< Marko 5 >
1 Basi, wakafika katika nchi ya Wagerase, ng'ambo ya ziwa.
atha tuu sindhupaara. m gatvaa gideriiyaprade"sa upatasthu. h|
2 Mara tu Yesu aliposhuka mashuani, mtu mmoja aliyepagawa na pepo mchafu alitoka makaburini, akakutana naye.
naukaato nirgatamaatraad apavitrabhuutagrasta eka. h "sma"saanaadetya ta. m saak. saac cakaara|
3 Mtu huyo alikuwa akiishi makaburini wala hakuna mtu aliyeweza tena kumfunga kwa minyororo.
sa "sma"saane. avaatsiit kopi ta. m "s. r"nkhalena badvvaa sthaapayitu. m naa"saknot|
4 Mara nyingi walimfunga kwa pingu na minyororo lakini kila mara aliweza kuikata hiyo minyororo na kuzivunja hizo pingu, wala hakuna mtu aliyeweza kumzuia.
janairvaara. m niga. dai. h "s. r"nkhalai"sca sa baddhopi "s. r"nkhalaanyaak. r.sya mocitavaan niga. daani ca bha. mktvaa kha. n.da. m kha. n.da. m k. rtavaan kopi ta. m va"siikarttu. m na "sa"saka|
5 Mchana na usiku alikaa makaburini na milimani akipaaza sauti na kujikatakata kwa mawe.
divaani"sa. m sadaa parvvata. m "sma"saana nca bhramitvaa ciit"sabda. m k. rtavaan graavabhi"sca svaya. m sva. m k. rtavaan|
6 Alipomwona Yesu kwa mbali, alimkimbilia, akamwinamia
sa yii"su. m duuraat pa"syanneva dhaavan ta. m pra. nanaama ucairuva. m"scovaaca,
7 akisema kwa sauti kubwa, “Una shauri gani nami, wewe Yesu Mwana wa Mungu aliye juu? Kwa jina la Mungu, nakusihi usinitese!”
he sarvvoparisthe"svaraputra yii"so bhavataa saha me ka. h sambandha. h? aha. m tvaamii"svare. na "saapaye maa. m maa yaataya|
8 (Alisema hivyo kwa kuwa Yesu alikuwa amemwambia, “Pepo mchafu, mtoke mtu huyu.”)
yato yii"susta. m kathitavaan re apavitrabhuuta, asmaannaraad bahirnirgaccha|
9 Basi, Yesu akamwuliza, “Jina lako nani?” Naye akajibu, “Jina langu ni Jeshi, maana sisi tu wengi.”
atha sa ta. m p. r.s. tavaan kinte naama? tena pratyukta. m vayamaneke. asmastato. asmannaama baahinii|
10 Kisha akamsihi Yesu asiwafukuze hao pepo katika nchi ile.
tatosmaan de"saanna pre. sayeti te ta. m praarthayanta|
11 Kulikuwa na kundi kubwa la nguruwe malishoni kwenye mteremko wa mlima.
tadaanii. m parvvata. m nika. saa b. rhan varaahavraja"scarannaasiit|
12 Basi, hao pepo wakamsihi, “Utupeleke kwa hao nguruwe, tuwaingie.”
tasmaad bhuutaa vinayena jagadu. h, amu. m varaahavrajam aa"srayitum asmaan prahi. nu|
13 Naye akawaruhusu. Basi, hao pepo wachafu wakatoka, wakawaingia wale nguruwe. Kundi lote la nguruwe wapatao elfu mbili likaporomoka kwenye ule mteremko mkali mpaka ziwani, likatumbukia majini.
yii"sunaanuj naataaste. apavitrabhuutaa bahirniryaaya varaahavraja. m praavi"san tata. h sarvve varaahaa vastutastu praayodvisahasrasa. m"nkhyakaa. h ka. takena mahaajavaad dhaavanta. h sindhau praa. naan jahu. h|
14 Wachungaji wa hao nguruwe walikimbia, wakatangaza jambo hilo mjini na mashambani. Watu wakafika kuona yaliyotukia.
tasmaad varaahapaalakaa. h palaayamaanaa. h pure graame ca tadvaartta. m kathayaa ncakru. h| tadaa lokaa gha. tita. m tatkaaryya. m dra. s.tu. m bahirjagmu. h
15 Wakamwendea Yesu, wakamwona na mtu yuleyule aliyekuwa amepagawa na jeshi la pepo ameketi chini, amevaa nguo na ana akili yake sawa, wakaogopa.
yii"so. h sannidhi. m gatvaa ta. m bhuutagrastam arthaad baahiniibhuutagrasta. m nara. m savastra. m sacetana. m samupavi. s.ta nca d. r.s. tvaa bibhyu. h|
16 Watu walishuhudia tukio hilo wakaeleza wengine mambo yaliyompata huyo mtu aliyekuwa amepagawa na pepo na juu ya wale nguruwe.
