< Marko 5 >

1 Basi, wakafika katika nchi ya Wagerase, ng'ambo ya ziwa.
And they came to the opposite side of the sea, into the country of the Gadarenes.
2 Mara tu Yesu aliposhuka mashuani, mtu mmoja aliyepagawa na pepo mchafu alitoka makaburini, akakutana naye.
And when he had come out of the ship, immediately there met him from the tombs a man with an unclean spirit,
3 Mtu huyo alikuwa akiishi makaburini wala hakuna mtu aliyeweza tena kumfunga kwa minyororo.
who had his dwelling among the tombs; and no one could keep him bound even with chains;
4 Mara nyingi walimfunga kwa pingu na minyororo lakini kila mara aliweza kuikata hiyo minyororo na kuzivunja hizo pingu, wala hakuna mtu aliyeweza kumzuia.
because he had often been bound with fetters and chains, and the chains had been pulled to pieces by him, and the fetters had been broken, and no one had strength to subdue him;
5 Mchana na usiku alikaa makaburini na milimani akipaaza sauti na kujikatakata kwa mawe.
and always, night and day, he was in the tombs, and in the mountains, crying out, and cutting himself with stones.
6 Alipomwona Yesu kwa mbali, alimkimbilia, akamwinamia
And when he saw Jesus at a distance, he ran and did him homage;
7 akisema kwa sauti kubwa, “Una shauri gani nami, wewe Yesu Mwana wa Mungu aliye juu? Kwa jina la Mungu, nakusihi usinitese!”
and crying out with a loud voice, he said: What have I to do with thee, Jesus, Son of God Most High? I adjure thee by God, that thou torment me not.
8 (Alisema hivyo kwa kuwa Yesu alikuwa amemwambia, “Pepo mchafu, mtoke mtu huyu.”)
For he had said to him: Unclean spirit, come out of the man.
9 Basi, Yesu akamwuliza, “Jina lako nani?” Naye akajibu, “Jina langu ni Jeshi, maana sisi tu wengi.”
And he asked him: What is your name? And he said to him: My name is Legion; for we are many.
10 Kisha akamsihi Yesu asiwafukuze hao pepo katika nchi ile.
And he earnestly besought him that he would not send them out of the country.
11 Kulikuwa na kundi kubwa la nguruwe malishoni kwenye mteremko wa mlima.
Now a great herd of swine was feeding there near the mountain.
12 Basi, hao pepo wakamsihi, “Utupeleke kwa hao nguruwe, tuwaingie.”
And the demons besought him, saying: Send us to the swine, that we may enter into them.
13 Naye akawaruhusu. Basi, hao pepo wachafu wakatoka, wakawaingia wale nguruwe. Kundi lote la nguruwe wapatao elfu mbili likaporomoka kwenye ule mteremko mkali mpaka ziwani, likatumbukia majini.
And Jesus immediately gave them leave. And the unclean spirits came out and entered into the swine; and the herd (they were about two thousand, ) rushed down a steep place into the sea, and were strangled in the sea.
14 Wachungaji wa hao nguruwe walikimbia, wakatangaza jambo hilo mjini na mashambani. Watu wakafika kuona yaliyotukia.
And those who fed them fled, and told it in the city, and in the country. And they came out to see what had been done;
15 Wakamwendea Yesu, wakamwona na mtu yuleyule aliyekuwa amepagawa na jeshi la pepo ameketi chini, amevaa nguo na ana akili yake sawa, wakaogopa.
and they came to Jesus and saw the demoniac, who had had the legion, sitting, and clothed, and in his right mind: and they were afraid.
16 Watu walishuhudia tukio hilo wakaeleza wengine mambo yaliyompata huyo mtu aliyekuwa amepagawa na pepo na juu ya wale nguruwe.
And those who had seen it told them how it had happened to the demoniac, and also concerning the swine.
17 Basi, wakaanza kumwomba aondoke katika nchi yao.
And they began to beseech him to depart from their borders.
18 Yesu alipokuwa anapanda mashuani, yule mtu aliyekuwa amepagawa na pepo akamwomba amruhusu kwenda naye.
And when he had entered the ship, he that had been possessed with the demons besought him that he might be with him.
19 Lakini Yesu akamkatalia. Badala yake akamwambia, “Nenda nyumbani kwa jamaa yako, ukawaambie mambo yote Bwana aliyokutendea na jinsi alivyokuonea huruma.”
And he did not permit him, but said to him: Go home to your relatives, and make known to them what things the Lord has done for you, and that he has had compassion on you.
20 Basi, huyo mtu akaenda, akaanza kutangaza huko Dekapoli mambo yote Yesu aliyomtendea; watu wote wakashangaa.
And he went away and began to proclaim in Decapolis what things Jesus had done for him. And all were astonished.
21 Yesu alivukia tena upande wa pili wa ziwa kwa mashua. Umati mkubwa wa watu ukakusanyika mbele yake, naye akawa amesimama kando ya ziwa.
And when Jesus had again gone over in the ship to the opposite side, a great multitude came together to him; and he was near the sea.
