< Mathayo 12 >

1 Wakati huo, Yesu alikuwa anapita katika mashamba ya ngano siku ya Sabato. Basi, wanafunzi wake wakaona njaa, wakaanza kukwanyua masuke ya ngano, wakala punje zake.
At that time Jesus was going, on the Sabbath, through the fields of grain; and his disciples were hungry, and began to pull the ears of grain, and to eat.
2 Mafarisayo walipoona hayo, wakamwambia Yesu, “Tazama, wanafunzi wako wanafanya jambo ambalo si halali siku ya Sabato.”
But when the Pharisees saw it, they said to him: Behold, your disciples are doing what it is not lawful to do on the Sabbath.
3 Yesu akawajibu, “Je, hamjasoma alivyofanya Daudi pamoja na wenzake wakati walipokuwa na njaa?
But he said to them: Have you not read what David did, when he and those who were with him were hungry?
4 Yeye aliingia katika Nyumba ya Mungu pamoja na wenzake, wakala ile mikate iliyowekwa mbele ya Mungu. Yeye wala hao wenzake hawakuruhusiwa kula mikate hiyo isipokuwa tu makuhani peke yao.
how he entered the house of God, and ate the loaves of the presence, which it was not lawful for him to eat, nor for those who were with him, but for the priests only?
5 Au je, hamjasoma katika Sheria kwamba kila siku ya Sabato makuhani huivunja Sheria Hekaluni, lakini hawafikiriwi kuwa na hatia?
Or, have you not read in the law that on the Sabbath-days the priests in the temple profane the Sabbath, and are blameless?
6 Basi, nawaambieni kwamba hapa pana kikuu kuliko Hekalu.
But I say to you, that something greater than the temple is here.
7 Kama tu mngejua maana ya maneno haya: Nataka huruma wala si dhabihu, hamngewahukumu watu wasio na hatia.
But if you had known what this means―I desire mercy, and not sacrifice―you would not have condemned the blameless.
8 Maana Mwana wa Mtu ni Bwana wa Sabato.”
For the Son of man is Lord of the Sabbath.
9 Yesu alitoka hapo, akaenda katika sunagogi lao.
And he departed thence, and went into their synagogue.
10 Kulikuwa na mtu mmoja mwenye mkono uliopooza. Basi, watu wakamwuliza Yesu, “Je, ni halali kumponya mtu siku ya Sabato?” Walimwuliza hivyo wapate kisa cha kumshtaki.
And behold, a man was there that had a withered hand. And they asked him, saying: Is it lawful to cure on the Sabbath-days? that they might accuse him.
11 Lakini Yesu akawaambia, “Tuseme mmoja wenu ana kondoo wake ambaye ametumbukia shimoni; je, hatamshika na kumtoa humo siku ya Sabato?
And he said to them: What man shall there be among you, that shall have one sheep, and if this fall into a pit on the Sabbath-day, will he not lay hold on it and lift it out?
12 Mtu ana thamani kuliko kondoo! Basi, ni halali kutenda mema siku ya Sabato.”
How much better, then, is a man than a sheep! So it is lawful to do well on the Sabbath-days.
13 Kisha akamwambia yule mtu, “Nyosha mkono wako.” Akaunyosha, nao ukawa mzima kabisa kama ule mwingine.
Then he said to the man: Stretch forth your hand. And he stretched it forth; and it was restored to soundness, like the other.
14 Basi, Mafarisayo wakatoka nje, wakashauriana jinsi watakavyomwangamiza Yesu.
But the Pharisees went out and took counsel against him, that they might destroy him.
15 Lakini Yesu alipojua jambo hilo, akatoka mahali pale. Watu wengi walimfuata, akawaponya wagonjwa wote,
But Jesus perceived it, and withdrew from that place. And many multitudes followed him, and he cured them all.
16 akawaamuru wasiwaambie watu habari zake,
And he charged them not to make him known;
17 ili yale aliyosema nabii Isaya yatimie:
that the word might be fulfilled which was spoken by Isaiah the prophet, saying:
18 “Hapa ni mtumishi wangu niliyemteua, mpendwa wangu anipendezaye moyoni. Nitaiweka Roho yangu juu yake, naye atatangaza hukumu yangu kwa mataifa yote.
Be hold, my servant whom I have chosen; my beloved, in whom my soul delights. I will put my Spirit upon him, and he shall declare law to the Gentiles.
19 Hatakuwa na ubishi wala kupiga kelele, wala sauti yake haitasikika barabarani.
He shall not contend, nor cry out; nor shall any one hear his voice in the streets.
