< Mathayo 14 >

1 Wakati huo, mtawala Herode alisikia sifa za Yesu.
At that time Herod the tetrarch heard the report about Jesus
2 Basi, akawaambia watumishi wake, “Mtu huyu ni Yohane mbatizaji, amefufuka kutoka wafu; ndiyo maana nguvu za miujiza zinafanya kazi ndani yake.”
and said to his servants, “This is John the Baptizer; he has been raised from the dead, and therefore the powers are at work in him.”
3 Herode ndiye aliyekuwa amemtia Yohane nguvuni, akamfunga minyororo na kumtia gerezani kwa sababu ya Herodia, mke wa Filipo, ndugu yake. Sababu hasa ni
For Herod had laid hold of John and bound him, and put him in prison because of Herodias, his brother Philip's wife.
4 kwamba alikuwa amemwambia Herode, “Si halali kwako kuishi na huyo mwanamke!”
For John would say to him, “It is not lawful for you to have her.”
5 Herode alitaka kumwua Yohane, lakini aliogopa watu kwa sababu kwao Yohane alikuwa nabii.
And although he wanted to kill him, he feared the crowd, because they counted him as a prophet.
6 Katika sherehe za sikukuu ya kuzaliwa kwake Herode, binti ya Herodia alicheza mbele ya wageni. Herode alifurahiwa,
But while Herod's birthday was being celebrated, the daughter of Herodias danced before them and she pleased Herod.
7 hata akaahidi kwa kiapo kumpa huyo msichana chochote atakachoomba.
So he promised with an oath to give her whatever she might ask.
8 Naye, huku akichochewa na mama yake, akaomba, “Nipe papahapa katika sinia kichwa cha Yohane mbatizaji.”
So she, having been prompted by her mother, she says, “Give me here on a platter the head of John the Baptizer!”
9 Mfalme alihuzunika, lakini kwa sababu ya kile kiapo chake na kwa sababu ya wale wageni karamuni, akaamuru apewe.
And the king was sorry; nevertheless, because of the oaths and those who were reclining at the table with him, he commanded it to be given.
10 Basi, Herode akatuma mtu gerezani amkate kichwa Yohane.
So he sent and had John beheaded in prison.
11 Kichwa chake kikaletwa katika sinia, wakampa yule msichana, naye akampelekea mama yake.
And his head was brought on a platter and given to the girl, and she brought it to her mother.
12 Wanafunzi wa Yohane wakaja, wakauchukua mwili wake, wakauzika. Kisha wakaenda kumpasha habari Yesu.
Then his disciples came forward and took the body and buried it, and they went and told Jesus.
13 Yesu alipopata habari hiyo, aliondoka mahali pale kwa mashua, akaenda mahali pa faragha peke yake. Lakini watu walipata habari, wakamfuata kwa miguu toka mijini.
Upon hearing it, Jesus departed from there by boat to a deserted place privately. But when the crowds heard it, they followed Him on foot from the towns.
14 Basi, aliposhuka pwani, aliona umati mkubwa wa watu, akawaonea huruma, akawaponya wagonjwa wao.
So when Jesus disembarked He saw a large crowd, and He had compassion on them and healed their sick.
15 Kulipokuwa jioni, wanafunzi wake walimwendea wakamwambia, “Mahali hapa ni nyikani, na saa zimepita. Basi, uwaage watu ili waende vijijini wakajinunulie chakula.”
Now with evening coming on His disciples approached Him saying: “The place is uninhabited and the hour is already late. Dismiss the crowds, that they may go into the villages and buy themselves food.”
16 Yesu akawaambia, “Si lazima waende, wapeni ninyi chakula.”
But Jesus said to them: “They do not need to go away. You give them to eat.”
17 Lakini wao wakamwambia, “Tunayo mikate mitano tu na samaki wawili.”
But they say to Him, “We have nothing here except five loaves and two fish.”
18 Yesu akawaambia, “Nileteeni hapa.”
So He said, “Bring them here to me.”
