< Marko 15 >

1 Kulipopambazuka, makuhani wakuu walifanya shauri pamoja na wazee, walimu wa Sheria na Baraza lote, wakamfunga Yesu pingu, wakampeleka na kumkabidhi kwa Pilato.
And as soon as ever it was light the chief priests holding a consultation with the elders and scribes, they and the whole sanhedrim, bound Jesus, and carried Him away, and delivered Him to Pilate.
2 Pilato akamwuliza Yesu, “Je, wewe ni mfalme wa Wayahudi?” Yesu akajibu, “Wewe umesema.”
And Pilate asked Him, Art thou the king of the Jews? and He answered It is as thou sayst.
3 Makuhani wakuu wakamshtaki Yesu mambo mengi.
And the chief priests accused Him of many things: but he answered nothing.
4 Pilato akamwuliza tena Yesu, “Je, hujibu neno? Tazama wanavyotoa mashtaka mengi juu yako.”
So Pilate asked Him again, saying, Dost thou answer nothing? See how many things they witness against thee:
5 Lakini Yesu hakujibu neno, hata pilato akashangaa.
but Jesus still answered nothing, so that Pilate was amazed.
6 Kila wakati wa sikukuu ya Pasaka, Pilato alikuwa na desturi ya kuwafungulia mfungwa mmoja waliyemtaka.
Now at the feast he used to release to them one prisoner, whomsoever they desired:
7 Basi, kulikuwa na mtu mmoja aitwaye Baraba, ambaye alikuwa amefungwa pamoja na waasi wengine kwa kusababisha uasi na mauaji.
and there was one Barabbas under confinement with some of his accomplices in sedition, who had committed murder in the insurrection.
8 Watu wengi wakamwendea Pilato wakamwomba awafanyie kama kawaida yake.
And the people clamoured and desired him to do as he always used to do for them.
9 Pilato akawauliza, “Je, mwataka niwafungulieni Mfalme wa Wayahudi?”
But Pilate answered them, saying, Would ye have me release to you the king of the Jews?
10 Alisema hivyo kwa sababu alijua wazi kwamba makuhani wakuu walimkabidhi Yesu kwake kwa sababu ya wivu.
(for he knew that the chief priests had delivered Him up to him out of envy: )
11 Lakini makuhani wakuu wakawachochea watu wamwombe Pilato awafungulie Baraba.
but the chief priests incited the people to desire that he would rather release Barabbas to them.
12 Pilato akawauliza tena, “Basi, sasa mwataka nifanye nini na mtu huyu mnayemwita Mfalme wa Wayahudi?”
And Pilate answered, and said to them again, What then would you have me do with Him, whom ye call king of the Jews?
13 Watu wote wakapaaza sauti tena: “Msulubishe!”
And they cried out again, Crucify Him.
14 Lakini Pilato akawauliza, “Kwa nini! Amefanya kosa gani?” Lakini wao wakazidi kupaaza sauti, “Msulubishe!”
But Pilate said unto them, Why, what ill has He done? And they cried out the more vehemently, Crucify Him.
15 Pilato alitaka kuuridhisha huo umati wa watu; basi, akamwachilia Baraba kutoka gerezani. Akaamuru Yesu apigwe viboko, kisha akamtoa asulubiwe.
So Pilate being willing to ingratiate with the multitude, released Barabbas to them, and having scourged Jesus, delivered Him up to be crucified.
16 Kisha askari walimpeleka Yesu ndani ukumbini, katika ikulu, wakakusanya kikosi kizima cha askari.
And the soldiers led Him away into the hall, which is called the Pretorium; and gathered their whole company together:
17 Wakamvika vazi la rangi ya zambarau, wakasokota taji ya miiba, wakamwekea kichwani.
and they clad Him in purple, and platted a crown of thorns and put it on his head,
18 Wakaanza kumsalimu, “Shikamoo Mfalme wa Wayahudi!”
and saluted Him, saying, Hail king of the Jews;
19 Wakampiga kichwani kwa mwanzi, wakamtemea mate; wakampigia magoti na kumsujudia.
and struck Him on the head with a reed, and spit upon Him, and bowed their knees, and did Him homage.
20 Baada ya kumdhihaki, walimvua lile joho, wakamvika nguo zake, kisha wakampeleka kumsulubisha.
And when they had thus abused Him, they took off the purple from Him, and put his own clothes on Him, and brought Him out to crucify Him.
21 Walipokuwa njiani, walikutana na mtu mmoja aitwaye Simoni, mwenyeji wa Kurene. Yeye alikuwa baba wa Aleksanda na Rufo, na wakati huo alikuwa akitoka shambani. Basi, wakamlazimisha auchukue msalaba wa Yesu.
And they compel one Simon a Cyrenian, the father of Alexander and Rufus, as he was passing by, coming out of the country, to carry his cross:
22 Kisha wakampeleka Yesu mpaka mahali palipoitwa Golgotha, maana yake, “Mahali pa Fuvu la Kichwa.”
and they brought Him to a place called Golgotha, which is, being interpreted, the place of a scull.
23 Wakampa divai iliyochanganywa na manemane, lakini yeye akaikataa.
And they offered Him wine mingled with myrrh to drink, but He would not take it.
24 Basi, wakamsulubisha, wakagawana mavazi yake kwa kuyapigia kura waamue nani angepata nini.
And when they had fastened Him to the cross, they parted his garments, casting lots upon them, what each of them should take.
25 Ilikuwa saa tatu asubuhi walipomsulubisha.
And it was the third hour, when they fixed Him on the cross:
26 Na mshtaka wake ulikuwa umeandikwa: “Mfalme wa Wayahudi.”
and the title of his charge was written over Him, THE KING OF THE JEWS.
