< Marko 4 >
1 Yesu alianza kufundisha tena akiwa kando ya ziwa. Umati mkubwa wa watu ulimzunguka hata ikambidi aingie katika mashua na kuketi. Watu wakawa wamekaa katika nchi kavu, kando ya ziwa.
In zopet začne učiti ob morji. In zbere se pri njem mnogo ljudstva, toliko, da stopi v ladjo, ter je sedel na morji; in vse ljudstvo je bilo ob morji na tléh.
2 Aliwafundisha mambo mengi kwa mifano, na katika mafundisho yake aliwaambia,
In učil jih je v prilikah mnogo, in pravil jim je v nauku svojem:
3 “Sikilizeni! Mpanzi alikwenda kupanda mbegu.
Poslušajte! Glej, izšel je sejavec sejat.
4 Alipokuwa akipanda, nyingine zilianguka njiani, ndege wakaja wakazila.
In zgodí se, ko je sejal, padlo je nekaj zrnja poleg ceste; in priletele so tice nebeške in ga pozobale.
5 Nyingine zilianguka penye mawe pasipokuwa na udongo mwingi. Mbegu hizo ziliota mara kwa kuwa udongo haukuwa na kina.
A drugo je padlo na skalnata tlá, kjer ni imelo mnogo zemlje, in precej je pognalo, ker ni imelo globoke zemlje.
6 Jua lilipochomoza, zikachomeka; na kwa kuwa mizizi yake haikuwa na nguvu, zikanyauka.
Ko je pa solnce vzšlo, ovenelo je; in ker ni imelo korenine, usahnilo je.
7 Nyingine zilianguka kwenye miti ya miiba, nayo ikakua na kuzisonga, nazo hazikuzaa nafaka.
In drugo je padlo v trnje. In trnje je zrastlo in ga udušilo; in ni dalo sadú.
8 Nyingine zilianguka katika udongo mzuri, zikakua na kuzaa: moja punje thelathini, moja sitini na nyingine mia.”
In drugo je padlo na dobro zemljo, in dajalo je sad, kteri je rastel in se množil, in rodilo je po trideset, in po šestdeset, in po sto.
9 Kisha akawaambia, “Mwenye masikio na asikie!”
In reče jim: Kdor ima ušesa, da sliši, naj sliši!
10 Yesu alipokuwa peke yake, baadhi ya wale waliomsikia walimwendea pamoja na wale kumi na wawili, wakamwuliza juu ya hiyo mifano.
Ko je pa ostal sam, vprašajo ga tisti, kteri so bili pri njem z dvanajsterimi, za to priliko.
11 Naye akawaambia, “Ninyi mmejaliwa kujua siri ya Utawala wa Mungu, lakini wale walio nje wataambiwa kila kitu kwa mifano,
Pa jim reče: Vam je dano, da spoznate skrivnost kraljestva Božjega; onim pa, ki so zunej, godí se vse v prilikah;
12 ili, Watazame kweli, lakini wasione. Wasikie kweli, lakini wasielewe. La sivyo, wangemgeukia Mungu, naye angewasamehe.”
Da vidijo in gledajo, pa ne ugledajo; in slišijo ter poslušajo, pa ne umejo; da se ne bi kedaj spreobrnili, in bi se jim odpustili grehi.
13 Basi, Yesu akawauliza, “Je, ninyi hamwelewi mfano huu? Mtawezaje basi, kuelewa mfano wowote?
In reče jim: Ne umete li te prilike? a kako boste vse prilike umeli?
14 Mpanzi hupanda neno la Mungu.
Sejavec seje besedo.
15 Watu wengine ni kama wale walio njiani ambapo mbegu zilianguka. Hawa hulisikia hilo neno lakini mara Shetani huja na kuliondoa neno hilo lililopandwa ndani yao.
Ti so pa, ki so poleg ceste: kjer se seje beseda, in so jo slišali, precej pride satan in vzeme besedo, ktera je posejana v njih srca,
16 Watu wengine ni kama zile mbegu zilizopandwa penye mawe. Mara tu wanapolisikia hilo neno hulipokea kwa furaha.
In enako so ti, ki so na skalnata tlá posejani: kteri besedo, ki so jo slišali, precej z veseljem sprejmó;
17 Lakini haliwaingii na kuwa na mizizi ndani yao; huendelea kulizingatia kwa kitambo tu, na wakati taabu au udhalimu vinapotokea kwa sababu ya hilo neno mara wanakata tamaa.
Pa nimajo korenine v sebi, nego so nestanovitni; potem ko nastane stiska ali preganjanje za voljo besede, pohujšujejo se precej.
18 Watu wengine ni kama zile mbegu zilizoanguka penye miti ya miiba. Huo ni mfano wa wale wanaolisikia hilo neno,
In ti so, ki so v trnje posejani: ti so, kteri besedo slišijo;
19 lakini wasiwasi wa ulimwengu huu, anasa za mali na tamaa za kila namna huwaingia na kulisonga hilo neno, nao hawazai matunda. (aiōn )
Pa skrbí tega sveta, in ničemurnost bogastva, in druge slasti se prikradejo, in udušé besedo, in brez sadú je. (aiōn )
20 Lakini wengine ni kama zile mbegu zilizopandwa katika udongo mzuri. Hawa hulisikia hilo neno, wakalipokea, wakazaa matunda: wengine thelathini, wengine sitini na wengine mia moja.”
In ti so, ki so na dobro zemljo posejani: kteri besedo poslušajo in sprejemajo, ter prinašajo sad, po trideset, in po šestdeset, in po sto.
