< Mathayo 16 >
1 Mafarisayo na Masadukayo walimwendea Yesu, na kwa kumjaribu, wakamwomba afanye ishara itokayo mbinguni.
AVafalisayi na Vasadukayi vamonga vakaluka kukumughela uYesu, vakasuuma kuuti ahufie ikivalilo kino kivonia kuuti asung'hilue nu Nguluve
2 Lakini Yesu akawajibu, “Wakati wa jioni ukifika ninyi husema: Hali ya hewa itakuwa nzuri kwa maana anga ni jekundu!
UYesu akavamula akati, “Pano jifikile ivwilile mwiti, “Pakilaavo kukia vunofu, ulwakuva kukyanya kuvalafu.
3 Na alfajiri mwasema: Leo hali ya hewa itakuwa ya dhoruba, maana anga ni jekundu na tena mawingu yametanda! Basi, ninyi mnajua sana kusoma majira kwa kuangalia anga, lakini kutambua dalili za nyakati hizi hamjui.
Palwakilo mwiti, 'uMusyughu ifula imbaha jitoonya, ilwakuva kulimafunde kange kughuvile.' Mwe vakedusi umue, mukagwile kuluvulania ifivalilo ifya kukyanya ku palanga, lwandaani mukunua kukufitang'hania ifivalilo fino fivombeka lino kuuti fili nu muluvo muki!
4 Kizazi kiovu kisicho na uaminifu! Mnataka ishara, lakini hamtapewa ishara yoyote isipokuwa tu ile ya Yona.” Basi, akawaacha, akaenda zake.
Avaanhu va kisina iki ikihosi, vano navikum'bikila mwojo uNguluve, vilonda ikivalilo. Looli navalapelue ikivalilo, ulwene ikivalilo kino uNguluve alyahufisie vwimila uYoona.” Pepano uYesu akavaleka, akavuuka, iluta.
5 Wanafunzi wake walipokwisha vukia upande wa pili wa ziwa, walijikuta wamesahau kuchukua mikate.
Avavulanisivua va Yesu ye vilovoka inyanja, vakasyemua kutoola amakate.
6 Yesu akawaambia, “Muwe macho na mjihadhari na chachu ya Mafarisayo na Masadukayo!”
UYesu akavavuula akati, “Muvisaghe maaso ni kilule ikya Vafalisayi na Vasadukayi.”
7 Lakini wao wakawa wanajadiliana: “Anasema hivyo kwa kuwa hatukuchukua mikate.”
Avavulanisivua vala vakatengula piposania veene viiti, “Ijova enendiiki ulwakuva natugadile amakate!
8 Yesu alijua mawazo yao, akawaambia, “Enyi watu wenye imani haba! Mbona mnajadiliana juu ya kutokuwa na mikate?
UYesu akasikagula sino vaka vijova, akavavuula akati, Mwe vanya lwitiko ludebe umue! kiki mukaning'haniajumue mwitu muli vasila makate?
9 Je, hamjaelewa bado? Je, hamkumbuki nilipoimega ile mikate mitano kwa ajili ya wale watu elfu tano? Je, mlijaza vikapu vingapi vya makombo?
Mujiighe namukulutang'hania, nambe kukumbuka amakate ghala ghahaano ghano vakaliile avaanhu vala imbilima ihaano. asi, ifisighasi mukamemisie indiilo ilingi?
10 Au, ile mikate saba waliyogawiwa wale watu elfu nne, je, mlikusanya vikapu vingapi vya mabaki?
Nambe amakate ghala lekelalubale ku vaanhu vala imbilima ine, asi, mukakong'hanisie ifisighasi indiilo ilingi?
11 Inawezekanaje hamwelewi ya kwamba sikuwa nikisema juu ya mikate? Jihadharini na chachu ya Mafarisayo na Masadukayo!”
Lwandaani namukulutang'hania kuuti imhola sino nijova numue nasa makate? Une nijova kuuti, muvisaghe maaso ni kilule ikya Vafalisayi na Vasadukayi.”
12 Hapo wanafunzi wakafahamu kwamba aliwaambia wajihadhari siyo na chachu ya mikate, bali na mafundisho ya Mafarisayo na Masadukayo.
Apuo avavulanisivua vaake vakalutang'hania kuuti naaveele ijova imbulanisio imbiivi isa Vafalisayi na Vasadukayi.
13 Yesu alipofika pande za Kaisarea Filipi, aliwauliza wanafunzi wake, “Watu wanasema Mwana wa Mtu kuwa ni nani?”
Pepano uYesu akaluta imbale isa ku Kaisalia-Filipi. Ye afikile akavaposia avavulanisivua vaake akati, Avaanhu viiti une ne Mwana ghwa Muunhu, neene veen?
14 Wakamjibu, “Wengine wanasema kuwa ni Yohane mbatizaji, wengine Eliya, wengine Yeremia au mmojawapo wa manabii.”
Vakamwamula vakati, “Vamo viiti veeve Yohani Mwafughi, vamonga viiti veeve Eliya, avange viiti veeve Yelemia, nambe kuuti uve uli umo mu vavili.'
15 Yesu akawauliza, “Na ninyi je, mwasema mimi ni nani?”
UYesu akavaposia kange akati, “Neke umue mwiti neene veeni?
