< Marko 5 >
1 Basi, wakafika katika nchi ya Wagerase, ng'ambo ya ziwa.
And they came beyond the sea, into the country of the Gadarenes,
2 Mara tu Yesu aliposhuka mashuani, mtu mmoja aliyepagawa na pepo mchafu alitoka makaburini, akakutana naye.
And a man from the tombs, with an unclean spirit met Him, having come out of the ship;
3 Mtu huyo alikuwa akiishi makaburini wala hakuna mtu aliyeweza tena kumfunga kwa minyororo.
who had his dwelling among the tombs: neither was any one able to bind him with chains;
4 Mara nyingi walimfunga kwa pingu na minyororo lakini kila mara aliweza kuikata hiyo minyororo na kuzivunja hizo pingu, wala hakuna mtu aliyeweza kumzuia.
because frequently he had been bound with fetters and chains, and the chains were slipped off by him, and the fetters torn to pieces.
5 Mchana na usiku alikaa makaburini na milimani akipaaza sauti na kujikatakata kwa mawe.
No one was able to tame him: and all the time, night and day, he was among the tombs in the mountains, crying, and cutting himself with stones.
6 Alipomwona Yesu kwa mbali, alimkimbilia, akamwinamia
And seeing Jesus a great way off, he ran to Him, and worshiped Him;
7 akisema kwa sauti kubwa, “Una shauri gani nami, wewe Yesu Mwana wa Mungu aliye juu? Kwa jina la Mungu, nakusihi usinitese!”
and crying with a loud voice, he says, What is there to me and to thee, O Jesus, thou Son of the Most High God? I adjure thee in the name of God, that you may not torment me.
8 (Alisema hivyo kwa kuwa Yesu alikuwa amemwambia, “Pepo mchafu, mtoke mtu huyu.”)
For He said to him, Unclean spirit, come out from the man.
9 Basi, Yesu akamwuliza, “Jina lako nani?” Naye akajibu, “Jina langu ni Jeshi, maana sisi tu wengi.”
And He asked him, What is thy name? And he says to Him, My name is Legion; because we are many.
10 Kisha akamsihi Yesu asiwafukuze hao pepo katika nchi ile.
And he continued to intreat Him much, that He would not send them out of the country.
11 Kulikuwa na kundi kubwa la nguruwe malishoni kwenye mteremko wa mlima.
And there was a great herd of swine feeding in the mountain.
12 Basi, hao pepo wakamsihi, “Utupeleke kwa hao nguruwe, tuwaingie.”
And they intreated Him, saying, Send us into the swine, in order that we may go into them.
13 Naye akawaruhusu. Basi, hao pepo wachafu wakatoka, wakawaingia wale nguruwe. Kundi lote la nguruwe wapatao elfu mbili likaporomoka kwenye ule mteremko mkali mpaka ziwani, likatumbukia majini.
And Jesus immediately permitted them. And the unclean spirits having gone out, came into the swine: and the herd rushed down a precipice into the sea, and there were about two thousand: and they were strangled in the sea.
14 Wachungaji wa hao nguruwe walikimbia, wakatangaza jambo hilo mjini na mashambani. Watu wakafika kuona yaliyotukia.
And those herding them fled, and reported in the city, and in the country. And they came out to see what it was that came to pass.
15 Wakamwendea Yesu, wakamwona na mtu yuleyule aliyekuwa amepagawa na jeshi la pepo ameketi chini, amevaa nguo na ana akili yake sawa, wakaogopa.
And they come to Jesus, and see the demonized man sitting down, both clothed and in his right mind, the one called Legion; and they were afraid.
16 Watu walishuhudia tukio hilo wakaeleza wengine mambo yaliyompata huyo mtu aliyekuwa amepagawa na pepo na juu ya wale nguruwe.
And those seeing, related to them how it happened to the demonized man and concerning the swine.
17 Basi, wakaanza kumwomba aondoke katika nchi yao.
And they began to intreat Him to depart from their coasts.
18 Yesu alipokuwa anapanda mashuani, yule mtu aliyekuwa amepagawa na pepo akamwomba amruhusu kwenda naye.
And He having come to the ship, the demonized man intreated Him that he should be with Him.
19 Lakini Yesu akamkatalia. Badala yake akamwambia, “Nenda nyumbani kwa jamaa yako, ukawaambie mambo yote Bwana aliyokutendea na jinsi alivyokuonea huruma.”
And He did not permit him, but says to him, Go to thine own house to thy people, and proclaim to them how many things the Lord has done for thee, and had mercy on thee.
20 Basi, huyo mtu akaenda, akaanza kutangaza huko Dekapoli mambo yote Yesu aliyomtendea; watu wote wakashangaa.
And he went away, and began to preach in Decapolis, how many things Jesus did to him. And all were astonished.
21 Yesu alivukia tena upande wa pili wa ziwa kwa mashua. Umati mkubwa wa watu ukakusanyika mbele yake, naye akawa amesimama kando ya ziwa.
And Jesus crossing over in the ship again to the other side, a great multitude was gathered unto Him; and He was by the sea.
