< Marko 15 >
1 Kulipopambazuka, makuhani wakuu walifanya shauri pamoja na wazee, walimu wa Sheria na Baraza lote, wakamfunga Yesu pingu, wakampeleka na kumkabidhi kwa Pilato.
Et aussitôt, au matin, les principaux sacrificateurs avec les anciens et les scribes et tout le sanhédrin, ayant tenu conseil, lièrent Jésus et l’emmenèrent et le livrèrent à Pilate.
2 Pilato akamwuliza Yesu, “Je, wewe ni mfalme wa Wayahudi?” Yesu akajibu, “Wewe umesema.”
Et Pilate l’interrogea: Toi, tu es le roi des Juifs? Et répondant, il lui dit: Tu le dis.
3 Makuhani wakuu wakamshtaki Yesu mambo mengi.
Et les principaux sacrificateurs l’accusaient de beaucoup de choses.
4 Pilato akamwuliza tena Yesu, “Je, hujibu neno? Tazama wanavyotoa mashtaka mengi juu yako.”
Et Pilate l’interrogea encore, disant: Ne réponds-tu rien? Vois de combien de choses ils portent témoignage contre toi.
5 Lakini Yesu hakujibu neno, hata pilato akashangaa.
Mais encore Jésus ne répondit rien, de sorte que Pilate s’en étonnait.
6 Kila wakati wa sikukuu ya Pasaka, Pilato alikuwa na desturi ya kuwafungulia mfungwa mmoja waliyemtaka.
Or il leur relâchait à la fête un prisonnier, lequel que ce soit qu’ils demandent.
7 Basi, kulikuwa na mtu mmoja aitwaye Baraba, ambaye alikuwa amefungwa pamoja na waasi wengine kwa kusababisha uasi na mauaji.
Et il y avait le nommé Barabbas qui était détenu avec ses compagnons de sédition, lesquels, dans la sédition, avaient commis un meurtre.
8 Watu wengi wakamwendea Pilato wakamwomba awafanyie kama kawaida yake.
Et la foule, poussant des cris, se mit à lui demander [de faire] comme il leur avait toujours fait.
9 Pilato akawauliza, “Je, mwataka niwafungulieni Mfalme wa Wayahudi?”
Et Pilate leur répondit, disant: Voulez-vous que je vous relâche le roi des Juifs?
10 Alisema hivyo kwa sababu alijua wazi kwamba makuhani wakuu walimkabidhi Yesu kwake kwa sababu ya wivu.
Car il savait que les principaux sacrificateurs l’avaient livré par envie.
11 Lakini makuhani wakuu wakawachochea watu wamwombe Pilato awafungulie Baraba.
Mais les principaux sacrificateurs excitèrent le peuple [à demander] que plutôt il leur relâche Barabbas.
12 Pilato akawauliza tena, “Basi, sasa mwataka nifanye nini na mtu huyu mnayemwita Mfalme wa Wayahudi?”
Et Pilate, répondant, leur dit encore: Que voulez-vous donc que je fasse de celui que vous appelez roi des Juifs?
13 Watu wote wakapaaza sauti tena: “Msulubishe!”
Et ils s’écrièrent encore: Crucifie-le!
14 Lakini Pilato akawauliza, “Kwa nini! Amefanya kosa gani?” Lakini wao wakazidi kupaaza sauti, “Msulubishe!”
Et Pilate leur dit: Mais quel mal a-t-il fait? Et ils s’écrièrent encore plus fort: Crucifie-le!
15 Pilato alitaka kuuridhisha huo umati wa watu; basi, akamwachilia Baraba kutoka gerezani. Akaamuru Yesu apigwe viboko, kisha akamtoa asulubiwe.
Et Pilate, voulant contenter la foule, leur relâcha Barabbas; et, ayant fait fouetter Jésus, il le livra pour être crucifié.
16 Kisha askari walimpeleka Yesu ndani ukumbini, katika ikulu, wakakusanya kikosi kizima cha askari.
Et les soldats l’emmenèrent dans la cour, qui est le prétoire. Et ils assemblent toute la cohorte;
17 Wakamvika vazi la rangi ya zambarau, wakasokota taji ya miiba, wakamwekea kichwani.
et ils le revêtent de pourpre, et ayant tressé une couronne d’épines, ils la lui mettent autour [de la tête].
