< Mathayo 19 >

1 Yesu alipomaliza kusema maneno hayo, alitoka Galilaya, akaenda katika mkoa wa Yudea, ng'ambo ya mto Yordani.
When Jesus had finished saying these things, he departed from Galilee and came into the region of Judea beyond the Jordan.
2 Watu wengi walimfuata huko, naye akawaponya.
Large crowds followed him, and he healed them there.
3 Mafarisayo kadhaa walimjia, wakamwuliza kwa kumtega, “Je, ni halali mume kumpa talaka mkewe kwa kisa chochote?”
Then the Pharisees came up to Jesus and tested him by asking him, “Is it lawful for a man to divorce his wife for any reason?”
4 Yesu akawajibu, “Je, hamkusoma katika Maandiko Matakatifu kwamba Mungu aliyemuumba mtu tangu mwanzo alimfanya mwanamume na mwanamke,
He answered them, “Have you not read that he who made them from the beginning ‘made them male and female,’
5 na akasema: Kwa sababu hiyo mwanamume atamwacha baba yake na mama yake, ataungana na mke wake, nao wawili watakuwa mwili mmoja?
and said, ‘For this reason a man will leave his father and mother and be joined to his wife, and the two will become one flesh’?
6 Kwa hiyo wao si wawili tena, bali mwili mmoja. Basi, alichounganisha Mungu, binadamu asikitenganishe.”
So then, they are no longer two, but one flesh. Therefore what God has joined together, let no one separate.”
7 Lakini wao wakamwuliza, “Kwa nini basi, Mose alituagiza mwanamke apewe hati ya talaka na kuachwa?”
They said to him, “Why then did Moses command us to give her a certificate of divorce and send her away?”
8 Yesu akawajibu, “Mose aliwaruhusu kuwaacha wake zenu kwa sababu ya ugumu wa mioyo yenu.
He said to them, “Because of your hardness of heart Moses allowed you to divorce your wives, but from the beginning it was not so.
9 Lakini haikuwa hivyo tangu mwanzo. Basi nawaambieni, yeyote atakayemwacha mke wake isipokuwa kwa sababu ya uzinzi, akaoa mke mwingine, anazini.”
I tell you that whoever divorces his wife, except for fornication, and marries another, commits adultery. And whoever marries a divorced woman commits adultery.”
10 Wanafunzi wake wakamwambia, “Ikiwa mambo ya mume na mkewe ni hivyo, ni afadhali kutooa kabisa.”
His disciples said to him, “If such is the case of a man with his wife, it is better not to marry.”
11 Yesu akawaambia, “Si wote wanaoweza kulipokea fundisho hili, isipokuwa tu wale waliojaliwa na Mungu.
But Jesus said to them, “Not all men can accept this statement, but only those to whom it is given.
12 Maana kuna sababu kadhaa za kutoweza kuoa: wengine ni kwa sababu wamezaliwa hivyo, wengine kwa sababu wamefanywa hivyo na watu, na wengine wameamua kutooa kwa ajili ya Ufalme wa mbinguni. Awezaye kulipokea fundisho hili na alipokee.”
For there are eunuchs who were born that way from their mother's womb, and there are eunuchs who have been made eunuchs by men, and there are eunuchs who have made themselves eunuchs for the sake of the kingdom of heaven. Whoever is able to accept this should accept it.”
13 Kisha watu wakamletea Yesu watoto wadogo ili awawekee mikono na kuwaombea. Lakini wanafunzi wakawakemea.
Then little children were brought to Jesus so that he might lay his hands on them and pray, but the disciples rebuked those who brought them.
14 Yesu akasema, “Waacheni hao watoto waje kwangu, wala msiwazuie; maana Ufalme wa mbinguni ni wa watu walio kama watoto hawa.”
Yet Jesus said, “Let the little children come to me and do not hinder them, for the kingdom of heaven belongs to such as these.”
15 Basi, akawawekea mikono, kisha akaondoka mahali hapo.
And after laying his hands on them, he departed from there.
