< Marko 9 >
1 Yesu akaendelea kuwaambia, “Kweli nawaambieni, wako wengine papa hapa ambao hawatakufa kabla ya kuuona Ufalme wa Mungu ukija kwa enzi.”
He said to them, "Truly I tell you, there are some standing here who will in no way taste death until they see the Kingdom of God come with power."
2 Baada ya siku sita, Yesu aliwachukua Petro, Yakobo na Yohane juu ya mlima mrefu peke yao. Huko, Yesu akageuka sura mbele yao,
After six days Jesus took with him Peter, James, and John, and brought them up onto a high mountain privately by themselves, and he was changed into another form in front of them.
3 mavazi yake yakang'aa, yakawa meupe sana, jinsi dobi yeyote duniani asingeweza kuyafanya meupe.
His clothing became glistening, exceedingly white, such as no launderer on earth can whiten them.
4 Eliya na Mose wakawatokea, wakazungumza na Yesu.
Elijah and Moses appeared to them, and they were talking with Jesus.
5 Petro akamwambia Yesu, “Mwalimu, ni vizuri sana kwamba tuko hapa. Basi, afadhali tujenge vibanda vitatu: kimoja chako, kimoja cha Mose na kimoja cha Eliya.”
Peter said to Jesus, "Rabbi, it is good for us to be here. Let us make three tents: one for you, one for Moses, and one for Elijah."
6 Yeye na wenzake waliogopa hata hakujua la kusema.
For he did not know what to answer, for they became very afraid.
7 Kisha likatokea wingu likawafunika, na sauti ikasikika kutoka katika hilo wingu, “Huyu ni Mwanangu mpendwa, msikilizeni.”
A cloud came, overshadowing them, and a voice came out of the cloud, "This is my beloved Son. Listen to him."
8 Mara wanafunzi hao wakatazama tena, lakini hawakumwona mtu mwingine, ila Yesu peke yake pamoja nao.
Suddenly looking around, they saw no one with them anymore, except Jesus alone.
9 Walipokuwa wakishuka mlimani, Yesu aliwakataza wasimwambie mtu yeyote mambo waliyoyaona, mpaka Mwana wa Mtu atakapokuwa amefufuka kutoka wafu.
As they were coming down from the mountain, he commanded them that they should tell no one what things they had seen, until after the Son of Man had risen from the dead.
10 Basi, wakashika agizo hilo, lakini wakawa wanajadiliana wao kwa wao maana ya kufufuka kutoka wafu.
They kept this saying to themselves, questioning what the "rising from the dead" meant.
11 Wakamwuliza Yesu, “Mbona walimu wa Sheria wanasema kwamba ni lazima Eliya aje kwanza?”
They asked him, saying, "Why do the scribes say that Elijah must come first?"
12 Naye akawajibu, “Naam, Eliya anakuja kwanza kutayarisha yote. Hata hivyo, kwa nini basi imeandikwa katika Maandiko Matakatifu kwamba Mwana wa Mtu atapatwa na mateso mengi na kudharauliwa?
And he said to them, "Elijah indeed comes first, and restores all things. And why is it written of the Son of Man that he should suffer many things and be rejected?
13 Lakini nawaambieni, Eliya amekwisha kuja, nao wakamtendea walivyotaka kama ilivyoandikwa juu yake.”
But I tell you that Elijah has come, and they have also done to him whatever they wanted to, even as it is written about him."
14 Walipowafikia wale wanafunzi wengine, waliona umati mkubwa wa watu hapo. Na baadhi ya walimu wa Sheria walikuwa wanajadiliana nao.
And when they came to the disciples, they saw a large crowd around them, and scribes questioning them.
15 Mara tu ule umati wa watu ulipomwona, wote walishangaa sana, wakamkimbilia wamsalimu.
Immediately all the crowd, when they saw him, were greatly amazed, and running to him greeted him.
16 Yesu akawauliza, “Mnajadiliana nini nao?”
He asked them, "What are you arguing about with them?"
