< Mathayo 20 >
1 “Ufalme wa mbinguni unafanana na mtu mwenye shamba la mizabibu, ambaye alitoka asubuhi na mapema kuwaajiri wafanyakazi katika shamba lake.
«En effet, le royaume des cieux est semblable à un chef de famille, qui sortit dès le matin, afin de louer des ouvriers pour sa vigne.
2 Akapatana nao kuwalipa dinari moja kwa siku, kisha akawapeleka katika shamba lake la mizabibu.
Il fit accord avec eux à raison d'un denier par jour, et les envoya à sa vigne.
3 Akatoka mnamo saa tatu asubuhi, akaona watu wengine wamesimama sokoni, hawana kazi.
Il sortit vers la troisième heure, et ayant vu d'autres ouvriers qui étaient sur la place, sans rien faire,
4 Akawaambia, Nendeni nanyi mkafanye kazi katika shamba la mizabibu, nami nitawapeni haki yenu.
il leur dit: «Allez, vous aussi à ma vigne, et je vous donnerai ce qui sera raisonnable; » et ils y allèrent.
5 Basi, wakaenda. Huyo mwenye shamba akatoka tena mnamo saa sita na saa tisa, akafanya vivyo hivyo.
Il sortit encore vers la sixième heure et vers la neuvième, et fit de même.
6 Hata mnamo saa kumi na moja jioni, akatoka tena; akakuta watu wengine wamesimama pale sokoni. Basi, akawauliza, Mbona mmesimama hapa mchana kutwa bila kazi?
Etant sorti vers la onzième heure, il en trouva d'autres qui se tenaient sur la place, et leur dit: «Pourquoi vous tenez-vous ici toute la journée, sans rien faire?»
7 Wakamjibu: Kwa sababu hakuna mtu aliyetuajiri. Yeye akawaambia, Nendeni nanyi mkafanye kazi katika shamba la mizabibu.
— «C'est que personne, lui dirent-ils, ne nous a loués.» Et il leur dit: «Allez, vous aussi, à ma vigne.»
8 “Kulipokuchwa, huyo mwenye shamba alimwambia mtunza hazina wake, Waite wafanyakazi ukawalipe mshahara wao, ukianzia na wale walioajiriwa mwisho, na kumalizia na wale wa kwanza.
Quand le soir fut venu, le maître de la vigne dit à son intendant: «Appelle les ouvriers, et leur donne leur salaire, en allant des derniers aux premiers.»
9 Basi, wakaja wale walioajiriwa mnamo saa kumi na moja, wakapokea kila mmoja dinari moja.
Les ouvriers loués à la onzième heure vinrent, et reçurent chacun un denier.
10 Wale wa kwanza walipofika, walikuwa wanadhani watapewa zaidi; lakini hata wao wakapewa kila mmoja dinari moja.
Puis vinrent les premiers, qui croyaient recevoir davantage, et ils reçurent, eux aussi, un denier chacun.
11 Wakazipokea fedha zao, wakaanza kumnung'unikia yule bwana.
En le touchant, ils murmuraient contre le maître, et disaient:
12 Wakasema, Watu hawa walioajiriwa mwisho walifanya kazi kwa muda wa saa moja tu, mbona umetutendea sawa na wao hali sisi tumevumilia kazi ngumu kutwa na jua kali?
«Ces derniers n'ont fait qu'une heure, et tu les mets sur le même pied que nous, qui avons supporté la fatigue et l'ardeur brûlante du jour.»
13 “Hapo yule bwana akamjibu mmoja wao, Rafiki, sikukupunja kitu! Je, hukupatana nami mshahara wa denari moja?
Mais le maître, prenant la parole, dit à l'un d'eux: «Mon ami, je ne te fais point de tort: n'es-tu pas convenu d'un denier avec moi?
14 Chukua haki yako, uende zako. Napenda kumpa huyu wa mwisho sawa na wewe.
Prends ce qui te revient, et t'en va. Pour moi, je veux donner à ce dernier autant qu'à toi.
15 Je, sina haki ya kufanya na mali yangu nipendavyo? Je, unaona kijicho kwa kuwa mimi ni mwema?”
Ne suis-je pas libre de faire ce que je veux de mon bien? ou vois-tu de mauvais oeil que je sois bon?»
16 Yesu akamaliza kwa kusema, “Hivyo, walio wa mwisho watakuwa wa kwanza na wa kwanza watakuwa wa mwisho.”
Ainsi les derniers seront les premiers, et les premiers seront les derniers.»
17 Yesu alipokuwa anakwenda Yerusalemu, aliwachukua wale wanafunzi kumi na wawili faraghani, na njiani akawaambia,
Comme Jésus montait à Jérusalem, il prit à part les douze disciples, en chemin, et leur dit:
18 “Sikilizeni! Tunakwenda Yerusalemu, na huko Mwana wa Mtu atakabidhiwa kwa makuhani wakuu na walimu wa Sheria, nao watamhukumu auawe.
