< Marko 14 >

1 Ilikuwa siku mbili tu kabla ya sikukuu ya Pasaka na ya Mikate Isiyotiwa Chachu. Makuhani wakuu na walimu wa Sheria walikuwa wakitafuta njia ya kumtia Yesu nguvuni kwa hila wamuue.
After two days was the feast of the passover, and of unleavened bread: and the chief priests and the scribes sought how they might take him by craft, and put him to death.
2 Lakini walisema, “Tusimtie nguvuni wakati wa sikukuu, watu wasije wakafanya ghasia.”
But they said, Not on the feast day, lest there be an uproar of the people.
3 Yesu alikuwa Bethania, nyumbani kwa Simoni, Mkoma. Alipokuwa mezani kula chakula, mama mmoja aliyekuwa na chupa ya alabasta yenye marashi ya nardo safi ya thamani kubwa alikuja, akaivunja hiyo chupa, akammiminia Yesu marashi hayo kichwani.
And being in Bethany in the house of Simon the leper, as he sat at meat, there came a woman having an alabaster box of ointment of spikenard very precious; and she broke the box, and poured it on his head.
4 Baadhi ya watu waliokuwa hapo walikasirika wakajisemea, “Kwa nini kupoteza ovyo marashi haya?
And there were some that had indignation within themselves, and said, Why was this waste of the ointment made?
5 Yangaliweza kuuzwa kwa fedha kiasi cha denari mia tatu, wakapewa maskini!” Wakamkemea huyo mama.
For it might have been sold for more than three hundred pence, and have been given to the poor. And they murmured against her.
6 Lakini Yesu akawaambia, “Mwacheni; kwa nini mnamsumbua? Amenitendea jambo jema.
And Jesus said, Let her alone; why trouble you her? she has worked a good work on me.
7 Maskini mnao daima pamoja nanyi; mnaweza kuwasaidia wakati wowote mnaopenda. Lakini mimi sitakuwapo pamoja nanyi daima.
For you have the poor with you always, and whenever you will you may do them good: but me you have not always.
8 Yeye amefanya alivyoweza; ameupaka mwili wangu marashi kuutayarisha kwa maziko.
She has done what she could: she is come beforehand to anoint my body to the burying.
9 Nawaambieni kweli, popote ulimwenguni Habari Njema itakapohubiriwa, kitendo hiki alichofanya kitatajwa kwa ajili ya kumkumbuka.”
Truly I say to you, Wherever this gospel shall be preached throughout the whole world, this also that she has done shall be spoken of for a memorial of her.
10 Kisha Yuda Iskarioti, mmoja wa wale kumi na wawili, alienda kwa makuhani wakuu ili kumsaliti Yesu.
And Judas Iscariot, one of the twelve, went to the chief priests, to betray him to them.
11 Makuhani wakuu waliposikia habari hiyo, walifurahi, wakaahidi kumpa fedha. Basi, Yuda akaanza kutafuta nafasi ya kumsaliti Yesu.
And when they heard it, they were glad, and promised to give him money. And he sought how he might conveniently betray him.
12 Siku ya kwanza ya sikukuu ya Mikate Isiyotiwa Chachu, wakati ambapo mwana kondoo wa Pasaka huchinjwa, wanafunzi wake walimwuliza, “Wataka tukuandalie wapi karamu ya Pasaka?”
And the first day of unleavened bread, when they killed the passover, his disciples said to him, Where will you that we go and prepare that you may eat the passover?
13 Basi Yesu akawatuma wawili wa wanafunzi wake akiwaambia, “Nendeni mjini, nanyi mtakutana na mtu anayebeba mtungi wa maji. Mfuateni
And he sends forth two of his disciples, and says to them, Go you into the city, and there shall meet you a man bearing a pitcher of water: follow him.
14 mpaka katika nyumba atakayoingia, mkamwambie mwenye nyumba, Mwalimu anasema: wapi chumba changu ambamo nitakula Pasaka pamoja na wanafunzi wangu?
And wherever he shall go in, say you to the manager of the house, The Master says, Where is the guest room, where I shall eat the passover with my disciples?
15 Naye atawaonyesha chumba kikubwa ghorofani kilichotayarishwa na kupambwa. Tuandalieni humo.”
And he will show you a large upper room furnished and prepared: there make ready for us.
16 Wanafunzi wakaondoka, wakaenda mjini, wakakuta kila kitu sawa kama Yesu alivyokuwa amewaambia. Wakaandaa karamu ya Pasaka.
And his disciples went forth, and came into the city, and found as he had said to them: and they made ready the passover.
