< Marko 4 >
1 Yesu alianza kufundisha tena akiwa kando ya ziwa. Umati mkubwa wa watu ulimzunguka hata ikambidi aingie katika mashua na kuketi. Watu wakawa wamekaa katika nchi kavu, kando ya ziwa.
Ahanda abha manyizywe mu shinjhe izhumbi. Ni bhunga ingosi ihubhungana ihazyhungula, ahinjila muhati inyitu li musumbi, ahakhala. Ibhuga yunthi ihali izywungulile mushinje munsumbi mu fukweni.
2 Aliwafundisha mambo mengi kwa mifano, na katika mafundisho yake aliwaambia,
Abhamanyizhwa inongwa inyinji huvifwani, ayanga wa bhene hunsundo zyakwe.
3 “Sikilizeni! Mpanzi alikwenda kupanda mbegu.
Uvhi ikopba ihabhalile atote.
4 Alipokuwa akipanda, nyingine zilianguka njiani, ndege wakaja wakazila.
Pali atota, zimo imbeyu zyalagala mwidala, inyonyizywahinza zywalya.
5 Nyingine zilianguka penye mawe pasipokuwa na udongo mwingi. Mbegu hizo ziliota mara kwa kuwa udongo haukuwa na kina.
Imbeyu zimo zywalaga mumwala, pasipali ninzhi inyinji iyaye. Mara zikanyauka, kwa sababu hazikuwa na udongo wakutosha.
6 Jua lilipochomoza, zikachomeka; na kwa kuwa mizizi yake haikuwa na nguvu, zikanyauka.
Lelo isanya palyahatukula, zywatenguha, lelo pheposazywali na kholo zyahumaa.
7 Nyingine zilianguka kwenye miti ya miiba, nayo ikakua na kuzisonga, nazo hazikuzaa nafaka.
Imbeyu zimo zywalagala pahati pamivhwa. Amivhwagazi puta, saga zhwasiga indundu zywa zwunthi.
8 Nyingine zilianguka katika udongo mzuri, zikakua na kuzaa: moja punje thelathini, moja sitini na nyingine mia.”
Imbeyu izwenje zhwalagala munzhi inyinza zhwapa indundu pazi wonjelela, zimo zihasagala along gatatu sana, zimo malogo tanda, na zimo malogo mia.”
9 Kisha akawaambia, “Mwenye masikio na asikie!”
Ahayanga, “Wabhunti uwi makutu agahuvhwe, naayuvhaje!”
10 Yesu alipokuwa peke yake, baadhi ya wale waliomsikia walimwendea pamoja na wale kumi na wawili, wakamwuliza juu ya hiyo mifano.
U Yesu pahavha mwene, bhala habha phiphi nu mwene bhala ilongo nabhantu bhantu bhahabhuzywa ehusu ivifwani.
11 Naye akawaambia, “Ninyi mmejaliwa kujua siri ya Utawala wa Mungu, lakini wale walio nje wataambiwa kila kitu kwa mifano,
Ahayanga wavhene, “Amwe mpewilwe utawala uwa Nguluvhi. Lelo bhala abhalihunzi shila hatu wayanje nivifwani, ili gawenya, ena wenya,
12 ili, Watazame kweli, lakini wasione. Wasikie kweli, lakini wasielewe. La sivyo, wangemgeukia Mungu, naye angewasamehe.”
lelo hawenya, phepo pahuvhwa, lelo sahuvhwa wawenya, lelo sawenya wala hawe lewa nahuvhe, lelo gabhe bhagaluhananga Ungulubhi abhahoshelanga.”
13 Basi, Yesu akawauliza, “Je, ninyi hamwelewi mfano huu? Mtawezaje basi, kuelewa mfano wowote?
Ahayanga wabhene, “Ishi samuwelewa ivifwani ivhi? Mugawezwa bhuli awelewe ifwani ivhinje?
14 Mpanzi hupanda neno la Mungu.
Ikopha itotile izyo.
