< Marko 1 >
1 Habari Njema ya Yesu Kristo, Mwana wa Mungu.
A beginning of the good news of Jesus Christ, Son of God.
2 Ilianza kama ilivyoandikwa katika kitabu cha nabii Isaya: “Tazama, namtuma mjumbe wangu akutangulie; yeye atakutayarishia njia yako.
As it hath been written in the prophets, 'Lo, I send My messenger before thy face, who shall prepare thy way before thee,' —
3 Sauti ya mtu imesikika jangwani: Mtayarishieni Bwana njia yake, nyoosheni mapito yake.”
'A voice of one calling in the wilderness, Prepare ye the way of the Lord, straight make ye his paths,' —
4 Yohane Mbatizaji alitokea jangwani, akahubiri kwamba ni lazima watu watubu na kubatizwa ili Mungu awasamehe dhambi zao.
John came baptizing in the wilderness, and proclaiming a baptism of reformation — to remission of sins,
5 Watu kutoka sehemu zote za Yudea na wenyeji wote wa Yerusalemu walimwendea, wakaziungama dhambi zao, naye akawabatiza katika mto Yordani.
and there were going forth to him all the region of Judea, and they of Jerusalem, and they were all baptized by him in the river Jordan, confessing their sins.
6 Yohane alikuwa amevaa vazi lililofumwa kwa manyoya ya ngamia, na mkanda wa ngozi kiunoni mwake. Chakula chake kilikuwa nzige na asali ya mwituni.
And John was clothed with camel's hair, and a girdle of skin around his loins, and eating locusts and honey of the field,
7 Naye alihubiri akisema, “Baada yangu anakuja mwenye uwezo zaidi kuliko mimi, ambaye mimi sistahili hata kuinama na kufungua kamba za viatu vyake.
and he proclaimed, saying, 'He doth come — who is mightier than I — after me, of whom I am not worthy — having stooped down — to loose the latchet of his sandals;
8 Mimi ninawabatiza kwa maji, lakini yeye atawabatiza kwa Roho Mtakatifu.”
I indeed did baptize you with water, but he shall baptize you with the Holy Spirit.'
9 Siku hizo, Yesu alifika kutoka Nazareti, mji wa Galilaya, akabatizwa na Yohane katika mto Yordani.
And it came to pass in those days, Jesus came from Nazareth of Galilee, and was baptized by John at the Jordan;
10 Mara tu alipotoka majini, aliona mbingu zimefunguliwa, na Roho akishuka juu yake kama njiwa.
and immediately coming up from the water, he saw the heavens dividing, and the Spirit as a dove coming down upon him;
11 Sauti ikasikika kutoka mbinguni: “Wewe ni Mwanangu mpendwa, nimependezwa nawe.”
and a voice came out of the heavens, 'Thou art My Son — the Beloved, in whom I did delight.'
12 Mara akaongozwa na Roho kwenda jangwani,
And immediately doth the Spirit put him forth to the wilderness,
13 akakaa huko siku arubaini akijaribiwa na Shetani. Alikuwa huko pamoja na wanyama wa porini, nao malaika wakawa wanamtumikia.
and he was there in the wilderness forty days, being tempted by the Adversary, and he was with the beasts, and the messengers were ministering to him.
14 Yohane alipokwisha fungwa gerezani, Yesu alikwenda Galilaya, akahubiri Habari Njema ya Mungu, akisema,
And after the delivering up of John, Jesus came to Galilee, proclaiming the good news of the reign of God,
15 “Wakati umetimia, na Ufalme wa Mungu umekaribia. Tubuni na kuiamini Habari Njema!”
and saying — 'Fulfilled hath been the time, and the reign of God hath come nigh, reform ye, and believe in the good news.'
16 Alipokuwa anapita kando ya ziwa Galilaya, aliwaona wavuvi wawili: Simoni na Andrea ndugu yake wakivua samaki kwa wavu.
And, walking by the sea of Galilee, he saw Simon, and Andrew his brother, casting a drag into the sea, for they were fishers,
17 Yesu akawaambia, “Nifuateni nami nitawafanya ninyi wavuvi wa watu.”
and Jesus said to them, 'Come ye after me, and I shall make you to become fishers of men;'
18 Mara wakaziacha nyavu zao, wakamfuata.
and immediately, having left their nets, they followed him.
19 Alipokwenda mbele kidogo, aliwaona Yakobo na Yohane, wana wa Zebedayo. Nao pia walikuwa ndani ya mashua yao wakizitengeneza nyavu zao.
And having gone on thence a little, he saw James of Zebedee, and John his brother, and they were in the boat refitting the nets,
20 Yesu akawaita mara, nao wakamwacha baba yao Zebedayo katika mashua pamoja na wafanyakazi, wakamfuata.
and immediately he called them, and, having left their father Zebedee in the boat with the hired servants, they went away after him.
21 Wakafika mjini Kafarnaumu, na mara ilipofika Sabato, Yesu akaingia katika Sunagogi, akaanza kufundisha.
And they go on to Capernaum, and immediately, on the sabbaths, having gone into the synagogue, he was teaching,
22 Watu wote waliomsikia walishangazwa na mafundisho yake, maana hakuwa anafundisha kama walimu wao wa Sheria, bali kama mtu mwenye mamlaka.
and they were astonished at his teaching, for he was teaching them as having authority, and not as the scribes.
