< Marko 4 >

1 Yesu alianza kufundisha tena akiwa kando ya ziwa. Umati mkubwa wa watu ulimzunguka hata ikambidi aingie katika mashua na kuketi. Watu wakawa wamekaa katika nchi kavu, kando ya ziwa.
Jeesus hakkas taas õpetama järve ääres. Tema juurde kogunes nii palju rahvast, et ta pidi astuma paati ja istuma selles järvel, samal ajal kui inimesed seisid piki kallast vee serval.
2 Aliwafundisha mambo mengi kwa mifano, na katika mafundisho yake aliwaambia,
Ta õpetas neile palju asju tähendamissõnadega ja rääkis neile oma õpetuses:
3 “Sikilizeni! Mpanzi alikwenda kupanda mbegu.
„Kuulake! Põllumees läks välja külvama.
4 Alipokuwa akipanda, nyingine zilianguka njiani, ndege wakaja wakazila.
Kui ta külvas, kukkus osa seemet teeveerele ning linnud tulid ja nokkisid selle.
5 Nyingine zilianguka penye mawe pasipokuwa na udongo mwingi. Mbegu hizo ziliota mara kwa kuwa udongo haukuwa na kina.
Osa kukkus kivisele maale, kus ei olnud palju mulda, ja see idanes kohe, sest muld ei olnud sügav.
6 Jua lilipochomoza, zikachomeka; na kwa kuwa mizizi yake haikuwa na nguvu, zikanyauka.
Aga kui päike tõusis, kuivasid taimed ära, sest neil ei olnud juurt.
7 Nyingine zilianguka kwenye miti ya miiba, nayo ikakua na kuzisonga, nazo hazikuzaa nafaka.
Osa seemet kukkus ohakate sekka, ning ohakad sirgusid ja lämmatasid taimed, nii et need ei kandnud vilja.
8 Nyingine zilianguka katika udongo mzuri, zikakua na kuzaa: moja punje thelathini, moja sitini na nyingine mia.”
Aga osa seemet kukkus heasse mulda. See idanes ja kasvas ja kandis vilja: mõni kolmkümmend, mõni kuuskümmend, mõni sada korda rohkem.“
9 Kisha akawaambia, “Mwenye masikio na asikie!”
Ja ta ütles: „Kellel kõrvad on kuulda, see kuulgu!“
10 Yesu alipokuwa peke yake, baadhi ya wale waliomsikia walimwendea pamoja na wale kumi na wawili, wakamwuliza juu ya hiyo mifano.
Kui Jeesus üksi oli, küsisid kaksteist jüngrit, ja teised tema ümber, temalt seletust tähendamissõnade kohta.
11 Naye akawaambia, “Ninyi mmejaliwa kujua siri ya Utawala wa Mungu, lakini wale walio nje wataambiwa kila kitu kwa mifano,
Ta ütles neile: „Teie kätte on antud Jumala riigi saladus, aga neile, kes on väljas, räägitakse kõike tähendamissõnadega,
12 ili, Watazame kweli, lakini wasione. Wasikie kweli, lakini wasielewe. La sivyo, wangemgeukia Mungu, naye angewasamehe.”
„et nad vaataksid ega näeks ja kuuleksid ega mõistaks, sest muidu nad pöörduksid, ja neile antaks andeks.““
13 Basi, Yesu akawauliza, “Je, ninyi hamwelewi mfano huu? Mtawezaje basi, kuelewa mfano wowote?
Siis ütles Jeesus neile: „Kas te ei mõista selle tähendamissõna tähendust? Kuidas te siis võiksite mõista ühtki tähendamissõna?
14 Mpanzi hupanda neno la Mungu.
Külvaja külvab sõna.
15 Watu wengine ni kama wale walio njiani ambapo mbegu zilianguka. Hawa hulisikia hilo neno lakini mara Shetani huja na kuliondoa neno hilo lililopandwa ndani yao.