22 Hapo akaja mmojawapo wa maofisa wa sunagogi, jina lake Yairo. Alipomwona Yesu, akajitupa mbele ya miguu yake,
And behold, there came one of the rulers of the synagogue, named Jairus; and when he saw him, he fell at his feet,
23 akamsihi akisema, “Binti yangu mdogo ni mgonjwa karibu kufa. Twende tafadhali, ukamwekee mikono yako, apate kupona na kuishi.”
and besought him earnestly, saying: My little daughter is at the point of death; come, lay thy hands on her, that she may be saved, and she will live.
24 Basi, Yesu akaondoka pamoja naye. Watu wengi sana wakamfuata, wakawa wanamsonga kila upande.
And he went with him; and a great multitude followed him, and pressed upon him.
25 Mmojawapo alikuwa mwanamke mwenye ugonjwa wa kutokwa damu kwa muda wa miaka kumi na miwili.
And a certain woman who had had an issue of blood for twelve years,
26 Mwanamke huyo alikuwa amekwisha sumbuka sana kuwaendea waganga wengi. Na ingawa alikuwa amekwisha tumia mali yake yote, hakupata nafuu bali hali yake ilizidi kuwa mbaya.
and had suffered much from many physicians, and had spent all that she had, and was in no way benefited, but rather grew worse,
27 Alikuwa amesikia habari za Yesu, na hivyo akaupenya msongamano wa watu kutoka nyuma, akagusa vazi lake.
when she heard of Jesus, came behind him in the multitude, and touched his mantle;
28 Alifanya hivyo, maana alijisemea, “Nikigusa tu vazi lake, nitapona.”
for she said: If I may even touch his clothes, I shall be saved.
29 Mara chemchemi ya damu yake ikakauka, akajisikia mwilini mwake kwamba ameponywa ugonjwa wake.
And immediately the fountain of her blood dried up, and she knew in her body that she was cured of that plague.
30 Yesu alitambua mara kwamba nguvu imemtoka. Basi akaugeukia ule umati wa watu, akauliza, “Nani aliyegusa mavazi yangu?”
And Jesus, immediately perceiving in himself that power had gone forth from him, turned around in the multitude and said: Who touched my clothes?
31 Wanafunzi wake wakamjibu, “Unaona jinsi watu wanavyokusonga; mbona wauliza nani aliyekugusa?”
And his disciples said to him: Thou seest the multitude pressing upon thee, and dost thou say, Who touched me?
32 Lakini Yesu akaendelea kutazama amwone huyo aliyefanya hivyo.
And he looked around to see her that had done this.
33 Hapo huyo mwanamke, akifahamu yaliyompata, akajitokeza akitetemeka kwa hofu, akajitupa chini mbele ya Yesu na kusema ukweli wote.
But the woman, fearing and trembling, knowing; what had been done within her, came and fell down before him; and told him all the truth.
34 Yesu akamwambia, “Binti, imani yako imekuponya. Nenda kwa amani, upone kabisa ugonjwa wako.”
And he said to her: Daughter, your faith has saved you; go in peace, and be cured of your plague.
35 Yesu alipokuwa bado anaongea, watu walifika kutoka nyumbani kwa yule ofisa wa sunagogi, wakamwambia, “Binti yako amekwisha kufa. Ya nini kuendelea kumsumbua Mwalimu?”
While he was yet speaking, some came from the ruler of the synagogue, who said: Your daughter is dead; why give the Teacher further trouble?
36 Lakini, bila kujali walichosema, Yesu akamwambia mkuu wa sunagogi, “Usiogope, amini tu.”
But as soon as Jesus heard what was spoken, he said to the ruler of the synagogue: Fear not, only believe.
37 Wala hakumruhusu mtu yeyote kufuatana naye ila Petro, Yakobo na Yohane nduguye Yakobo.
And he suffered no one to follow him, except Peter and James and John the brother of James.
38 Wakafika nyumbani kwa ofisa wa sunagogi naye Yesu akasikia makelele, kilio na maombolezo mengi.
And he came to the house of the ruler of the synagogue, and saw the tumult, and those who were weeping and wailing greatly.
39 Akaingia ndani, akawaambia, “Mbona mnapiga kelele na kulia? Msichana hakufa, amelala tu.”
And he went in and said to them: Why do you make a tumult and weep? The child is not dead, but sleeps.
40 Lakini wao wakamcheka. Basi, akawaondoa wote nje, akawachukua baba na mama ya huyo msichana na wale wanafunzi wake, wakaingia chumbani alimokuwa huyo msichana.
And they derided him. But when he had put them all out, he took the father and mother of the child, and those who were with him, and went in where the child was lying.
41 Kisha akamshika mkono, akamwambia, “Talitha, kumi,” maana yake, “Msichana, nakwambia, amka!”
And he took the child by the hand, and said to her: Talitha kumi; which is, when translated, Maiden, (I say to you, ) arise.
42 Mara msichana akasimama, akaanza kutembea. (Alikuwa na umri wa miaka kumi na miwili.) Hapo watu wakashangaa kupita kiasi.
And the maiden immediately arose and walked, for she was twelve years old. And they were greatly astonished.
43 Yesu akawakataza sana wasimjulishe mtu jambo hilo. Kisha akawaambia wampe huyo msichana chakula.
And he charged them strictly that no one should know this. And he commanded that something should be given her to eat.

< Marko 5 >