17 Ilipokuwa jioni, Yesu alifika pamoja na wanafunzi wake kumi na wawili.
And in the evening he comes with the twelve.
18 Walipokuwa mezani wakila, Yesu alisema, “Kweli nawaambieni, mmoja wenu anayekula pamoja nami, atanisaliti.”
And as they sat and did eat, Jesus said, Truly I say to you, One of you which eats with me shall betray me.
19 Hapo wanafunzi wake wakaanza kuhuzunika, wakamwuliza mmojammoja, “Je, ni mimi?”
And they began to be sorrowful, and to say to him one by one, Is it I? and another said, Is it I?
20 Yesu akawaambia, “Ni mmoja wenu ninyi kumi na wawili, anayechovya mkate pamoja nami katika bakuli.
And he answered and said to them, It is one of the twelve, that dips with me in the dish.
21 Kweli Mwana wa Mtu anakwenda zake kama Maandiko Matakatifu yanavyosema juu yake; lakini, ole wake mtu yule anayemsaliti Mwana wa Mtu! Ingalikuwa afadhali kwa mtu huyo kama hangalizaliwa!”
The Son of man indeed goes, as it is written of him: but woe to that man by whom the Son of man is betrayed! good were it for that man if he had never been born.
22 Walipokuwa wanakula, Yesu alitwaa mkate, akashukuru, akaumega na kuwapa wanafunzi wake akisema, “Twaeni; huu ni mwili wangu.”
And as they did eat, Jesus took bread, and blessed, and broke it, and gave to them, and said, Take, eat: this is my body.
23 Kisha akatwaa kikombe, akamshukuru Mungu, akawapa; nao wote wakanywa katika kikombe hicho.
And he took the cup, and when he had given thanks, he gave it to them: and they all drank of it.
24 Akawaambia, “Hii ni damu yangu inayothibitisha agano la Mungu, damu inayomwagwa kwa ajili ya watu wengi.
And he said to them, This is my blood of the new testament, which is shed for many.
25 Kweli nawaambieni, sitakunywa tena divai ya zabibu mpaka siku ile nitakapoinywa upya katika Ufalme wa Mungu.”
Truly I say to you, I will drink no more of the fruit of the vine, until that day that I drink it new in the kingdom of God.
26 Kisha wakaimba wimbo, wakaondoka, wakaenda katika mlima wa Mizeituni.
And when they had sung an hymn, they went out into the mount of Olives.
27 Yesu akawaambia wanafunzi wake, “Ninyi nyote mtakuwa na mashaka nami; maana Maandiko Matakatifu yasema: Nitampiga mchungaji nao kondoo watatawanyika.
And Jesus says to them, All you shall be offended because of me this night: for it is written, I will smite the shepherd, and the sheep shall be scattered.
28 Lakini nikisha fufuka, nitawatangulieni kule Galilaya.”
But after that I am risen, I will go before you into Galilee.
29 Petro akamwambia “Hata kama wote watakuwa na mashaka nawe na kukuacha, mimi sitakukana kamwe!”
But Peter said to him, Although all shall be offended, yet will not I.
30 Yesu akamwambia, “Kweli nakwambia, usiku huu, kabla jogoo hajawika mara mbili, utanikana mara tatu.”
And Jesus says to him, Truly I say to you, That this day, even in this night, before the cock crow twice, you shall deny me thrice.
31 Lakini Petro akasisitiza, “Hata kama ni lazima nife pamoja nawe, sitakuacha kamwe.” Wanafunzi wote pia wakasema vivyo hivyo.
But he spoke the more vehemently, If I should die with you, I will not deny you in any wise. Likewise also said they all.
32 Basi, wakafika katika bustani iitwayo Gethsemane. Yesu akawaambia wanafunzi wake, “Kaeni hapa wakati mimi nasali.”
And they came to a place which was named Gethsemane: and he says to his disciples, Sit you here, while I shall pray.
33 Kisha akawachukua Petro, Yakobo na Yohane; akaanza kufadhaika sana na kuhangaika.
And he takes with him Peter and James and John, and began to be sore amazed, and to be very heavy;
34 Akawaambia, “Nina huzuni kubwa moyoni hata karibu kufa. Kaeni hapa mkeshe.”
And says to them, My soul is exceeding sorrowful to death: tarry you here, and watch.
35 Akaenda mbele kidogo, akajitupa chini kifudifudi, akasali kwamba, kama ingewezekana, asiipitie saa hiyo ya mateso.
And he went forward a little, and fell on the ground, and prayed that, if it were possible, the hour might pass from him.