Mõned inimesed on nagu teeveered, kuhu sõna langeb. Niipea kui nad seda kuulevad, tuleb saatan ja võtab ära neisse külvatud sõna.
16 Watu wengine ni kama zile mbegu zilizopandwa penye mawe. Mara tu wanapolisikia hilo neno hulipokea kwa furaha.
Kivisele maale külvatu sarnased on need, kes sõna kuuldes võtavad selle kohe rõõmuga vastu,
17 Lakini haliwaingii na kuwa na mizizi ndani yao; huendelea kulizingatia kwa kitambo tu, na wakati taabu au udhalimu vinapotokea kwa sababu ya hilo neno mara wanakata tamaa.
ent neil pole juurt ja nad püsivad lühikest aega. Kui siis sõna pärast tuleb tüli või tagakius, langevad nad kiiresti.
18 Watu wengine ni kama zile mbegu zilizoanguka penye miti ya miiba. Huo ni mfano wa wale wanaolisikia hilo neno,
Ohakate sekka külvatu sarnased on need, kes sõna küll kuulevad,
19 lakini wasiwasi wa ulimwengu huu, anasa za mali na tamaa za kila namna huwaingia na kulisonga hilo neno, nao hawazai matunda. (aiōn g165)
ent elumured ja rikkuse petlik ahvatlus ja mitmesugused muud soovid tulevad ja lämmatavad sõna nii, et see jääb viljatuks. (aiōn g165)
20 Lakini wengine ni kama zile mbegu zilizopandwa katika udongo mzuri. Hawa hulisikia hilo neno, wakalipokea, wakazaa matunda: wengine thelathini, wengine sitini na wengine mia moja.”
Kuid heasse mulda külvatu on need, kes sõna kuulevad ja selle vastu võtavad ja vilja kannavad: mõni kolmkümmend, mõni kuuskümmend, mõni sada korda rohkem.“
21 Yesu akaendelea kuwaambia, “Je, watu huwasha taa wakaileta ndani na kuifunika kwa pishi au kuiweka mvunguni? La! Huiweka juu ya kinara.
Jeesus ütles neile: „Kas lamp tuuakse tuppa selleks, et see panna vaka või voodi alla? Eks panda see pigem lambijalale?
22 Basi, kila kilichofichwa kitafichuliwa, na kila kilichofunikwa kitafunuliwa.
Sest kõik peidetu on olemas vaid avalikuks saamiseks, kõik varjatu vaid ilmsiks tulemiseks.
23 Mwenye masikio na asikie!”
Kui kellelgi on kõrvad kuulda, see kuulgu!“
24 Akawaambia pia, “Sikilizeni kwa makini mnachosikia! Kipimo kilekile mnachowapimia watu wengine, ndicho mtakachopimiwa; tena mtazidishiwa.
Ja Jeesus ütles neile: „Pange tähele, mida te kuulete! Mis mõõduga teie mõõdate, sellega mõõdetakse ka teile, ja enamgi veel.
25 Aliye na kitu atapewa zaidi; asiye na kitu, hata kile alicho nacho kitachukuliwa.”
Kellel on, sellele antakse, ja kellel ei ole, selle käest võetakse seegi, mis tal on.“
26 Yesu akaendelea kusema, “Ufalme wa Mungu ni kama ifuatavyo. Mtu hupanda mbegu shambani.
Jeesus ütles ka: „Just selline on Jumala riik: mees viskab seemne mulda.
27 Usiku hulala, mchana yu macho na wakati huo mbegu zinaota na kukua; yeye hajui inavyofanyika.
Ta heidab magama või ärkab üles, öösel ja päeval, ning seeme idaneb ja kasvab, kuid ta ei tea, kuidas.
28 Udongo wenyewe huiwezesha mimea kukua na kuzaa matunda: kwanza huchipua jani changa, kisha suke, na mwishowe nafaka ndani ya suke.
