< Mathayo 12 >

1 Wakati huo, Yesu alikuwa anapita katika mashamba ya ngano siku ya Sabato. Basi, wanafunzi wake wakaona njaa, wakaanza kukwanyua masuke ya ngano, wakala punje zake.
At that time Jesus went on the sabbath through the grain-fields; and his disciples were hungry, and began to pluck the ears of grain, and to eat.
2 Mafarisayo walipoona hayo, wakamwambia Yesu, “Tazama, wanafunzi wako wanafanya jambo ambalo si halali siku ya Sabato.”
But the Pharisees, seeing it, said to him, Lo! thy disciples are doing that which it is not lawful to do on the sabbath.
3 Yesu akawajibu, “Je, hamjasoma alivyofanya Daudi pamoja na wenzake wakati walipokuwa na njaa?
But he said to them, Have ye not read what David did, when he and those who were with him were hungry?
4 Yeye aliingia katika Nyumba ya Mungu pamoja na wenzake, wakala ile mikate iliyowekwa mbele ya Mungu. Yeye wala hao wenzake hawakuruhusiwa kula mikate hiyo isipokuwa tu makuhani peke yao.
how he went into the house of God, and they ate the show-bread, which it was not lawful for him to eat, nor for those who were with him, but for the priests alone?
5 Au je, hamjasoma katika Sheria kwamba kila siku ya Sabato makuhani huivunja Sheria Hekaluni, lakini hawafikiriwi kuwa na hatia?
Or have ye not read in the Law, that on the sabbaths the priests in the temple profane the sabbath, and are blameless?
6 Basi, nawaambieni kwamba hapa pana kikuu kuliko Hekalu.
But I say to you, that something greater than the temple is here.
7 Kama tu mngejua maana ya maneno haya: Nataka huruma wala si dhabihu, hamngewahukumu watu wasio na hatia.
But if ye had known what this meaneth, “I desire mercy and not sacrifice,” ye would not have condemned the guiltless.
8 Maana Mwana wa Mtu ni Bwana wa Sabato.”
For the Son of man is lord of the sabbath.
9 Yesu alitoka hapo, akaenda katika sunagogi lao.
And departing thence, he went into their synagogue.
10 Kulikuwa na mtu mmoja mwenye mkono uliopooza. Basi, watu wakamwuliza Yesu, “Je, ni halali kumponya mtu siku ya Sabato?” Walimwuliza hivyo wapate kisa cha kumshtaki.
And, lo! there was a man having a withered hand. And they asked him, saying, Is it lawful to heal on the sabbath? that they might accuse him.
11 Lakini Yesu akawaambia, “Tuseme mmoja wenu ana kondoo wake ambaye ametumbukia shimoni; je, hatamshika na kumtoa humo siku ya Sabato?
And he said to them, Who of you that owneth one sheep, if it fall into a pit on the sabbath, will not lay hold of it, and lift it out?
12 Mtu ana thamani kuliko kondoo! Basi, ni halali kutenda mema siku ya Sabato.”
Of how much more worth now is a man than a sheep! So then it is lawful to do well on the sabbath.
13 Kisha akamwambia yule mtu, “Nyosha mkono wako.” Akaunyosha, nao ukawa mzima kabisa kama ule mwingine.
Then saith he to the man, Stretch forth thy hand. And he stretched it forth; and it was restored sound as the other.
14 Basi, Mafarisayo wakatoka nje, wakashauriana jinsi watakavyomwangamiza Yesu.
Then the Pharisees went out, and consulted together against him, how they might destroy him.
15 Lakini Yesu alipojua jambo hilo, akatoka mahali pale. Watu wengi walimfuata, akawaponya wagonjwa wote,
But Jesus, knowing it, withdrew from thence; and many followed him; and he healed them all,
16 akawaamuru wasiwaambie watu habari zake,
and strictly charged them not to make him known;
17 ili yale aliyosema nabii Isaya yatimie:
that it might be fulfilled which was spoken through Isaiah the prophet, saying,
18 “Hapa ni mtumishi wangu niliyemteua, mpendwa wangu anipendezaye moyoni. Nitaiweka Roho yangu juu yake, naye atatangaza hukumu yangu kwa mataifa yote.
“Behold my servant, whom I chose; my beloved, with whom my soul is well pleased; I will put my Spirit upon him, and he will declare judgment to the nations.
19 Hatakuwa na ubishi wala kupiga kelele, wala sauti yake haitasikika barabarani.
He will not strive, nor cry aloud, nor will any one hear his voice in the streets.
