< Marko 14 >

1 Ilikuwa siku mbili tu kabla ya sikukuu ya Pasaka na ya Mikate Isiyotiwa Chachu. Makuhani wakuu na walimu wa Sheria walikuwa wakitafuta njia ya kumtia Yesu nguvuni kwa hila wamuue.
After two days was the feast of the passover, and of unleavened bread. And the chief priests and the scribes were contriving how they might take Jesus by surprise, and kill him.
2 Lakini walisema, “Tusimtie nguvuni wakati wa sikukuu, watu wasije wakafanya ghasia.”
They said, however, Not during the festival, for fear of an insurrection among the people.
3 Yesu alikuwa Bethania, nyumbani kwa Simoni, Mkoma. Alipokuwa mezani kula chakula, mama mmoja aliyekuwa na chupa ya alabasta yenye marashi ya nardo safi ya thamani kubwa alikuja, akaivunja hiyo chupa, akammiminia Yesu marashi hayo kichwani.
Now being at table in Bethany, in the house of Simon, formerly a leper, there came a woman with an alabaster box of the balsam of spikenard, which was very costly; and she broken open the box, and poured the liquor upon his head.
4 Baadhi ya watu waliokuwa hapo walikasirika wakajisemea, “Kwa nini kupoteza ovyo marashi haya?
There were some present, who said with indignation, Why this profusion of the balsam?
5 Yangaliweza kuuzwa kwa fedha kiasi cha denari mia tatu, wakapewa maskini!” Wakamkemea huyo mama.
For it could have been sold for more than three hundred denarii, which might have been given to the poor. And they murmured against her.
6 Lakini Yesu akawaambia, “Mwacheni; kwa nini mnamsumbua? Amenitendea jambo jema.
But Jesus said, Let her alone. Why do you molest her? She has done me a good office.
7 Maskini mnao daima pamoja nanyi; mnaweza kuwasaidia wakati wowote mnaopenda. Lakini mimi sitakuwapo pamoja nanyi daima.
For you will have the poor always amongst you, and can do them good whenever you please; but me you will not always have.
8 Yeye amefanya alivyoweza; ameupaka mwili wangu marashi kuutayarisha kwa maziko.
She has done what she could. She has beforehand embalmed my body for the funeral.
9 Nawaambieni kweli, popote ulimwenguni Habari Njema itakapohubiriwa, kitendo hiki alichofanya kitatajwa kwa ajili ya kumkumbuka.”
Indeed, I say to you, in whatsoever corner of the world the glad tidings shall be proclaimed, what this woman has now done, shall be mentioned to her honor.
10 Kisha Yuda Iskarioti, mmoja wa wale kumi na wawili, alienda kwa makuhani wakuu ili kumsaliti Yesu.
Then Judas Iscariot, one of the twelve, repaired to the chief priests, to betray Jesus to them.
11 Makuhani wakuu waliposikia habari hiyo, walifurahi, wakaahidi kumpa fedha. Basi, Yuda akaanza kutafuta nafasi ya kumsaliti Yesu.
And they listened to him with joy, and promised to give him money. Afterward he sought a favorable opportunity to deliver him up.
12 Siku ya kwanza ya sikukuu ya Mikate Isiyotiwa Chachu, wakati ambapo mwana kondoo wa Pasaka huchinjwa, wanafunzi wake walimwuliza, “Wataka tukuandalie wapi karamu ya Pasaka?”
Now the first day of unleavened bread, when the passover is sacrificed, his disciples said to him, Whither shall we go to prepare for your eating the passover?
13 Basi Yesu akawatuma wawili wa wanafunzi wake akiwaambia, “Nendeni mjini, nanyi mtakutana na mtu anayebeba mtungi wa maji. Mfuateni
Then he sent two of his disciples, saying to them, Go into the city, where you will meet a man carrying a pitcher of water; follow him;
14 mpaka katika nyumba atakayoingia, mkamwambie mwenye nyumba, Mwalimu anasema: wapi chumba changu ambamo nitakula Pasaka pamoja na wanafunzi wangu?
and wherever he shall enter, say to the master of the house, The Teacher says, Where is the guest chamber, in which I may eat the passover with my disciples?
15 Naye atawaonyesha chumba kikubwa ghorofani kilichotayarishwa na kupambwa. Tuandalieni humo.”
And he will show you a large upper room ready furnished. There prepare for us.
16 Wanafunzi wakaondoka, wakaenda mjini, wakakuta kila kitu sawa kama Yesu alivyokuwa amewaambia. Wakaandaa karamu ya Pasaka.
Accordingly, his disciples went away, and being come into the city, found everything as he had told them, and prepared the passover.
