< Mathayo 20 >
1 “Ufalme wa mbinguni unafanana na mtu mwenye shamba la mizabibu, ambaye alitoka asubuhi na mapema kuwaajiri wafanyakazi katika shamba lake.
PWE wein nanlang rasong kaun pan im amen, me sangkonai ong raparapaki toundodok kai nan a mat en wain.
2 Akapatana nao kuwalipa dinari moja kwa siku, kisha akawapeleka katika shamba lake la mizabibu.
Irail lao inauki pena, me denar eu ni ran eu, ap kadar ir ala nan a mat en wain.
3 Akatoka mnamo saa tatu asubuhi, akaona watu wengine wamesimama sokoni, hawana kazi.
A pil kotila ni auer kasilu, ap masani akai, me momod mal nan deun saunet akan,
4 Akawaambia, Nendeni nanyi mkafanye kazi katika shamba la mizabibu, nami nitawapeni haki yenu.
Ap masani ong irail: Komail pil kola nan mat en wain o, o meakot me pung, i pan pwain ong komail; irail ari kola.
5 Basi, wakaenda. Huyo mwenye shamba akatoka tena mnamo saa sita na saa tisa, akafanya vivyo hivyo.
A pil kola ni auer kawonu o kaduau o wiadar dueta.
6 Hata mnamo saa kumi na moja jioni, akatoka tena; akakuta watu wengine wamesimama pale sokoni. Basi, akawauliza, Mbona mmesimama hapa mchana kutwa bila kazi?
A pil kotila ni auer eisokeu, ap diaradar akai, me momod mal, ap masani ong irail: Da me komail momodeki mal ran pon?
7 Wakamjibu: Kwa sababu hakuna mtu aliyetuajiri. Yeye akawaambia, Nendeni nanyi mkafanye kazi katika shamba la mizabibu.
Irail potoan ong: Aki sota amen, me kadokeki kit. Ap masani ong irail: Komail pil kola nan mat en wain o, komail pan ale me pung.
8 “Kulipokuchwa, huyo mwenye shamba alimwambia mtunza hazina wake, Waite wafanyakazi ukawalipe mshahara wao, ukianzia na wale walioajiriwa mwisho, na kumalizia na wale wa kwanza.
A lao sautik penaer monsap en mat en wain masani ong a saunkoa: Kapokon pena toundodok kan o pwain ong irail. Tapiada sang ren men pwand oko lao kokodo lel men madang kan,
9 Basi, wakaja wale walioajiriwa mnamo saa kumi na moja, wakapokea kila mmoja dinari moja.
Me kadodokier ni klok eisokeu kan ap kodo, amen amen ap ale denar eu.
10 Wale wa kwanza walipofika, walikuwa wanadhani watapewa zaidi; lakini hata wao wakapewa kila mmoja dinari moja.
A men mas akan lao kodo, rap kiki ong, me re pan ale siki sang, a re pil aleer denar ta ieu.
11 Wakazipokea fedha zao, wakaanza kumnung'unikia yule bwana.
Irail lao ale, rap lipaned ong monsap o.
12 Wakasema, Watu hawa walioajiriwa mwisho walifanya kazi kwa muda wa saa moja tu, mbona umetutendea sawa na wao hali sisi tumevumilia kazi ngumu kutwa na jua kali?
Indada: Mepukat dodok auer ta ieu, a komui karasai kit pena; kit me dodokki apwal en ran o karakar en katipin.
13 “Hapo yule bwana akamjibu mmoja wao, Rafiki, sikukupunja kitu! Je, hukupatana nami mshahara wa denari moja?
A ap kotin sapeng masani ong amen re’rail: Kompoke pai, kaidin me sapung, me i wiai ong uk. Kita sota inauki pena denar eu?
14 Chukua haki yako, uende zako. Napenda kumpa huyu wa mwisho sawa na wewe.
Ale me om, kowei, i men pwain ong me pwand pukat rasong uk.
15 Je, sina haki ya kufanya na mali yangu nipendavyo? Je, unaona kijicho kwa kuwa mimi ni mwema?”
De iaduen, a sota pung, i en wiaki me udan ai, me i mauki? De por en mas om me sued pweki ai kadek?
16 Yesu akamaliza kwa kusema, “Hivyo, walio wa mwisho watakuwa wa kwanza na wa kwanza watakuwa wa mwisho.”
Ari, me pwand akan pan moa, a me moa kan pan pwand, pwe me toto paeker, a me malaulau me piladar.
17 Yesu alipokuwa anakwenda Yerusalemu, aliwachukua wale wanafunzi kumi na wawili faraghani, na njiani akawaambia,
Iesus lao kotin kodala Ierusalem, a kotin kelepe kila tounpadak ekriamen pon al a, masani ong irail:
18 “Sikilizeni! Tunakwenda Yerusalemu, na huko Mwana wa Mtu atakabidhiwa kwa makuhani wakuu na walimu wa Sheria, nao watamhukumu auawe.