36 Akasema, “Baba yangu, kwako mambo yote yanawezekana. Uniondolee kikombe hiki; lakini isiwe kama nitakavyo mimi, bali utakavyo wewe.”
And he said, Abba, Father, all things are possible to you; take away this cup from me: nevertheless not what I will, but what you will.
37 Kisha akarudi kwa wanafunzi wale watatu, akawakuta wamelala. Basi, akamwuliza Petro, “Simoni, je umelala? Hukuweza kukesha hata saa moja?”
And he comes, and finds them sleeping, and says to Peter, Simon, sleep you? could not you watch one hour?
38 Kisha akawaambia, “Kesheni na kusali ili msije mkaingia katika majaribu. Roho i radhi, lakini mwili ni dhaifu.”
Watch you and pray, lest you enter into temptation. The spirit truly is ready, but the flesh is weak.
39 Akaenda kusali tena akirudia maneno yaleyale.
And again he went away, and prayed, and spoke the same words.
40 Kisha akarudi tena, akawakuta wamelala. Macho yao yalikuwa yamebanwa na usingizi. Hawakujua la kumjibu.
And when he returned, he found them asleep again, (for their eyes were heavy, ) neither knew they what to answer him.
41 Alipowajia mara ya tatu aliwaambia, “Mnalala bado na kupumzika? Sasa imetosha! Saa imefika! Mwana wa Mtu anakabidhiwa kwa watu waovu.
And he comes the third time, and says to them, Sleep on now, and take your rest: it is enough, the hour is come; behold, the Son of man is betrayed into the hands of sinners.
42 Amkeni, twendeni zetu. Tazameni, yule atakayenisaliti amekaribia.”
Rise up, let us go; see, he that betrays me is at hand.
43 Yesu alipokuwa bado anasema, Yuda, mmoja wa wale kumi na wawili, akafika pamoja na umati wa watu wenye mapanga na marungu. Watu hao walikuwa wametumwa na makuhani wakuu, walimu wa Sheria na wazee.
And immediately, while he yet spoke, comes Judas, one of the twelve, and with him a great multitude with swords and staves, from the chief priests and the scribes and the elders.
44 Msaliti Yuda alikuwa amewapa ishara: “Yule nitakayembusu ndiye; mkamateni, mkampeleke chini ya ulinzi.”
And he that betrayed him had given them a token, saying, Whomsoever I shall kiss, that same is he; take him, and lead him away safely.
45 Yuda alipofika tu, alimwendea Yesu moja kwa moja, akasema, “Mwalimu!” Kisha akambusu.
And as soon as he was come, he goes straightway to him, and says, Master, master; and kissed him.
46 Basi, hao watu wakamkamata Yesu, wakamtia nguvuni.
And they laid their hands on him, and took him.
47 Mmoja wa wale waliokuwa wamesimama hapo pamoja na Yesu akauchomoa upanga wake, akampiga mtumishi wa Kuhani Mkuu, akamkata sikio.
And one of them that stood by drew a sword, and smote a servant of the high priest, and cut off his ear.
48 Yesu akawaambia, “Je, mmekuja na mapanga na marungu kunikamata kana kwamba mimi ni mnyang'anyi?
And Jesus answered and said to them, Are you come out, as against a thief, with swords and with staves to take me?
49 Kila siku nilikuwa pamoja nanyi nikifundisha Hekaluni, wala hamkunikamata. Lakini sasa lazima Maandiko Matakatifu yatimie.”
I was daily with you in the temple teaching, and you took me not: but the scriptures must be fulfilled.
50 Hapo wanafunzi wote wakamwacha, wakakimbia.
And they all forsook him, and fled.
51 Kulikuwa na kijana mmoja aliyekuwa anamfuata Yesu akiwa amevaa shuka. Nao wakajaribu kumkamata.
And there followed him a certain young man, having a linen cloth cast about his naked body; and the young men laid hold on him:
52 Lakini yeye akaponyoka, akaiachilia ile shuka, akakimbia uchi.
And he left the linen cloth, and fled from them naked.
53 Basi, wakampeleka Yesu kwa Kuhani Mkuu ambapo makuhani wakuu wote, wazee na walimu wa Sheria walikuwa wamekutanika.
And they led Jesus away to the high priest: and with him were assembled all the chief priests and the elders and the scribes.
54 Petro alimfuata Yesu kwa mbali, akaingia ndani ya ya wa Kuhani Mkuu, akaketi pamoja na walinzi akiota moto.
And Peter followed him afar off, even into the palace of the high priest: and he sat with the servants, and warmed himself at the fire.