17 Hapo mtu mmoja katika ule umati wa watu akamjibu, “Mwalimu, nimemleta mwanangu kwako, ana pepo aliyemfanya kuwa bubu.
And one out of the crowd answered him, "Teacher, I brought to you my son, who has a mute spirit;
18 Kila mara anapomvamia, humwangusha chini na kumfanya atokwe na povu kinywani, akisaga meno na kuwa mkavu mwili wote. Niliwaomba wanafunzi wako wamtoe huyo pepo lakini hawakuweza.”
and wherever it seizes him, it throws him down, and he foams at the mouth, and grinds his teeth, and wastes away. I asked your disciples to cast it out, and they weren't able."
19 Yesu akawaambia, “Enyi kizazi kisicho na imani! Nitakaa nanyi mpaka lini? Nitawavumilia mpaka lini? Mleteni kwangu.”
And answering, he said to them, "You unbelieving generation, how long must I be with you? How long must I put up with you? Bring him to me."
20 Wakampeleka. Mara tu huyo pepo alipomwona Yesu, alimtia mtoto kifafa, naye mtoto akaanguka chini, akagaagaa na kutoka povu kinywani. Yesu akamwuliza baba yake huyo mtoto,
They brought him to him, and when he saw him, immediately the spirit convulsed him, and he fell on the ground, wallowing and foaming at the mouth.
21 “Amepatwa na mambo hayo tangu lini?” Naye akamjibu, “Tangu utoto wake.
He asked his father, "How long has it been since this has come to him?" He said, "From childhood.
22 Na mara nyingi pepo huyo amemwangusha motoni na majini, ili amwangamize kabisa. Basi, ikiwa waweza, utuhurumie na kutusaidia!”
And it has often cast him both into fire and into water, to destroy him. But if you can do anything, have compassion on us, and help us."
23 Yesu akamwambia, “Eti ikiwa waweza! Mambo yote yanawezekana kwa mtu aliye na imani.”
Jesus said to him, "'If you can?' All things are possible to him who believes."
24 Hapo, huyo baba akalia kwa sauti, “Naamini! Lakini imani yangu haitoshi, nisaidie!”
Immediately the father of the child cried out and said, "I believe. Help my unbelief."
25 Yesu alipouona umati wa watu unaongezeka upesi mbele yake, alimkemea yule pepo mchafu, “Pepo unayemfanya huyu mtoto kuwa bubu-kiziwi, nakuamuru, mtoke mtoto huyu wala usimwingie tena!”
When Jesus saw that a crowd came running together, he rebuked the unclean spirit, saying to him, "You deaf and mute spirit, I command you, come out of him, and never enter him again."
26 Hapo huyo pepo alipaaza sauti, akamwangusha huyo mtoto chini, kisha akamtoka. Mtoto alionekana kama maiti, hata wengine walisema, “Amekufa!”
Having screamed, and convulsed greatly, it came out of him. The boy became like one dead; so much that most of them said, "He is dead."
27 Lakini Yesu akamshika mkono, akamwinua, naye akasimama.
But Jesus took him by the hand, and raised him up; and he arose.
28 Yesu alipoingia nyumbani, wanafunzi wake walimwuliza kwa faragha, “Kwa nini sisi hatukuweza kumtoa?”
And when he had come into the house, his disciples asked him privately, "Why could we not cast it out?"
29 Naye akawaambia, “Pepo wa aina hii hawezi kutoka isipokuwa kwa sala tu.”
And he said to them, "This kind cannot come out by anything but prayer and fasting."
30 Yesu na wanafunzi wake waliondoka hapo, wakaendelea na safari kupitia wilaya ya Galilaya. Yesu hakupenda watu wajue alipokuwa,
They went out from there, and passed through Galilee. He did not want anyone to know it.
31 kwa sababu alikuwa anawafundisha wanafunzi wake. Aliwaambia, “Mwana wa Mtu atakabidhiwa kwa watu ambao watamuua; lakini siku ya tatu baada ya kuuawa atafufuka.”
For he was teaching his disciples, and said to them, "The Son of Man is being handed over to the hands of men, and they will kill him; and when he is killed, after three days he will rise again."
32 Wanafunzi hawakufahamu jambo hilo. Wakaogopa kumwuliza.
But they did not understand the saying, and were afraid to ask him.
33 Basi, walifika Kafarnaumu. Na alipokuwa nyumbani, aliwauliza, “Mlikuwa mnajadiliana nini njiani?”
He came to Capernaum, and when he was in the house he asked them, "What were you arguing on the way?"