tato d. r.s. tatatkaaryyalokaastasya bhuutagrastanarasya varaahavrajasyaapi taa. m dha. tanaa. m var. nayaamaasu. h|
17 Basi, wakaanza kumwomba aondoke katika nchi yao.
tataste svasiimaato bahirgantu. m yii"su. m vinetumaarebhire|
18 Yesu alipokuwa anapanda mashuani, yule mtu aliyekuwa amepagawa na pepo akamwomba amruhusu kwenda naye.
atha tasya naukaaroha. nakaale sa bhuutamukto naa yii"sunaa saha sthaatu. m praarthayate;
19 Lakini Yesu akamkatalia. Badala yake akamwambia, “Nenda nyumbani kwa jamaa yako, ukawaambie mambo yote Bwana aliyokutendea na jinsi alivyokuonea huruma.”
kintu sa tamananumatya kathitavaan tva. m nijaatmiiyaanaa. m samiipa. m g. rha nca gaccha prabhustvayi k. rpaa. m k. rtvaa yaani karmmaa. ni k. rtavaan taani taan j naapaya|
20 Basi, huyo mtu akaenda, akaanza kutangaza huko Dekapoli mambo yote Yesu aliyomtendea; watu wote wakashangaa.
ata. h sa prasthaaya yii"sunaa k. rta. m tatsarvvaa"scaryya. m karmma dikaapalide"se pracaarayitu. m praarabdhavaan tata. h sarvve lokaa aa"scaryya. m menire|
21 Yesu alivukia tena upande wa pili wa ziwa kwa mashua. Umati mkubwa wa watu ukakusanyika mbele yake, naye akawa amesimama kando ya ziwa.
anantara. m yii"sau naavaa punaranyapaara uttiir. ne sindhuta. te ca ti. s.thati sati tatsamiipe bahulokaanaa. m samaagamo. abhuut|
22 Hapo akaja mmojawapo wa maofisa wa sunagogi, jina lake Yairo. Alipomwona Yesu, akajitupa mbele ya miguu yake,
apara. m yaayiir naamnaa ka"scid bhajanag. rhasyaadhipa aagatya ta. m d. r.s. tvaiva cara. nayo. h patitvaa bahu nivedya kathitavaan;
23 akamsihi akisema, “Binti yangu mdogo ni mgonjwa karibu kufa. Twende tafadhali, ukamwekee mikono yako, apate kupona na kuishi.”
mama kanyaa m. rtapraayaabhuud ato bhavaanetya tadaarogyaaya tasyaa gaatre hastam arpayatu tenaiva saa jiivi. syati|
24 Basi, Yesu akaondoka pamoja naye. Watu wengi sana wakamfuata, wakawa wanamsonga kila upande.
tadaa yii"sustena saha calita. h kintu tatpa"scaad bahulokaa"scalitvaa taadgaatre patitaa. h|
25 Mmojawapo alikuwa mwanamke mwenye ugonjwa wa kutokwa damu kwa muda wa miaka kumi na miwili.
atha dvaada"savar. saa. ni pradararoge. na
26 Mwanamke huyo alikuwa amekwisha sumbuka sana kuwaendea waganga wengi. Na ingawa alikuwa amekwisha tumia mali yake yote, hakupata nafuu bali hali yake ilizidi kuwa mbaya.
"siir. naa cikitsakaanaa. m naanaacikitsaabhi"sca du. hkha. m bhuktavatii ca sarvvasva. m vyayitvaapi naarogya. m praaptaa ca punarapi pii. ditaasiicca
27 Alikuwa amesikia habari za Yesu, na hivyo akaupenya msongamano wa watu kutoka nyuma, akagusa vazi lake.
yaa strii saa yii"so rvaarttaa. m praapya manasaakathayat yadyaha. m tasya vastramaatra spra. s.tu. m labheya. m tadaa rogahiinaa bhavi. syaami|
28 Alifanya hivyo, maana alijisemea, “Nikigusa tu vazi lake, nitapona.”
atoheto. h saa lokaara. nyamadhye tatpa"scaadaagatya tasya vastra. m paspar"sa|
29 Mara chemchemi ya damu yake ikakauka, akajisikia mwilini mwake kwamba ameponywa ugonjwa wake.
tenaiva tatk. sa. na. m tasyaa raktasrota. h "su. ska. m svaya. m tasmaad rogaanmuktaa ityapi dehe. anubhuutaa|
30 Yesu alitambua mara kwamba nguvu imemtoka. Basi akaugeukia ule umati wa watu, akauliza, “Nani aliyegusa mavazi yangu?”
atha svasmaat "sakti rnirgataa yii"suretanmanasaa j naatvaa lokanivaha. m prati mukha. m vyaav. rtya p. r.s. tavaan kena madvastra. m sp. r.s. ta. m?
