! Mko kama makaburi yaliyopakwa chokaa ambayo kwa nje yanaonekana kuwa mazuri, lakini ndani yamejaa mifupa ya maiti na kila namna ya uchafu.
Wo be to you, Scribes and Pharises, hypocrites: for ye are like vnto whited tombes, which appeare beautifull outward, but are within full of dead mens bones, and all filthines.
28 Hali kadhalika ninyi mnaonekana na watu kwa nje kuwa wema, lakini kwa ndani mmejaa unafiki na uovu.
So are ye also: for outwarde ye appeare righteous vnto men, but within ye are full of hypocrisie and iniquitie.
29 “Ole wenu walimu wa Sheria na Mafarisayo, wanafiki! Mnajenga makaburi ya manabii na kuyapamba makaburi ya watu wema.
Wo be vnto you, Scribes and Pharises, hypocrites: for ye build the tombes of the Prophets, and garnish the sepulchres of the righteous,
30 Mwasema: Kama sisi tungaliishi nyakati za wazee wetu hatungalishirikiana nao katika mauaji ya manabii!
And say, If we had bene in the dayes of our fathers, we would not haue bene partners with them in the blood of the Prophets.
31 Hivyo mnathibitisha ninyi wenyewe kwamba ninyi ni watoto wa watu waliowaua manabii.
So then ye be witnesses vnto your selues, that ye are the children of them that murthered the Prophets.
32 Haya, kamilisheni ile kazi wazee wenu waliyoianza!
Fulfill ye also ye measure of your fathers.
33 Enyi kizazi cha nyoka wenye sumu! Mnawezaje kuiepa hukumu ya moto wa Jehanamu? (Geenna )
O serpents, the generation of vipers, howe should ye escape the damnation of hell! (Geenna )
34 Ndiyo maana mimi ninawapelekea ninyi manabii, watu wenye hekima na walimu; mtawaua na kuwasulubisha baadhi yao, na wengine mtawapiga viboko katika masunagogi yenu na kuwasaka katika kila mji.
Wherefore beholde, I send vnto you Prophets, and wise men, and Scribes, and of them ye shall kill and crucifie: and of them shall ye scourge in your Synagogues, and persecute from citie to citie,
35 Hivyo lawama yote itawapateni kwa ajili ya damu yote ya watu wema iliyomwagwa juu ya ardhi. Naam, tangu kuuawa kwa Abeli ambaye hakuwa na hatia, mpaka kuuawa kwa Zakariya, mwana wa Barakia, ambaye mlimuua Hekaluni kati ya patakatifu na madhabahu.
That vpon you may come all the righteous blood that was shed vpon the earth, from the blood of Abel the righteous, vnto the blood of Zacharias the sonne of Barachias, whome ye slewe betweene the Temple and the altar.
36 Nawaambieni kweli, kizazi hiki kitapata adhabu kwa sababu ya mambo haya.
Verely I say vnto you, all these things shall come vpon this generation.
37 “Yerusalemu, Ee Yerusalemu! Unawaua manabii na kuwapiga mawe wale waliotumwa kwako. Mara ngapi nimejaribu kuwakusanya watoto wako kwangu, kama vile kuku anavyokusanya vifaranga vyake chini ya mabawa yake, lakini hukutaka.
Hierusalem, Hierusalem, which killest the Prophets, and stonest them which are sent to thee, how often would I haue gathered thy children together, as the henne gathereth her chickins vnder her wings, and ye would not!
38 Haya basi, nyumba yako itaachwa mahame.
Beholde, your habitation shalbe left vnto you desolate,
39 Nakwambia kweli, hutaniona tena mpaka wakati utakaposema: Abarikiwe huyo ajaye kwa jina la Bwana.”
For I say vnto you, ye shall not see mee henceforth till that ye say, Blessed is he that commeth in the Name of the Lord.