< Marko 1 >
1 Habari Njema ya Yesu Kristo, Mwana wa Mungu.
The beginning of the gospel of JESUS CHRIST the Son of GOD.
2 Ilianza kama ilivyoandikwa katika kitabu cha nabii Isaya: “Tazama, namtuma mjumbe wangu akutangulie; yeye atakutayarishia njia yako.
As it is written in the prophets, "Behold, I send my messenger before thy face, who shall prepare thy way before thee:"
3 Sauti ya mtu imesikika jangwani: Mtayarishieni Bwana njia yake, nyoosheni mapito yake.”
and again, "The voice of one crying in the wilderness, Prepare ye the way of the Lord, make his paths straight:" accordingly John came baptizing in the wilderness,
4 Yohane Mbatizaji alitokea jangwani, akahubiri kwamba ni lazima watu watubu na kubatizwa ili Mungu awasamehe dhambi zao.
and preaching the baptism of repentance in order to the remission of sins;
5 Watu kutoka sehemu zote za Yudea na wenyeji wote wa Yerusalemu walimwendea, wakaziungama dhambi zao, naye akawabatiza katika mto Yordani.
and all the country of Judea, and those of Jerusalem, went out to him, and were all baptized by him in the river Jordan, confessing their sins.
6 Yohane alikuwa amevaa vazi lililofumwa kwa manyoya ya ngamia, na mkanda wa ngozi kiunoni mwake. Chakula chake kilikuwa nzige na asali ya mwituni.
And John was clothed with camels hair, and a leathern girdle about his loins, and he lived upon locusts and wild honey: and he preached,
7 Naye alihubiri akisema, “Baada yangu anakuja mwenye uwezo zaidi kuliko mimi, ambaye mimi sistahili hata kuinama na kufungua kamba za viatu vyake.
saying, There cometh after me one mightier than I, the latchet of whose shoes I am not worthy to stoop and unloose.
8 Mimi ninawabatiza kwa maji, lakini yeye atawabatiza kwa Roho Mtakatifu.”
I indeed have baptized you with water, but He will baptize you with the holy Spirit.
9 Siku hizo, Yesu alifika kutoka Nazareti, mji wa Galilaya, akabatizwa na Yohane katika mto Yordani.
And in those days Jesus came from Nazareth of Galilee, and was baptized by John in Jordan:
10 Mara tu alipotoka majini, aliona mbingu zimefunguliwa, na Roho akishuka juu yake kama njiwa.
and as soon as He came up from the water, he saw the heavens opened, and the Spirit like a dove descending upon Him.
11 Sauti ikasikika kutoka mbinguni: “Wewe ni Mwanangu mpendwa, nimependezwa nawe.”
And there was a voice from heaven, saying, This is my beloved Son, in whom I am well pleased.
12 Mara akaongozwa na Roho kwenda jangwani,
And immediately the Spirit taketh Him out into the wilderness:
13 akakaa huko siku arubaini akijaribiwa na Shetani. Alikuwa huko pamoja na wanyama wa porini, nao malaika wakawa wanamtumikia.
and He was there in the wilderness forty days tempted by Satan, and among the wild beasts: and angels ministred unto Him.
14 Yohane alipokwisha fungwa gerezani, Yesu alikwenda Galilaya, akahubiri Habari Njema ya Mungu, akisema,
Now after John was cast into prison, Jesus came into Galilee, preaching the gospel of the kingdom of God,
15 “Wakati umetimia, na Ufalme wa Mungu umekaribia. Tubuni na kuiamini Habari Njema!”
and saying, The time is fulfilled, and the kingdom of God is at hand: repent, and believe the gospel.
16 Alipokuwa anapita kando ya ziwa Galilaya, aliwaona wavuvi wawili: Simoni na Andrea ndugu yake wakivua samaki kwa wavu.
And as He was walking by the sea of Galilee, He saw Simon and Andrew his brother, casting a net into the sea,
17 Yesu akawaambia, “Nifuateni nami nitawafanya ninyi wavuvi wa watu.”
(for they were fishermen, ) and Jesus said unto them, Come after me, and I will make you fishers of men:
18 Mara wakaziacha nyavu zao, wakamfuata.
and immediately they left their nets and followed Him.
19 Alipokwenda mbele kidogo, aliwaona Yakobo na Yohane, wana wa Zebedayo. Nao pia walikuwa ndani ya mashua yao wakizitengeneza nyavu zao.
And going a little farther, He saw James the son of Zebedee, and John his brother, in a ship, mending their nets, and immediately called them likewise:
20 Yesu akawaita mara, nao wakamwacha baba yao Zebedayo katika mashua pamoja na wafanyakazi, wakamfuata.
and they left their father Zebedee in the ship with the men he had hired, and went along with Him.
21 Wakafika mjini Kafarnaumu, na mara ilipofika Sabato, Yesu akaingia katika Sunagogi, akaanza kufundisha.
And they went into Capernaum: and going directly into the synagogue on the sabbath, He taught the people: and they were astonished at his doctrine;
22 Watu wote waliomsikia walishangazwa na mafundisho yake, maana hakuwa anafundisha kama walimu wao wa Sheria, bali kama mtu mwenye mamlaka.
for He taught them as one that had authority, and not as the scribes.