16 Simoni Petro akajibu, “Wewe ndiwe Kristo, Mwana wa Mungu aliye hai.”
uSimoni Peteli akamwamulila akati, “uve veeve Kilisite, Mwana ghwa Nguluve juno mwimi.”
17 Yesu akasema, “Heri wewe Simoni mwana wa Yona, kwa maana si binadamu aliyekufunulia ukweli huu, ila Baba yangu aliye mbinguni.
UYesu akam'buula akati, “Simoni mwana ghwa Yoona ufunyilue, ulwakuva nakwale umuunhu juno akuhufisie isio, looli uNhaata ghwango juno alikukyanya.
18 Nami nakwambia: wewe ni Petro, na juu ya mwamba huu nitalijenga kanisa langu; wala kifo chenyewe hakitaweza kulishinda. (Hadēs )
Lino nikuvuula kuuti, veeve Peteli, kwekuti linhalavue. Pakyanya pa linhaalavue ili nijenga inyumba jango jino kye kipugha kya vikiti, ingufu isa kuvufie nasingajilema lusiku. (Hadēs )
19 Nitakupa funguo za Ufalme wa mbinguni; kila utakachofunga duniani, kitafungwa pia mbinguni; kila utakachofungua duniani, kitafunguliwa pia mbinguni.”
Nikukupeela ifuunguluo isa vutwa vwa kukyanya, sooni sino ukanile nu iisi iji, ghwope UNguluve iiva akanile kukyanya. Kange, sooni sino ghwitikisie mu iisi iji, naju Nguluve iiva itikisie kukyanya.
20 Kisha akawaonya wanafunzi wasimwambie mtu yeyote kwamba yeye ndiye Kristo.
Pe UYesu akavakaana avavulanisivua vaake vala kuuti, navangam'bulaghe muunhu kuuti umwene ghwe Kilisite.
21 Tangu wakati huo Yesu alianza kuwajulisha waziwazi wanafunzi wake: “Ni lazima mimi niende Yerusalemu, na huko nikapate mateso mengi yatakayosababishwa na wazee, makuhani wakuu na walimu wa Sheria. Nitauawa, na siku ya tatu nitafufuliwa.”
Kutengula unsiki ughuo, uYesu akava ikuvavuula pa vuvalafu avavulanisivua vaake kuuti, lunoghiile umwene kuluta ku Yelusalemu na kuuva ni mhumuko nyinga kuhuma ku vagojo, ku vavaha va vatekesi na ku vavulanis va ndaghilo isa Moosi, na kubudua. Neke ikighono ikya vutatu isyuka.
22 Hapo Petro akamchukua kando, akaanza kumkemea: “Isiwe hivyo Bwana! Jambo hili halitakupata!”
Pe uPeteli akaluta naghwope palubale, akatengula kukun'dalikila akati, “Luleke pivombeka uluo Mutwa! Isio nasingakwaghe!
23 Lakini Yesu akageuka, akamwambia Petro, “Ondoka mbele yangu Shetani! Wewe ni kikwazo kwangu. Mawazo yako si ya mungu bali ni ya kibinadamu!”
Neke UYesu akansyetukila uPeteli, akam'buula akati, 'Vuuka apa ghwe Setano uve! Ghulonda kukusigha une kuvomba uvughane vwa Nguluve ulwene masaagha gha vaanha.
24 Kisha Yesu akawaambia wanafunzi wake, “Kama mtu yeyote anataka kuwa mfuasi wangu, ni lazima ajikane mwenyewe, auchukue msalaba wake, anifuate.
Pe akavavuula avavulanisivua vaake akati, “Umuunhu juno ulonda kukumbilila une, avuleke uvughane vwake, itavule ambingililaghe nambe kuuve kwe kufua.
25 Maana, mtu anayetaka kuyaokoa maisha yake mwenyewe, atayapoteza;
Ulwakuva umuunhu juno ilonda kupoka uvwumi vwake, ujuo alambusia, looli umuunhu juno ikwambusia uvwumi vwake, ujuo alambusia, looli umuunhu juno ikwambusia uvwumi vwake vwimila une, ujuo iliiva nu vwumi uvwa kuvusila kusila.
26 lakini mtu anayeyapoteza maisha yake kwa ajili yangu, atayapata. Je, mtu atafaidi nini akiupata utajiri wote wa ulimwengu na hali amepoteza maisha yake? Au, mtu atatoa kitu gani kiwe badala ya maisha yake?
Lino, umuunhu ndepoonu ivumbulila kiki kuuva nu vumofu vwoni uvwa iisi, neke ambusie uvwumi vwake? nambe umuunhu ahumie kiki apyanisia pa vwumi vwake?
27 Maana, Mwana wa Mtu atakuja katika utukufu wa Baba yake pamoja na malaika wake, na hapo ndipo atakapomlipa kila mtu kadiri ya matendo yake.
Ulwakuva une ne Mwana ghwa Muunhu nilikwisa na vanyamhola vango mu vuvaha vwa Nhaata ghwango. pe nilikumhomba nujunge kuling'hana ni mbombo saake,
28 Kweli nawaambieni, wako wengine papahapa ambao hawatakufa kabla ya kumwona Mwana wa Mtu akija katika Ufalme wake.”
kyang'haani nikuvavuula, vamonga nkate mulyumue mwe vano muli apa, navalafua kuhanga pano vikunyaagha ne Mwana ghwa Muunhu nilaava nikwisa mu vutwa vwango.