«Voici que nous montons à Jérusalem, et le Fils de l'homme sera livré aux principaux sacrificateurs et aux scribes: ils le condamneront à mort
19 Watamkabidhi kwa watu wa mataifa mengine ili adhihakiwe, apigwe viboko na kusulubiwa; lakini siku ya tatu atafufuliwa.”
et le livreront aux Gentils, pour le bafouer, le flageller et le crucifier; mais, le troisième jour, il ressuscitera.»
20 Hapo mama yao wana wa Zebedayo alimjia Yesu pamoja na wanawe, akapiga magoti mbele yake na kumwomba kitu.
Alors la mère des fils de Zébédée s'approcha de lui avec ses fils, et se prosterna pour lui faire une demande.
21 Yesu akamwuliza, “Unataka nini?” Huyo mama akamwambia, “Ahidi kwamba katika Ufalme wako, hawa wanangu wawili watakaa mmoja upande wako wa kulia na mwingine upande wako wa kushoto.”
Jésus lui dit: «Que veux-tu?» — «Ordonne, dit-elle, que mes deux fils que voici, soient assis, l'un à ta droite, l'autre à ta gauche, dans ton royaume.»
22 Yesu akajibu, “Hamjui mnaomba nini. Je, mnaweza kunywa kikombe nitakachokunywa mimi?” Wakamjibu, “Tunaweza.”
Jésus répondit: «Vous ne savez ce que vous demandez. Pouvez-vous boire le calice que je dois boire?» — «Nous le pouvons, » dirent-ils.
23 Yesu akawaambia, “Kweli mtakunywa kikombe changu, lakini kuketi kulia au kushoto kwangu si kazi yangu kupanga; jambo hilo watapewa wale waliowekewa tayari na Baba yangu.”
Et Jésus répondit: «Oui, vous boirez mon calice; quant à être assis à ma droite et à ma gauche, il ne m'appartient pas de l'accorder: cette distinction sera pour ceux à qui mon Père l'a réservée.»
24 Wale wanafunzi wengine kumi waliposikia hayo, wakawakasirikia hao ndugu wawili.
Les dix autres disciples, ayant entendu cette demande, furent irrités contre les deux frères.
25 Hivyo Yesu akawaita, akawaambia, “Mnajua kwamba watawala wa mataifa hutawala watu wao kwa mabavu na wakuu hao huwamiliki watu wao.
Jésus les appela, et leur dit: «Vous savez que les princes des nations les maîtrisent, et que les grands les dominent.
26 Lakini kwenu isiwe hivyo, ila yeyote anayetaka kuwa mkuu kati yenu sharti awe mtumishi wa wote;
Il n'en sera point ainsi parmi vous; mais que celui qui aspire à être grand parmi vous, soit votre serviteur,
27 na anayetaka kuwa wa kwanza kati yenu sharti awe mtumishi wenu.
et que celui qui veut être le premier parmi vous, soit votre esclave.
28 Jinsi hiyohiyo, Mwana wa Mtu hakuja kutumikiwa, bali kutumikia na kutoa maisha yake kuwa fidia ya watu wengi.”
C'est ainsi que le Fils de l'homme est venu, non pour être servi, mais pour servir et donner sa vie pour la rançon de beaucoup.»
29 Yesu alipokuwa anaondoka mjini Yeriko, umati wa watu ulimfuata.
Comme ils sortaient de Jéricho, une grande foule suivit Jésus.
30 Basi, kulikuwa na vipofu wawili wameketi kando ya njia, na waliposikia kwamba Yesu alikuwa anapitia hapo, walipaaza sauti: “Mheshimiwa, Mwana wa Daudi, utuhurumie!”
Deux aveugles assis au bord de la route, entendant dire que Jésus passait, se mirent à crier: «Aie pitié de nous, Seigneur, Fils de David.»
31 Ule umati wa watu ukawakemea na kuwaambia wanyamaze. Lakini wao wakazidi kupaaza sauti: “Mheshimiwa, Mwana wa Daudi, utuhurumie!”
La foule les reprenait pour les faire taire; mais ils criaient plus fort: «Aie pitié de nous, Seigneur, Fils de David.»
32 Yesu akasimama, akawaita na kuwauliza, “Mnataka niwafanyie nini?”
Jésus s'arrêta, les appela, et leur dit: «Que voulez-vous que je vous fasse?»
33 Wakamjibu, “Mheshimiwa, tunaomba macho yetu yafumbuliwe.”
Ils lui dirent: «Seigneur, que nous recouvrions la vue.»
34 Basi, Yesu akawaonea huruma, akawagusa macho yao, na papo hapo wakaweza kuona, wakamfuata.
Jésus, ému de compassion, leur toucha les yeux: et aussitôt ils recouvrèrent la vue et le suivirent.