22 Hapo akaja mmojawapo wa maofisa wa sunagogi, jina lake Yairo. Alipomwona Yesu, akajitupa mbele ya miguu yake,
And one of the chief rulers of the synagogue, by name jairus, comes; and seeing Him falls at His feet,
23 akamsihi akisema, “Binti yangu mdogo ni mgonjwa karibu kufa. Twende tafadhali, ukamwekee mikono yako, apate kupona na kuishi.”
and intreats Him much saying, My little daughter is at the point of death: that coming He may lay hands on her, in order that she may be saved and live.
24 Basi, Yesu akaondoka pamoja naye. Watu wengi sana wakamfuata, wakawa wanamsonga kila upande.
And He departed with him; and a great multitude followed Him, even treading on Him.
25 Mmojawapo alikuwa mwanamke mwenye ugonjwa wa kutokwa damu kwa muda wa miaka kumi na miwili.
And a certain woman, being in an issue of blood twelve years,
26 Mwanamke huyo alikuwa amekwisha sumbuka sana kuwaendea waganga wengi. Na ingawa alikuwa amekwisha tumia mali yake yote, hakupata nafuu bali hali yake ilizidi kuwa mbaya.
and having suffered much from many physicians, and expended all things which were with her, and being profited as to nothing, but rather having come to the worse,
27 Alikuwa amesikia habari za Yesu, na hivyo akaupenya msongamano wa watu kutoka nyuma, akagusa vazi lake.
hearing concerning Jesus, having come in the crowd behind, touched His garment.
28 Alifanya hivyo, maana alijisemea, “Nikigusa tu vazi lake, nitapona.”
For she was saying, If I may touch His garment, I shall be saved.
29 Mara chemchemi ya damu yake ikakauka, akajisikia mwilini mwake kwamba ameponywa ugonjwa wake.
And immediately the issue of her blood was dried up: and she knew in her body that she is healed of her plague.
30 Yesu alitambua mara kwamba nguvu imemtoka. Basi akaugeukia ule umati wa watu, akauliza, “Nani aliyegusa mavazi yangu?”
And immediately Jesus, knowing in Himself that the powerhas gone out from Him, turning in the crowd, said, Who touched my garments?
31 Wanafunzi wake wakamjibu, “Unaona jinsi watu wanavyokusonga; mbona wauliza nani aliyekugusa?”
And His disciples continued to say to Him, You see the crowd treading upon you, and you say, Who touched me?
32 Lakini Yesu akaendelea kutazama amwone huyo aliyefanya hivyo.
And He looked round to see her who did it.
33 Hapo huyo mwanamke, akifahamu yaliyompata, akajitokeza akitetemeka kwa hofu, akajitupa chini mbele ya Yesu na kusema ukweli wote.
And the woman fearing and trembling, knowing what has taken place unto herself, came and fell down before Him, and told Him the whole truth.
34 Yesu akamwambia, “Binti, imani yako imekuponya. Nenda kwa amani, upone kabisa ugonjwa wako.”
And He said unto her, Daughter, thy faith hath saved thee; go in peace, and be whole of thy plague.
35 Yesu alipokuwa bado anaongea, watu walifika kutoka nyumbani kwa yule ofisa wa sunagogi, wakamwambia, “Binti yako amekwisha kufa. Ya nini kuendelea kumsumbua Mwalimu?”
And He still speaking, they come from the house of the chief ruler of the synagogue, saying, Thy daughter is dead: why do you still trouble the Teacher?
36 Lakini, bila kujali walichosema, Yesu akamwambia mkuu wa sunagogi, “Usiogope, amini tu.”
And Jesus, immediately hearing the word spoken, says to the chief ruler, Fear not, only believe.
37 Wala hakumruhusu mtu yeyote kufuatana naye ila Petro, Yakobo na Yohane nduguye Yakobo.
and He did not permit any one to accompany Him, except Peter, and James, and John the brother of James.
38 Wakafika nyumbani kwa ofisa wa sunagogi naye Yesu akasikia makelele, kilio na maombolezo mengi.
And He comes into the house of the chief ruler of the synagogue; And He sees a tumult, weeping and wailing much;
39 Akaingia ndani, akawaambia, “Mbona mnapiga kelele na kulia? Msichana hakufa, amelala tu.”
and having come in, He says to them, Why are you excited and weeping? The child is not dead, but sleepeth.
40 Lakini wao wakamcheka. Basi, akawaondoa wote nje, akawachukua baba na mama ya huyo msichana na wale wanafunzi wake, wakaingia chumbani alimokuwa huyo msichana.
And they hooted at Him. And putting them all out, He takes the father and mother of the child and those with Him, and goes in where the child was.
41 Kisha akamshika mkono, akamwambia, “Talitha, kumi,” maana yake, “Msichana, nakwambia, amka!”
And taking the child by the hand, says to her, Talitha cumi; which is interpreted, Damsel, I say unto thee, Arise.
42 Mara msichana akasimama, akaanza kutembea. (Alikuwa na umri wa miaka kumi na miwili.) Hapo watu wakashangaa kupita kiasi.
And immediately the damsel stood up, and walked about; for she was twelve years old. And they were immediately delighted with great delight.
43 Yesu akawakataza sana wasimjulishe mtu jambo hilo. Kisha akawaambia wampe huyo msichana chakula.
And He charged them much that no one should know it; and He said that something should be given to her to eat.