+ Mathayo 1 >
1 Yesu Kristo alikuwa mzawa wa Daudi, mzawa wa Abrahamu. Hii ndiyo orodha ya ukoo wake:
Hin cun Davita capa, Abrahama capa, Jesuh Khritawa ksawn tähnak cajina kyaki.
2 Abrahamu alimzaa Isaka, Isaka alimzaa Yakobo, Yakobo alimzaa Yuda na ndugu zake,
Abrahama ca Isak, Isaka ca Jakop, acunüng Jakop naw Judah ja a bena he a jah canak.
3 Yuda alimzaa Faresi na Zera (mama yao alikuwa Tamari), Faresi alimzaa Hesroni, Hesroni alimzaa Rami,
Judah naw Tamari am Pereh ja Sherah a jah canak, Pereh naw Heron ca na lü, acunüng Heron naw Ram a canak.
4 Rami alimzaa Aminadabu, Aminadabu alimzaa Nashoni, Nashoni alimzaa Salmoni,
Rama ca Aminadap, Aminadapa ca Nashon, Nashona ca Salmon.
5 Salmoni alimzaa Boazi (mama yake Boazi alikuwa Rahabu). Boazi na Ruthi walikuwa wazazi wa Obedi, Obedi alimzaa Yese,
Salmon naw Rahap am Bozah a canak, Bozah naw Rutah am Obet a canak, Obet naw Jise a canak.
6 naye Yese alimzaa Mfalme Daudi. Daudi alimzaa Solomoni (mama yake Solomoni alikuwa mke wa Uria).
Jise naw Sangpuxang Davit a canak. Sangpuxang Davit naw Sangpuxang Solamon a canak, a nu cun Urijaa khyu Davit naw a khämbea kyaki.
7 Solomoni alimzaa Rehoboamu, Rehoboamu alimzaa Abiya, Abiya alimzaa Asa,
Solamona ca Rehobawm, Rehobawma ca Abijah, Abijaha ca Asa.
8 Asa alimzaa Yehoshafati, Yehoshafati alimzaa Yoramu, Yoramu alimzaa Uzia,
Asaa ca Jehosaphat, Jehosaphata ca Jehoram, Jehoram naw Usia a canak.
9 Uzia alimzaa Yothamu, Yothamu alimzaa Ahazi, Ahazi alimzaa Hezekia,
Usiaa ca Jotham, Jothama ca Ahaz, Ahaza ca Hezakiha kyaki.
10 Hezekia alimzaa Manase, Manase alimzaa Amoni, Amoni alimzaa Yosia,
Hezakiha ca Manaseh, Manaseha ca Amon, Amona ca Josiah.
11 Yosia alimzaa Yekonia na ndugu zake. Huo ulikuwa wakati Wayahudi walipopelekwa uhamishoni Babuloni.
Isarel he jah man u lü Babalunga ami jah cehpüi, acun k'um üng Josiah naw Jekhonih ja a bena he a jah canak.
12 Baada ya Wayahudi kupelekwa uhamishomi Babuloni: Yekonia alimzaa Shealtieli, Shealtieli alimzaa Zerobabeli,
Babalunga ami jah cehpüi käna Jekhoniha ca Shaltilah, Shaltilaha ca Zerubabel.
13 Zerobabeli alimzaa Abiudi, Abiudi alimzaa Eliakimu, Eliakimu alimzaa Azori,
Zerubabela ca Abiud, Abiuda ca Eliakim, Eliakima ca Azora kyaki.
14 Azori alimzaa Zadoki, Zadoki alimzaa Akimu, Akimu alimzaa Eliudi,
Azora ca Zadok, Zadoka ca Achim, Achima ca Eliud.
15 Eliudi alimzaa Eleazeri, Eleazeri alimzaa Mathani, Mathani alimzaa Yakobo,
Eliuda ca Elezar, Elezara ca Matthan, Matthana ca Jakopa kyaki.
