< Marko 9 >
1 Yesu akaendelea kuwaambia, “Kweli nawaambieni, wako wengine papa hapa ambao hawatakufa kabla ya kuuona Ufalme wa Mungu ukija kwa enzi.”
And he said to them: Verily I say to you, There are some standing here, who will not taste of death, until they shall see the kingdom of God to be coming with power.
2 Baada ya siku sita, Yesu aliwachukua Petro, Yakobo na Yohane juu ya mlima mrefu peke yao. Huko, Yesu akageuka sura mbele yao,
And after six days, Jesus took Cephas and James and John, and led them to a high mountain, apart; and was transformed before them.
3 mavazi yake yakang'aa, yakawa meupe sana, jinsi dobi yeyote duniani asingeweza kuyafanya meupe.
And his raiment shone and was very white, like snow, so as men on earth can never whiten.
4 Eliya na Mose wakawatokea, wakazungumza na Yesu.
And there appeared to them Moses and Elijah, in conversation with Jesus.
5 Petro akamwambia Yesu, “Mwalimu, ni vizuri sana kwamba tuko hapa. Basi, afadhali tujenge vibanda vitatu: kimoja chako, kimoja cha Mose na kimoja cha Eliya.”
And Cephas said to him: Rabbi, it is delightful for us to be here. And let us make three booths; one for thee, and one for Moses, and one for Elijah.
6 Yeye na wenzake waliogopa hata hakujua la kusema.
But he did not know what he said, for they were in trepidation.
7 Kisha likatokea wingu likawafunika, na sauti ikasikika kutoka katika hilo wingu, “Huyu ni Mwanangu mpendwa, msikilizeni.”
And there was a cloud, and it overshadowed them. And a voice issued from the cloud, which said: This is my beloved Son. Hear ye him.
8 Mara wanafunzi hao wakatazama tena, lakini hawakumwona mtu mwingine, ila Yesu peke yake pamoja nao.
And suddenly, when the disciples looked up, they saw no one with them, except Jesus only.
9 Walipokuwa wakishuka mlimani, Yesu aliwakataza wasimwambie mtu yeyote mambo waliyoyaona, mpaka Mwana wa Mtu atakapokuwa amefufuka kutoka wafu.
And as they descended the mountain, he commanded them to tell no man what they had seen, till after the Son of man should be risen from the dead.
10 Basi, wakashika agizo hilo, lakini wakawa wanajadiliana wao kwa wao maana ya kufufuka kutoka wafu.
And they kept that saying in their mind; and inquired, What doth this saying mean: " When he shall be risen from the dead!"
11 Wakamwuliza Yesu, “Mbona walimu wa Sheria wanasema kwamba ni lazima Eliya aje kwanza?”
And they asked him, and said: Why then do the Scribes say, that Elijah must first come?
12 Naye akawajibu, “Naam, Eliya anakuja kwanza kutayarisha yote. Hata hivyo, kwa nini basi imeandikwa katika Maandiko Matakatifu kwamba Mwana wa Mtu atapatwa na mateso mengi na kudharauliwa?
He said to them: Elijah truly first cometh, to prepare all things: and, as it is written of the Son of man, he will suffer much, and be rejected.
13 Lakini nawaambieni, Eliya amekwisha kuja, nao wakamtendea walivyotaka kama ilivyoandikwa juu yake.”
But I say to you: That Elijah hath come; and they have done to him all that they desired, as it was written of him.
14 Walipowafikia wale wanafunzi wengine, waliona umati mkubwa wa watu hapo. Na baadhi ya walimu wa Sheria walikuwa wanajadiliana nao.
And when he came to his disciples, he saw a great multitude with them, and the Scribes disputing with them.
15 Mara tu ule umati wa watu ulipomwona, wote walishangaa sana, wakamkimbilia wamsalimu.
And immediately the multitude saw him, and were surprised: and they ran and saluted him.
16 Yesu akawauliza, “Mnajadiliana nini nao?”
And he asked the Scribes: What were ye disputing with them?
17 Hapo mtu mmoja katika ule umati wa watu akamjibu, “Mwalimu, nimemleta mwanangu kwako, ana pepo aliyemfanya kuwa bubu.
And one of the multitude replied, and said: Teacher, I have brought to thee my son, who hath a spirit that will not speak.