17 Ilipokuwa jioni, Yesu alifika pamoja na wanafunzi wake kumi na wawili.
In the evening he went thither with the twelve.
18 Walipokuwa mezani wakila, Yesu alisema, “Kweli nawaambieni, mmoja wenu anayekula pamoja nami, atanisaliti.”
As they were at table eating, Jesus said, Indeed, I say to you, that one of you who eats with me, will betray me.
19 Hapo wanafunzi wake wakaanza kuhuzunika, wakamwuliza mmojammoja, “Je, ni mimi?”
Upon this they became very sorrowful; and asked him, all of them, one after another, Is it I?
20 Yesu akawaambia, “Ni mmoja wenu ninyi kumi na wawili, anayechovya mkate pamoja nami katika bakuli.
He answering, said to them, It is one of the twelve; he who dips his morsel in the dish with me.
21 Kweli Mwana wa Mtu anakwenda zake kama Maandiko Matakatifu yanavyosema juu yake; lakini, ole wake mtu yule anayemsaliti Mwana wa Mtu! Ingalikuwa afadhali kwa mtu huyo kama hangalizaliwa!”
The Son of Man departs in the manner foretold in the scripture concerning him; but alas for that man! by whom the Son of Man is betrayed: it had been better for that man never to have been born.
22 Walipokuwa wanakula, Yesu alitwaa mkate, akashukuru, akaumega na kuwapa wanafunzi wake akisema, “Twaeni; huu ni mwili wangu.”
While they were at supper, Jesus took bread, and after blessing, broke it, and gave it to them, saying, Take; this is my body.
23 Kisha akatwaa kikombe, akamshukuru Mungu, akawapa; nao wote wakanywa katika kikombe hicho.
Then he took the cup, and having given thanks, gave it to them; and they all drank of it.
24 Akawaambia, “Hii ni damu yangu inayothibitisha agano la Mungu, damu inayomwagwa kwa ajili ya watu wengi.
And he said to them, This is my blood, the blood of the new institution, shed for many.
25 Kweli nawaambieni, sitakunywa tena divai ya zabibu mpaka siku ile nitakapoinywa upya katika Ufalme wa Mungu.”
Indeed, I say to you, that I will drink no more of the product of the vine, till that day when I shall drink it new in the kingdom of God.
26 Kisha wakaimba wimbo, wakaondoka, wakaenda katika mlima wa Mizeituni.
And after the hymn, they went to the Mount of Olives.
27 Yesu akawaambia wanafunzi wake, “Ninyi nyote mtakuwa na mashaka nami; maana Maandiko Matakatifu yasema: Nitampiga mchungaji nao kondoo watatawanyika.
And Jesus said to them, This night I shall prove a stumbling stone to you all; for it is written, "I will smite the Shepherd, and the sheep shall be dispersed."
28 Lakini nikisha fufuka, nitawatangulieni kule Galilaya.”
Nevertheless, after I am raised again, I will go before you to Galilee.
29 Petro akamwambia “Hata kama wote watakuwa na mashaka nawe na kukuacha, mimi sitakukana kamwe!”
Peter then said to him, Though they all should stumble, I never will.
30 Yesu akamwambia, “Kweli nakwambia, usiku huu, kabla jogoo hajawika mara mbili, utanikana mara tatu.”
Jesus answered him, Indeed, I say to you, that to-day, this very night, before the cock crow twice, even you will disown me thrice.
31 Lakini Petro akasisitiza, “Hata kama ni lazima nife pamoja nawe, sitakuacha kamwe.” Wanafunzi wote pia wakasema vivyo hivyo.
But Peter insisted on it, adding, Although I should die with you, I will never disown you. And all the rest said the same.
32 Basi, wakafika katika bustani iitwayo Gethsemane. Yesu akawaambia wanafunzi wake, “Kaeni hapa wakati mimi nasali.”
Then they came to a place named Gethsemane, where he said to his disciples, Stay here while I pray.
33 Kisha akawachukua Petro, Yakobo na Yohane; akaanza kufadhaika sana na kuhangaika.
And he took with him Peter, and James, and John, and being seized with grief and horror,
34 Akawaambia, “Nina huzuni kubwa moyoni hata karibu kufa. Kaeni hapa mkeshe.”
said to them, My soul is overwhelmed with a deadly anguish; tarry here and watch.