20 Mwanzi uliopondeka hatauvunja, wala utambi ufukao moshi hatauzima, mpaka atakapoifanya hukumu ya haki itawale.
A bruised reed he will not break, and smoking flax he will not quench, till he send forth judgment unto victory.
21 Katika jina lake mataifa yatakuwa na tumaini.”
And in his name will nations hope.”
22 Hapo watu wakamletea Yesu kipofu mmoja ambaye alikuwa bubu kwa sababu alikuwa amepagawa na pepo. Yesu akamponya hata, akaweza kusema na kuona.
Then was brought to him one possessed by a demon, blind and dumb; and he healed him, so that the dumb man spoke and saw.
23 Umati wote wa watu ulishangaa ukasema, “Je, huenda ikawa huyu ndiye Mwana wa Daudi?”
And all the multitudes were amazed, and said, Is this the son of David?
24 Lakini Mafarisayo waliposikia hayo, wakasema, “Mtu huyu anawafukuza pepo kwa uwezo wa Beelzebuli, mkuu wa pepo.”
But the Pharisees, hearing it, said, This man doth not cast out the demons, except through Beelzebul, the prince of the demons.
25 Yesu, akiwa anayajua mawazo yao, akawaambia, “Ufalme wowote uliogawanyika makundimakundi yanayopingana, hauwezi kudumu, na mji wowote au jamaa yoyote iliyogawanyika makundimakundi yanayopingana, itaanguka.
And he, knowing their thoughts, said to them, Every kingdom divided against itself is brought to desolation; and no city or house divided against itself will stand.
26 Ikiwa Shetani anamfukuza Shetani, anajipinga mwenyewe. Basi, ufalme wake utasimamaje?
And if Satan cast out Satan, he is divided against himself; how then shall his kingdom stand?
27 Ninyi mnasema ati nawafukuza pepo kwa uwezo wa Beelzebuli; je, watoto wenu huwafukuza kwa uwezo wa nani? Kwa sababu hiyo wao ndio watakaowahukumu ninyi.
And if I cast out the demons through Beelzebul, through whom do your sons cast them out? Therefore shall they be judges of you.
28 Lakini ikiwa ninawafukuza pepo kwa nguvu ya Roho wa Mungu, basi jueni kwamba Ufalme wa Mungu umekwisha fika kwenu.
But if I cast out the demons through the Spirit of God, then hath the kingdom of God already come to you.
29 “Au, anawezaje mtu kuivamia nyumba ya mtu mwenye nguvu na kumnyang'anya mali yake, bila kwanza kumfunga huyo mtu mwenye nguvu? Hapo ndipo atakapoweza kumnyang'anya mali yake.
Or how can one enter into a strong man's house, and seize upon his goods, unless he first bind the strong man, and then plunder his house?
30 “Yeyote asiyejiunga nami, anapingana nami; na yeyote asiyekusanya pamoja nami, hutawanya.
He that is not with me is against me; and he that gathereth not with me scattereth abroad.
31 Kwa sababu hiyo, nawaambieni, watu watasamehewa dhambi na kufuru zao zote, lakini hawatasamehewa dhambi ya kumkufuru Roho Mtakatifu.
Therefore I say to you, All manner of sin and evil-speaking will be forgiven to men; but blasphemy against the Spirit will not be forgiven.
32 Tena, asemaye neno la kumpinga Mwana wa Mtu atasamehewa, lakini yule asemaye neno la kumpinga Roho Mtakatifu, hatasamehewa, wala katika ulimwengu huu, wala katika ulimwengu ujao. (aiōn g165)
And whoever speaketh a word against the Son of man, it will be forgiven him; but whoever speaketh against the Holy Spirit, it will not be forgiven him, either in this world, or in the world to come. (aiōn g165)
33 “Ufanyeni mti kuwa mzuri na matunda yake yatakuwa mema; ufanyeni kuwa mbaya na matunda yake yatakuwa mabaya. Mti hujulikana kwa matunda yake.
Either say that the tree is good, and its fruit good; or say that the tree is bad, and its fruit bad; for the tree is known by its fruit. Brood of vipers!
34 Enyi kizazi cha nyoka! Mnawezaje kusema mambo mema hali ninyi ni waovu? Maana mtu husema kutokana na yale yaliyojaa moyoni.
How can ye, evil as ye are, speak good things? For out of the abundance of the heart the mouth speaketh.
35 Mtu mwema hutoa mambo mema katika hazina yake njema; na mtu mbaya hutoa mambo mabaya katika hazina yake mbaya.
The good man, from his good treasure, bringeth out good things; and the evil man, from his evil treasure, bringeth out evil things.