18 Kila mara anapomvamia, humwangusha chini na kumfanya atokwe na povu kinywani, akisaga meno na kuwa mkavu mwili wote. Niliwaomba wanafunzi wako wamtoe huyo pepo lakini hawakuweza.”
And wherever he seizeth him, he shaketh and teareth him: and he gnasheth his teeth, and pineth away. And I spoke to thy disciples, to cast him out; and they could not.
19 Yesu akawaambia, “Enyi kizazi kisicho na imani! Nitakaa nanyi mpaka lini? Nitawavumilia mpaka lini? Mleteni kwangu.”
Jesus answered, and said to them: O incredulous generation! How long shall I be with you? how long bear with you? Bring him to me.
20 Wakampeleka. Mara tu huyo pepo alipomwona Yesu, alimtia mtoto kifafa, naye mtoto akaanguka chini, akagaagaa na kutoka povu kinywani. Yesu akamwuliza baba yake huyo mtoto,
And they brought him to him. And when the spirit saw him, immediately he shook him; and he fell upon the ground, and wallowed and foamed.
21 “Amepatwa na mambo hayo tangu lini?” Naye akamjibu, “Tangu utoto wake.
And Jesus asked his father, how long a time he had been thus. He said to him: Lo, from his childhood.
22 Na mara nyingi pepo huyo amemwangusha motoni na majini, ili amwangamize kabisa. Basi, ikiwa waweza, utuhurumie na kutusaidia!”
And many times it hath thrown him into the fire, and into the water, to destroy him. But, if thou canst do any thing, aid me and have compassion on me.
23 Yesu akamwambia, “Eti ikiwa waweza! Mambo yote yanawezekana kwa mtu aliye na imani.”
Jesus said to him: If thou canst believe; every thing can be, to him that believeth.
24 Hapo, huyo baba akalia kwa sauti, “Naamini! Lakini imani yangu haitoshi, nisaidie!”
And immediately the father of the child cried out, while he wept and said: I believe; aid thou the defect of my faith.
25 Yesu alipouona umati wa watu unaongezeka upesi mbele yake, alimkemea yule pepo mchafu, “Pepo unayemfanya huyu mtoto kuwa bubu-kiziwi, nakuamuru, mtoke mtoto huyu wala usimwingie tena!”
And when Jesus saw that the people were, running and collecting around him, he rebuked the unclean spirit, and said to him: Thou deaf and unspeaking spirit, I command thee, come out of him; and no more enter him.
26 Hapo huyo pepo alipaaza sauti, akamwangusha huyo mtoto chini, kisha akamtoka. Mtoto alionekana kama maiti, hata wengine walisema, “Amekufa!”
And the demon cried out greatly, and bruised him, and came out. And he was as a dead person; so that many would say, he is dead.
27 Lakini Yesu akamshika mkono, akamwinua, naye akasimama.
And Jesus took him by the hand, and raised him up.
28 Yesu alipoingia nyumbani, wanafunzi wake walimwuliza kwa faragha, “Kwa nini sisi hatukuweza kumtoa?”
And when Jesus entered the house, his disciples asked him privately: Why could not we cast him out?
29 Naye akawaambia, “Pepo wa aina hii hawezi kutoka isipokuwa kwa sala tu.”
He saith to them: This kind can come out, by nothing but fasting and prayer.
30 Yesu na wanafunzi wake waliondoka hapo, wakaendelea na safari kupitia wilaya ya Galilaya. Yesu hakupenda watu wajue alipokuwa,
And when he departed from there, they passed through Galilee: and he desired that no one might know him.
31 kwa sababu alikuwa anawafundisha wanafunzi wake. Aliwaambia, “Mwana wa Mtu atakabidhiwa kwa watu ambao watamuua; lakini siku ya tatu baada ya kuuawa atafufuka.”
For he taught his disciples, and said to them: The Son of man is delivered into the hands of men, and they will kill him; and when he is killed, on the third day, he will rise.
32 Wanafunzi hawakufahamu jambo hilo. Wakaogopa kumwuliza.
But they did not understand that speech; and they were afraid to ask him.
33 Basi, walifika Kafarnaumu. Na alipokuwa nyumbani, aliwauliza, “Mlikuwa mnajadiliana nini njiani?”
And they came to Capernaum. And when they entered the house, he asked them: What disputed ye among yourselves by the way?
