< Mathayo 20 >

1 “Ufalme wa mbinguni unafanana na mtu mwenye shamba la mizabibu, ambaye alitoka asubuhi na mapema kuwaajiri wafanyakazi katika shamba lake.
For the kingdom of heaven is like the master of a house, who went out early in the morning to get workers into his vine-garden.
2 Akapatana nao kuwalipa dinari moja kwa siku, kisha akawapeleka katika shamba lake la mizabibu.
And when he had made an agreement with the workmen for a penny a day, he sent them into his vine-garden.
3 Akatoka mnamo saa tatu asubuhi, akaona watu wengine wamesimama sokoni, hawana kazi.
And he went out about the third hour, and saw others in the market-place doing nothing;
4 Akawaambia, Nendeni nanyi mkafanye kazi katika shamba la mizabibu, nami nitawapeni haki yenu.
And he said to them, Go into the vine-garden with the others, and whatever is right I will give you. And they went to work.
5 Basi, wakaenda. Huyo mwenye shamba akatoka tena mnamo saa sita na saa tisa, akafanya vivyo hivyo.
Again he went out about the sixth and the ninth hour, and did the same.
6 Hata mnamo saa kumi na moja jioni, akatoka tena; akakuta watu wengine wamesimama pale sokoni. Basi, akawauliza, Mbona mmesimama hapa mchana kutwa bila kazi?
And about the eleventh hour he went out and saw others doing nothing; and he says to them, Why are you here all the day doing nothing?
7 Wakamjibu: Kwa sababu hakuna mtu aliyetuajiri. Yeye akawaambia, Nendeni nanyi mkafanye kazi katika shamba la mizabibu.
They say to him, Because no man has given us work. He says to them, Go in with the rest, into the vine-garden.
8 “Kulipokuchwa, huyo mwenye shamba alimwambia mtunza hazina wake, Waite wafanyakazi ukawalipe mshahara wao, ukianzia na wale walioajiriwa mwisho, na kumalizia na wale wa kwanza.
And when evening came, the lord of the vine-garden said to his manager, Let the workers come, and give them their payment, from the last to the first.
9 Basi, wakaja wale walioajiriwa mnamo saa kumi na moja, wakapokea kila mmoja dinari moja.
And when those men came who had gone to work at the eleventh hour, they were given every man a penny.
10 Wale wa kwanza walipofika, walikuwa wanadhani watapewa zaidi; lakini hata wao wakapewa kila mmoja dinari moja.
Then those who came first had the idea that they would get more; and they, like the rest, were given a penny.
11 Wakazipokea fedha zao, wakaanza kumnung'unikia yule bwana.
And when they got it, they made a protest against the master of the house,
12 Wakasema, Watu hawa walioajiriwa mwisho walifanya kazi kwa muda wa saa moja tu, mbona umetutendea sawa na wao hali sisi tumevumilia kazi ngumu kutwa na jua kali?
Saying, These last have done only one hour's work, and you have made them equal to us, who have undergone the hard work of the day and the burning heat.
13 “Hapo yule bwana akamjibu mmoja wao, Rafiki, sikukupunja kitu! Je, hukupatana nami mshahara wa denari moja?
But he in answer said to one of them, Friend, I do you no wrong: did you not make an agreement with me for a penny?
14 Chukua haki yako, uende zako. Napenda kumpa huyu wa mwisho sawa na wewe.
Take what is yours, and go away; it is my pleasure to give to this last, even as to you.
15 Je, sina haki ya kufanya na mali yangu nipendavyo? Je, unaona kijicho kwa kuwa mimi ni mwema?”
Have I not the right to do as seems good to me in my house? or is your eye evil, because I am good?
16 Yesu akamaliza kwa kusema, “Hivyo, walio wa mwisho watakuwa wa kwanza na wa kwanza watakuwa wa mwisho.”
So the last will be first, and the first last.
17 Yesu alipokuwa anakwenda Yerusalemu, aliwachukua wale wanafunzi kumi na wawili faraghani, na njiani akawaambia,
And when Jesus was going up to Jerusalem, he took the twelve disciples on one side, and said to them,
18 “Sikilizeni! Tunakwenda Yerusalemu, na huko Mwana wa Mtu atakabidhiwa kwa makuhani wakuu na walimu wa Sheria, nao watamhukumu auawe.