27 Pamoja naye waliwasulubisha wanyang'anyi wawili, mmoja upande wake wa kulia na mwingine upande wake wa kushoto.
And they crucified two thieves with Him, one on his right hand and one on his left:
28 Hapo yakatimia Maandiko Matakatifu yanayosema, “Aliwekwa kundi moja na waovu.”
so that the scripture was fulfilled, which saith, "And He was numbered with the transgressors."
29 Watu waliokuwa wanapita mahali hapo walimtukana, wakitikisa vichwa vyao na kusema, “Aha! Wewe mwenye kuvunja Hekalu na kulijenga kwa siku tatu!
And they that passed by reviled Him, shaking their heads and saying, Ah, thou that destroyest, the temple,
30 Sasa, shuka msalabani ujiokoe mwenyewe!”
and buildest it in three days, save thyself and come down from the cross.
31 Nao makuhani wakuu pamoja na walimu wa Sheria walimdhihaki wakisema, “Aliwaokoa wengine, lakini kujiokoa mwenyewe hawezi!
And the chief priests likewise scoffing at Him among themselves, with the scribes, said, He saved others, Himself He cannot save: let Christ,
32 Eti yeye ni Kristo, Mfalme wa Israeli! Basi, na ashuke msalabani ili tuone na kuamini.” Hata watu wale waliosulubiwa pamoja naye walimtukana.
the king of Israel, come down now from the cross, that we may see and believe in Him. And even they that were crucified with Him, reviled Him.
33 Tangu saa sita mchana mpaka saa tisa kulikuwa giza nchini kote.
Now at the sixth hour there was darkness over the whole land, until the ninth hour.
34 Saa tisa alasiri Yesu akalia kwa sauti kubwa, “Eloi, Eloi, lema sabakthani?” Maana yake, “Mungu wangu, Mungu wangu, mbona umeniacha?”
And at the ninth hour Jesus cried out with a loud voice, saying, "Eloi, Eloi, lama sabachthani," which is being interpreted, My God, my God, why hast thou forsaken me?
35 Baadhi ya watu waliosimama pale waliposikia hivyo, walisema, “Sikiliza! Anamwita Eliya!”
And some of them that stood by hearing it, said, Behold He calleth upon Elias.
36 Mtu mmoja akakimbia, akachovya sifongo katika siki, akaiweka juu ya mwanzi, akampa anywe akisema, “Hebu tuone kama Eliya atakuja kumteremsha msalabani!”
And there ran one, and filled a spunge with vinegar, and putting it on a reed offered it Him to drink, saying, Let Him alone, let us see whether Elias will come to take Him down.
37 Yesu akapaaza sauti kubwa, akakata roho.
But Jesus cried with a loud voice and expired.
38 Basi, pazia la Hekalu likapasuka vipande viwili toka juu mpaka chini.
And the veil of the temple was rent in two from the top to the bottom.
39 Jemadari mmoja aliyekuwa amesimama mbele yake aliona jinsi Yesu alivyolia kwa sauti na kukata roho, akasema, “Kweli mtu huyu alikuwa Mwana wa Mungu!”
And when the centurion, that stood over against Him, saw that He expired with such a cry, he said, Truly this man was the Son of God.
40 Walikuwako pia wanawake waliotazama kwa mbali, miongoni mwao akiwa Maria toka mji wa Magdala, Salome, na Maria mama wa kina Yakobo mdogo na Yose.
There were also women at a distance looking on: among whom was Mary Magdalene, and Mary the mother of James the less and of Joses, and Salome;
41 Hawa walimfuata Yesu alipokuwa Galilaya na kumtumikia. Kulikuwa na wanawake wengine wengi waliokuja Yerusalemu pamoja naye.
who also when He was in Galilee, followed Him and waited on Him: and several others who came up to Jerusalem with Him.
42 Wakati wa jioni ulikuwa umekwisha fika. Hiyo ilikuwa siku ya Maandalio, yaani siku inayotangulia Sabato.
And the evening being now come, (because it was the preparation,
43 Hapo akaja Yosefu mwenyeji wa Armathaya, mjumbe wa Baraza Kuu, aliyeheshimika sana. Yeye pia alikuwa anatazamia kuja kwa Ufalme wa Mungu. Basi, alimwendea Pilato bila uoga, akaomba apewe mwili wa Yesu.
or the day before the sabbath, ) Joseph of Arimathea, an honorable counsellor, who also was expecting the kingdom of God, came and went in boldly to Pilate, and begged the body of Jesus.
44 Pilato alishangaa kusikia kwamba Yesu alikuwa amekwisha kufa. Basi, akamwita jemadari, akamwuliza kama Yesu alikuwa amekufa kitambo.
But Pilate wondered that He was dead already, and therefore calling for the centurion he asked him if He had been dead any time:
45 Pilato alipoarifiwa na huyo jemadari kwamba Yesu alikuwa amekwisha kufa, akamruhusu Yosefu auchukue mwili wake.
and when he heard it from the centurion, he granted the body to Joseph.
46 Hapo Yosefu akanunua sanda ya kitani, akauteremsha chini huo mwili, akauzungushia sanda. Akauweka katika kaburi lililokuwa limechongwa mwambani, kisha akavingirisha jiwe kubwa mbele ya mlango.
And he bought fine linen, and took Him down, and wrapped Him in the linen, and laid Him in a sepulchre which was hewn out of a rock; and rolled a stone to the door of the sepulchre.
47 Nao Maria Magdalene na Maria mama yake Yose walipaona hapo alipolazwa.
And Mary Magdalene, and Mary the mother of Joses observed where He was laid.

< Marko 15 >