< Mathayo 20 >
1 “Ufalme wa mbinguni unafanana na mtu mwenye shamba la mizabibu, ambaye alitoka asubuhi na mapema kuwaajiri wafanyakazi katika shamba lake.
"For the kingdom of heaven is like a householder who went out at dawn to hire workmen for his vineyard.
2 Akapatana nao kuwalipa dinari moja kwa siku, kisha akawapeleka katika shamba lake la mizabibu.
"And when he had agreed with the workmen for two shillings a day, he sent them into his vineyard.
3 Akatoka mnamo saa tatu asubuhi, akaona watu wengine wamesimama sokoni, hawana kazi.
"About nine o’clock he went out and noticed some other workmen standing idle in the market-place;
4 Akawaambia, Nendeni nanyi mkafanye kazi katika shamba la mizabibu, nami nitawapeni haki yenu.
"and he said to them, "‘Do you also go into the vineyard, and whatever is just I will pay you.’
5 Basi, wakaenda. Huyo mwenye shamba akatoka tena mnamo saa sita na saa tisa, akafanya vivyo hivyo.
"So they went. Again at noon, and about three o’clock, he went out and did the same thing.
6 Hata mnamo saa kumi na moja jioni, akatoka tena; akakuta watu wengine wamesimama pale sokoni. Basi, akawauliza, Mbona mmesimama hapa mchana kutwa bila kazi?
"When he went out about five o’clock, he found others standing around, and said to them, "‘Why have you been standing here idle, all the day long?’
7 Wakamjibu: Kwa sababu hakuna mtu aliyetuajiri. Yeye akawaambia, Nendeni nanyi mkafanye kazi katika shamba la mizabibu.
"‘Because no one has hired us,’ they replied. "He said to them, ‘Do you also go into the vineyard.’
8 “Kulipokuchwa, huyo mwenye shamba alimwambia mtunza hazina wake, Waite wafanyakazi ukawalipe mshahara wao, ukianzia na wale walioajiriwa mwisho, na kumalizia na wale wa kwanza.
"And when evening came, the Lord of the vineyard said to his steward, "‘Call the workmen and pay them their wages, beginning with the last hired and ending with the first.’
9 Basi, wakaja wale walioajiriwa mnamo saa kumi na moja, wakapokea kila mmoja dinari moja.
"When those came who had begun at five o’clock, they received two shillings apiece;
10 Wale wa kwanza walipofika, walikuwa wanadhani watapewa zaidi; lakini hata wao wakapewa kila mmoja dinari moja.
"and when the first came they supposed that they would get more, but they also received each two shillings.
11 Wakazipokea fedha zao, wakaanza kumnung'unikia yule bwana.
"And as they took it they began to grumble against the master of the house.
12 Wakasema, Watu hawa walioajiriwa mwisho walifanya kazi kwa muda wa saa moja tu, mbona umetutendea sawa na wao hali sisi tumevumilia kazi ngumu kutwa na jua kali?
"‘Those last men,’ they said, ‘have toiled only one hour, and you have made them equal to us who have borne the burden and the burning heat of the day.’
13 “Hapo yule bwana akamjibu mmoja wao, Rafiki, sikukupunja kitu! Je, hukupatana nami mshahara wa denari moja?
"In reply he said to one of them. ‘My friend, I am doing no wrong. Did you not agree with me for two shillings?
14 Chukua haki yako, uende zako. Napenda kumpa huyu wa mwisho sawa na wewe.
"Take your wage and begone! I chose to give to this last man the same as to you.
15 Je, sina haki ya kufanya na mali yangu nipendavyo? Je, unaona kijicho kwa kuwa mimi ni mwema?”
"Have I not the right to do what I choose with my own property? Or is your eye evil because I am generous?’
16 Yesu akamaliza kwa kusema, “Hivyo, walio wa mwisho watakuwa wa kwanza na wa kwanza watakuwa wa mwisho.”
"So the last shall be first, and the first, last."
17 Yesu alipokuwa anakwenda Yerusalemu, aliwachukua wale wanafunzi kumi na wawili faraghani, na njiani akawaambia,
When Jesus was about to go up to Jerusalem, he took the Twelve aside by themselves, and as they went he said to them.