36 “Basi, nawaambieni, Siku ya hukumu watu watapaswa kujibu juu ya kila neno lisilofaa wanalosema.
And I say to you, that for every idle word that men shall speak, they will give account in the day of judgment.
37 Maana kwa maneno yako, utakubaliwa kuwa mwadilifu, na kwa maneno yako, utahukumiwa kuwa na hatia.”
For by thy words thou wilt be justified, and by thy words thou wilt be condemned.
38 Kisha baadhi ya walimu wa Sheria na Mafarisayo wakamwambia Yesu, “Mwalimu, tunataka kuona ishara kutoka kwako.”
Then some of the scribes and Pharisees answered him, saying, Teacher, we wish to see a sign from thee.
39 Naye akawajibu, “Kizazi kiovu kisicho na uaminifu! Mnataka ishara; hamtapewa ishara nyingine, ila tu ile ishara ya nabii Yona.
But he answered and said to them, A wicked and adulterous generation is seeking for a sign; and no sign will be given to it, but the sign of Jonah the prophet.
40 Jinsi Yona alivyokaa siku tatu kutwa kucha tumboni mwa nyangumi, ndivyo naye Mwana wa Mtu atakavyokaa ndani ya ardhi siku tatu kutwa kucha.
For as Jonah was three days and three nights in the belly of the great fish, so will the Son of man be three days and three nights in the heart of the earth.
41 Watu wa Ninewi watatokea siku ya hukumu, nao watakihukumu kizazi hiki kwamba kina hatia. Maana Waninewi walitubu kwa sababu ya mahubiri ya Yona, na kumbe hapa kuna kikuu kuliko Yona!
The men of Nineveh will stand up in the judgment with this generation, and will condemn it; for they repented at the preaching of Jonah; and, lo! something more than Jonah is here.
42 Malkia wa kusini atatokea wakati kizazi hiki kitakapohukumiwa, naye atakihukumu kwamba kina hatia. Maana yeye alisafiri kutoka mbali akaja kusikiliza maneno ya hekima ya Solomoni, na kumbe hapa kuna kikuu kuliko Solomoni.
The queen of the south will rise up in the judgment with this generation, and will condemn it; for she came from the ends of the earth to hear the wisdom of Solomon; and lo! something more than Solomon is here.
43 “Pepo mchafu akifukuzwa kwa mtu, huzururazurura jangwani akitafuta mahali pa kupumzika asipate.
But when the unclean spirit is gone out from a man, it goeth through dry places, seeking rest, and findeth it not.
44 Hapo hujisemea: Nitarudi nyumbani kwangu nilikotoka. Lakini anaporudi na kuikuta tupu, imefagiwa na kupambwa,
Then it saith, I will return to my house whence I came out. And on coming, it findeth it empty, and swept, and put in order.
45 huenda kuwachukua pepo wengine saba, wabaya kuliko yeye; na wote huja wakamwingia huyo mtu. Na hali ya mtu huyo sasa huwa mbaya kuliko hapo mwanzo. Ndivyo itakavyokuwa kwa watu hawa waovu.”
Then it goeth and taketh with it seven other spirits more wicked than itself, and they enter in, and dwell there; and the last state of that man becometh worse than the first. So will it be also with this wicked generation.
46 Yesu alikuwa bado anasema na umati wa watu wakati mama yake na ndugu zake walipofika na kusimama nje, wakitaka kusema naye.
While he was yet speaking to the multitudes, lo! his mother and his brothers were standing without, seeking to speak with him.
47 Basi, mtu mmoja akamwambia, “Mama yako na ndugu zako wako nje, wanataka kusema nawe.”
And one said to him, Behold, thy mother and thy brothers are standing without, seeking to speak with thee.
48 Lakini Yesu akamjibu mtu huyo, “Mama yangu ni nani? Na ndugu zangu ni kina nani?”
But he answered and said to him that told him, Who is my mother, and who are my brothers?
49 Kisha akaunyosha mkono wake kuelekea wanafunzi wake, akasema, “Hawa ndio mama yangu na ndugu zangu!
And stretching forth his hand toward his disciples, be said, Behold, my mother and my brothers!
50 Maana yeyote anayefanya anavyotaka Baba yangu aliye mbinguni, huyo ndiye ndugu yangu, dada yangu na mama yangu.”
For whoever doeth the will of my Father who is in heaven, he is my brother, and sister, and mother.

< Mathayo 12 >