34 Lakini wao wakanyamaza, maana njiani walikuwa wamebishana ni nani aliye mkuu kati yao.
And they were silent; for by the way they had contended with one another, which should be the great among them.
35 Yesu akaketi chini, akawaita wale kumi na wawili, akawaambia, “Yeyote anayetaka kuwa wa kwanza lazima awe wa mwisho na kuwa mtumishi wa wote.”
And Jesus sat down, and called the twelve, and said to them: Whoever would be first, let him be last of all, and servitor to all.
36 Kisha akamchukua mtoto mdogo, akamsimamisha kati yao, akamku mbatia, halafu akawaambia,
And he took a child, and set him in the midst, and took him in his arms and said to them:
37 “Anayempokea mtoto kama huyu kwa jina langu, ananipokea mimi; na anayenipokea mimi, hanipokei mimi tu, bali anampokea yule aliyenituma.”
Whoever receiveth one in my name, like this child, he receiveth me; and he that receiveth me, receiveth not me only, but him that sent me.
38 Yohane akamwambia, “Mwalimu, tumemwona mtu mmoja akitoa pepo kwa kulitumia jina lako, nasi tukajaribu kumkataza kwa kuwa yeye si mmoja wetu.”
John said to him: Rabbi, we saw one casting out demons in thy name, and we forbad him, because he adhereth not to us.
39 Lakini Yesu akasema, “Msimkataze, maana hakuna mtu anayefanya muujiza kwa jina langu, na papo hapo akaweza kusema mabaya juu yangu.
Jesus said to them: Forbid him not; for there is no one who doeth mighty works in my name, that can readily speak evil of me.
40 Maana, asiyepingana nasi, yuko upande wetu.
Whoever therefore is not against you, is for you.
41 Mtu yeyote atakeyewapeni kikombe cha maji ya kunywa kwa sababu ninyi ni watu wake Kristo, hakika hatakosa kupata tuzo lake.
For whoever shall give you to drink a cup of water only, on the ground that ye are Messiah's followers, verily I say to you, he will not lose his reward.
42 “Mtu yeyote atakayemfanya mmoja wa hawa wadogo wanaoniamini atende dhambi, ingekuwa afadhali kwa mtu huyo kufungiwa shingoni mwake jiwe kubwa la kusagia na kutupwa baharini.
And whoever shall cause one of these little ones that believe in me to stumble, it were better for him, if a millstone were put to his neck, and he cast into the sea.
43 Mkono wako ukikukosesha, ukate! Afadhali kuingia kwenye uzima bila mkono mmoja, kuliko kuwa na mikono miwili na kwenda katika moto wa Jehanamu. (Geenna )
And if thy hand make thee offend, cut it off: it is better for thee to enter into life maimed, than, having two hands, to go into hell; (Geenna )
44 Humo, wadudu wake hawafi na moto hauzimiki.
where their worm dieth not, and their fire is not extinguished.
45 Na mguu wako ukikukosesha, ukate! Afadhali kuingia katika uzima bila mguu mmoja, kuliko kuwa na miguu yote miwili na kutupwa katika moto wa Jehanamu. (Geenna )
And if thy foot make thee offend, cut it off: it is better for thee to enter into life lamed, than, having two feet, to fall into hell; (Geenna )
46 Humo, wadudu wake hawafi na moto hauzimiki.
where their worm dieth not, and their fire is not extinguished.
47 Na jicho lako likikukosesha, ling'oe! Afadhali kuingia katika utawala wa Mungu ukiwa na jicho moja tu, kuliko kuwa na macho yako yote mawili na kutupwa katika moto wa Jehanamu. (Geenna )
And if thy eye make thee offend, pluck it out: it is better for thee to enter with one eye into the kingdom of God, than, having two eyes, to fall into the hell of fire; (Geenna )
48 Humo wadudu wake hawafi, na moto hauzimiki.
where their worm dieth not, and their fire is not extinguished.
49 “Maana kila mmoja atakolezwa kwa moto.
For every thing will be salted with fire; and every sacrifice will be salted with salt.
50 Chumvi ni nzuri, lakini ikipoteza ladha yake, itakolezwa na nini? Muwe na chumvi ndani yenu na kudumisha amani kati yenu.”
Salt is a good thing: but if the salt become insipid, with what will it be salted? Let there be salt in you: and be ye in peace, one with another.