23 Mara akatokea mle ndani ya sunagogi mtu mmoja mwenye pepo mchafu,
And there was in their synagogue a man with an impure spirit,
24 akapaaza sauti, “Una nini nasi, wewe Yesu wa Nazareti? Je, umekuja kutuangamiza? Najua wewe ni nani: wewe ni Mtakatifu wa Mungu!”
and he cried out, saying, Let us alone, what have we to do with thee, Jesus of Nazareth? art thou come to destroy us? I know thee, who thou art, the holy one of God.
25 Yesu akamkemea, “Nyamaza! Mtoke mtu huyu.”
And Jesus rebuked him, saying, Be silent, and come out of him: and the impure spirit threw him into convulsions,
26 Basi, huyo pepo mchafu akamtikisatikisa mtu huyo, kisha akalia kwa sauti kubwa, akamtoka.
and roaring with a loud voice, came out of him.
27 Watu wote wakashangaa, wakaulizana, “Ni mambo gani haya? Je, ni mafundisho mapya? Mtu huyu anayo mamlaka ya kuamuru hata pepo wachafu, nao wanamtii!”
And they were all amazed, so that they inquired of each other, saying, What is this, what new kind of doctrine is this? for He commands with authority even the impure spirits, and they obey Him.
28 Habari za Yesu zikaenea upesi kila mahali katika wilaya ya Galilaya.
And straitway his fame spread into all the country round about Galilee.
29 Wakatoka katika sunagogi, wakaenda moja kwa moja hadi nyumbani kwa Simoni na Andrea; Yakobo na Yohane walikwenda pamoja nao.
And as soon as they came out of the synagogue, they went into the house of Simon and Andrew, together with James and John.
30 Basi, mama mmoja, mkwewe Simoni, alikuwa kitandani ana homa kali. Wakamwarifu Yesu mara alipowasili.
And Simon's wife's mother lay sick of a fever: and they immediately told Him of her:
31 Yesu akamwendea huyo mama, akamshika mkono, akamwinua. Na ile homa ikamwacha, akaanza kuwatumikia.
and He came to her, and taking her by the hand raised her up; and immediately the fever left her, and she waited upon them.
32 Jioni, jua lilipokwisha tua, wakamletea Yesu wagonjwa wote na watu waliopagawa na pepo.
And in the evening, when the sun set, they brought to Him all that were ill, and demoniacs:
33 Watu wote wa mji ule wakakusanyika nje ya mlango.
and the whole city was gathered together at the door;
34 Naye Yesu akawaponya watu wengi waliokuwa na magonjwa mbalimbali; aliwafukuza pepo wengi, lakini hakuwaruhusu kusema kitu maana walikuwa wanamjua yeye ni nani.
and He healed many that were ill of various diseases, and cast out many devils, and suffered not the devils to say that they knew Him.
35 Kesho yake, kabla ya mapambazuko, Yesu alitoka, akaenda mahali pa faragha kusali.
And in the morning, before it was light, He rose up and went out, and retired into a solitary place, and there prayed.
36 Simoni na wenzake wakaenda kumtafuta.
And Simon, and they that were with him, went in quest of Him:
37 Walipomwona wakamwambia, “Kila mtu anakutafuta.”
and when they found Him, they said to Him, all the people are seeking for thee.
38 Yesu akawaambia, “Twendeni katika miji mingine ya jirani nikahubiri huko pia, maana nimekuja kwa sababu hiyo.”
And He saith unto them, Let us go into the neighbouring towns, that I may preach there also; for this was the end of my coming.
39 Basi, akaenda kila mahali Galilaya akihubiri katika masunagogi na kufukuza pepo.
And He went preaching in their synagogues, through all Galilee, and casting out devils.
40 Mtu mmoja mwenye ukoma alimwendea Yesu, akapiga magoti, akamwomba, “Ukitaka, waweza kunitakasa!”
And there came to Him a leper, beseeching Him, and kneeling down to Him, and saying unto Him, If thou wilt, thou canst cleanse me:
41 Yesu akamwonea huruma, akanyosha mkono wake, akamgusa na kumwambia, “Nataka, takasika!”
and Jesus, being moved with compassion, stretched out his hand and touched him, and saith unto Him, I will;
42 Mara ukoma ukamwacha mtu huyo, akatakasika.
be thou healed: and as soon as He had spoken, immediately the leprosy left him, and he was healed.
43 Kisha Yesu akamwambia aende zake upesi na kumwonya vikali,
And he gave him a strict charge, and immediately dismissed him,
44 “Usimwambie mtu yeyote jambo hili, ila nenda ukajionyeshe kwa kuhani; kisha utoe sadaka kwa ajili ya kutakasika kwako kama alivyoamuru Mose, iwe uthibitisho kwao kwamba umepona.”
and saith unto him, See thou tell no man: but go, shew thyself to the priest, and offer for thy purification what Moses has commanded, for a testimony to them.
45 Lakini huyo mtu akaenda, akaanza kueneza habari hiyo kila mahali na kusema mambo mengi hata Yesu hakuweza tena kuingia katika mji wowote waziwazi; ikamlazimu kukaa nje, mahali pa faragha. Hata hivyo, watu wakamwendea kutoka kila upande.
But when he was gone he began to publish it much, and to spread abroad the report: so that Jesus could no more go openly into the city, but kept out in country places: and they came to Him from all parts.