35 Akaenda mbele kidogo, akajitupa chini kifudifudi, akasali kwamba, kama ingewezekana, asiipitie saa hiyo ya mateso.
And going a little before, he threw himself on the ground, and prayed that, if it were possible, he might be delivered from that hour,
36 Akasema, “Baba yangu, kwako mambo yote yanawezekana. Uniondolee kikombe hiki; lakini isiwe kama nitakavyo mimi, bali utakavyo wewe.”
and said, Abba, (that is, Father, ) all things are possible to thee; take this cup away from me; yet not what I would, but what thou wilt.
37 Kisha akarudi kwa wanafunzi wale watatu, akawakuta wamelala. Basi, akamwuliza Petro, “Simoni, je umelala? Hukuweza kukesha hata saa moja?”
Then he returned, and finding them asleep, said to Peter, Simon, do you sleep? Could you not keep awake a single hour?
38 Kisha akawaambia, “Kesheni na kusali ili msije mkaingia katika majaribu. Roho i radhi, lakini mwili ni dhaifu.”
Watch and pray, that you be not overcome by temptation: the spirit indeed is willing, but the flesh is weak.
39 Akaenda kusali tena akirudia maneno yaleyale.
Again, he retired and prayed, using the same words.
40 Kisha akarudi tena, akawakuta wamelala. Macho yao yalikuwa yamebanwa na usingizi. Hawakujua la kumjibu.
When he returned, he again found them sleeping; for their eyes were overpowered, and they knew not what to answer him.
41 Alipowajia mara ya tatu aliwaambia, “Mnalala bado na kupumzika? Sasa imetosha! Saa imefika! Mwana wa Mtu anakabidhiwa kwa watu waovu.
A third time he came, and said to them, Do you now sleep, and take your rest? All is over: the hour is come: and the Son of Man is delivered into the hands of sinners.
42 Amkeni, twendeni zetu. Tazameni, yule atakayenisaliti amekaribia.”
Arise. Let us be going. Lo! he who betrays me is drawing near.
43 Yesu alipokuwa bado anasema, Yuda, mmoja wa wale kumi na wawili, akafika pamoja na umati wa watu wenye mapanga na marungu. Watu hao walikuwa wametumwa na makuhani wakuu, walimu wa Sheria na wazee.
Immediately, before he had done speaking, appeared Judas, one of the twelve, with a great multitude armed with swords and clubs, who were sent by the chief priests, the scribes, and the elders.
44 Msaliti Yuda alikuwa amewapa ishara: “Yule nitakayembusu ndiye; mkamateni, mkampeleke chini ya ulinzi.”
Now the betrayer had given them this signal: The man whom I shall kiss, is he; seize him, and lead him away safely.
45 Yuda alipofika tu, alimwendea Yesu moja kwa moja, akasema, “Mwalimu!” Kisha akambusu.
He was no sooner come, than accosting Jesus, he said, Rabbi, Rabbi, and kissed him.
46 Basi, hao watu wakamkamata Yesu, wakamtia nguvuni.
Then they laid hands on him and seized him.
47 Mmoja wa wale waliokuwa wamesimama hapo pamoja na Yesu akauchomoa upanga wake, akampiga mtumishi wa Kuhani Mkuu, akamkata sikio.
But one of those who were present, drew his sword, and smiting the high priest's servant, cut off his ear.
48 Yesu akawaambia, “Je, mmekuja na mapanga na marungu kunikamata kana kwamba mimi ni mnyang'anyi?
Then Jesus addressing them, said, Do you come with swords and clubs to apprehend me, like people in pursuit of a robber?
49 Kila siku nilikuwa pamoja nanyi nikifundisha Hekaluni, wala hamkunikamata. Lakini sasa lazima Maandiko Matakatifu yatimie.”
I was daily amongst you, teaching in the temple, and you did not arrest me. But in this the scriptures are accomplished.
50 Hapo wanafunzi wote wakamwacha, wakakimbia.
Then they all forsook him and fled.
51 Kulikuwa na kijana mmoja aliyekuwa anamfuata Yesu akiwa amevaa shuka. Nao wakajaribu kumkamata.
Now there followed him a youth, who had only a linen cloth wrapped about his body; the soldiers having laid hold of him,
52 Lakini yeye akaponyoka, akaiachilia ile shuka, akakimbia uchi.
he left the cloth, and fled from them naked.
53 Basi, wakampeleka Yesu kwa Kuhani Mkuu ambapo makuhani wakuu wote, wazee na walimu wa Sheria walikuwa wamekutanika.
Then they took Jesus away to the high priest, with whom all the chief priests, the elders, and the scribes, were convened.
54 Petro alimfuata Yesu kwa mbali, akaingia ndani ya ya wa Kuhani Mkuu, akaketi pamoja na walinzi akiota moto.
And Peter followed him at a distance, as far as the court of the high priest's house, and sat there with the officers, warming himself at the fire.