23 Mara akatokea mle ndani ya sunagogi mtu mmoja mwenye pepo mchafu,
And there was in their synagogue a man with an unclean spirit, and he cried out,
24 akapaaza sauti, “Una nini nasi, wewe Yesu wa Nazareti? Je, umekuja kutuangamiza? Najua wewe ni nani: wewe ni Mtakatifu wa Mungu!”
saying, 'Away! what — to us and to thee, Jesus the Nazarene? thou didst come to destroy us; I have known thee who thou art — the Holy One of God.'
25 Yesu akamkemea, “Nyamaza! Mtoke mtu huyu.”
And Jesus rebuked him, saying, 'Be silenced, and come forth out of him,'
26 Basi, huyo pepo mchafu akamtikisatikisa mtu huyo, kisha akalia kwa sauti kubwa, akamtoka.
and the unclean spirit having torn him, and having cried with a great voice, came forth out of him,
27 Watu wote wakashangaa, wakaulizana, “Ni mambo gani haya? Je, ni mafundisho mapya? Mtu huyu anayo mamlaka ya kuamuru hata pepo wachafu, nao wanamtii!”
and they were all amazed, so as to reason among themselves, saying, 'What is this? what new teaching [is] this? that with authority also the unclean spirits he commandeth, and they obey him!'
28 Habari za Yesu zikaenea upesi kila mahali katika wilaya ya Galilaya.
And the fame of him went forth immediately to all the region, round about, of Galilee.
29 Wakatoka katika sunagogi, wakaenda moja kwa moja hadi nyumbani kwa Simoni na Andrea; Yakobo na Yohane walikwenda pamoja nao.
And immediately, having come forth out of the synagogue, they went to the house of Simon and Andrew, with James and John,
30 Basi, mama mmoja, mkwewe Simoni, alikuwa kitandani ana homa kali. Wakamwarifu Yesu mara alipowasili.
and the mother-in-law of Simon was lying fevered, and immediately they tell him about her,
31 Yesu akamwendea huyo mama, akamshika mkono, akamwinua. Na ile homa ikamwacha, akaanza kuwatumikia.
and having come near, he raised her up, having laid hold of her hand, and the fever left her immediately, and she was ministering to them.
32 Jioni, jua lilipokwisha tua, wakamletea Yesu wagonjwa wote na watu waliopagawa na pepo.
And evening having come, when the sun did set, they brought unto him all who were ill, and who were demoniacs,
33 Watu wote wa mji ule wakakusanyika nje ya mlango.
and the whole city was gathered together near the door,
34 Naye Yesu akawaponya watu wengi waliokuwa na magonjwa mbalimbali; aliwafukuza pepo wengi, lakini hakuwaruhusu kusema kitu maana walikuwa wanamjua yeye ni nani.
and he healed many who were ill of manifold diseases, and many demons he cast forth, and was not suffering the demons to speak, because they knew him.
35 Kesho yake, kabla ya mapambazuko, Yesu alitoka, akaenda mahali pa faragha kusali.
And very early, it being yet night, having risen, he went forth, and went away to a desert place, and was there praying;
36 Simoni na wenzake wakaenda kumtafuta.
and Simon and those with him went in quest of him,
37 Walipomwona wakamwambia, “Kila mtu anakutafuta.”
and having found him, they say to him, — 'All do seek thee;'
38 Yesu akawaambia, “Twendeni katika miji mingine ya jirani nikahubiri huko pia, maana nimekuja kwa sababu hiyo.”
and he saith to them, 'We may go to the next towns, that there also I may preach, for for this I came forth.'
39 Basi, akaenda kila mahali Galilaya akihubiri katika masunagogi na kufukuza pepo.
And he was preaching in their synagogues, in all Galilee, and is casting out the demons,
40 Mtu mmoja mwenye ukoma alimwendea Yesu, akapiga magoti, akamwomba, “Ukitaka, waweza kunitakasa!”
and there doth come to him a leper, calling on him, and kneeling to him, and saying to him — 'If thou mayest will, thou art able to cleanse me.'
41 Yesu akamwonea huruma, akanyosha mkono wake, akamgusa na kumwambia, “Nataka, takasika!”
And Jesus having been moved with compassion, having stretched forth the hand, touched him, and saith to him, 'I will; be thou cleansed;'
42 Mara ukoma ukamwacha mtu huyo, akatakasika.
and he having spoken, immediately the leprosy went away from him, and he was cleansed.
43 Kisha Yesu akamwambia aende zake upesi na kumwonya vikali,
And having sternly charged him, immediately he put him forth,
44 “Usimwambie mtu yeyote jambo hili, ila nenda ukajionyeshe kwa kuhani; kisha utoe sadaka kwa ajili ya kutakasika kwako kama alivyoamuru Mose, iwe uthibitisho kwao kwamba umepona.”
and saith to him, 'See thou mayest say nothing to any one, but go away, thyself shew to the priest, and bring near for thy cleansing the things Moses directed, for a testimony to them.'
45 Lakini huyo mtu akaenda, akaanza kueneza habari hiyo kila mahali na kusema mambo mengi hata Yesu hakuweza tena kuingia katika mji wowote waziwazi; ikamlazimu kukaa nje, mahali pa faragha. Hata hivyo, watu wakamwendea kutoka kila upande.
And he, having gone forth, began to proclaim much, and to spread abroad the thing, so that no more he was able openly to enter into the city, but he was without in desert places, and they were coming unto him from every quarter.