16 Yakobo alimzaa Yosefu, aliyekuwa mume wake Maria, mama yake Yesu, aitwaye Kristo.
Acunüng Jakopa ca cun Josep, Mariha ceia kyaki, Marih cun Khritaw Mesijah ti Jesuha nua kyaki.
17 Basi, kulikuwa na vizazi kumi na vinne tangu Abrahamu mpaka Daudi, vizazi kumi na vinne tangu Daudi mpaka Wayahudi walipochukuliwa mateka Babuloni, na vizazi kumi na vinne tangu kuchukuliwa mateka mpaka wakati wa Kristo.
Abraham üngka naw Davit cäpa ksawn xaleikphyü lawki. Davit üngka naw Babalung mpya vaia ami jah cehpüi cäpa ksawn xaleikphyü lawki. Acunüng Babalung mpya üngka naw Messijah hmi law cäpa ksawn xaleikphyü lawki.
18 Basi, hivi ndivyo Yesu Kristo alivyozaliwa: Maria, mama yake, alikuwa ameposwa na Yosefu. Lakini kabla hawajakaa pamoja kama mume na mke, alionekana kuwa mja mzito kwa uwezo wa Roho Mtakatifu.
Jesuh Khritaw a hmi lawa mawng cun hikbaa kyaki. A nu Marih cun Josepa khyu vaia ami mkhyäp käna, atänga am ani awm ham üng, Marih cun Ngmüimkhya Ngcim naw a mpyaisak.
19 Yosefu, mumewe, kwa vile alikuwa mwadilifu, hakutaka kumwaibisha hadharani; hivyo alikusudia kumwacha kwa siri.
A cei vaia Josep cun khyang ngsungpyuna kya lü, khyang he maa Marih cun am luthui hmaiset hlüsak lü, ampyua hawih be khaia büki.
20 Alipokuwa bado anawaza jambo hilo, malaika wa Bwana alimtokea katika ndoto, akamwambia, “Yosefu, mwana wa Daudi, usiogope kumchukua Maria awe mke wako, maana amekuwa mja mzito kwa uwezo wa Roho Mtakatifu.
Acunüngpi, acukba a ngaih k'um üng, a ngmang üng Bawipaa khankhawngsä ngdang vai lü, “Davita capa Josep, Marih na khyunak vai käh cäia. Isetiakyaküng a mpyai hin ta Ngmüimkhya Ngcima mpyaisak ni.
21 Atajifungua mtoto wa kiume, nawe utampa jina Yesu, kwa kuwa yeye atawaokoa watu wake kutoka katika dhambi zao.”
Ani cun kpamicaa ca khai, a khyang he ami mkhyekatnak üngkhyüh jah küikyan khaia kyase a ngming cun Jesuha na sui khai,” a ti.
22 Basi, haya yote yalitukia ili litimie lile neno Bwana alilosema kwa njia ya nabii:
Ahina mawng cun Bawipa naw Sahma he üngkhyüh a pyen khawi a kümnak vaia kyaki.
23 “Bikira atachukua mimba, atamzaa mtoto wa kiume, naye ataitwa Emanueli” (maana yake, “Mungu yu pamoja nasi”).
Pamhnama ngthu ta, “Teng ua, nglamica mpyai law lü, cangpyang ca na law khai, a ngming cun Imanuelaha sui law khai he,” ti hlü ta, “Pamhnam cun mi hlawnga awmki,” tinaka kyaki.
24 Hivyo, Yosefu alipoamka usingizini alifanya kama malaika huyo alivyomwambia, akamchukua mke wake nyumbani.
Josep cun ip lü a let law üng, Bawipa khankhawngsä naw a pyena kba Marih a khyunak.
25 Lakini hakumjua kamwe kimwili hata Maria alipojifungua mtoto wa kiume. Naye Yosefu akampa jina Yesu.
Acunüngpi, Josep ja Marih cun Marih a camah veia alanga am ip khawi ni. Josep naw hnasena ngming cun Jesuha a sui.