20 Mwanzi uliopondeka hatauvunja, wala utambi ufukao moshi hatauzima, mpaka atakapoifanya hukumu ya haki itawale.
A bruised reed he shall not break, and a smoking wick he shall not extinguish, till he shall send forth his law for conquest.
21 Katika jina lake mataifa yatakuwa na tumaini.”
And in his name shall the Gentiles trust.
22 Hapo watu wakamletea Yesu kipofu mmoja ambaye alikuwa bubu kwa sababu alikuwa amepagawa na pepo. Yesu akamponya hata, akaweza kusema na kuona.
Then was brought to him a demoniac, blind and dumb: and he cured him, so that the blind and dumb man both spoke and saw.
23 Umati wote wa watu ulishangaa ukasema, “Je, huenda ikawa huyu ndiye Mwana wa Daudi?”
And all the people were amazed, and said: Is not this the son of David?
24 Lakini Mafarisayo waliposikia hayo, wakasema, “Mtu huyu anawafukuza pepo kwa uwezo wa Beelzebuli, mkuu wa pepo.”
But the Pharisees, when they heard it, said: This man does not cast out the demons, unless by Beelzebul, the prince of the demons.
25 Yesu, akiwa anayajua mawazo yao, akawaambia, “Ufalme wowote uliogawanyika makundimakundi yanayopingana, hauwezi kudumu, na mji wowote au jamaa yoyote iliyogawanyika makundimakundi yanayopingana, itaanguka.
But Jesus, knowing their thoughts, said to them: Every kingdom divided against itself is brought to desolation. And no city or house divided against itself shall stand.
26 Ikiwa Shetani anamfukuza Shetani, anajipinga mwenyewe. Basi, ufalme wake utasimamaje?
And if Satan cast out Satan, he is divided against himself; how then shall his kingdom stand?
27 Ninyi mnasema ati nawafukuza pepo kwa uwezo wa Beelzebuli; je, watoto wenu huwafukuza kwa uwezo wa nani? Kwa sababu hiyo wao ndio watakaowahukumu ninyi.
And if I cast out demons by Beelzebul, by whom do your sons cast them out? For this reason, they shall be your judges.
28 Lakini ikiwa ninawafukuza pepo kwa nguvu ya Roho wa Mungu, basi jueni kwamba Ufalme wa Mungu umekwisha fika kwenu.
But if I cast out demons by the Spirit of God, then the kingdom of God has already come upon you.
29 “Au, anawezaje mtu kuivamia nyumba ya mtu mwenye nguvu na kumnyang'anya mali yake, bila kwanza kumfunga huyo mtu mwenye nguvu? Hapo ndipo atakapoweza kumnyang'anya mali yake.
Or, how can any one enter the house of the strong man and spoil his goods, unless he first bind the strong man? and then he will plunder his house.
30 “Yeyote asiyejiunga nami, anapingana nami; na yeyote asiyekusanya pamoja nami, hutawanya.
He that is not with me, is against me; and he that gathers not with me, scatters.
31 Kwa sababu hiyo, nawaambieni, watu watasamehewa dhambi na kufuru zao zote, lakini hawatasamehewa dhambi ya kumkufuru Roho Mtakatifu.
Therefore I say to you, That every sin and impious speech shad be forgiven men: but the impious speech against the Spirit shall not be forgiven men.
32 Tena, asemaye neno la kumpinga Mwana wa Mtu atasamehewa, lakini yule asemaye neno la kumpinga Roho Mtakatifu, hatasamehewa, wala katika ulimwengu huu, wala katika ulimwengu ujao. (aiōn g165)
And whoever shall speak a word against the Son of man, it shall be forgiven him: but whoever shall speak against the Holy Spirit, it shall not be forgiven him, either in the present age, or in that which is to come. (aiōn g165)
33 “Ufanyeni mti kuwa mzuri na matunda yake yatakuwa mema; ufanyeni kuwa mbaya na matunda yake yatakuwa mabaya. Mti hujulikana kwa matunda yake.
Either make the tree good, and its fruit good; or make the tree unsound, and its fruit unsound. For by the fruit the tree is known.
34 Enyi kizazi cha nyoka! Mnawezaje kusema mambo mema hali ninyi ni waovu? Maana mtu husema kutokana na yale yaliyojaa moyoni.
Generation of vipers, how can you, being evil, speak good things? For out of the abundance of the heart, the mouth speaks.