15 Watu wengine ni kama wale walio njiani ambapo mbegu zilianguka. Hawa hulisikia hilo neno lakini mara Shetani huja na kuliondoa neno hilo lililopandwa ndani yao.
Lelo bhala bhalagala mushinjhe mwidala, papizywa lwatotilwe. Pala pabhahuvha, pepo uSetano ahiza naweje izywo lila lwatotilwe muhati yao.
16 Watu wengine ni kama zile mbegu zilizopandwa penye mawe. Mara tu wanapolisikia hilo neno hulipokea kwa furaha.
Na bhamo bhala bhatwa mumwala palyuvha izywa, shalubhilo shalulo bhalipola huwaushe.
17 Lakini haliwaingii na kuwa na mizizi ndani yao; huendelea kulizingatia kwa kitambo tu, na wakati taabu au udhalimu vinapotokea kwa sababu ya hilo neno mara wanakata tamaa.
Sabhanakholo gangunthi muhahati yao, lelo vhajimba humuda ufupi. Amayimba na yushe wao paviweza hunongwa yizyo vhafiha bhambumila.
18 Watu wengine ni kama zile mbegu zilizoanguka penye miti ya miiba. Huo ni mfano wa wale wanaolisikia hilo neno,
Bhamo vhala bhatotwa kati yimivha bhahuvha izywo,
19 lakini wasiwasi wa ulimwengu huu, anasa za mali na tamaa za kila namna huwaingia na kulisonga hilo neno, nao hawazai matunda. (aiōn )
lelo ayimba agamunzhi akhopelwe nishuma nivinyonya zwa mambo aganji, huhuwaingia nasupe izywo na limenwa apape amadudu. (aiōn )
20 Lakini wengine ni kama zile mbegu zilizopandwa katika udongo mzuri. Hawa hulisikia hilo neno, wakalipokea, wakazaa matunda: wengine thelathini, wengine sitini na wengine mia moja.”
Na bhawili abhabhatotilwe munzhi inyinza. Bhalwuvha izywo nali pashele bhapapa amandundu: bhamo malongo gatatu bhamo malongo tanda bhamo mia moja.”
21 Yesu akaendelea kuwaambia, “Je, watu huwasha taa wakaileta ndani na kuifunika kwa pishi au kuiweka mvunguni? La! Huiweka juu ya kinara.
U Yesu abhambula, “Je unaleta ta ndani ya nyumba nakuweka panzhi ishitundu, au pansi pashitala? Uleta muhati na bhishe pamwanya pakinara.
22 Basi, kila kilichofichwa kitafichuliwa, na kila kilichofunikwa kitafunuliwa.
Na hami hahabhajile afise asahagabhoneha, nahakuna siri iyasiga abhapazeru.
23 Mwenye masikio na asikie!”
Khawele uwimakutu gahuvhe ayuvhwaje!”
24 Akawaambia pia, “Sikilizeni kwa makini mnachosikia! Kipimo kilekile mnachowapimia watu wengine, ndicho mtakachopimiwa; tena mtazidishiwa.
Akawaambia, “Mubhanje maso na hala amuhuvhwa, alingane ishipimo shila ishampima ndio shisho shamwapimilwa shayonjelezewa hulimwe.
25 Aliye na kitu atapewa zaidi; asiye na kitu, hata kile alicho nacho kitachukuliwa.”
Afutane aje uhula uwanao ayejelela vinji tee, ulakwasanao afume wamwe ene vyayegwa navila uvya navyo.”
26 Yesu akaendelea kusema, “Ufalme wa Mungu ni kama ifuatavyo. Mtu hupanda mbegu shambani.
Ayanga, “Utawala uwa Ngulubhi ufananasiwa nu muntu uwa vyala imbeyu mwilongo.
27 Usiku hulala, mchana yu macho na wakati huo mbegu zinaota na kukua; yeye hajui inavyofanyika.
Pahagona adamula na shabwi imbeyu zyatiuha nakule, ikiwa haga hamanya shifumile.
28 Udongo wenyewe huiwezesha mimea kukua na kuzaa matunda: kwanza huchipua jani changa, kisha suke, na mwishowe nafaka ndani ya suke.