Maa kannab vilja iseenesest, esmalt orast, siis päid, siis täit tera viljapea sees.
29 Nafaka inapoiva, huyo mtu huanza kutumia mundu wake, maana wakati wa mavuno umefika.”
Aga niipea kui vili on küps, saadab ta sirbi, sest lõikusaeg on käes.“
30 Tena, Yesu akasema, “Tuufananishe Utawala wa Mungu na nini? Tuueleze kwa mifano gani?
Ja Jeesus ütles: „Millega võiks võrrelda Jumala riiki või millise tähendamissõnaga seda kujutada?
31 Ni kama mbegu ya haradali ambayo ni ndogo kuliko mbegu zote.
See on nagu sinepiseeme, mis on väikseim kõigist seemneist maa peal.
32 Lakini ikisha pandwa, huota na kuwa mmea mkubwa kuliko mimea yote ya shambani. Matawi yake huwa makubwa hata ndege wa angani huweza kujenga viota vyao katika kivuli chake.”
Ent kui see on külvatud, siis see võrsub ja kasvab suuremaks kõigist aiataimedest ja kasvatab suured oksad, nii et taeva linnud võivad pesitseda selle varjus.“
33 Yesu aliwahubiria ujumbe wake kwa mifano mingine mingi ya namna hiyo; aliongea nao kadiri walivyoweza kusikia.
Ja Jeesus rääkis neile Jumala sõna paljude selliste tähendamissõnadega, nii palju kui nad suutsid mõista.
34 Hakuongea nao chochote bila kutumia mifano; lakini alipokuwa pamoja na wanafunzi wake peke yao alikuwa akiwafafanulia kila kitu.
Aga ilma tähendamissõnata ei rääkinud ta neile midagi. Kuid omavahel olles seletas ta jüngritele kõike.
35 Jioni, siku hiyohiyo, Yesu aliwaambia wanafunzi wake, “Tuvuke ziwa, twende ng'ambo.”
Samal päeval õhtu jõudes ütles Jeesus jüngritele: „Lähme vastaskaldale!“
36 Basi, wakauacha ule umati wa watu, wakamchukua Yesu katika mashua alimokuwa. Palikuwapo pia mashua nyingine hapo.
Nad jätsid rahvahulga maha ning võtsid Jeesuse kaasa, nii nagu ta paadis oli; ka teisi paate oli temaga.
37 Basi, dhoruba kali ikaanza kuvuma, mawimbi yakaipiga ile mashua hata ikaanza kujaa maji.
Järsku tõusis tugev raju ja lained lõid üle paadi, nii et paat juba täitus veest.
38 Yesu alikuwa sehemu ya nyuma ya mashua, amelala juu ya mto. Basi, wanafunzi wakamwamsha na kumwambia, “Mwalimu, je, hujali kwamba sisi tunaangamia?”
Aga Jeesus magas paadipäras, pea padjal. „Õpetaja, kas sa ei hooli sellest, et me upume?“hüüdsid jüngrid teda üles äratades.
39 Basi, akaamka, akaukemea ule upepo na kuyaamrisha mawimbi ya ziwa, “Kimya! Tulia!” Hapo upepo ukakoma, kukawa shwari kabisa.
Jeesus tõusis püsti, sõitles tuult ja ütles lainetele: „Vait! Olge tasa!“Ja tuul rauges ning järvepind muutus täiesti tasaseks.
40 Kisha Yesu akawaambia wanafunzi wake, “Mbona mnaogopa? Je, bado hamna imani?”
Jeesus ütles jüngritele: „Miks te olete nii hirmul? Kuidas teil ei ole usku?“
41 Nao wakaogopa sana, wakawa wanaulizana, “Huyu ni nani basi, hata upepo na mawimbi vinamtii?”
Neid valdas aga suur aukartus ja nad küsisid üksteiselt: „Kes see mees küll on, et isegi tuul ja lained kuuletuvad talle?“

< Marko 4 >