See, we go up to Jerusalem; and the Son of man will be given into the hands of the chief priests and scribes; and they will give orders for him to be put to death,
19 Watamkabidhi kwa watu wa mataifa mengine ili adhihakiwe, apigwe viboko na kusulubiwa; lakini siku ya tatu atafufuliwa.”
And will give him up to the Gentiles to be made sport of and to be whipped and to be put to death on the cross: and the third day he will come back again from the dead.
20 Hapo mama yao wana wa Zebedayo alimjia Yesu pamoja na wanawe, akapiga magoti mbele yake na kumwomba kitu.
Then the mother of the sons of Zebedee came to him with her sons, giving him worship and making a request of him.
21 Yesu akamwuliza, “Unataka nini?” Huyo mama akamwambia, “Ahidi kwamba katika Ufalme wako, hawa wanangu wawili watakaa mmoja upande wako wa kulia na mwingine upande wako wa kushoto.”
And he said to her, What is your desire? She says to him, Let my two sons be seated, the one at your right hand, and the other at your left, in your kingdom.
22 Yesu akajibu, “Hamjui mnaomba nini. Je, mnaweza kunywa kikombe nitakachokunywa mimi?” Wakamjibu, “Tunaweza.”
But Jesus made answer and said, You have no idea what you are requesting. Are you able to take of the cup which I am about to take?
23 Yesu akawaambia, “Kweli mtakunywa kikombe changu, lakini kuketi kulia au kushoto kwangu si kazi yangu kupanga; jambo hilo watapewa wale waliowekewa tayari na Baba yangu.”
They say to him, We are able. He says to them, Truly, you will take of my cup: but to be seated at my right hand and at my left is not for me to give, but it is for those for whom my Father has made it ready.
24 Wale wanafunzi wengine kumi waliposikia hayo, wakawakasirikia hao ndugu wawili.
And when it came to the ears of the ten, they were angry with the two brothers.
25 Hivyo Yesu akawaita, akawaambia, “Mnajua kwamba watawala wa mataifa hutawala watu wao kwa mabavu na wakuu hao huwamiliki watu wao.
But Jesus said to them, You see that the rulers of the Gentiles are lords over them, and their great ones have authority over them.
26 Lakini kwenu isiwe hivyo, ila yeyote anayetaka kuwa mkuu kati yenu sharti awe mtumishi wa wote;
Let it not be so among you: but if anyone has a desire to become great among you, let him be your servant;
27 na anayetaka kuwa wa kwanza kati yenu sharti awe mtumishi wenu.
And whoever has a desire to be first among you, let him take the lowest place:
28 Jinsi hiyohiyo, Mwana wa Mtu hakuja kutumikiwa, bali kutumikia na kutoa maisha yake kuwa fidia ya watu wengi.”
Even as the Son of man did not come to have servants, but to be a servant, and to give his life for the salvation of men.
29 Yesu alipokuwa anaondoka mjini Yeriko, umati wa watu ulimfuata.
And when they were going out from Jericho, a great number went after him.
30 Basi, kulikuwa na vipofu wawili wameketi kando ya njia, na waliposikia kwamba Yesu alikuwa anapitia hapo, walipaaza sauti: “Mheshimiwa, Mwana wa Daudi, utuhurumie!”
And two blind men seated by the wayside, when they had the news that Jesus was going by, gave a loud cry, saying, Lord, Son of David, have mercy on us.
31 Ule umati wa watu ukawakemea na kuwaambia wanyamaze. Lakini wao wakazidi kupaaza sauti: “Mheshimiwa, Mwana wa Daudi, utuhurumie!”
And the people gave them orders to be quiet; but they went on crying even louder, Lord, Son of David, have mercy on us.
32 Yesu akasimama, akawaita na kuwauliza, “Mnataka niwafanyie nini?”
And Jesus, stopping, sent for them, and said, What would you have me do to you?
33 Wakamjibu, “Mheshimiwa, tunaomba macho yetu yafumbuliwe.”
They say to him, Lord, that our eyes may be open.
34 Basi, Yesu akawaonea huruma, akawagusa macho yao, na papo hapo wakaweza kuona, wakamfuata.
And Jesus, being moved with pity, put his fingers on their eyes: and straight away they were able to see, and went after him.

< Mathayo 20 >