55 Makuhani wakuu na Baraza lote wakatafuta ushahidi wa kumshtaki Yesu wapate kumwua, lakini hawakupata.
Meanwhile, the chief priests, and all the Sanhedrin, sought for evidence against Jesus, in order to condemn him to die, but found none:
56 Watu wengi walitoa ushahidi wa uongo juu ya Yesu, lakini ushahidi wao haukupatana.
for many gave false testimony against him, but their testimonies were insufficient.
57 Kisha wengine walisimama, wakatoa ushahidi wa uongo wakisema:
The some arose, who testified falsely against him, saying,
58 “Tulimsikia mtu huyu akisema, Nitaliharibu Hekalu hili lililojengwa kwa mikono, na kwa siku tatu nitajenga lingine lisilojengwa kwa mikono.”
We heard him say, I will demolish this temple made with hands, and in three days will build another without hands.
59 Lakini hata hivyo, ushahidi wao haukupatana.
But even here their testimony was defective.
60 Basi, Kuhani Mkuu akasimama katikati yao, akamwuliza Yesu, “Je, hujibu neno? Watu hawa wanashuhudia nini dhidi yako?”
Then the high priest, standing up in the midst, interrogated Jesus, saying, Do you answer nothing to what these men testify against you?
61 Lakini yeye akakaa kimya; hakusema hata neno moja. Kuhani Mkuu akamwuliza tena, “Je, wewe ndiwe Kristo, Mwana wa Mungu Mtukufu?”
But he was silent, and gave no answer. Again, the high priest interrogating him, said, Are you the Messiah, the Son of the blessed One?
62 Yesu akajibu, “Naam, mimi ndiye. Tena, mtamwona Mwana wa Mtu amekaa upande wa kulia wa Mwenyezi, akija katika mawingu ya mbinguni.”
Jesus answered, I am; nay, you shall see the Son of Man sitting at the right hand of the Almighty, and coming in the clouds of heaven.
63 Hapo Kuhani Mkuu akararua joho lake, akasema, “Tuna haja gani tena ya mashahidi?
Then the high priest rent his garments, saying, What further need have we of witnesses?
64 Mmesikia kufuru yake! Ninyi mwaonaje?” Wote wakaamua kwamba anastahili kuuawa.
You have heard the blasphemy. What is your opinion? And they all pronounced him worthy of death.
65 Basi, baadhi yao wakaanza kumtemea mate, wakamfunika uso, wakampiga na kumwambia, “Bashiri ni nani aliyekupiga!” Hata watumishi wakamchukua, wakampiga makofi.
Then some began to spit on him; others to cover his face and buffet him, saying to him, Divine who it is. And the officers gave him blows on the cheeks.
66 Petro alipokuwa bado chini ukumbini, mmoja wa wajakazi wa kuhani Mkuu alikuja.
Now Peter being below in the court, one of the maids of the high priest came thither,
67 Alipomwona Petro akiota moto, alimtazama, akamwambia, “Hata wewe ulikuwa pamoja na Yesu Mnazareti.”
who seeing Peter warming himself, looked on him, and said, You also were with the Nazarene Jesus.
68 Lakini Petro akakana, “Sijui, wala sielewi unayosema!” Kisha Petro akaondoka, akaenda nje uani. Hapo jogoo akawika.
But he denied it, saying, I know him not: nor do I understand what you mean. Immediately he went out into the portico, and the cock crew.
69 Yule mjakazi alipomwona tena Petro, akaanza tena kuwaambia watu waliokuwa wamesimama hapo, “Mtu huyu ni mmoja wao.”
The maid seeing him again, said to the bystanders, This is one of them.
70 Petro akakana tena. Baadaye kidogo, watu waliokuwa wamesimama hapo wakamwambia Petro, “Hakika wewe ni mmoja wao, maana wewe ni Mgalilaya.”
Again he denied. And a little after, those who were present said to Peter, You are certainly one of them; for you are a Galilean, your speech shows it.
71 Lakini Petro akaanza kulaani na kuapa akisema, “Mimi simjui mtu huyu mnayesema habari zake.”
Upon this he affirmed, with imprecations, and oaths, that he did not know the man of whom they spoke.
72 Hapo jogoo akawika mara ya pili. Basi, Petro akakumbuka jinsi Yesu alivyokuwa amemwambia: “Kabla jogoo hajawika mara mbili, utanikana mara tatu.” Petro akabubujika machozi.
The cock crew the second time: and Peter recollected the word which Jesus had said to him, Before the cock crow twice, you will disown me thrice. And reflecting upon this, he wept.

< Marko 14 >