21 Yesu akaendelea kuwaambia, “Je, watu huwasha taa wakaileta ndani na kuifunika kwa pishi au kuiweka mvunguni? La! Huiweka juu ya kinara.
In reče jim; Prižiga li se sveča, da se pod mernik postavi ali pod posteljo? a ne, da se na svečnik postavi?
22 Basi, kila kilichofichwa kitafichuliwa, na kila kilichofunikwa kitafunuliwa.
Kajti nič ni skrivnega, kar se ne bi razodelo; in nič ni tako skritega, da ne bi prišlo na svetlo.
23 Mwenye masikio na asikie!”
Če ima kdo ušesa, da sliši, naj sliši!
24 Akawaambia pia, “Sikilizeni kwa makini mnachosikia! Kipimo kilekile mnachowapimia watu wengine, ndicho mtakachopimiwa; tena mtazidishiwa.
In reče jim: Pomislite, kaj slišite! S kakoršno mero boste merili, merilo se bo vam, in pridalo se bo vam, ki poslušate.
25 Aliye na kitu atapewa zaidi; asiye na kitu, hata kile alicho nacho kitachukuliwa.”
Kajti kdor ima, dalo mu se bo; a kdor nima, odvzelo mu se bo tudi to, ka ima.
26 Yesu akaendelea kusema, “Ufalme wa Mungu ni kama ifuatavyo. Mtu hupanda mbegu shambani.
In reče: Tako je kraljestvo Božje, kakor človek, če vrže seme v zemljo,
27 Usiku hulala, mchana yu macho na wakati huo mbegu zinaota na kukua; yeye hajui inavyofanyika.
In spí in vstaja po noči in po dnevu, in seme poganja, in raste, da ne vé on.
28 Udongo wenyewe huiwezesha mimea kukua na kuzaa matunda: kwanza huchipua jani changa, kisha suke, na mwishowe nafaka ndani ya suke.
Kajti zemlja sama od sebe rodí, najprej travo, potem klas, potem polno pšenico v klasu.
29 Nafaka inapoiva, huyo mtu huanza kutumia mundu wake, maana wakati wa mavuno umefika.”
Ko pa sad dozorí, precej pošlje srp; kajti nastala je žetev.
30 Tena, Yesu akasema, “Tuufananishe Utawala wa Mungu na nini? Tuueleze kwa mifano gani?
In reče: Komu bomo primerili kraljestvo Božje? ali v kakošnej priliki ga bomo upodobili?
31 Ni kama mbegu ya haradali ambayo ni ndogo kuliko mbegu zote.
Ono je, kakor zrno gorušično, ktero je, ko se vseje v zemljo, manjše od vseh semen, ktera so na zemlji;
32 Lakini ikisha pandwa, huota na kuwa mmea mkubwa kuliko mimea yote ya shambani. Matawi yake huwa makubwa hata ndege wa angani huweza kujenga viota vyao katika kivuli chake.”
In ko je vsejano, raste, in postane veče od vseh zelišč, in dela velike veje, da se morejo pod senco njegovo tice nebeške nastanjevati.
33 Yesu aliwahubiria ujumbe wake kwa mifano mingine mingi ya namna hiyo; aliongea nao kadiri walivyoweza kusikia.
In v mnogih takošnih prilikah jim je govoril besedo, ko so jo mogli poslušati.
34 Hakuongea nao chochote bila kutumia mifano; lakini alipokuwa pamoja na wanafunzi wake peke yao alikuwa akiwafafanulia kila kitu.
Brez prilike jim pa ni govoril; a posebej je učencem svojim razlagal vse.
35 Jioni, siku hiyohiyo, Yesu aliwaambia wanafunzi wake, “Tuvuke ziwa, twende ng'ambo.”
In reče jim tisti dan, ko se je zvečerilo: Prepeljimo se na oni kraj.
36 Basi, wakauacha ule umati wa watu, wakamchukua Yesu katika mashua alimokuwa. Palikuwapo pia mashua nyingine hapo.
In zapustivši ljudstvo, vzemó ga, kakor je bil v ladji; bile so pa tudi druge ladjice ž njim.
37 Basi, dhoruba kali ikaanza kuvuma, mawimbi yakaipiga ile mashua hata ikaanza kujaa maji.
Kar nastane vélik vihar od vetra; in valovi so se vlivali v ladjo, da se je uže napolnjevala.
38 Yesu alikuwa sehemu ya nyuma ya mashua, amelala juu ya mto. Basi, wanafunzi wakamwamsha na kumwambia, “Mwalimu, je, hujali kwamba sisi tunaangamia?”
In on je bil na krmi, spé na vzglavji; in zbudé ga, in rekó mu: Učenik, ali ti ni nič mar, da pogibamo?
39 Basi, akaamka, akaukemea ule upepo na kuyaamrisha mawimbi ya ziwa, “Kimya! Tulia!” Hapo upepo ukakoma, kukawa shwari kabisa.
In vstavši, zapretí vetru, in reče morju; Umolkni, umiri se! In nehal je veter, in nastala je velika tihota.
40 Kisha Yesu akawaambia wanafunzi wake, “Mbona mnaogopa? Je, bado hamna imani?”
In reče jim: Kaj ste tako plašni? Kako, da nimate vere?
41 Nao wakaogopa sana, wakawa wanaulizana, “Huyu ni nani basi, hata upepo na mawimbi vinamtii?”
In uplašili so se z velikim strahom, in govorili so med seboj: Kdo vendar je ta, da sta mu tudi veter in morje pokorna?