31 Wanafunzi wake wakamjibu, “Unaona jinsi watu wanavyokusonga; mbona wauliza nani aliyekugusa?”
tatastasya "si. syaa uucu. h bhavato vapu. si lokaa. h sa. mghar. santi tad d. r.s. tvaa kena madvastra. m sp. r.s. tamiti kuta. h kathayati?
32 Lakini Yesu akaendelea kutazama amwone huyo aliyefanya hivyo.
kintu kena tat karmma k. rta. m tad dra. s.tu. m yii"su"scaturdi"so d. r.s. tavaan|
33 Hapo huyo mwanamke, akifahamu yaliyompata, akajitokeza akitetemeka kwa hofu, akajitupa chini mbele ya Yesu na kusema ukweli wote.
tata. h saa strii bhiitaa kampitaa ca satii svasyaa rukpratikriyaa jaateti j naatvaagatya tatsammukhe patitvaa sarvvav. rttaanta. m satya. m tasmai kathayaamaasa|
34 Yesu akamwambia, “Binti, imani yako imekuponya. Nenda kwa amani, upone kabisa ugonjwa wako.”
tadaanii. m yii"sustaa. m gaditavaan, he kanye tava pratiitistvaam arogaamakarot tva. m k. seme. na vraja svarogaanmuktaa ca ti. s.tha|
35 Yesu alipokuwa bado anaongea, watu walifika kutoka nyumbani kwa yule ofisa wa sunagogi, wakamwambia, “Binti yako amekwisha kufa. Ya nini kuendelea kumsumbua Mwalimu?”
itivaakyavadanakaale bhajanag. rhaadhipasya nive"sanaal lokaa etyaadhipa. m babhaa. sire tava kanyaa m. rtaa tasmaad guru. m puna. h kuta. h kli"snaasi?
36 Lakini, bila kujali walichosema, Yesu akamwambia mkuu wa sunagogi, “Usiogope, amini tu.”
kintu yii"sustad vaakya. m "srutvaiva bhajanag. rhaadhipa. m gaditavaan maa bhai. sii. h kevala. m vi"svaasihi|
37 Wala hakumruhusu mtu yeyote kufuatana naye ila Petro, Yakobo na Yohane nduguye Yakobo.
atha pitaro yaakuub tadbhraataa yohan ca etaan vinaa kamapi svapa"scaad yaatu. m naanvamanyata|
38 Wakafika nyumbani kwa ofisa wa sunagogi naye Yesu akasikia makelele, kilio na maombolezo mengi.
tasya bhajanag. rhaadhipasya nive"sanasamiipam aagatya kalaha. m bahurodana. m vilaapa nca kurvvato lokaan dadar"sa|
39 Akaingia ndani, akawaambia, “Mbona mnapiga kelele na kulia? Msichana hakufa, amelala tu.”
tasmaan nive"sana. m pravi"sya proktavaan yuuya. m kuta ittha. m kalaha. m rodana nca kurutha? kanyaa na m. rtaa nidraati|
40 Lakini wao wakamcheka. Basi, akawaondoa wote nje, akawachukua baba na mama ya huyo msichana na wale wanafunzi wake, wakaingia chumbani alimokuwa huyo msichana.
tasmaatte tamupajahasu. h kintu yii"su. h sarvvaana bahi. sk. rtya kanyaayaa. h pitarau svasa"ngina"sca g. rhiitvaa yatra kanyaasiit tat sthaana. m pravi. s.tavaan|
41 Kisha akamshika mkono, akamwambia, “Talitha, kumi,” maana yake, “Msichana, nakwambia, amka!”
atha sa tasyaa. h kanyaayaa hastau dh. rtvaa taa. m babhaa. se. taaliithaa kuumii, arthato he kanye tvamutti. s.tha ityaaj naapayaami|
42 Mara msichana akasimama, akaanza kutembea. (Alikuwa na umri wa miaka kumi na miwili.) Hapo watu wakashangaa kupita kiasi.
tunaiva tatk. sa. na. m saa dvaada"savar. savayaskaa kanyaa potthaaya calitumaarebhe, ita. h sarvve mahaavismaya. m gataa. h|
43 Yesu akawakataza sana wasimjulishe mtu jambo hilo. Kisha akawaambia wampe huyo msichana chakula.
tata etasyai ki ncit khaadya. m datteti kathayitvaa etatkarmma kamapi na j naapayateti d. r.dhamaadi. s.tavaan|