35 Mtu mwema hutoa mambo mema katika hazina yake njema; na mtu mbaya hutoa mambo mabaya katika hazina yake mbaya.
The good man, out of his good treasury, brings forth good things; and the evil man, out of his evil treasury, brings forth evil things.
36 “Basi, nawaambieni, Siku ya hukumu watu watapaswa kujibu juu ya kila neno lisilofaa wanalosema.
But I say to you, That for every idle word which men speak, they shall give account in the day of judgment.
37 Maana kwa maneno yako, utakubaliwa kuwa mwadilifu, na kwa maneno yako, utahukumiwa kuwa na hatia.”
For by your words you shall be justified, and by your words you shall be condemned.
38 Kisha baadhi ya walimu wa Sheria na Mafarisayo wakamwambia Yesu, “Mwalimu, tunataka kuona ishara kutoka kwako.”
Then some of the scribes and Pharisees answered and said: Teacher, we wish to see a sign from you.
39 Naye akawajibu, “Kizazi kiovu kisicho na uaminifu! Mnataka ishara; hamtapewa ishara nyingine, ila tu ile ishara ya nabii Yona.
But he answered and said to them: A wicked and adulterous generation seeks for a sign; and no sign shall be given to it, but the sign of Jonah the prophet.
40 Jinsi Yona alivyokaa siku tatu kutwa kucha tumboni mwa nyangumi, ndivyo naye Mwana wa Mtu atakavyokaa ndani ya ardhi siku tatu kutwa kucha.
For as Jonah was three days and three nights in the belly of the great fish, so shall the Son of man be three days and three nights in the heart of the earth.
41 Watu wa Ninewi watatokea siku ya hukumu, nao watakihukumu kizazi hiki kwamba kina hatia. Maana Waninewi walitubu kwa sababu ya mahubiri ya Yona, na kumbe hapa kuna kikuu kuliko Yona!
Tho men of Nineveh shall rise in the judgment with this generation, and condemn it; for they repented in accordance with the preaching of Jonah; and behold, something greater than Jonah is here.
42 Malkia wa kusini atatokea wakati kizazi hiki kitakapohukumiwa, naye atakihukumu kwamba kina hatia. Maana yeye alisafiri kutoka mbali akaja kusikiliza maneno ya hekima ya Solomoni, na kumbe hapa kuna kikuu kuliko Solomoni.
The queen of the south shall rise in the judgment with this generation, and shall condemn it; for she came from the most distant parts of the earth to hear the wisdom of Solomon; and behold, something greater than Solomon is here.
43 “Pepo mchafu akifukuzwa kwa mtu, huzururazurura jangwani akitafuta mahali pa kupumzika asipate.
When the unclean spirit has gone out of a man, he goes through dry places seeking rest, and finds none.
44 Hapo hujisemea: Nitarudi nyumbani kwangu nilikotoka. Lakini anaporudi na kuikuta tupu, imefagiwa na kupambwa,
Then he says: I will return to my house, out of which I came. And he comes and finds it empty, swept, and set in order.
45 huenda kuwachukua pepo wengine saba, wabaya kuliko yeye; na wote huja wakamwingia huyo mtu. Na hali ya mtu huyo sasa huwa mbaya kuliko hapo mwanzo. Ndivyo itakavyokuwa kwa watu hawa waovu.”
Then he goes and takes with himself seven other spirits more wicked than himself; and they enter in and dwell there. And the last state of that man is worse than the first. So shall it be with this wicked generation.
46 Yesu alikuwa bado anasema na umati wa watu wakati mama yake na ndugu zake walipofika na kusimama nje, wakitaka kusema naye.
While he was yet speaking to the multitudes, behold, his mother and his brothers stood without, desiring to speak to him.
47 Basi, mtu mmoja akamwambia, “Mama yako na ndugu zako wako nje, wanataka kusema nawe.”
And some one said to him: Behold, your mother and your brothers stand without, desiring to speak to you.
48 Lakini Yesu akamjibu mtu huyo, “Mama yangu ni nani? Na ndugu zangu ni kina nani?”
But he answered and said to him that told him: Who is my mother? and who are my brothers?
49 Kisha akaunyosha mkono wake kuelekea wanafunzi wake, akasema, “Hawa ndio mama yangu na ndugu zangu!
And he stretched out his hand toward his disciples, and said: Behold my mother and my brothers.
50 Maana yeyote anayefanya anavyotaka Baba yangu aliye mbinguni, huyo ndiye ndugu yangu, dada yangu na mama yangu.”
For whoever will do the will of my Father who is in heaven, the same is my brother, and sister, and mother.

< Mathayo 12 >