19 Akawaamuru watu waketi katika nyasi. Kisha akaitwaa ile mikate mitano na wale samaki wawili, akatazama juu mbinguni, akamshukuru Mungu. Halafu akaimega hiyo mikate, akawapa wanafunzi wake, nao wakawapa watu.
Then He commanded the crowds to recline on the grass. And taking the five loaves and two fish and looking up to heaven, He blessed; and breaking the loaves He gave to the disciples, and the disciples to the crowds.
20 Watu wote wakala, wakashiba. Kisha wanafunzi wakakusanya mabaki, wakajaza vikapu kumi na viwili.
So they all ate and were filled; and they took up the fragments that remained, twelve baskets full.
21 Jumla ya waliokula ilikuwa wanaume wapatao elfu tano, bila kuhesabu wanawake na watoto.
Now those who ate were about five thousand men, besides women and children.
22 Mara, Yesu akawaamuru wanafunzi wake wapande mashua, wamtangulie ng'ambo ya ziwa wakati yeye anawaaga watu.
Immediately Jesus made His disciples get into the boat and go ahead of Him to the other side, while He dismissed the crowds.
23 Baada ya kuwaaga, alipanda mlimani peke yake kusali. Ilipokuwa jioni, yeye alikuwa huko peke yake,
And having dismissed the crowds He went up on the mountain by Himself to pray. So when night came He was alone there.
24 na wakati huo ile mashua ilikwishafika karibu katikati ya ziwa, lakini ilikuwa inakwenda mrama kwa sababu upepo ulikuwa unaipinga.
But the boat was already in the middle of the sea, being harassed by the waves, for the wind was contrary.
25 Usiku, karibu na mapambazuko, Yesu aliwaendea wanafunzi akitembea juu ya maji.
So in the fourth watch of the night Jesus went to them, walking on the sea.
26 Wanafunzi wake walipomwona akitembea juu ya maji waliingiwa na hofu, wakasema, “Ni mzimu!” Wakapiga kelele kwa hofu.
And when the disciples saw Him walking on the sea, they became agitated saying, “It's a ghost!” And they cried out for fear.
27 Mara, Yesu akasema nao, “Tulieni, ni mimi. Msiogope!”
But immediately Jesus spoke to them saying: “Courage! It is I; don't be afraid!”
28 Petro akamwambia, “Bwana, ikiwa ni wewe kweli, amuru nitembee juu ya maji nije kwako.”
So in answer Peter said, “Lord, since it's you, command me to come to you on the water.”
29 Yesu akasema, “Haya, njoo.” Basi, Petro akashuka kutoka ile mashua, akatembea juu ya maji, akamwendea Yesu.
So He said to him, “Come!” And stepping down from the boat Peter walked on the water to go to Jesus.
30 Lakini alipouona ule upepo, aliogopa, akaanza kuzama; akalia kwa sauti, “Bwana, niokoe!”
But seeing the strong wind he became afraid, and beginning to sink he cried out saying, “Lord, save me!”
31 Hapo, Yesu akaunyosha mkono wake, akamshika na kumwambia, “Ewe mwenye imani haba! Kwa nini uliona shaka?”
And immediately Jesus reached out His hand and caught him and says to him: “You little-faith! Why did you doubt?”
32 Basi, wakapanda mashuani, na upepo ukatulia.
And when they got into the boat the wind ceased.
33 Wote waliokuwa ndani ya mashua walimsujudia, wakasema, “Hakika wewe ni Mwana wa Mungu.”
Then those who were in the boat came and worshiped Him saying, “Truly you are the Son of God!”
34 Walivuka ziwa, wakafika nchi ya Genesareti.
When they had crossed over they came to the land of Genesaret.
35 Watu wa huko walipomtambua, wakaeneza habari pote katika sehemu hizo. Basi, wakamletea Yesu wagonjwa wote,
And when the men of that place recognized Him they sent messengers into all that surrounding region and they brought to Him all who were sick.
36 wakamwomba awaruhusu waguse tu pindo la vazi lake; wote waliomgusa walipona.
And they would beg Him that if only they might at least touch the hem of His garment; and as many as touched were completely healed.

< Mathayo 14 >