34 Lakini wao wakanyamaza, maana njiani walikuwa wamebishana ni nani aliye mkuu kati yao.
But they were silent, for they had disputed one with another on the way about who was the greatest.
35 Yesu akaketi chini, akawaita wale kumi na wawili, akawaambia, “Yeyote anayetaka kuwa wa kwanza lazima awe wa mwisho na kuwa mtumishi wa wote.”
And he sat down, and called the twelve; and he said to them, "If anyone wants to be first, he must be last of all, and servant of all."
36 Kisha akamchukua mtoto mdogo, akamsimamisha kati yao, akamku mbatia, halafu akawaambia,
He took a little child, and set him in the midst of them. Taking him in his arms, he said to them,
37 “Anayempokea mtoto kama huyu kwa jina langu, ananipokea mimi; na anayenipokea mimi, hanipokei mimi tu, bali anampokea yule aliyenituma.”
"Whoever receives one such little child in my name, receives me, and whoever receives me, does not receive me, but him who sent me."
38 Yohane akamwambia, “Mwalimu, tumemwona mtu mmoja akitoa pepo kwa kulitumia jina lako, nasi tukajaribu kumkataza kwa kuwa yeye si mmoja wetu.”
John said to him, "Teacher, we saw someone casting out demons in your name; and we forbade him, because he was not following us."
39 Lakini Yesu akasema, “Msimkataze, maana hakuna mtu anayefanya muujiza kwa jina langu, na papo hapo akaweza kusema mabaya juu yangu.
But Jesus said, "Do not forbid him, for there is no one who will do a mighty work in my name, and be able quickly to speak evil of me.
40 Maana, asiyepingana nasi, yuko upande wetu.
For whoever is not against us is for us.
41 Mtu yeyote atakeyewapeni kikombe cha maji ya kunywa kwa sababu ninyi ni watu wake Kristo, hakika hatakosa kupata tuzo lake.
For whoever will give you a cup of water to drink in my name, because you belong to the Christ, truly I tell you, he will in no way lose his reward.
42 “Mtu yeyote atakayemfanya mmoja wa hawa wadogo wanaoniamini atende dhambi, ingekuwa afadhali kwa mtu huyo kufungiwa shingoni mwake jiwe kubwa la kusagia na kutupwa baharini.
Whoever will cause one of these little ones who believe in me to stumble, it would be better for him if he was thrown into the sea with a millstone hung around his neck.
43 Mkono wako ukikukosesha, ukate! Afadhali kuingia kwenye uzima bila mkono mmoja, kuliko kuwa na mikono miwili na kwenda katika moto wa Jehanamu. (Geenna )
If your hand causes you to stumble, cut it off. It is better for you to enter into life maimed, rather than having your two hands to go into hell, into the unquenchable fire, (Geenna )
44 Humo, wadudu wake hawafi na moto hauzimiki.
45 Na mguu wako ukikukosesha, ukate! Afadhali kuingia katika uzima bila mguu mmoja, kuliko kuwa na miguu yote miwili na kutupwa katika moto wa Jehanamu. (Geenna )
If your foot causes you to stumble, cut it off. It is better for you to enter into life lame, rather than having your two feet to be cast into hell. (Geenna )
46 Humo, wadudu wake hawafi na moto hauzimiki.
47 Na jicho lako likikukosesha, ling'oe! Afadhali kuingia katika utawala wa Mungu ukiwa na jicho moja tu, kuliko kuwa na macho yako yote mawili na kutupwa katika moto wa Jehanamu. (Geenna )
If your eye causes you to stumble, cast it out. It is better for you to enter into the Kingdom of God with one eye, rather than having two eyes to be cast into hell, (Geenna )
48 Humo wadudu wake hawafi, na moto hauzimiki.
'where their worm does not die, and the fire is not quenched.'
49 “Maana kila mmoja atakolezwa kwa moto.
For everyone will be salted with fire, and every sacrifice will be salted with salt.
50 Chumvi ni nzuri, lakini ikipoteza ladha yake, itakolezwa na nini? Muwe na chumvi ndani yenu na kudumisha amani kati yenu.”
Salt is good, but if the salt has lost its saltiness, how can you make it salty? Have salt in yourselves, and be at peace with one another."