18 Wakaanza kumsalimu, “Shikamoo Mfalme wa Wayahudi!”
Et ils se mirent à le saluer, [disant]: Salut, roi des Juifs!
19 Wakampiga kichwani kwa mwanzi, wakamtemea mate; wakampigia magoti na kumsujudia.
Et ils lui frappaient la tête avec un roseau et crachaient contre lui, et, se mettant à genoux, ils lui rendaient hommage.
20 Baada ya kumdhihaki, walimvua lile joho, wakamvika nguo zake, kisha wakampeleka kumsulubisha.
Et après qu’ils se furent moqués de lui, ils le dépouillèrent de la pourpre et le revêtirent de ses propres vêtements; et ils l’emmènent dehors pour le crucifier.
21 Walipokuwa njiani, walikutana na mtu mmoja aitwaye Simoni, mwenyeji wa Kurene. Yeye alikuwa baba wa Aleksanda na Rufo, na wakati huo alikuwa akitoka shambani. Basi, wakamlazimisha auchukue msalaba wa Yesu.
Et ils contraignent un certain homme, Simon, Cyrénéen, père d’Alexandre et de Rufus, qui passait par là, venant des champs, de porter sa croix.
22 Kisha wakampeleka Yesu mpaka mahali palipoitwa Golgotha, maana yake, “Mahali pa Fuvu la Kichwa.”
Et ils le mènent au lieu [appelé] Golgotha, ce qui, interprété, est: lieu du crâne.
23 Wakampa divai iliyochanganywa na manemane, lakini yeye akaikataa.
Et ils lui donnèrent à boire du vin mixtionné de myrrhe; mais il ne le prit pas.
24 Basi, wakamsulubisha, wakagawana mavazi yake kwa kuyapigia kura waamue nani angepata nini.
Et l’ayant crucifié, ils partagent ses vêtements, en tirant au sort [pour savoir] ce que chacun en prendrait.
25 Ilikuwa saa tatu asubuhi walipomsulubisha.
Et c’était la troisième heure, et ils le crucifièrent.
26 Na mshtaka wake ulikuwa umeandikwa: “Mfalme wa Wayahudi.”
Et l’écriteau concernant le sujet de son accusation portait écrit: Le roi des Juifs.
27 Pamoja naye waliwasulubisha wanyang'anyi wawili, mmoja upande wake wa kulia na mwingine upande wake wa kushoto.
Et, avec lui, ils crucifient deux brigands, un à sa droite, et un à sa gauche.
28 Hapo yakatimia Maandiko Matakatifu yanayosema, “Aliwekwa kundi moja na waovu.”
[Et l’écriture fut accomplie, qui dit: « Et il a été compté parmi les iniques »].
29 Watu waliokuwa wanapita mahali hapo walimtukana, wakitikisa vichwa vyao na kusema, “Aha! Wewe mwenye kuvunja Hekalu na kulijenga kwa siku tatu!
Et ceux qui passaient par là, l’injuriaient, hochant la tête et disant: Hé! toi qui détruis le temple et qui le bâtis en trois jours,
30 Sasa, shuka msalabani ujiokoe mwenyewe!”
sauve-toi toi-même, et descends de la croix!
31 Nao makuhani wakuu pamoja na walimu wa Sheria walimdhihaki wakisema, “Aliwaokoa wengine, lakini kujiokoa mwenyewe hawezi!
Pareillement aussi les principaux sacrificateurs, se moquant entre eux avec les scribes, disaient: Il a sauvé les autres, il ne peut se sauver lui-même.
32 Eti yeye ni Kristo, Mfalme wa Israeli! Basi, na ashuke msalabani ili tuone na kuamini.” Hata watu wale waliosulubiwa pamoja naye walimtukana.
Que le Christ, le roi d’Israël, descende maintenant de la croix, afin que nous voyions et que nous croyions! Ceux aussi qui étaient crucifiés avec lui l’insultaient.
33 Tangu saa sita mchana mpaka saa tisa kulikuwa giza nchini kote.
Et quand la sixième heure fut venue, il y eut des ténèbres sur tout le pays jusqu’à la neuvième heure.
34 Saa tisa alasiri Yesu akalia kwa sauti kubwa, “Eloi, Eloi, lema sabakthani?” Maana yake, “Mungu wangu, Mungu wangu, mbona umeniacha?”