Izhi ifumia imbeyu yiiyo asoti amatundu baada yipo uwezya, nanthele imbeyu izyazikhomile.
29 Nafaka inapoiva, huyo mtu huanza kutumia mundu wake, maana wakati wa mavuno umefika.”
Lelo imbeyu ya payakho ma atwala inhengo, pipo avune hufishile.”
30 Tena, Yesu akasema, “Tuufananishe Utawala wa Mungu na nini? Tuueleze kwa mifano gani?
Ayaanga, “Tufwananiswe utawala wa Ngulubhi nahanthushi, au tumile hanthuuli amatumile hanthu uwuli awelezyezye?
31 Ni kama mbegu ya haradali ambayo ni ndogo kuliko mbegu zote.
Ili nishi imbeyu yiladai, lelo pihatotwaga hali hadodo sana kuko imbeyu zywunthi munshi.
32 Lakini ikisha pandwa, huota na kuwa mmea mkubwa kuliko mimea yote ya shambani. Matawi yake huwa makubwa hata ndege wa angani huweza kujenga viota vyao katika kivuli chake.”
Hata lula ulwitothilwe igosi sana kuliko vhu nthi ivha vitotilwe mubusitani ivheha inzamba ingosi nazi inyenji ziwezya akhale nabheshe ivhansu ali nganaje inzunda yakwe.”
33 Yesu aliwahubiria ujumbe wake kwa mifano mingine mingi ya namna hiyo; aliongea nao kadiri walivyoweza kusikia.
Amafano aminji amanyizywe ayanjile inongwa wa bhene, shinza ishabhawezizye awelewe,
34 Hakuongea nao chochote bila kutumia mifano; lakini alipokuwa pamoja na wanafunzi wake peke yao alikuwa akiwafafanulia kila kitu.
haga ayangaga anabho bila fwano. Lelo lula ulimwene, ahabha bhula asundwa bhakwe shila hantu.
35 Jioni, siku hiyohiyo, Yesu aliwaambia wanafunzi wake, “Tuvuke ziwa, twende ng'ambo.”
Lelo isiku ilwo ulwe vhela pawafishile, ayanga wabhene,
36 Basi, wakauacha ule umati wa watu, wakamchukua Yesu katika mashua alimokuwa. Palikuwapo pia mashua nyingine hapo.
“Sanli upande uwa bhili”. Pipo bhaileha ibhuga, bhahamwenga uYesu, uwakati bhuwo ahavha mwituli. Amatuli aganji galipandwimo numwene.
37 Basi, dhoruba kali ikaanza kuvuma, mawimbi yakaipiga ile mashua hata ikaanza kujaa maji.
Ihala ihali ihavhulungwe amawimbi gahijilaga muhati mwintuli na ituli nagamimile.
38 Yesu alikuwa sehemu ya nyuma ya mashua, amelala juu ya mto. Basi, wanafunzi wakamwamsha na kumwambia, “Mwalimu, je, hujali kwamba sisi tunaangamia?”
Lelo uYesu yuyo alikuwa kwenye shetri, ali agonelile mwisoho. Bhahadamusya, bhayanga, “Wamwalimo, hangu saga ati tufwa?”
39 Basi, akaamka, akaukemea ule upepo na kuyaamrisha mawimbi ya ziwa, “Kimya! Tulia!” Hapo upepo ukakoma, kukawa shwari kabisa.
Abhuha audamila ihala aibhula inzumbi, '“Ibhe shinza, huwaushe”. Ihala ihaleha, wahavha miee sana.
40 Kisha Yesu akawaambia wanafunzi wake, “Mbona mnaogopa? Je, bado hamna imani?”
Ayanga wa bhene, “Yenu mu hwogopa? Samulinima bado?”
41 Nao wakaogopa sana, wakawa wanaulizana, “Huyu ni nani basi, hata upepo na mawimbi vinamtii?”
Bhahabha nihofu moyo gabho bhayangana vhene kwa vhene, “Unu yunanu antele, hata ihula ihumwogopa?”.