55 Makuhani wakuu na Baraza lote wakatafuta ushahidi wa kumshtaki Yesu wapate kumwua, lakini hawakupata.
And the chief priests and all the council sought for witness against Jesus to put him to death; and found none.
56 Watu wengi walitoa ushahidi wa uongo juu ya Yesu, lakini ushahidi wao haukupatana.
For many bore false witness against him, but their witness agreed not together.
57 Kisha wengine walisimama, wakatoa ushahidi wa uongo wakisema:
And there arose certain, and bore false witness against him, saying,
58 “Tulimsikia mtu huyu akisema, Nitaliharibu Hekalu hili lililojengwa kwa mikono, na kwa siku tatu nitajenga lingine lisilojengwa kwa mikono.”
We heard him say, I will destroy this temple that is made with hands, and within three days I will build another made without hands.
59 Lakini hata hivyo, ushahidi wao haukupatana.
But neither so did their witness agree together.
60 Basi, Kuhani Mkuu akasimama katikati yao, akamwuliza Yesu, “Je, hujibu neno? Watu hawa wanashuhudia nini dhidi yako?”
And the high priest stood up in the middle, and asked Jesus, saying, Answer you nothing? what is it which these witness against you?
61 Lakini yeye akakaa kimya; hakusema hata neno moja. Kuhani Mkuu akamwuliza tena, “Je, wewe ndiwe Kristo, Mwana wa Mungu Mtukufu?”
But he held his peace, and answered nothing. Again the high priest asked him, and said to him, Are you the Christ, the Son of the Blessed?
62 Yesu akajibu, “Naam, mimi ndiye. Tena, mtamwona Mwana wa Mtu amekaa upande wa kulia wa Mwenyezi, akija katika mawingu ya mbinguni.”
And Jesus said, I am: and you shall see the Son of man sitting on the right hand of power, and coming in the clouds of heaven.
63 Hapo Kuhani Mkuu akararua joho lake, akasema, “Tuna haja gani tena ya mashahidi?
Then the high priest rent his clothes, and says, What need we any further witnesses?
64 Mmesikia kufuru yake! Ninyi mwaonaje?” Wote wakaamua kwamba anastahili kuuawa.
You have heard the blasphemy: what think you? And they all condemned him to be guilty of death.
65 Basi, baadhi yao wakaanza kumtemea mate, wakamfunika uso, wakampiga na kumwambia, “Bashiri ni nani aliyekupiga!” Hata watumishi wakamchukua, wakampiga makofi.
And some began to spit on him, and to cover his face, and to buffet him, and to say to him, Prophesy: and the servants did strike him with the palms of their hands.
66 Petro alipokuwa bado chini ukumbini, mmoja wa wajakazi wa kuhani Mkuu alikuja.
And as Peter was beneath in the palace, there comes one of the maids of the high priest:
67 Alipomwona Petro akiota moto, alimtazama, akamwambia, “Hata wewe ulikuwa pamoja na Yesu Mnazareti.”
And when she saw Peter warming himself, she looked on him, and said, And you also were with Jesus of Nazareth.
68 Lakini Petro akakana, “Sijui, wala sielewi unayosema!” Kisha Petro akaondoka, akaenda nje uani. Hapo jogoo akawika.
But he denied, saying, I know not, neither understand I what you say. And he went out into the porch; and the cock crew.
69 Yule mjakazi alipomwona tena Petro, akaanza tena kuwaambia watu waliokuwa wamesimama hapo, “Mtu huyu ni mmoja wao.”
And a maid saw him again, and began to say to them that stood by, This is one of them.
70 Petro akakana tena. Baadaye kidogo, watu waliokuwa wamesimama hapo wakamwambia Petro, “Hakika wewe ni mmoja wao, maana wewe ni Mgalilaya.”
And he denied it again. And a little after, they that stood by said again to Peter, Surely you are one of them: for you are a Galilaean, and your speech agrees thereto.
71 Lakini Petro akaanza kulaani na kuapa akisema, “Mimi simjui mtu huyu mnayesema habari zake.”
But he began to curse and to swear, saying, I know not this man of whom you speak.
72 Hapo jogoo akawika mara ya pili. Basi, Petro akakumbuka jinsi Yesu alivyokuwa amemwambia: “Kabla jogoo hajawika mara mbili, utanikana mara tatu.” Petro akabubujika machozi.
And the second time the cock crew. And Peter called to mind the word that Jesus said to him, Before the cock crow twice, you shall deny me thrice. And when he thought thereon, he wept.

< Marko 14 >