Et à la neuvième heure, Jésus s’écria d’une forte voix, disant: Éloï, Éloï, lama sabachthani? ce qui, interprété, est: Mon Dieu, mon Dieu, pourquoi m’as-tu abandonné?
35 Baadhi ya watu waliosimama pale waliposikia hivyo, walisema, “Sikiliza! Anamwita Eliya!”
Et quelques-uns de ceux qui étaient là présents, ayant entendu cela, disaient: Voici, il appelle Élie.
36 Mtu mmoja akakimbia, akachovya sifongo katika siki, akaiweka juu ya mwanzi, akampa anywe akisema, “Hebu tuone kama Eliya atakuja kumteremsha msalabani!”
Et l’un d’eux courut, et ayant rempli une éponge de vinaigre et l’ayant mise au bout d’un roseau, il lui donna à boire, disant: Laissez, voyons si Élie vient pour le faire descendre.
37 Yesu akapaaza sauti kubwa, akakata roho.
Et Jésus, ayant jeté un grand cri, expira.
38 Basi, pazia la Hekalu likapasuka vipande viwili toka juu mpaka chini.
Et le voile du temple se déchira en deux, depuis le haut jusqu’en bas.
39 Jemadari mmoja aliyekuwa amesimama mbele yake aliona jinsi Yesu alivyolia kwa sauti na kukata roho, akasema, “Kweli mtu huyu alikuwa Mwana wa Mungu!”
Et le centurion qui était là vis-à-vis de lui, voyant qu’il avait expiré en criant ainsi, dit: Certainement, cet homme était Fils de Dieu.
40 Walikuwako pia wanawake waliotazama kwa mbali, miongoni mwao akiwa Maria toka mji wa Magdala, Salome, na Maria mama wa kina Yakobo mdogo na Yose.
Et il y avait aussi des femmes qui regardaient de loin, entre lesquelles étaient aussi Marie de Magdala, et Marie, la mère de Jacques le mineur et de Joses, et Salomé,
41 Hawa walimfuata Yesu alipokuwa Galilaya na kumtumikia. Kulikuwa na wanawake wengine wengi waliokuja Yerusalemu pamoja naye.
qui, lorsqu’il était en Galilée, l’avaient suivi et l’avaient servi, et plusieurs autres qui étaient montées avec lui à Jérusalem.
42 Wakati wa jioni ulikuwa umekwisha fika. Hiyo ilikuwa siku ya Maandalio, yaani siku inayotangulia Sabato.
Et le soir étant déjà venu, puisque c’était la Préparation, ce qui est le jour qui précède un sabbat,
43 Hapo akaja Yosefu mwenyeji wa Armathaya, mjumbe wa Baraza Kuu, aliyeheshimika sana. Yeye pia alikuwa anatazamia kuja kwa Ufalme wa Mungu. Basi, alimwendea Pilato bila uoga, akaomba apewe mwili wa Yesu.
Joseph qui était d’Arimathée, conseiller honorable, qui aussi lui-même attendait le royaume de Dieu, vint et prit sur lui d’entrer auprès de Pilate, et lui demanda le corps de Jésus.
44 Pilato alishangaa kusikia kwamba Yesu alikuwa amekwisha kufa. Basi, akamwita jemadari, akamwuliza kama Yesu alikuwa amekufa kitambo.
Et Pilate s’étonna, [ayant peine à croire] qu’il soit déjà mort; et ayant appelé le centurion, il lui demanda s’il y avait longtemps qu’il était mort.
45 Pilato alipoarifiwa na huyo jemadari kwamba Yesu alikuwa amekwisha kufa, akamruhusu Yosefu auchukue mwili wake.
Et l’ayant appris du centurion, il donna le corps à Joseph.
46 Hapo Yosefu akanunua sanda ya kitani, akauteremsha chini huo mwili, akauzungushia sanda. Akauweka katika kaburi lililokuwa limechongwa mwambani, kisha akavingirisha jiwe kubwa mbele ya mlango.
Et Joseph, ayant acheté un linceul, le descendit, et l’enveloppa du linceul, et le mit dans un sépulcre qui était taillé dans le roc, et roula une pierre contre la porte du sépulcre.
47 Nao Maria Magdalene na Maria mama yake Yose walipaona hapo alipolazwa.
Et Marie de Magdala, et Marie, la [mère] de Joses, regardaient où on le mettait.