Kilang, kitail kin kodalang Ierusalem o Nain aramas pan ko ong ren samero lapalap o saunkawewe kan, o irail pan kadeikada, en kamela i.
19 Watamkabidhi kwa watu wa mataifa mengine ili adhihakiwe, apigwe viboko na kusulubiwa; lakini siku ya tatu atafufuliwa.”
O re pan pangala i ren men liki kan, pwen kapikapiti i, o kaloke, o kalopuela, a ni ran kasilu a pan maureda.
20 Hapo mama yao wana wa Zebedayo alimjia Yesu pamoja na wanawe, akapiga magoti mbele yake na kumwomba kitu.
In en nain Sepedäus ap poto dong i, a na putak riamen iang i, pongi i o poeki okotme re a.
21 Yesu akamwuliza, “Unataka nini?” Huyo mama akamwambia, “Ahidi kwamba katika Ufalme wako, hawa wanangu wawili watakaa mmoja upande wako wa kulia na mwingine upande wako wa kushoto.”
A ap kotin masani ong i: Da me koe mauki? A potoan ong i: Re kotin mueid ong ai tungol putak riamen, en mondi re ir, amen ni pali maun omui, amen ni pali maing omui nan omui wei.
22 Yesu akajibu, “Hamjui mnaomba nini. Je, mnaweza kunywa kikombe nitakachokunywa mimi?” Wakamjibu, “Tunaweza.”
A Iesus kotin sapeng masani: Koma sota asa, me koma poeki. Koma kak nim dal me I pan nim? Ira potoan ong: Se kak.
23 Yesu akawaambia, “Kweli mtakunywa kikombe changu, lakini kuketi kulia au kushoto kwangu si kazi yangu kupanga; jambo hilo watapewa wale waliowekewa tayari na Baba yangu.”
A kotin masani ong ira: Melel, komail pan tungole ai dal, a momod ni pali maun o maing i, I sota kak mueid ong, pwe pwais en irail me a onop onger sang ren Sam ai.
24 Wale wanafunzi wengine kumi waliposikia hayo, wakawakasirikia hao ndugu wawili.
Ni en ek oko ar rongadar, ap suede kidar pirien o.
25 Hivyo Yesu akawaita, akawaambia, “Mnajua kwamba watawala wa mataifa hutawala watu wao kwa mabavu na wakuu hao huwamiliki watu wao.
A Iesus kotin molipe ir do masani: Komail asa, duen saupeidi en wei pokon ar kin poe irail edi, o me lapalap akan kin manaman ong irail.
26 Lakini kwenu isiwe hivyo, ila yeyote anayetaka kuwa mkuu kati yenu sharti awe mtumishi wa wote;
A duen met a sota pan wiaui nan pung omail. A me men laud nan pung omail, en papa komail.
27 na anayetaka kuwa wa kwanza kati yenu sharti awe mtumishi wenu.
O meamen re omail, me men saumas, i en lidui komail.
28 Jinsi hiyohiyo, Mwana wa Mtu hakuja kutumikiwa, bali kutumikia na kutoa maisha yake kuwa fidia ya watu wengi.”
Dueta Nain aramas, me kaidin kodo, pwe aramas en papa, a pwe i en papa o kida maur a wiliandi me toto.
29 Yesu alipokuwa anaondoka mjini Yeriko, umati wa watu ulimfuata.
Ni arail kotila sang Ieriko, pokon kalaimun idauen la i.
30 Basi, kulikuwa na vipofu wawili wameketi kando ya njia, na waliposikia kwamba Yesu alikuwa anapitia hapo, walipaaza sauti: “Mheshimiwa, Mwana wa Daudi, utuhurumie!”
A kilang, ol maskun riamen momod ni kailan al o. Ni ara rongadar, me Iesus kotin daulul, ira ap likelikwir indada: Maing kupura kit, ir me sapwilim en Dawid!
31 Ule umati wa watu ukawakemea na kuwaambia wanyamaze. Lakini wao wakazidi kupaaza sauti: “Mheshimiwa, Mwana wa Daudi, utuhurumie!”
A pokon o kidau ira da, pwen nenenla. A ira kalaudela ara likelikwir indada: Maing, kupura kit, ir me sapwilim en Dawid!
32 Yesu akasimama, akawaita na kuwauliza, “Mnataka niwafanyie nini?”
Iesus ari kotin udi, molipe ira do masani: Da me koma mauki, I en wiai ong koma?
33 Wakamjibu, “Mheshimiwa, tunaomba macho yetu yafumbuliwe.”
Ira potoan ong: Maing, mas at en kapad pasang!
34 Basi, Yesu akawaonea huruma, akawagusa macho yao, na papo hapo wakaweza kuona, wakamfuata.
Iesus ari kupuro kin ira dar o kotin sair mas ara. Mas ara ari madang pad pasanger; ira ap idauenla i.