16 Mtu mmoja alimjia Yesu, akamwuliza, “Mwalimu, nifanye kitu gani chema ili niupate uzima wa milele?” (aiōnios g166)
And behold, a man came and said to him, “Good Teacher, what good thing must I do to have eternal life?” (aiōnios g166)
17 Yesu akamwambia, “Mbona unaniuliza kuhusu jambo jema? Kuna mmoja tu aliye mwema. Ukitaka kuingia katika uzima, shika amri.”
Jesus said to him, “Why do yoʋ call me good? No one is good except God alone. But if yoʋ wish to enter life, keep the commandments.”
18 Yule mtu akamwuliza, “Amri zipi?” Yesu akasema, “Usiue, usizini, usiibe, usitoe ushahidi wa uongo,
The man said to him, “Which ones?” Jesus said, “Yoʋ shall not murder, Yoʋ shall not commit adultery, Yoʋ shall not steal, Yoʋ shall not give false testimony,
19 waheshimu baba yako na mama yako; na, mpende jirani yako kama unavyojipenda mwenyewe.”
Honor yoʋr father and yoʋr mother, and, Yoʋ shall love yoʋr neighbor as yoʋrself.”
20 Huyo kijana akamwambia, “Hayo yote nimeyazingatia tangu utoto wangu; sasa nifanye nini zaidi?”
The young man said to him, “I have kept all these commandments from the time I was a young boy; what do I still lack?”
21 Yesu akamwambia, “Kama unapenda kuwa mkamilifu, nenda ukauze mali yako uwape maskini hiyo fedha, nawe utakuwa na hazina mbinguni, kisha njoo unifuate.”
Jesus said to him, “If yoʋ wish to be perfect, go sell what yoʋ have and give to the poor, and yoʋ will have treasure in heaven; then come follow me.”
22 Huyo kijana aliposikia hayo, alienda zake akiwa mwenye huzuni, maana alikuwa na mali nyingi.
But when the young man heard this, he went away sorrowful, for he had many possessions.
23 Hapo Yesu akawaambia wanafunzi wake, “Kweli nawaambieni, itakuwa vigumu sana kwa tajiri kuingia katika Ufalme wa mbinguni.
Then Jesus said to his disciples, “Truly I say to you, only with difficulty will a rich person enter the kingdom of heaven.
24 Tena nawaambieni, ni rahisi zaidi kwa ngamia kupita katika tundu la sindano, kuliko kwa tajiri kuingia katika Ufalme wa mbinguni.”
Again I say to you, it is easier for a camel to go through the eye of a needle than for a rich person to enter the kingdom of God.”
25 Wale wanafunzi waliposikia hivyo walishangaa, wakamwuliza, “Ni nani basi, awezaye kuokoka?”
When his disciples heard this, they were greatly astonished and said, “Who then can be saved?”
26 Yesu akawatazama, akasema, “Kwa binadamu jambo hili haliwezekani, lakini kwa Mungu mambo yote huwezekana.”
Jesus looked at them and said to them, “With men it is impossible, but with God all things are possible.”
27 Kisha Petro akasema, “Na sisi je? Tumeacha yote tukakufuata; tutapata nini basi?”
Then Peter said to him in response, “Behold, we have left everything and followed yoʋ; what then will there be for us?”
28 Yesu akawaambia, “Nawaambieni kweli, Mwana wa Mtu atakapoketi katika kiti cha enzi cha utukufu wake katika ulimwengu mpya, ninyi mlionifuata mtaketi katika viti kumi na viwili mkiyahukumu makabila kumi na mawili ya Israeli.
Jesus said to them, “Truly I say to you, when all things are made new and the Son of Man sits on his throne of glory, you who have followed me will also sit on twelve thrones, judging the twelve tribes of Israel.
29 Na kila aliyeacha nyumba, au ndugu, au dada, au baba, au mama, au watoto, au mashamba, kwa ajili yangu, atapokea mara mia zaidi, na kupata uzima wa milele. (aiōnios g166)
And everyone who has left houses, brothers, sisters, father, mother, wife, children, or fields for my name's sake, will receive a hundred times more and will inherit eternal life. (aiōnios g166)
30 Lakini walio wa kwanza watakuwa wa mwisho, na walio wa mwisho watakuwa wa kwanza.
But many who are first will be last, and many who are last will be first.

< Mathayo 19 >