18 “Sikilizeni! Tunakwenda Yerusalemu, na huko Mwana wa Mtu atakabidhiwa kwa makuhani wakuu na walimu wa Sheria, nao watamhukumu auawe.
"Look! We are on the way up to Jerusalem, and the Son of man will be betrayed to the chief priests and the scribes. They will condemn him to death,
19 Watamkabidhi kwa watu wa mataifa mengine ili adhihakiwe, apigwe viboko na kusulubiwa; lakini siku ya tatu atafufuliwa.”
"and hand him over to the Gentiles to be mocked and scourged and crucified; and on the third day he will rise from the grave."
20 Hapo mama yao wana wa Zebedayo alimjia Yesu pamoja na wanawe, akapiga magoti mbele yake na kumwomba kitu.
Then came to him the mother of the sons of Zebedee, with her sons, kneeling down and begging a favor of him.
21 Yesu akamwuliza, “Unataka nini?” Huyo mama akamwambia, “Ahidi kwamba katika Ufalme wako, hawa wanangu wawili watakaa mmoja upande wako wa kulia na mwingine upande wako wa kushoto.”
"What is it you wish?" he said. She answered, "Command that these my two sons may sit upon your right hand and your left in your kingdom."
22 Yesu akajibu, “Hamjui mnaomba nini. Je, mnaweza kunywa kikombe nitakachokunywa mimi?” Wakamjibu, “Tunaweza.”
23 Yesu akawaambia, “Kweli mtakunywa kikombe changu, lakini kuketi kulia au kushoto kwangu si kazi yangu kupanga; jambo hilo watapewa wale waliowekewa tayari na Baba yangu.”
"None of you indeed shall drink," he answered, "but to sit at my right hand or at my left is not mine to grant, but belongs to those for whom it has been prepared by my Father."
24 Wale wanafunzi wengine kumi waliposikia hayo, wakawakasirikia hao ndugu wawili.
When the ten heard of this, they were indignant at the two brothers;
25 Hivyo Yesu akawaita, akawaambia, “Mnajua kwamba watawala wa mataifa hutawala watu wao kwa mabavu na wakuu hao huwamiliki watu wao.
but Jesus called them to him and said. "You know how the rulers of the Gentiles lord it over them, and their great men exercise authority over them.
26 Lakini kwenu isiwe hivyo, ila yeyote anayetaka kuwa mkuu kati yenu sharti awe mtumishi wa wote;
"Not so shall it be among you. But whoever among you wishes to become great, shall be your minister,
27 na anayetaka kuwa wa kwanza kati yenu sharti awe mtumishi wenu.
"and whoever wishes to be first among you, shall be your slave;
28 Jinsi hiyohiyo, Mwana wa Mtu hakuja kutumikiwa, bali kutumikia na kutoa maisha yake kuwa fidia ya watu wengi.”
"just as the Son of man came not to be ministered unto, but to minister, and to give his life as a ransom for many."
29 Yesu alipokuwa anaondoka mjini Yeriko, umati wa watu ulimfuata.
Now as they were leaving Jericho a great crowd followed him.
30 Basi, kulikuwa na vipofu wawili wameketi kando ya njia, na waliposikia kwamba Yesu alikuwa anapitia hapo, walipaaza sauti: “Mheshimiwa, Mwana wa Daudi, utuhurumie!”
And two blind men, sitting by the side of the road, heard that it was Jesus who was passing by, and cried out, "Have pity on us, Master, Son of David!"
31 Ule umati wa watu ukawakemea na kuwaambia wanyamaze. Lakini wao wakazidi kupaaza sauti: “Mheshimiwa, Mwana wa Daudi, utuhurumie!”
But the crowd checked them, to make them keep still. They cried out all the louder, saying, "Master, have pity on us, Son of David!"
32 Yesu akasimama, akawaita na kuwauliza, “Mnataka niwafanyie nini?”
Then Jesus stopped and called to them, "What do you want me to do for you?"
33 Wakamjibu, “Mheshimiwa, tunaomba macho yetu yafumbuliwe.”
"Master," they answered, "let our eyes be opened."
34 Basi, Yesu akawaonea huruma, akawagusa macho yao, na papo hapo wakaweza kuona, wakamfuata.
Then Jesus, moved with compassion, touched their eyes, and they saw at once, and followed him.